Header Include

Swahili translation - Ali Muhsen Al-Berwani

Translated by Ali Muhsen Al-Berwani

QR Code https://quran.islamcontent.com/luy/swahili_barawani

تَبَّتۡ يَدَآ أَبِي لَهَبٖ وَتَبَّ

Imeangamia mikono ya Abu Lahab, na yeye pia ameangamia. [1]

[1] Imeteketea mikono ya Abu Lahab iliyo kuwa ikiwaudhi Waislamu, na yeye mwenyewe amehiliki pia.
Imeangamia mikono ya Abu Lahab, na yeye pia ameangamia. [1]

مَآ أَغۡنَىٰ عَنۡهُ مَالُهُۥ وَمَا كَسَبَ

Hayatamfaa mali yake, wala alivyo vichuma. [2]

[2] Hayatolindwa na adhabu ya Mwenyezi Mungu mali yake aliyo kuwa nayo, wala cheo chake alicho kichuma.
Hayatamfaa mali yake, wala alivyo vichuma. [2]

سَيَصۡلَىٰ نَارٗا ذَاتَ لَهَبٖ

Atauingia Moto wenye mwako. [3]

[3] Ataingia katika Moto unao waka, aungue.
Atauingia Moto wenye mwako. [3]

وَٱمۡرَأَتُهُۥ حَمَّالَةَ ٱلۡحَطَبِ

Na mkewe, mchukuzi wa kuni, [4]

[4] Na ataingia pia kwenye Moto mkewe huyo aliye kuwa akibeba masengenyo baina ya watu, kama alivyo ingia yeye (mumewe).
Na mkewe, mchukuzi wa kuni, [4]

فِي جِيدِهَا حَبۡلٞ مِّن مَّسَدِۭ

Shingoni mwake iko kamba iliyo sokotwa. [5]

[5] Juu ya shingo yake itakuwa kamba ya mtende ya kumtesa.
Shingoni mwake iko kamba iliyo sokotwa. [5]
Footer Include