Header Include

الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني

ترجمها علي محسن البرواني.

QR Code https://quran.islamcontent.com/51/swahili_barawani

وَٱلضُّحَىٰ

Naapa kwa mchana! [1]

[1] Naapa kwa wakati wa kupanda juu jua, na ni wakati wa uchangamfu na kazi!
Naapa kwa mchana! [1]

وَٱلَّيۡلِ إِذَا سَجَىٰ

Na kwa usiku unapo tanda! [2]

[2] Na naapa kwa usiku unapo tulia na ukatanda kote kiza chake!
Na kwa usiku unapo tanda! [2]

مَا وَدَّعَكَ رَبُّكَ وَمَا قَلَىٰ

Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe. [3]

[3] Ewe Muhammad! Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukuchukia.
Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe. [3]

وَلَلۡأٓخِرَةُ خَيۡرٞ لَّكَ مِنَ ٱلۡأُولَىٰ

Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko ulio tangulia. [4]

[4] Na matokeo ya mambo yako, mwisho wake, yatakuwa bora kuliko mwanzo wake.
Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko ulio tangulia. [4]

وَلَسَوۡفَ يُعۡطِيكَ رَبُّكَ فَتَرۡضَىٰٓ

Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike. [5]

[5] Na ninaapa kuwa bila ya shaka hapo Mola wako Mlezi atakupa kheri za duniani na Akhera hata utaridhia.
Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike. [5]

أَلَمۡ يَجِدۡكَ يَتِيمٗا فَـَٔاوَىٰ

Kwani hakukukuta yatima akakupa makaazi? [6]

[6] Kwani hakukukuta wewe yatima unahitaji wa kukutunza naye akakupa makaazi ya kukuhifadhi kwa mwenye kukuangalia vyema kwa mambo yako?
Kwani hakukukuta yatima akakupa makaazi? [6]

وَوَجَدَكَ ضَآلّٗا فَهَدَىٰ

Na akakukuta umepotea akakuongoa? [7]

[7] Na akakuona umebabaika hukukinaika na itikadi zilizo kuzunguka, naye akakuongoa kwenye Njia ya Haki?
Na akakukuta umepotea akakuongoa? [7]

وَوَجَدَكَ عَآئِلٗا فَأَغۡنَىٰ

Akakukuta mhitaji akakutosheleza? [8]

[8] Akakukuta fakiri wa mali naye akakutajirisha kwa kukupa riziki?
Akakukuta mhitaji akakutosheleza? [8]

فَأَمَّا ٱلۡيَتِيمَ فَلَا تَقۡهَرۡ

Basi yatima usimwonee! [9]

[9] Ikiwa hii ndiyo hali yetu nawe, basi yatima usimdhili,
Basi yatima usimwonee! [9]

وَأَمَّا ٱلسَّآئِلَ فَلَا تَنۡهَرۡ

Na anaye omba au kuuliza usimkaripie! [10]

[10] Na mwenye kuomba au kuuliza usimjibu kwa ukavu,
Na anaye omba au kuuliza usimkaripie! [10]

وَأَمَّا بِنِعۡمَةِ رَبِّكَ فَحَدِّثۡ

Na neema za Mola wako Mlezi zisimlie. [11]

[11] Na ama neema za Mola wako Mlezi zitangaze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kuwa ndio kudhihirisha neema.
Na neema za Mola wako Mlezi zisimlie. [11]
Footer Include