الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني
ترجمها علي محسن البرواني.
أَلَمۡ تَرَ كَيۡفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِأَصۡحَٰبِ ٱلۡفِيلِ
Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo watenda wale wenye tembo? [1]
[1] Hakika, ewe Muhammad, unajua kwa ujuzi usio ingiliwa na shaka yoyote, alivyo fanya Mola wako Mlezi kuwafanyia wale watu wenye tembo (ndovu), wakataka kuishambulia Nyumba takatifu ya Al-Kaaba.
Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo watenda wale wenye tembo? [1]
أَلَمۡ يَجۡعَلۡ كَيۡدَهُمۡ فِي تَضۡلِيلٖ
Kwani hakujaalia vitimbi vyao kuharibika? [2]
[2] Unajua ya kwamba hakika Mwenyezi Mungu amejaalia juhudi yao kutaka kuibomoa Al-Kaaba ivize na ipotelee mbali. Juhudi yao ikapeperuka, na wao wasipate makusudio yao.
Kwani hakujaalia vitimbi vyao kuharibika? [2]
وَأَرۡسَلَ عَلَيۡهِمۡ طَيۡرًا أَبَابِيلَ
Na akawapelekea ndege makundi kwa makundi, [3]
[3] Na Mwenyezi Mungu aliwasalitisha na majeshi ya ndege yaliyo watokea makundi kwa makundi yakifuatana, na yakawazunguka kila upande.
Na akawapelekea ndege makundi kwa makundi, [3]
تَرۡمِيهِم بِحِجَارَةٖ مِّن سِجِّيلٖ
Wakiwatupia mawe ya udongo wa Motoni, [4]
[4] Wakiwatupia mawe kutoka Jahannamu.
Wakiwatupia mawe ya udongo wa Motoni, [4]
فَجَعَلَهُمۡ كَعَصۡفٖ مَّأۡكُولِۭ
Akawafanya kama majani yaliyo liwa! [5]
[5] Akawafanya kama majani ya mimea yaliyo sibiwa yakatilifu.
Akawafanya kama majani yaliyo liwa! [5]
مشاركة عبر