Header Include

الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني

ترجمها علي محسن البرواني.

QR Code https://quran.islamcontent.com/58/swahili_barawani

وَيۡلٞ لِّكُلِّ هُمَزَةٖ لُّمَزَةٍ

Ole wake kila safihi, msengenyaji! [1]

[1] Atapata adhabu kali na maangamio huyo ambaye mtindo wake ni kuwafedhehi watu kwa kauli au kwa ishara, au kuwasengenya kuwavunjia hishima zao.
Ole wake kila safihi, msengenyaji! [1]

ٱلَّذِي جَمَعَ مَالٗا وَعَدَّدَهُۥ

Aliye kusanya mali na kuyahisabu. [2]

[2] Ambaye amekusanya chungu ya mali na akawa kazi yake kuyahisabu tu, kwa kuona ladha huko kuhisabu.
Aliye kusanya mali na kuyahisabu. [2]

يَحۡسَبُ أَنَّ مَالَهُۥٓ أَخۡلَدَهُۥ

Anadhani ya kuwa mali yake yatambakisha milele! [3]

[3] Anadhani huyo kuwa mali yake yatamweka milele duniani, na yatamkinga na hayo anayo yachukia?
Anadhani ya kuwa mali yake yatambakisha milele! [3]

كَلَّاۖ لَيُنۢبَذَنَّ فِي ٱلۡحُطَمَةِ

Hasha! Atavurumishwa katika H'ut'ama. [4]

[4] Na aache dhana hiyo! Wallahi! Hapana shaka yoyote kwa vitendo vyake viovu hivyo atakuja tumbukizwa katika Moto unao vuruga kila kinacho tupwa humo!
Hasha! Atavurumishwa katika H'ut'ama. [4]

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡحُطَمَةُ

Na nani atakujuvya ni nini H'ut'ama? [5]

[5] Na kitu gani kitacho kujuvya nini ukweli wa Moto huu wa H'ut'ama?
Na nani atakujuvya ni nini H'ut'ama? [5]

نَارُ ٱللَّهِ ٱلۡمُوقَدَةُ

Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa. [6]

[6] Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa kwa amri yake, na daima unawaka!
Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa. [6]

ٱلَّتِي تَطَّلِعُ عَلَى ٱلۡأَفۡـِٔدَةِ

Ambao unapanda nyoyoni. [7]

[7] Ambao unafikilia nyoyoni na kuzizunguka nyoyo.
Ambao unapanda nyoyoni. [7]

إِنَّهَا عَلَيۡهِم مُّؤۡصَدَةٞ

Hakika huo utafungiwa nao [8]

[8] Huo utakuwa umefungwa milango yake, na wao watakuwa wamefungwa humo ndani
Hakika huo utafungiwa nao [8]

فِي عَمَدٖ مُّمَدَّدَةِۭ

Kwenye nguzo zilio nyooshwa. [9]

[9] Kwenye maguzo yaliyo nyooka. Hawawezi kutaharaki, wala kutoka.
Kwenye nguzo zilio nyooshwa. [9]
Footer Include