Header Include

Swahili translation - Rowad Translation Center

translated by Rowwad Translation Center, in cooperation with the Islamic Propagation Office in Rabwah and the Association for Serving Islamic Content in Languages.

QR Code https://quran.islamcontent.com/hr/swahili_rwwad

سَأَلَ سَآئِلُۢ بِعَذَابٖ وَاقِعٖ

Muulizaji aliuliza juu ya adhabu itakayotokea.

Muulizaji aliuliza juu ya adhabu itakayotokea.

لِّلۡكَٰفِرِينَ لَيۡسَ لَهُۥ دَافِعٞ

Kwa makafiri - ambayo hapana awezaye kuizuia.

Kwa makafiri - ambayo hapana awezaye kuizuia.

مِّنَ ٱللَّهِ ذِي ٱلۡمَعَارِجِ

Kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mwenye mbingu za daraja.

Kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mwenye mbingu za daraja.

تَعۡرُجُ ٱلۡمَلَٰٓئِكَةُ وَٱلرُّوحُ إِلَيۡهِ فِي يَوۡمٖ كَانَ مِقۡدَارُهُۥ خَمۡسِينَ أَلۡفَ سَنَةٖ

Malaika na Roho hupanda kwenda kwake katika siku ambayo kiasi chake ni miaka hamsini elfu!

Malaika na Roho hupanda kwenda kwake katika siku ambayo kiasi chake ni miaka hamsini elfu!

فَٱصۡبِرۡ صَبۡرٗا جَمِيلًا

Basi subiri kwa subira njema.

Basi subiri kwa subira njema.

إِنَّهُمۡ يَرَوۡنَهُۥ بَعِيدٗا

Hakika wao wanaiona iko mbali.

Hakika wao wanaiona iko mbali.

وَنَرَىٰهُ قَرِيبٗا

Na Sisi tunaiona iko karibu.

Na Sisi tunaiona iko karibu.

يَوۡمَ تَكُونُ ٱلسَّمَآءُ كَٱلۡمُهۡلِ

Siku ambayo mbingu zitakapokuwa kama madini iliyoyeyushwa.

Siku ambayo mbingu zitakapokuwa kama madini iliyoyeyushwa.

وَتَكُونُ ٱلۡجِبَالُ كَٱلۡعِهۡنِ

Na milima itakuwa kama sufi.

Na milima itakuwa kama sufi.

وَلَا يَسۡـَٔلُ حَمِيمٌ حَمِيمٗا

Wala jamaa hatamuuliza jamaa yake.

Wala jamaa hatamuuliza jamaa yake.

يُبَصَّرُونَهُمۡۚ يَوَدُّ ٱلۡمُجۡرِمُ لَوۡ يَفۡتَدِي مِنۡ عَذَابِ يَوۡمِئِذِۭ بِبَنِيهِ

Ijapokuwa wataonyeshwa waonane. Atatamani mkosefu lau ajikomboe na adhabu ya siku hiyo kwa kuwatoa fidia wanawe.

Ijapokuwa wataonyeshwa waonane. Atatamani mkosefu lau ajikomboe na adhabu ya siku hiyo kwa kuwatoa fidia wanawe.

وَصَٰحِبَتِهِۦ وَأَخِيهِ

Na mkewe, na nduguye.

Na mkewe, na nduguye.

وَفَصِيلَتِهِ ٱلَّتِي تُـٔۡوِيهِ

Na jamaa zake waliokuwa wakimkimu,

Na jamaa zake waliokuwa wakimkimu,

وَمَن فِي ٱلۡأَرۡضِ جَمِيعٗا ثُمَّ يُنجِيهِ

Na wote waliomo duniani, kisha aokoke yeye.

Na wote waliomo duniani, kisha aokoke yeye.

كَلَّآۖ إِنَّهَا لَظَىٰ

La, hasha! Kwa hakika huo ni Moto mkali kabisa,

La, hasha! Kwa hakika huo ni Moto mkali kabisa,

نَزَّاعَةٗ لِّلشَّوَىٰ

Unaobambua ngozi ya kichwa!

