Tradução Suaíli - Centro de tradução Rawad
Tradução dos significados do Nobre Alcorão
Tradução realizada pela equipe do Centro de Tradução Rowwad em cooperação com a Associação de Chamada em Al-Rabwah e a Associação para o Serviço do Conteúdo Islâmico em Idiomas.
وَيۡلٞ لِّكُلِّ هُمَزَةٖ لُّمَزَةٍ
Ole wake kila anayewakejeli watu kwa ishara na maneno.
ٱلَّذِي جَمَعَ مَالٗا وَعَدَّدَهُۥ
Aliyekusanya mali na kuihesabu.
يَحۡسَبُ أَنَّ مَالَهُۥٓ أَخۡلَدَهُۥ
Anadhani ya kuwa mali yake itambakisha milele!
كَلَّاۖ لَيُنۢبَذَنَّ فِي ٱلۡحُطَمَةِ
Hasha! Hakika atavurumishwa katika Hutwama.
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡحُطَمَةُ
Na ni nini kitakachokujulisha ni nini Hutwama?
نَارُ ٱللَّهِ ٱلۡمُوقَدَةُ
Ni Moto wa Mwenyezi Mungu uliowashwa.
ٱلَّتِي تَطَّلِعُ عَلَى ٱلۡأَفۡـِٔدَةِ
Ambao unapanda nyoyoni.
إِنَّهَا عَلَيۡهِم مُّؤۡصَدَةٞ
Hakika huo utafungwa sawasawa nao wako ndani yake.
فِي عَمَدٖ مُّمَدَّدَةِۭ
Kwenye nguzo zilizonyooshwa.
share_via