Swahili translation - Ali Muhsen Al-Berwani
Translated by Ali Muhsen Al-Berwani
وَٱلۡعَٰدِيَٰتِ ضَبۡحٗا
Naapa kwa farasi wendao mbio wakipumua, [1]
فَٱلۡمُورِيَٰتِ قَدۡحٗا
Na wakitoa moto kwa kupiga kwato zao chini, [2]
فَٱلۡمُغِيرَٰتِ صُبۡحٗا
Wakishambulia wakati wa asubuhi, [3]
فَأَثَرۡنَ بِهِۦ نَقۡعٗا
Huku wakitimua vumbi, [4]
فَوَسَطۡنَ بِهِۦ جَمۡعًا
Na wakijitoma kati ya kundi, [5]
إِنَّ ٱلۡإِنسَٰنَ لِرَبِّهِۦ لَكَنُودٞ
Hakika mwanaadamu ni mtovu wa fadhila kwa Mola wake Mlezi! [6]
وَإِنَّهُۥ عَلَىٰ ذَٰلِكَ لَشَهِيدٞ
Na hakika yeye mwenyewe bila ya shaka ni shahidi wa hayo! [7]
وَإِنَّهُۥ لِحُبِّ ٱلۡخَيۡرِ لَشَدِيدٌ
Naye hakika bila ya shaka ana nguvu za kupenda mali! [8]
۞ أَفَلَا يَعۡلَمُ إِذَا بُعۡثِرَ مَا فِي ٱلۡقُبُورِ
Kwani hajui watakapo fufuliwa waliomo makaburini? [9]
وَحُصِّلَ مَا فِي ٱلصُّدُورِ
Na yakakusanywa yaliomo vifuani? [10]
إِنَّ رَبَّهُم بِهِمۡ يَوۡمَئِذٖ لَّخَبِيرُۢ
Kuwa hakika Mola wao Mlezi siku hiyo bila ya shaka atakuwa na khabari zao wote! [11]
مشاركة عبر