الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني
ترجمها علي محسن البرواني.
وَيۡلٞ لِّكُلِّ هُمَزَةٖ لُّمَزَةٍ
Ole wake kila safihi, msengenyaji! [1]
[1] Atapata adhabu kali na maangamio huyo ambaye mtindo wake ni kuwafedhehi watu kwa kauli au kwa ishara, au kuwasengenya kuwavunjia hishima zao.
Ole wake kila safihi, msengenyaji! [1]
ٱلَّذِي جَمَعَ مَالٗا وَعَدَّدَهُۥ
Aliye kusanya mali na kuyahisabu. [2]
[2] Ambaye amekusanya chungu ya mali na akawa kazi yake kuyahisabu tu, kwa kuona ladha huko kuhisabu.
Aliye kusanya mali na kuyahisabu. [2]
يَحۡسَبُ أَنَّ مَالَهُۥٓ أَخۡلَدَهُۥ
Anadhani ya kuwa mali yake yatambakisha milele! [3]
[3] Anadhani huyo kuwa mali yake yatamweka milele duniani, na yatamkinga na hayo anayo yachukia?
Anadhani ya kuwa mali yake yatambakisha milele! [3]
كَلَّاۖ لَيُنۢبَذَنَّ فِي ٱلۡحُطَمَةِ
Hasha! Atavurumishwa katika H'ut'ama. [4]
[4] Na aache dhana hiyo! Wallahi! Hapana shaka yoyote kwa vitendo vyake viovu hivyo atakuja tumbukizwa katika Moto unao vuruga kila kinacho tupwa humo!
Hasha! Atavurumishwa katika H'ut'ama. [4]
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡحُطَمَةُ
Na nani atakujuvya ni nini H'ut'ama? [5]
[5] Na kitu gani kitacho kujuvya nini ukweli wa Moto huu wa H'ut'ama?
Na nani atakujuvya ni nini H'ut'ama? [5]
نَارُ ٱللَّهِ ٱلۡمُوقَدَةُ
Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa. [6]
[6] Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa kwa amri yake, na daima unawaka!
Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa. [6]
ٱلَّتِي تَطَّلِعُ عَلَى ٱلۡأَفۡـِٔدَةِ
Ambao unapanda nyoyoni. [7]
[7] Ambao unafikilia nyoyoni na kuzizunguka nyoyo.
Ambao unapanda nyoyoni. [7]
إِنَّهَا عَلَيۡهِم مُّؤۡصَدَةٞ
Hakika huo utafungiwa nao [8]
[8] Huo utakuwa umefungwa milango yake, na wao watakuwa wamefungwa humo ndani
Hakika huo utafungiwa nao [8]
فِي عَمَدٖ مُّمَدَّدَةِۭ
Kwenye nguzo zilio nyooshwa. [9]
[9] Kwenye maguzo yaliyo nyooka. Hawawezi kutaharaki, wala kutoka.
Kwenye nguzo zilio nyooshwa. [9]
مشاركة عبر