Header Include

Eggo e ɗemngal Swahili - Ali Muhsin Alberwani.

Eggi nde ko Ali Muhsin Alberwani.

QR Code https://quran.islamcontent.com/ff/swahili_barawani

عَبَسَ وَتَوَلَّىٰٓ

Alikunja kipaji na akageuka! [1]

[1] Uso wake ulitaghayari kwa kuchukia na akageuka,
Alikunja kipaji na akageuka! [1]

أَن جَآءَهُ ٱلۡأَعۡمَىٰ

Kwa sababu alimjia kipofu! [2]

[2] Kwa sababu kamjia kipofu anamuuliza khabari ya Dini yake.
Kwa sababu alimjia kipofu! [2]

وَمَا يُدۡرِيكَ لَعَلَّهُۥ يَزَّكَّىٰٓ

Na nini kitakujuulisha pengine yeye atatakasika? [3]

[3] Na wewe unajuaje, pengine huyo kipofu atatakasika kwa atayo yapata kwako,
Na nini kitakujuulisha pengine yeye atatakasika? [3]

أَوۡ يَذَّكَّرُ فَتَنفَعَهُ ٱلذِّكۡرَىٰٓ

Au atawaidhika, na mawaidha yamfae? [4]

[4] Au atawaidhika na mawaidha yamfae.
Au atawaidhika, na mawaidha yamfae? [4]

أَمَّا مَنِ ٱسۡتَغۡنَىٰ

Ama ajionaye hana haja! [5]

[5] Ama yule anaye jiona ametosheka kwa mali yake na nguvu zake,
Ama ajionaye hana haja! [5]

فَأَنتَ لَهُۥ تَصَدَّىٰ

Wewe ndio unamshughulikia? [6]

[6] Wewe ndio unamkabili na unamshughulikia kumfikishia wito wako.
Wewe ndio unamshughulikia? [6]

وَمَا عَلَيۡكَ أَلَّا يَزَّكَّىٰ

Na si juu yako kama hakutakasika. [7]

[7] Na wewe una lawama gani ikiwa yeye hakutakasika kwa Imani?
Na si juu yako kama hakutakasika. [7]

وَأَمَّا مَن جَآءَكَ يَسۡعَىٰ

Ama anaye kujia kwa juhudi . [8]

[8] Ama anaye kukimbilia kutafuta ilimu na uwongofu,
Ama anaye kujia kwa juhudi . [8]

وَهُوَ يَخۡشَىٰ

Naye anaogopa! [9]

[9] Naye anamkhofu Mwenyezi Mungu .
Naye anaogopa! [9]

فَأَنتَ عَنۡهُ تَلَهَّىٰ

Ndio wewe unampuuza? [10]

[10] Wewe unampuuza.
Ndio wewe unampuuza? [10]

كَلَّآ إِنَّهَا تَذۡكِرَةٞ

Sivyo hivyo! Huku ni kukumbushana. [11]

[11] Hakika Aya hizi ni mawaidha.
Sivyo hivyo! Huku ni kukumbushana. [11]

فَمَن شَآءَ ذَكَرَهُۥ

Basi anaye penda akumbuke. [12]

[12] Mwenye kutaka atawaidhika kwa Qur'ani.
Basi anaye penda akumbuke. [12]

فِي صُحُفٖ مُّكَرَّمَةٖ

Yamo katika kurasa zilizo hishimiwa, [13]

[13] Nayo Qur'ani imo katika kurasa zilizo tukuzwa kwa Mwenyezi Mungu,
Yamo katika kurasa zilizo hishimiwa, [13]

مَّرۡفُوعَةٖ مُّطَهَّرَةِۭ

Zilizo inuliwa, zilizo takaswa. [14]

[14] Zina cheo cha juu, na pahala palipo tukuka, zimetakasika na kila upungufu.
Zilizo inuliwa, zilizo takaswa. [14]

بِأَيۡدِي سَفَرَةٖ

Zimo mikononi mwa Malaika waandishi, [15]

