Eggo e ɗemngal Swahili - Ali Muhsin Alberwani.
Eggi nde ko Ali Muhsin Alberwani.
وَٱلسَّمَآءِ وَٱلطَّارِقِ
Naapa kwa mbingu na Kinacho kuja usiku! [1]
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلطَّارِقُ
Na nini kitakacho kujuulisha ni nini hicho Kinacho kuja usiku? [2]
ٱلنَّجۡمُ ٱلثَّاقِبُ
Ni Nyota yenye mwanga mkali. [3]
إِن كُلُّ نَفۡسٖ لَّمَّا عَلَيۡهَا حَافِظٞ
Hapana nafsi ila inayo mwangalizi. [4]
فَلۡيَنظُرِ ٱلۡإِنسَٰنُ مِمَّ خُلِقَ
Hebu naajitazame mwanaadamu ameumbwa kwa kitu gani? [5]
خُلِقَ مِن مَّآءٖ دَافِقٖ
Ameumbwa kwa maji yatokayo kwa kuchupa! [6]
يَخۡرُجُ مِنۢ بَيۡنِ ٱلصُّلۡبِ وَٱلتَّرَآئِبِ
Yatokayo baina ya mifupa ya mgongo na mbavu. [7]
إِنَّهُۥ عَلَىٰ رَجۡعِهِۦ لَقَادِرٞ
Hakika Yeye ana uweza wa kumrudisha. [8]
يَوۡمَ تُبۡلَى ٱلسَّرَآئِرُ
Siku zitakapo dhihirishwa siri. [9]
فَمَا لَهُۥ مِن قُوَّةٖ وَلَا نَاصِرٖ
Basi hatakuwa na nguvu wala msaidizi. [10]
وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلرَّجۡعِ
Naapa kwa mbingu yenye marejeo! [11]
وَٱلۡأَرۡضِ ذَاتِ ٱلصَّدۡعِ
Na kwa ardhi inayo pasuka! [12]
إِنَّهُۥ لَقَوۡلٞ فَصۡلٞ
Hakika hii ni kauli ya kupambanua. [13]
وَمَا هُوَ بِٱلۡهَزۡلِ
Wala si mzaha. [14]
إِنَّهُمۡ يَكِيدُونَ كَيۡدٗا
Hakika wao wanapanga mpango. [15]
وَأَكِيدُ كَيۡدٗا
Na Mimi napanga mpango. [16]
فَمَهِّلِ ٱلۡكَٰفِرِينَ أَمۡهِلۡهُمۡ رُوَيۡدَۢا
Basi wape muhula makafiri - wape muhula pole pole. [17]
مشاركة عبر