Header Include

الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني

ترجمها علي محسن البرواني.

QR Code https://quran.islamcontent.com/31/swahili_barawani

أَلَمۡ تَرَ كَيۡفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِأَصۡحَٰبِ ٱلۡفِيلِ

Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo watenda wale wenye tembo? [1]

[1] Hakika, ewe Muhammad, unajua kwa ujuzi usio ingiliwa na shaka yoyote, alivyo fanya Mola wako Mlezi kuwafanyia wale watu wenye tembo (ndovu), wakataka kuishambulia Nyumba takatifu ya Al-Kaaba.
Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo watenda wale wenye tembo? [1]

أَلَمۡ يَجۡعَلۡ كَيۡدَهُمۡ فِي تَضۡلِيلٖ

Kwani hakujaalia vitimbi vyao kuharibika? [2]

[2] Unajua ya kwamba hakika Mwenyezi Mungu amejaalia juhudi yao kutaka kuibomoa Al-Kaaba ivize na ipotelee mbali. Juhudi yao ikapeperuka, na wao wasipate makusudio yao.
Kwani hakujaalia vitimbi vyao kuharibika? [2]

وَأَرۡسَلَ عَلَيۡهِمۡ طَيۡرًا أَبَابِيلَ

Na akawapelekea ndege makundi kwa makundi, [3]

[3] Na Mwenyezi Mungu aliwasalitisha na majeshi ya ndege yaliyo watokea makundi kwa makundi yakifuatana, na yakawazunguka kila upande.
Na akawapelekea ndege makundi kwa makundi, [3]

تَرۡمِيهِم بِحِجَارَةٖ مِّن سِجِّيلٖ

Wakiwatupia mawe ya udongo wa Motoni, [4]

[4] Wakiwatupia mawe kutoka Jahannamu.
Wakiwatupia mawe ya udongo wa Motoni, [4]

فَجَعَلَهُمۡ كَعَصۡفٖ مَّأۡكُولِۭ

Akawafanya kama majani yaliyo liwa! [5]

[5] Akawafanya kama majani ya mimea yaliyo sibiwa yakatilifu.
Akawafanya kama majani yaliyo liwa! [5]
Footer Include