Header Include

الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني

ترجمها علي محسن البرواني.

QR Code https://quran.islamcontent.com/64/swahili_barawani

أَرَءَيۡتَ ٱلَّذِي يُكَذِّبُ بِٱلدِّينِ

Je! Umemwona anaye kadhibisha Malipo? [1]

[1] Unamjua anaye kanusha malipo na hisabu ya Akhera?
Je! Umemwona anaye kadhibisha Malipo? [1]

فَذَٰلِكَ ٱلَّذِي يَدُعُّ ٱلۡيَتِيمَ

Huyo ndiye anaye msukuma yatima, [2]

[2] Ukitaka kumjua basi ni huyo ambaye anaye msukuma yatima kwa nguvu, na anamtumilia mabavu, na anamdhulumu,
Huyo ndiye anaye msukuma yatima, [2]

وَلَا يَحُضُّ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلۡمِسۡكِينِ

Wala hahimizi kumlisha masikini. [3]

[3] Na wala hahimizi kulishwa masikini.
Wala hahimizi kumlisha masikini. [3]

فَوَيۡلٞ لِّلۡمُصَلِّينَ

Basi, ole wao wanao swali, [4]

[4] Maangamio yatawashukia wanao sali na wakasifika kwa sifa hizi, na wakaghafilika na Swala zao wasinafiike nazo.
Basi, ole wao wanao swali, [4]

ٱلَّذِينَ هُمۡ عَن صَلَاتِهِمۡ سَاهُونَ

Ambao wanapuuza Sala zao; [5]

[5] Maangamio yatawashukia wanao swali na wakasifika kwa sifa hizi, na wakaghafilika na Swala zao wasinafiike nazo.
Ambao wanapuuza Sala zao; [5]

ٱلَّذِينَ هُمۡ يُرَآءُونَ

Ambao wanajionyesha, [6]

[6] Ambao huonyesha kwa watu vitendo vyao, ili wapate cheo katika nyoyo za hao watu, na wasifiwe.
Ambao wanajionyesha, [6]

وَيَمۡنَعُونَ ٱلۡمَاعُونَ

Nao huku wanazuia msaada. [7]

[7] Na huku wanazuia hisani zao na msaada wao kwa watu
Nao huku wanazuia msaada. [7]
Footer Include