Unaobambua ngozi ya kichwa!

تَدۡعُواْ مَنۡ أَدۡبَرَ وَتَوَلَّىٰ

Utamwita kila aliyegeuza mgongo na akageuka.

Utamwita kila aliyegeuza mgongo na akageuka.

وَجَمَعَ فَأَوۡعَىٰٓ

Na akakusanya mali, kisha akayahifadhi.

Na akakusanya mali, kisha akayahifadhi.

۞ إِنَّ ٱلۡإِنسَٰنَ خُلِقَ هَلُوعًا

Hakika mtu ameumbwa na papara.

Hakika mtu ameumbwa na papara.

إِذَا مَسَّهُ ٱلشَّرُّ جَزُوعٗا

Inapomgusa shari hupapatika.

Inapomgusa shari hupapatika.

وَإِذَا مَسَّهُ ٱلۡخَيۡرُ مَنُوعًا

Na inapomgusa kheri huizuilia.

Na inapomgusa kheri huizuilia.

إِلَّا ٱلۡمُصَلِّينَ

Isipokuwa wanaosali.

Isipokuwa wanaosali.

ٱلَّذِينَ هُمۡ عَلَىٰ صَلَاتِهِمۡ دَآئِمُونَ

Ambao wanadumisha Sala zao.

Ambao wanadumisha Sala zao.

وَٱلَّذِينَ فِيٓ أَمۡوَٰلِهِمۡ حَقّٞ مَّعۡلُومٞ

Na ambao katika mali yao iko haki maalumu.

Na ambao katika mali yao iko haki maalumu.

لِّلسَّآئِلِ وَٱلۡمَحۡرُومِ

Kwa mwenye kuomba na anayejizuilia kuomba;

Kwa mwenye kuomba na anayejizuilia kuomba;

وَٱلَّذِينَ يُصَدِّقُونَ بِيَوۡمِ ٱلدِّينِ

Na ambao wanaisadiki Siku ya Malipo.

Na ambao wanaisadiki Siku ya Malipo.

وَٱلَّذِينَ هُم مِّنۡ عَذَابِ رَبِّهِم مُّشۡفِقُونَ

Na ambao wanaiogopa adhabu itokayo kwa Mola wao Mlezi.

Na ambao wanaiogopa adhabu itokayo kwa Mola wao Mlezi.

إِنَّ عَذَابَ رَبِّهِمۡ غَيۡرُ مَأۡمُونٖ

Hakika adhabu ya Mola wao Mlezi si ya kuwa na amani nayo.

Hakika adhabu ya Mola wao Mlezi si ya kuwa na amani nayo.

وَٱلَّذِينَ هُمۡ لِفُرُوجِهِمۡ حَٰفِظُونَ

Na ambao wanahifadhi tupu zao.

Na ambao wanahifadhi tupu zao.

إِلَّا عَلَىٰٓ أَزۡوَٰجِهِمۡ أَوۡ مَا مَلَكَتۡ أَيۡمَٰنُهُمۡ فَإِنَّهُمۡ غَيۡرُ مَلُومِينَ

Isipokuwa kwa wake zao, au iliyowamiliki mikono yao ya kuume, basi hao hawalaumiwi.

Isipokuwa kwa wake zao, au iliyowamiliki mikono yao ya kuume, basi hao hawalaumiwi.

فَمَنِ ٱبۡتَغَىٰ وَرَآءَ ذَٰلِكَ فَأُوْلَٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡعَادُونَ

Lakini wanaotaka kinyume cha haya, basi hao ndio wanaoruka mipaka.

Lakini wanaotaka kinyume cha haya, basi hao ndio wanaoruka mipaka.

