Swahili translation - Rowad Translation Center
translated by Rowwad Translation Center, in cooperation with the Islamic Propagation Office in Rabwah and the Association for Serving Islamic Content in Languages.
عَبَسَ وَتَوَلَّىٰٓ
Alikunja kipaji na akageuka mbali.
أَن جَآءَهُ ٱلۡأَعۡمَىٰ
Kwa sababu alimjia kipofu!
وَمَا يُدۡرِيكَ لَعَلَّهُۥ يَزَّكَّىٰٓ
Na nini kitakachokujulisha pengine yeye atatakasika?
أَوۡ يَذَّكَّرُ فَتَنفَعَهُ ٱلذِّكۡرَىٰٓ
Au atawaidhika, na mawaidha yamfae?
أَمَّا مَنِ ٱسۡتَغۡنَىٰ
Ama ajionaye hana haja,
فَأَنتَ لَهُۥ تَصَدَّىٰ
Wewe ndiyo unamshughulikia?
وَمَا عَلَيۡكَ أَلَّا يَزَّكَّىٰ
Na si juu yako kama hakutakasika.
وَأَمَّا مَن جَآءَكَ يَسۡعَىٰ
Ama anayekujia kwa juhudi.
وَهُوَ يَخۡشَىٰ
Naye anaogopa,
فَأَنتَ عَنۡهُ تَلَهَّىٰ
Ndiyo wewe unampuuza?
كَلَّآ إِنَّهَا تَذۡكِرَةٞ
Sivyo hivyo! Huku ni kukumbushana.
فَمَن شَآءَ ذَكَرَهُۥ
Basi anayependa akumbuke.
فِي صُحُفٖ مُّكَرَّمَةٖ
Yamo katika kurasa zilizoheshimiwa.
مَّرۡفُوعَةٖ مُّطَهَّرَةِۭ
Zilizoinuliwa, zilizotakaswa.
بِأَيۡدِي سَفَرَةٖ
Zimo mikononi mwa Malaika waandishi,
كِرَامِۭ بَرَرَةٖ
Watukufu, wema.
قُتِلَ ٱلۡإِنسَٰنُ مَآ أَكۡفَرَهُۥ
Ameangamia mwanadamu! Nini kinachomkufurisha?
مِنۡ أَيِّ شَيۡءٍ خَلَقَهُۥ
Kwa kitu gani amemuumba?
مِن نُّطۡفَةٍ خَلَقَهُۥ فَقَدَّرَهُۥ
Kwa tone la manii, amemuumba na akamkadiria.
ثُمَّ ٱلسَّبِيلَ يَسَّرَهُۥ
Kisha akamsahilishia njia.
ثُمَّ أَمَاتَهُۥ فَأَقۡبَرَهُۥ
Kisha akamfisha, akamtia kaburini.
ثُمَّ إِذَا شَآءَ أَنشَرَهُۥ
Kisha apendapo atamfufua.
كَلَّا لَمَّا يَقۡضِ مَآ أَمَرَهُۥ
La! Hajamaliza aliyomuamuru.
فَلۡيَنظُرِ ٱلۡإِنسَٰنُ إِلَىٰ طَعَامِهِۦٓ
Hebu mtu na atazame chakula chake.
أَنَّا صَبَبۡنَا ٱلۡمَآءَ صَبّٗا
Hakika Sisi tumemimina maji kwa nguvu.
ثُمَّ شَقَقۡنَا ٱلۡأَرۡضَ شَقّٗا
Tena tukaipasua pasua ardhi kwa nguvu.
فَأَنۢبَتۡنَا فِيهَا حَبّٗا
Kisha tukaotesha humo nafaka.
وَعِنَبٗا وَقَضۡبٗا
Na zabibu, na mimea ya majani.
وَزَيۡتُونٗا وَنَخۡلٗا
Na mizaituni, na mitende.
وَحَدَآئِقَ غُلۡبٗا
Na bustani zenye miti iliyosongana barabara.
وَفَٰكِهَةٗ وَأَبّٗا
Na matunda, na malisho ya wanyama.
مَّتَٰعٗا لَّكُمۡ وَلِأَنۡعَٰمِكُمۡ
Kwa manufaa yenu na mifugo yenu.
فَإِذَا جَآءَتِ ٱلصَّآخَّةُ
Basi utakapokuja Ukelele.
يَوۡمَ يَفِرُّ ٱلۡمَرۡءُ مِنۡ أَخِيهِ
Siku ambayo mtu atamkimbia nduguye.
وَأُمِّهِۦ وَأَبِيهِ
Na mamaye na babaye.
وَصَٰحِبَتِهِۦ وَبَنِيهِ
Na mkewe na wanawe.
لِكُلِّ ٱمۡرِيٕٖ مِّنۡهُمۡ يَوۡمَئِذٖ شَأۡنٞ يُغۡنِيهِ
Kila mtu miongoni mwao siku hiyo atakuwa na lake la kumtosha.
وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ مُّسۡفِرَةٞ
Siku hiyo ziko nyuso zitakazonawiri.
ضَاحِكَةٞ مُّسۡتَبۡشِرَةٞ
Zitacheka, zitachangamka.
وَوُجُوهٞ يَوۡمَئِذٍ عَلَيۡهَا غَبَرَةٞ
Na nyuso siku hiyo zitakuwa na mavumbi.
تَرۡهَقُهَا قَتَرَةٌ
Giza totoro litazifunika.
أُوْلَٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡكَفَرَةُ ٱلۡفَجَرَةُ
Hao ndio makafiri watenda maovu.
مشاركة عبر