الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني
ترجمها علي محسن البرواني.
إِذَا وَقَعَتِ ٱلۡوَاقِعَةُ
Litakapo tukia hilo Tukio . [1]
لَيۡسَ لِوَقۡعَتِهَا كَاذِبَةٌ
Hapana cha kukanusha kutukia kwake. [2]
خَافِضَةٞ رَّافِعَةٌ
Literemshalo linyanyualo! [3]
إِذَا رُجَّتِ ٱلۡأَرۡضُ رَجّٗا
Itakapo tikiswa ardhi kwa mtikiso! [4]
وَبُسَّتِ ٱلۡجِبَالُ بَسّٗا
Na milima itapo sagwasagwa! [5]
فَكَانَتۡ هَبَآءٗ مُّنۢبَثّٗا
Iwe mavumbi yanayo peperushwa! [6]
وَكُنتُمۡ أَزۡوَٰجٗا ثَلَٰثَةٗ
Na nyinyi mtakuwa namna tatu: . [7]
فَأَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ
Basi watakuwepo wa kuliani; je, ni wepi wa kuliani? [8]
وَأَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ
Na wa kushotoni; je, ni wepi wa kushotoni? [9]
وَٱلسَّٰبِقُونَ ٱلسَّٰبِقُونَ
Na wa mbele watakuwa mbele. [10]
أُوْلَٰٓئِكَ ٱلۡمُقَرَّبُونَ
Hao ndio watakao karibishwa [11]
فِي جَنَّٰتِ ٱلنَّعِيمِ
Katika Bustani zenye neema. [12]
ثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأَوَّلِينَ
Fungu kubwa katika wa mwanzo, [13]
وَقَلِيلٞ مِّنَ ٱلۡأٓخِرِينَ
Na wachache katika wa mwisho. [14]
عَلَىٰ سُرُرٖ مَّوۡضُونَةٖ
Watakuwa juu ya viti vya fakhari vilivyo tonewa. [15]
مُّتَّكِـِٔينَ عَلَيۡهَا مُتَقَٰبِلِينَ
Wakiviegemea wakielekeana. [16]
يَطُوفُ عَلَيۡهِمۡ وِلۡدَٰنٞ مُّخَلَّدُونَ
Wakitumikiwa na wavulana wa ujana wa milele, [17]
بِأَكۡوَابٖ وَأَبَارِيقَ وَكَأۡسٖ مِّن مَّعِينٖ
Kwa vikombe na mabirika na bilauri za vinywaji kutoka chemchem safi. [18]
لَّا يُصَدَّعُونَ عَنۡهَا وَلَا يُنزِفُونَ
Hawataumwa kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawatoleweshwa. [19]
وَفَٰكِهَةٖ مِّمَّا يَتَخَيَّرُونَ
Na matunda wayapendayo, [20]
وَلَحۡمِ طَيۡرٖ مِّمَّا يَشۡتَهُونَ
Na nyama za ndege kama wanavyo tamani. [21]
وَحُورٌ عِينٞ
Na Mahurulaini, [22]
كَأَمۡثَٰلِ ٱللُّؤۡلُوِٕ ٱلۡمَكۡنُونِ
Walio kama mfano wa lulu zilio hifadhiwa. [23]
جَزَآءَۢ بِمَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ
Ni malipo kwa waliyo kuwa wakiyatenda. [24]
لَا يَسۡمَعُونَ فِيهَا لَغۡوٗا وَلَا تَأۡثِيمًا
Humo hawatasikia porojo wala maneno ya dhambi, [25]
إِلَّا قِيلٗا سَلَٰمٗا سَلَٰمٗا
Isipo kuwa maneno ya Salama, Salama. [26]
وَأَصۡحَٰبُ ٱلۡيَمِينِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡيَمِينِ
