Header Include

Swahili translation - Rowad Translation Center

translated by Rowwad Translation Center, in cooperation with the Islamic Propagation Office in Rabwah and the Association for Serving Islamic Content in Languages.

QR Code https://quran.islamcontent.com/hr/swahili_rwwad

إِذَا ٱلسَّمَآءُ ٱنفَطَرَتۡ

Mbingu itakapochanika.

Mbingu itakapochanika.

وَإِذَا ٱلۡكَوَاكِبُ ٱنتَثَرَتۡ

Na nyota zitakapotawanyika.

Na nyota zitakapotawanyika.

وَإِذَا ٱلۡبِحَارُ فُجِّرَتۡ

Na bahari zitakapopasuliwa.

Na bahari zitakapopasuliwa.

وَإِذَا ٱلۡقُبُورُ بُعۡثِرَتۡ

Na makaburi yatakapofukuliwa.

Na makaburi yatakapofukuliwa.

عَلِمَتۡ نَفۡسٞ مَّا قَدَّمَتۡ وَأَخَّرَتۡ

Hapo kila nafsi itajua ilichotanguliza, na ilichobakisha nyuma.

Hapo kila nafsi itajua ilichotanguliza, na ilichobakisha nyuma.

يَٰٓأَيُّهَا ٱلۡإِنسَٰنُ مَا غَرَّكَ بِرَبِّكَ ٱلۡكَرِيمِ

Ewe mwanadamu! Nini kilichokudanganya ukamwacha Mola wako Mlezi Mtukufu?

Ewe mwanadamu! Nini kilichokudanganya ukamwacha Mola wako Mlezi Mtukufu?

ٱلَّذِي خَلَقَكَ فَسَوَّىٰكَ فَعَدَلَكَ

Aliyekuumba, akakuweka sawa, akakunyoosha.

Aliyekuumba, akakuweka sawa, akakunyoosha.

فِيٓ أَيِّ صُورَةٖ مَّا شَآءَ رَكَّبَكَ

Katika sura yoyote aliyoipenda akakujenga.

Katika sura yoyote aliyoipenda akakujenga.

كَلَّا بَلۡ تُكَذِّبُونَ بِٱلدِّينِ

Sivyo hivyo! Bali nyinyi mnaikanusha Siku ya Malipo.

Sivyo hivyo! Bali nyinyi mnaikanusha Siku ya Malipo.

وَإِنَّ عَلَيۡكُمۡ لَحَٰفِظِينَ

Na hakika bila ya shaka wapo walinzi juu yenu.

Na hakika bila ya shaka wapo walinzi juu yenu.

كِرَامٗا كَٰتِبِينَ

Waandishi wenye heshima.

Waandishi wenye heshima.

يَعۡلَمُونَ مَا تَفۡعَلُونَ

Wanayajua mnayoyatenda.

Wanayajua mnayoyatenda.

إِنَّ ٱلۡأَبۡرَارَ لَفِي نَعِيمٖ

Hakika wema bila ya shaka watakuwa katika neema.

Hakika wema bila ya shaka watakuwa katika neema.

وَإِنَّ ٱلۡفُجَّارَ لَفِي جَحِيمٖ

Na hakika waovu bila ya shaka watakuwa Motoni.

Na hakika waovu bila ya shaka watakuwa Motoni.

يَصۡلَوۡنَهَا يَوۡمَ ٱلدِّينِ

Wataingia humo Siku ya Malipo.

Wataingia humo Siku ya Malipo.

وَمَا هُمۡ عَنۡهَا بِغَآئِبِينَ

Na hawatoacha kuwamo humo.

Na hawatoacha kuwamo humo.

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلدِّينِ

Na nini kitakachokujulisha Siku ya Malipo ni siku gani?

Na nini kitakachokujulisha Siku ya Malipo ni siku gani?

ثُمَّ مَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلدِّينِ

Tena nini kitakachokujulisha Siku ya Malipo ni siku gani?

Tena nini kitakachokujulisha Siku ya Malipo ni siku gani?

يَوۡمَ لَا تَمۡلِكُ نَفۡسٞ لِّنَفۡسٖ شَيۡـٔٗاۖ وَٱلۡأَمۡرُ يَوۡمَئِذٖ لِّلَّهِ

Siku ambayo nafsi haitakuwa na mamlaka yoyote juu ya nafsi nyingine; na amri yote siku hiyo ni ya Mwenyezi Mungu tu.

Siku ambayo nafsi haitakuwa na mamlaka yoyote juu ya nafsi nyingine; na amri yote siku hiyo ni ya Mwenyezi Mungu tu.
Footer Include