وَٱلَّذِينَ هُمۡ لِأَمَٰنَٰتِهِمۡ وَعَهۡدِهِمۡ رَٰعُونَ

Na ambao wanazichunga amana zao na ahadi zao,

Na ambao wanazichunga amana zao na ahadi zao,

وَٱلَّذِينَ هُم بِشَهَٰدَٰتِهِمۡ قَآئِمُونَ

Na ambao wanasimama imara katika ushahidi wao,

Na ambao wanasimama imara katika ushahidi wao,

وَٱلَّذِينَ هُمۡ عَلَىٰ صَلَاتِهِمۡ يُحَافِظُونَ

Na ambao wanazihifadhi Sala zao.

Na ambao wanazihifadhi Sala zao.

أُوْلَٰٓئِكَ فِي جَنَّٰتٖ مُّكۡرَمُونَ

Hao ndio watakaoheshimiwa katika Bustani ya mbinguni.

Hao ndio watakaoheshimiwa katika Bustani ya mbinguni.

فَمَالِ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ قِبَلَكَ مُهۡطِعِينَ

Wana nini wale waliokufuru wanakutumbulia macho tu?

Wana nini wale waliokufuru wanakutumbulia macho tu?

عَنِ ٱلۡيَمِينِ وَعَنِ ٱلشِّمَالِ عِزِينَ

Makundi kwa makundi upande wa kulia na upande wa kushoto!

Makundi kwa makundi upande wa kulia na upande wa kushoto!

أَيَطۡمَعُ كُلُّ ٱمۡرِيٕٖ مِّنۡهُمۡ أَن يُدۡخَلَ جَنَّةَ نَعِيمٖ

Kwani kila mmoja wao anatumai kuingizwa katika Bustani ya mbinguni ya neema?

Kwani kila mmoja wao anatumai kuingizwa katika Bustani ya mbinguni ya neema?

كَلَّآۖ إِنَّا خَلَقۡنَٰهُم مِّمَّا يَعۡلَمُونَ

La, hasha! Hakika Sisi tumewaumba kutokana na wanachokijua.

La, hasha! Hakika Sisi tumewaumba kutokana na wanachokijua.

فَلَآ أُقۡسِمُ بِرَبِّ ٱلۡمَشَٰرِقِ وَٱلۡمَغَٰرِبِ إِنَّا لَقَٰدِرُونَ

Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mashariki zote na magharibi zote kwamba Sisi tunaweza.

Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mashariki zote na magharibi zote kwamba Sisi tunaweza.

عَلَىٰٓ أَن نُّبَدِّلَ خَيۡرٗا مِّنۡهُمۡ وَمَا نَحۡنُ بِمَسۡبُوقِينَ

Kuwabadili kwa walio bora kuliko wao; na Sisi hatushindwi.

Kuwabadili kwa walio bora kuliko wao; na Sisi hatushindwi.

فَذَرۡهُمۡ يَخُوضُواْ وَيَلۡعَبُواْ حَتَّىٰ يُلَٰقُواْ يَوۡمَهُمُ ٱلَّذِي يُوعَدُونَ

Basi waache wapige porojo na wacheze, mpaka wakutane na siku yao wanayoahidiwa.

Basi waache wapige porojo na wacheze, mpaka wakutane na siku yao wanayoahidiwa.

يَوۡمَ يَخۡرُجُونَ مِنَ ٱلۡأَجۡدَاثِ سِرَاعٗا كَأَنَّهُمۡ إِلَىٰ نُصُبٖ يُوفِضُونَ

Siku watakapotoka makaburini kwa upesi kama kwamba wanakimbilia mfundo.

Siku watakapotoka makaburini kwa upesi kama kwamba wanakimbilia mfundo.

خَٰشِعَةً أَبۡصَٰرُهُمۡ تَرۡهَقُهُمۡ ذِلَّةٞۚ ذَٰلِكَ ٱلۡيَوۡمُ ٱلَّذِي كَانُواْ يُوعَدُونَ

Macho yao yatainama, fedheha itawafunika. Hiyo ndiyo Siku waliyokuwa wakiahidiwa.

Macho yao yatainama, fedheha itawafunika. Hiyo ndiyo Siku waliyokuwa wakiahidiwa.
Footer Include