Fassarar Sawahil - Cibiyar fassara ta Ruwwad
Wani gungu na cibiyar fassara ta Ruwad ne suka fassarasu tare da haɗin gwiwar Ƙungiyar Da'awa ta Rabwah da Kungiyar hidimtawa abinda Musulunci ya kunsa da yaruka
بِسۡمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحۡمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu.
ٱلۡحَمۡدُ لِلَّهِ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa walimwengu.[1]
ٱلرَّحۡمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ
Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu.[1]
مَٰلِكِ يَوۡمِ ٱلدِّينِ
Mmiliki wa Siku ya Malipo.
إِيَّاكَ نَعۡبُدُ وَإِيَّاكَ نَسۡتَعِينُ
Ni Wewe tu tunayeabudu, na ni Wewe tu tunayeomba msaada.
ٱهۡدِنَا ٱلصِّرَٰطَ ٱلۡمُسۡتَقِيمَ
Tuongoe kwenye njia iliyonyooka.
صِرَٰطَ ٱلَّذِينَ أَنۡعَمۡتَ عَلَيۡهِمۡ غَيۡرِ ٱلۡمَغۡضُوبِ عَلَيۡهِمۡ وَلَا ٱلضَّآلِّينَ
Njia ya wale uliowaneemesha. Siyo ya wale waliokasirikiwa, wala waliopotea.
مشاركة عبر