[15] Katika mikono ya Malaika ambao Mwenyezi Mungu amewafanya ndio mabalozi baina yake na Mitume wake;
Zimo mikononi mwa Malaika waandishi, [15]

كِرَامِۭ بَرَرَةٖ

Watukufu, wema. [16]

[16] Walio bora, wema.
Watukufu, wema. [16]

قُتِلَ ٱلۡإِنسَٰنُ مَآ أَكۡفَرَهُۥ

Ameangamia mwanaadamu! Nini kinacho mkufurisha? [17]

[17] Ameangamia mwanaadamu! Nini kilicho mfanya akufuru na hali Mwenyezi Mungu amemfanyia hisani zote hizi?
Ameangamia mwanaadamu! Nini kinacho mkufurisha? [17]

مِنۡ أَيِّ شَيۡءٍ خَلَقَهُۥ

Kwa kitu gani amemuumba? [18]

[18] Hakumbuki yeye kaumbwa kutokana na nini?
Kwa kitu gani amemuumba? [18]

مِن نُّطۡفَةٍ خَلَقَهُۥ فَقَدَّرَهُۥ

Kwa tone la manii, akamuumba na akamkadiria. [19]

[19] Kutokana na maji ya kudharauliwa Yeye Mwenyezi Mungu alimwanzisha kumuumba akamjaalia apitie daraja mbali mbali za kukua.
Kwa tone la manii, akamuumba na akamkadiria. [19]

ثُمَّ ٱلسَّبِيلَ يَسَّرَهُۥ

Kisha akamsahilishia njia. [20]

[20] Kisha akamfanyia nyepesi njia ya kufikia Imani, na akamfunza njia hiyo.
Kisha akamsahilishia njia. [20]

ثُمَّ أَمَاتَهُۥ فَأَقۡبَرَهُۥ

Kisha akamfisha, akamtia kaburini. [21]

[21] Kisha akamfisha na akamtukuza kwa kumtia kaburini.
Kisha akamfisha, akamtia kaburini. [21]

ثُمَّ إِذَا شَآءَ أَنشَرَهُۥ

Kisha apendapo atamfufua. [22]

[22] Na tena akipenda atamhuisha baada ya kufa kwake.
Kisha apendapo atamfufua. [22]

كَلَّا لَمَّا يَقۡضِ مَآ أَمَرَهُۥ

La! Hajamaliza aliyo muamuru. [23]

[23] Ni kweli mwanaadamu, juu ya kuwa umri wake mrefu duniani, hakutimiza aliyo amrishwa na Mwenyezi Mungu katika mambo ya Imani na ut'iifu.
La! Hajamaliza aliyo muamuru. [23]

فَلۡيَنظُرِ ٱلۡإِنسَٰنُ إِلَىٰ طَعَامِهِۦٓ

Hebu mtu na atazame chakula chake. [24]

[24] Hebu mtu na aangalie shani ya chakula chake - vipi tulivyo kipanga na kumsahilishia!
Hebu mtu na atazame chakula chake. [24]

أَنَّا صَبَبۡنَا ٱلۡمَآءَ صَبّٗا

Hakika Sisi tumemimina maji kwa nguvu, [25]

[25] Ni Sisi tumeiteremsha mvua kutoka mbinguni, ikateremka.
Hakika Sisi tumemimina maji kwa nguvu, [25]

ثُمَّ شَقَقۡنَا ٱلۡأَرۡضَ شَقّٗا

Tena tukaipasua pasua ardhi kwa nguvu, [26]

[26] Tena tukaipasua pasua ardhi kwa ajili ya mimea.
Tena tukaipasua pasua ardhi kwa nguvu, [26]

فَأَنۢبَتۡنَا فِيهَا حَبّٗا

Kisha tukaotesha humo nafaka, [27]

[27] Tukaotesha humo nafaka ambazo watu huzila na huweka akiba.
Kisha tukaotesha humo nafaka, [27]

وَعِنَبٗا وَقَضۡبٗا

Na zabibu, na mimea ya majani, [28]