Na wale wa mkono wa kulia, ni yepi yatakuwa ya wa kuliani? [27]
فِي سِدۡرٖ مَّخۡضُودٖ
Katika mikunazi isiyo na miba, [28]
وَطَلۡحٖ مَّنضُودٖ
Na migomba iliyo pangiliwa, [29]
وَظِلّٖ مَّمۡدُودٖ
Na kivuli kilicho tanda, [30]
وَمَآءٖ مَّسۡكُوبٖ
Na maji yanayo miminika, [31]
وَفَٰكِهَةٖ كَثِيرَةٖ
Na matunda mengi, [32]
لَّا مَقۡطُوعَةٖ وَلَا مَمۡنُوعَةٖ
Hayatindikii wala hayakatazwi, [33]
وَفُرُشٖ مَّرۡفُوعَةٍ
Na matandiko yaliyo nyanyuliwa. [34]
إِنَّآ أَنشَأۡنَٰهُنَّ إِنشَآءٗ
Hakika Sisi tutawaumba (Mahurulaini) upya, [35]
فَجَعَلۡنَٰهُنَّ أَبۡكَارًا
Na tutawafanya vijana, [36]
عُرُبًا أَتۡرَابٗا
Wanapendana na waume zao, hirimu moja. [37]
لِّأَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ
Kwa ajili ya watu wa kuliani. [38]
ثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأَوَّلِينَ
Fungu kubwa katika wa mwanzo, [39]
وَثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأٓخِرِينَ
Na fungu kubwa katika wa mwisho. [40]
وَأَصۡحَٰبُ ٱلشِّمَالِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلشِّمَالِ
Na watu wa kushotoni; je ni yepi ya wa kushotoni? [41]
فِي سَمُومٖ وَحَمِيمٖ
Katika upepo wa moto, na maji yanayo chemka, [42]
وَظِلّٖ مِّن يَحۡمُومٖ
Na kivuli cha moshi mweusi, [43]
لَّا بَارِدٖ وَلَا كَرِيمٍ
Si cha kuburudisha wala kustarehesha. [44]
إِنَّهُمۡ كَانُواْ قَبۡلَ ذَٰلِكَ مُتۡرَفِينَ
Hakika hao walikuwa kabla ya haya wakiishi maisha ya anasa. [45]
وَكَانُواْ يُصِرُّونَ عَلَى ٱلۡحِنثِ ٱلۡعَظِيمِ
Na walikuwa wakishikilia kufanya madhambi makubwa, [46]
وَكَانُواْ يَقُولُونَ أَئِذَا مِتۡنَا وَكُنَّا تُرَابٗا وَعِظَٰمًا أَءِنَّا لَمَبۡعُوثُونَ
Na walikuwa wakisema: Tutakapo kufa na tukawa udongo na mafupa, ati ndio tutafufuliwa? [47]
أَوَءَابَآؤُنَا ٱلۡأَوَّلُونَ
Au baba zetu wa zamani? [48]
قُلۡ إِنَّ ٱلۡأَوَّلِينَ وَٱلۡأٓخِرِينَ
Sema: Hakika wa zamani na wa mwisho [49]
لَمَجۡمُوعُونَ إِلَىٰ مِيقَٰتِ يَوۡمٖ مَّعۡلُومٖ
Bila ya shaka watakusanywa kwa wakati wa siku maalumu. [50]
ثُمَّ إِنَّكُمۡ أَيُّهَا ٱلضَّآلُّونَ ٱلۡمُكَذِّبُونَ
Kisha nyinyi, mlio potea, mnao kanusha, [51]
لَأٓكِلُونَ مِن شَجَرٖ مِّن زَقُّومٖ
Kwa yakini mtakula mti wa Zaqqumu. [52]
فَمَالِـُٔونَ مِنۡهَا ٱلۡبُطُونَ
Na kwa mti huo mtajaza matumbo. [53]
