Eggo e ɗemngal Swahili - Ali Muhsin Alberwani.
Eggi nde ko Ali Muhsin Alberwani.
عَبَسَ وَتَوَلَّىٰٓ
Alikunja kipaji na akageuka! [1]
أَن جَآءَهُ ٱلۡأَعۡمَىٰ
Kwa sababu alimjia kipofu! [2]
وَمَا يُدۡرِيكَ لَعَلَّهُۥ يَزَّكَّىٰٓ
Na nini kitakujuulisha pengine yeye atatakasika? [3]
أَوۡ يَذَّكَّرُ فَتَنفَعَهُ ٱلذِّكۡرَىٰٓ
Au atawaidhika, na mawaidha yamfae? [4]
أَمَّا مَنِ ٱسۡتَغۡنَىٰ
Ama ajionaye hana haja! [5]
فَأَنتَ لَهُۥ تَصَدَّىٰ
Wewe ndio unamshughulikia? [6]
وَمَا عَلَيۡكَ أَلَّا يَزَّكَّىٰ
Na si juu yako kama hakutakasika. [7]
وَأَمَّا مَن جَآءَكَ يَسۡعَىٰ
Ama anaye kujia kwa juhudi . [8]
وَهُوَ يَخۡشَىٰ
Naye anaogopa! [9]
فَأَنتَ عَنۡهُ تَلَهَّىٰ
Ndio wewe unampuuza? [10]
كَلَّآ إِنَّهَا تَذۡكِرَةٞ
Sivyo hivyo! Huku ni kukumbushana. [11]
فَمَن شَآءَ ذَكَرَهُۥ
Basi anaye penda akumbuke. [12]
فِي صُحُفٖ مُّكَرَّمَةٖ
Yamo katika kurasa zilizo hishimiwa, [13]
مَّرۡفُوعَةٖ مُّطَهَّرَةِۭ
Zilizo inuliwa, zilizo takaswa. [14]
بِأَيۡدِي سَفَرَةٖ
Zimo mikononi mwa Malaika waandishi, [15]
كِرَامِۭ بَرَرَةٖ
Watukufu, wema. [16]
قُتِلَ ٱلۡإِنسَٰنُ مَآ أَكۡفَرَهُۥ
Ameangamia mwanaadamu! Nini kinacho mkufurisha? [17]
مِنۡ أَيِّ شَيۡءٍ خَلَقَهُۥ
Kwa kitu gani amemuumba? [18]
مِن نُّطۡفَةٍ خَلَقَهُۥ فَقَدَّرَهُۥ
Kwa tone la manii, akamuumba na akamkadiria. [19]
ثُمَّ ٱلسَّبِيلَ يَسَّرَهُۥ
Kisha akamsahilishia njia. [20]
ثُمَّ أَمَاتَهُۥ فَأَقۡبَرَهُۥ
Kisha akamfisha, akamtia kaburini. [21]
ثُمَّ إِذَا شَآءَ أَنشَرَهُۥ
Kisha apendapo atamfufua. [22]
كَلَّا لَمَّا يَقۡضِ مَآ أَمَرَهُۥ
La! Hajamaliza aliyo muamuru. [23]
فَلۡيَنظُرِ ٱلۡإِنسَٰنُ إِلَىٰ طَعَامِهِۦٓ
Hebu mtu na atazame chakula chake. [24]
أَنَّا صَبَبۡنَا ٱلۡمَآءَ صَبّٗا
Hakika Sisi tumemimina maji kwa nguvu, [25]
ثُمَّ شَقَقۡنَا ٱلۡأَرۡضَ شَقّٗا
Tena tukaipasua pasua ardhi kwa nguvu, [26]
فَأَنۢبَتۡنَا فِيهَا حَبّٗا
Kisha tukaotesha humo nafaka, [27]
وَعِنَبٗا وَقَضۡبٗا
Na zabibu, na mimea ya majani, [28]
وَزَيۡتُونٗا وَنَخۡلٗا
Na mizaituni, na mitende, [29]
وَحَدَآئِقَ غُلۡبٗا
Na bustani zenye miti iliyo songana baraabara, [30]
وَفَٰكِهَةٗ وَأَبّٗا
Na matunda, na malisho ya wanyama; [31]
مَّتَٰعٗا لَّكُمۡ وَلِأَنۡعَٰمِكُمۡ
Kwa manufaa yenu na mifugo yenu. [32]
فَإِذَا جَآءَتِ ٱلصَّآخَّةُ
Basi utakapo kuja ukelele, [33]
يَوۡمَ يَفِرُّ ٱلۡمَرۡءُ مِنۡ أَخِيهِ
Siku ambayo mtu atamkimbia nduguye, [34]
وَأُمِّهِۦ وَأَبِيهِ
Na mamaye na babaye, [35]
وَصَٰحِبَتِهِۦ وَبَنِيهِ
Na mkewe na wanawe. [36]
لِكُلِّ ٱمۡرِيٕٖ مِّنۡهُمۡ يَوۡمَئِذٖ شَأۡنٞ يُغۡنِيهِ
Kila mtu miongoni mwao siku hiyo atakuwa na lake la kumtosha [37]
وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ مُّسۡفِرَةٞ
Siku hiyo ziko nyuso zitazo nawiri, [38]
ضَاحِكَةٞ مُّسۡتَبۡشِرَةٞ
Zitacheka, zitachangamka; [39]
وَوُجُوهٞ يَوۡمَئِذٍ عَلَيۡهَا غَبَرَةٞ
Na nyuso siku hiyo zitakuwa na mavumbi, [40]
تَرۡهَقُهَا قَتَرَةٌ
Giza totoro litazifunika, [41]
أُوْلَٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡكَفَرَةُ ٱلۡفَجَرَةُ
Hao ndio makafiri watenda maovu [42]
مشاركة عبر