[28] Na mizabibu na mimea ya majani inayo liwa mibichi.
Na zabibu, na mimea ya majani, [28]

وَزَيۡتُونٗا وَنَخۡلٗا

Na mizaituni, na mitende, [29]

[29] Na mizaituni mizuri, na mitende yenye kuzaa,
Na mizaituni, na mitende, [29]

وَحَدَآئِقَ غُلۡبٗا

Na bustani zenye miti iliyo songana baraabara, [30]

[30] Na mabustani yaliyo songamana matawi ya miti yake,
Na bustani zenye miti iliyo songana baraabara, [30]

وَفَٰكِهَةٗ وَأَبّٗا

Na matunda, na malisho ya wanyama; [31]

[31] Na matunda ya kustaladhi nayo, na malisha ya kula nyama hoa (mifugo).
Na matunda, na malisho ya wanyama; [31]

مَّتَٰعٗا لَّكُمۡ وَلِأَنۡعَٰمِكُمۡ

Kwa manufaa yenu na mifugo yenu. [32]

[32] Tumeotesha yote hayo kwa ajili ya faida yenu na wanyama wenu wa kufuga.
Kwa manufaa yenu na mifugo yenu. [32]

فَإِذَا جَآءَتِ ٱلصَّآخَّةُ

Basi utakapo kuja ukelele, [33]

[33] Basi utakapo kuja ukelele wa Kiyama utakao tia uziwi masikio,
Basi utakapo kuja ukelele, [33]

يَوۡمَ يَفِرُّ ٱلۡمَرۡءُ مِنۡ أَخِيهِ

Siku ambayo mtu atamkimbia nduguye, [34]

[34] Siku mtu atakapo mkimbia ndugu yake,
Siku ambayo mtu atamkimbia nduguye, [34]

وَأُمِّهِۦ وَأَبِيهِ

Na mamaye na babaye, [35]

[35] Na mama yake, na baba yake,
Na mamaye na babaye, [35]

وَصَٰحِبَتِهِۦ وَبَنِيهِ

Na mkewe na wanawe. [36]

[36] Na mkewe, na wanawe!
Na mkewe na wanawe. [36]

لِكُلِّ ٱمۡرِيٕٖ مِّنۡهُمۡ يَوۡمَئِذٖ شَأۡنٞ يُغۡنِيهِ

Kila mtu miongoni mwao siku hiyo atakuwa na lake la kumtosha [37]

[37] Kila mmojapo katika hawa atakuwa na jambo lake la kumshughulisha!
Kila mtu miongoni mwao siku hiyo atakuwa na lake la kumtosha [37]

وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ مُّسۡفِرَةٞ

Siku hiyo ziko nyuso zitazo nawiri, [38]

[38] Zipo nyuso siku hii zenye mwangaza,
Siku hiyo ziko nyuso zitazo nawiri, [38]

ضَاحِكَةٞ مُّسۡتَبۡشِرَةٞ

Zitacheka, zitachangamka; [39]

[39] Zenye kung'ara na kufurahi kwa neema za Mwenyezi Mungu.
Zitacheka, zitachangamka; [39]

وَوُجُوهٞ يَوۡمَئِذٍ عَلَيۡهَا غَبَرَةٞ

Na nyuso siku hiyo zitakuwa na mavumbi, [40]

[40] Na nyuso nyengine siku hii zina vumbi zimesawijika.
Na nyuso siku hiyo zitakuwa na mavumbi, [40]

تَرۡهَقُهَا قَتَرَةٌ

Giza totoro litazifunika, [41]

[41] Zimegubikwa na kiza na weusi.
Giza totoro litazifunika, [41]

أُوْلَٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡكَفَرَةُ ٱلۡفَجَرَةُ

Hao ndio makafiri watenda maovu [42]

[42] Wenye nyuso hizi ni makafiri wapotovu, ambao walio kuwa hawabali maasi waliyo kuwa wakiyatenda.
Hao ndio makafiri watenda maovu [42]
Footer Include