الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني
ترجمها علي محسن البرواني.
هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلۡغَٰشِيَةِ
Je! Imekufikia khabari ya msiba wa kufudikiza? [1]
وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٍ خَٰشِعَةٌ
Siku hiyo nyuso zitainama! [2]
عَامِلَةٞ نَّاصِبَةٞ
Zikifanya kazi, nazo taabani. [3]
تَصۡلَىٰ نَارًا حَامِيَةٗ
Ziingie katika Moto unao waka . [4]
تُسۡقَىٰ مِنۡ عَيۡنٍ ءَانِيَةٖ
Zikinyweshwa kutoka chemchem inayo chemka. [5]
لَّيۡسَ لَهُمۡ طَعَامٌ إِلَّا مِن ضَرِيعٖ
Hawatakuwa na chakula isipo kuwa kichungu chenye miba. [6]
لَّا يُسۡمِنُ وَلَا يُغۡنِي مِن جُوعٖ
Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa. [7]
وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ نَّاعِمَةٞ
Siku hiyo nyuso nyengine zitakuwa kunjufu. [8]
لِّسَعۡيِهَا رَاضِيَةٞ
Zitakuwa radhi kwa juhudi yao! [9]
فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٖ
Katika Bustani ya juu. [10]
لَّا تَسۡمَعُ فِيهَا لَٰغِيَةٗ
Hawatasikia humo upuuzi.Humo imo chemchem inayo miminika. [11]
فِيهَا عَيۡنٞ جَارِيَةٞ
Humo imo chemchem inayo miminika. [12]
فِيهَا سُرُرٞ مَّرۡفُوعَةٞ
Humo vimo viti vilivyo nyanyuliwa, [13]
وَأَكۡوَابٞ مَّوۡضُوعَةٞ
Na bilauri zilizo pangwa, [14]
وَنَمَارِقُ مَصۡفُوفَةٞ
Na matakia safu safu, [15]
وَزَرَابِيُّ مَبۡثُوثَةٌ
Na mazulia yaliyo tandikwa. [16]
أَفَلَا يَنظُرُونَ إِلَى ٱلۡإِبِلِ كَيۡفَ خُلِقَتۡ
Je! Hawamtazami ngamia jinsi alivyo umbwa? [17]
وَإِلَى ٱلسَّمَآءِ كَيۡفَ رُفِعَتۡ
Na mbingu jinsi ilivyo inuliwa? [18]
وَإِلَى ٱلۡجِبَالِ كَيۡفَ نُصِبَتۡ
Na milima jinsi ilivyo thibitishwa? [19]
وَإِلَى ٱلۡأَرۡضِ كَيۡفَ سُطِحَتۡ
Na ardhi jinsi ilivyo tandazwa? [20]
فَذَكِّرۡ إِنَّمَآ أَنتَ مُذَكِّرٞ
Basi kumbusha! Hakika wewe ni Mkumbushaji. [21]
لَّسۡتَ عَلَيۡهِم بِمُصَيۡطِرٍ
Wewe si mwenye kuwatawalia. [22]
إِلَّا مَن تَوَلَّىٰ وَكَفَرَ
Lakini anaye rudi nyuma na kukataa, [23]
فَيُعَذِّبُهُ ٱللَّهُ ٱلۡعَذَابَ ٱلۡأَكۡبَرَ
Basi Mwenyezi Mungu atamuadhibu kwa adhabu iliyo kubwa kabisa! [24]
إِنَّ إِلَيۡنَآ إِيَابَهُمۡ
Hakika ni kwetu Sisi ndio marejeo yao. [25]
ثُمَّ إِنَّ عَلَيۡنَا حِسَابَهُم
Kisha hakika ni juu yetu Sisi hisabu yao! [26]
مشاركة عبر