فَشَٰرِبُونَ عَلَيۡهِ مِنَ ٱلۡحَمِيمِ
Na juu yake mtakunywa maji yanayo chemka. [54]
فَشَٰرِبُونَ شُرۡبَ ٱلۡهِيمِ
Tena mtakunywa kama wanavyo kunywa ngamia wenye kiu. [55]
هَٰذَا نُزُلُهُمۡ يَوۡمَ ٱلدِّينِ
Hiyo ndiyo karamu yao Siku ya Malipo. [56]
نَحۡنُ خَلَقۡنَٰكُمۡ فَلَوۡلَا تُصَدِّقُونَ
Sisi tumekuumbeni; basi hamsadiki? [57]
أَفَرَءَيۡتُم مَّا تُمۡنُونَ
Je! Mnaiona mbegu ya uzazi mnayo idondokeza? [58]
ءَأَنتُمۡ تَخۡلُقُونَهُۥٓ أَمۡ نَحۡنُ ٱلۡخَٰلِقُونَ
Je! Mnaiumba nyinyi, au ni Sisi ndio Waumbaji? [59]
نَحۡنُ قَدَّرۡنَا بَيۡنَكُمُ ٱلۡمَوۡتَ وَمَا نَحۡنُ بِمَسۡبُوقِينَ
Sisi tumekuwekeeni mauti; na wala Sisi hatushindwi [60]
عَلَىٰٓ أَن نُّبَدِّلَ أَمۡثَٰلَكُمۡ وَنُنشِئَكُمۡ فِي مَا لَا تَعۡلَمُونَ
Kuwaleta wengine badala yenu na kukuumbeni nyinyi kwa umbo msilo lijua. [61]
وَلَقَدۡ عَلِمۡتُمُ ٱلنَّشۡأَةَ ٱلۡأُولَىٰ فَلَوۡلَا تَذَكَّرُونَ
Na bila ya shaka mlikwisha jua umbo la kwanza, basi kwa nini hamkumbuki? [62]
أَفَرَءَيۡتُم مَّا تَحۡرُثُونَ
Je! Mnaona makulima mnayo yapanda? [63]
ءَأَنتُمۡ تَزۡرَعُونَهُۥٓ أَمۡ نَحۡنُ ٱلزَّٰرِعُونَ
Je! Ni nyinyi mnayo yaotesha au ni Sisi ndio wenye kuotesha? [64]
لَوۡ نَشَآءُ لَجَعَلۡنَٰهُ حُطَٰمٗا فَظَلۡتُمۡ تَفَكَّهُونَ
Tungeli taka tungeli yafanya yakawa mapepe, mkabaki mnastaajabu, [65]
إِنَّا لَمُغۡرَمُونَ
Mkisema: Hakika sisi tumegharimika; [66]
بَلۡ نَحۡنُ مَحۡرُومُونَ
Bali sisi tumenyimwa. [67]
أَفَرَءَيۡتُمُ ٱلۡمَآءَ ٱلَّذِي تَشۡرَبُونَ
Je! Mnayaona maji mnayo yanywa? [68]
ءَأَنتُمۡ أَنزَلۡتُمُوهُ مِنَ ٱلۡمُزۡنِ أَمۡ نَحۡنُ ٱلۡمُنزِلُونَ
Je! Ni nyinyi mnayo yateremsha kutoka mawinguni au ni Sisi ndio wenye kuyateremsha? [69]
لَوۡ نَشَآءُ جَعَلۡنَٰهُ أُجَاجٗا فَلَوۡلَا تَشۡكُرُونَ
Tungeli penda tungeli yafanya ya chumvi. Basi mbona hamshukuru? [70]
أَفَرَءَيۡتُمُ ٱلنَّارَ ٱلَّتِي تُورُونَ
Je! Mnauona moto mnao uwasha? [71]
ءَأَنتُمۡ أَنشَأۡتُمۡ شَجَرَتَهَآ أَمۡ نَحۡنُ ٱلۡمُنشِـُٔونَ
Ni nyinyi mlio uumba mti wake au Sisi ndio Waumbaji? [72]
نَحۡنُ جَعَلۡنَٰهَا تَذۡكِرَةٗ وَمَتَٰعٗا لِّلۡمُقۡوِينَ
Sisi tumeufanya uwe ni ukumbusho na manufaa kwa walioko nyikani. [73]
فَسَبِّحۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلۡعَظِيمِ
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkuu. [74]
۞ فَلَآ أُقۡسِمُ بِمَوَٰقِعِ ٱلنُّجُومِ
Basi naapa kwa maanguko ya nyota, [75]
وَإِنَّهُۥ لَقَسَمٞ لَّوۡ تَعۡلَمُونَ عَظِيمٌ
Na hakika bila ya shaka hichi ni kiapo kikubwa, laiti mngeli jua! [76]
إِنَّهُۥ لَقُرۡءَانٞ كَرِيمٞ
Hakika hii bila ya shaka ni Qur'ani Tukufu, [77]
فِي كِتَٰبٖ مَّكۡنُونٖ
Katika Kitabu kilicho hifadhiwa. [78]
لَّا يَمَسُّهُۥٓ إِلَّا ٱلۡمُطَهَّرُونَ
Hapana akigusaye ila walio takaswa. [79]
تَنزِيلٞ مِّن رَّبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Ni uteremsho unao toka kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote. [80]
أَفَبِهَٰذَا ٱلۡحَدِيثِ أَنتُم مُّدۡهِنُونَ
Ni maneno haya ndiyo nyinyi mnayapuuza? [81]
وَتَجۡعَلُونَ رِزۡقَكُمۡ أَنَّكُمۡ تُكَذِّبُونَ
Na badala ya kushukuru kwa riziki yenu mnafanya kuwa mnakadhibisha? [82]
فَلَوۡلَآ إِذَا بَلَغَتِ ٱلۡحُلۡقُومَ
Yawaje basi itakapo fika roho kwenye koo, [83]
وَأَنتُمۡ حِينَئِذٖ تَنظُرُونَ
Na nyinyi wakati huo mnatazama! [84]
وَنَحۡنُ أَقۡرَبُ إِلَيۡهِ مِنكُمۡ وَلَٰكِن لَّا تُبۡصِرُونَ
Na Sisi tuko karibu zaidi naye kuliko nyinyi. [85]
فَلَوۡلَآ إِن كُنتُمۡ غَيۡرَ مَدِينِينَ
Na lau kuwa nyinyi hamumo katika mamlaka yangu, [86]
تَرۡجِعُونَهَآ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ
Kwanini hamuirudishi hiyo roho, ikiwa nyinyi mnasema kweli? [87]
فَأَمَّآ إِن كَانَ مِنَ ٱلۡمُقَرَّبِينَ
Basi akiwa miongoni mwa walio karibishwa, [88]
فَرَوۡحٞ وَرَيۡحَانٞ وَجَنَّتُ نَعِيمٖ
Basi ni raha, na manukato, na Bustani zenye neema. [89]
وَأَمَّآ إِن كَانَ مِنۡ أَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ
Na akiwa katika watu wa upande wa kulia, [90]
فَسَلَٰمٞ لَّكَ مِنۡ أَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ
Basi ni Salamu kwako uliye miongoni mwa watu wa upande wa kulia. [91]
وَأَمَّآ إِن كَانَ مِنَ ٱلۡمُكَذِّبِينَ ٱلضَّآلِّينَ
Na ama akiwa katika walio kadhibisha wapotovu, [92]
فَنُزُلٞ مِّنۡ حَمِيمٖ
Basi karamu yake ni maji yanayo chemka, [93]
وَتَصۡلِيَةُ جَحِيمٍ
Na kutiwa Motoni. [94]
إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ حَقُّ ٱلۡيَقِينِ
Hakika hii ndiyo haki yenye yakini. [95]
فَسَبِّحۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلۡعَظِيمِ
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkubwa. [96]
مشاركة عبر