Header Include

الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني

ترجمها علي محسن البرواني.

QR Code https://quran.islamcontent.com/70/swahili_barawani

ٱلۡقَارِعَةُ

Inayo gonga! [1]

[1] AL-QAARIA'H, Inayo gonga, ni Kiyama, ambacho kinaanza kwa mpulizo wa mwanzo wa barugumu, na kinaishia itapo katwa hukumu baina ya watu.
Inayo gonga! [1]

مَا ٱلۡقَارِعَةُ

Nini Inayo gonga? [2]

[2] Kitu gani kilicho cha ajabu zaidi katika ukuu wake, na khatari zake na kitisho chake!
Nini Inayo gonga? [2]

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡقَارِعَةُ

Na nini kitacho kujuilisha nini Inayo gonga? [3]

[3] Na kitu gani kitacho kujuulisha hali ya AL-QAARIA'H katika kitisho chake juu ya nafsi za watu?
Na nini kitacho kujuilisha nini Inayo gonga? [3]

يَوۡمَ يَكُونُ ٱلنَّاسُ كَٱلۡفَرَاشِ ٱلۡمَبۡثُوثِ

Siku ambayo watu watakuwa kama nondo walio tawanyika; [4]

[4] Siku hiyo watu watakuwa kama vipepeo kwa wingi na kuhangaika kulia na kushoto, madhaifu na wanyonge!
Siku ambayo watu watakuwa kama nondo walio tawanyika; [4]

وَتَكُونُ ٱلۡجِبَالُ كَٱلۡعِهۡنِ ٱلۡمَنفُوشِ

Na milima itakuwa kama sufi zilizo chambuliwa! [5]

[5] Na milima itakuwa kama sufi iliyo tiwa rangi na kuchambuliwa kwa kutapanyika vipande mbali mbali na kupeperuka katika anga huku na huku.
Na milima itakuwa kama sufi zilizo chambuliwa! [5]

فَأَمَّا مَن ثَقُلَتۡ مَوَٰزِينُهُۥ

Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito, [6]

[6] Ama yule ambaye mizani yake itakuwa nzito, mema yake yakapindukia kuliko maovu yake,
Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito, [6]

فَهُوَ فِي عِيشَةٖ رَّاضِيَةٖ

Huyo atakuwa katika maisha ya kupendeza. [7]

[7] Basi huyo atakuwa na maisha yatayo mridhisha mwenyewe, na nafsi yake itue.
Huyo atakuwa katika maisha ya kupendeza. [7]

وَأَمَّا مَنۡ خَفَّتۡ مَوَٰزِينُهُۥ

Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu, [8]

[8] Na ama ambaye mizani yake itakuwa nyepesi, na maovu yake yakazidi kuliko mema yake,
Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu, [8]

فَأُمُّهُۥ هَاوِيَةٞ

Huyo maskani yake yatakuwa Moto wa Hawiya! [9]

[9] Basi makaazi yake yatakuwa Jahannamu.
Huyo maskani yake yatakuwa Moto wa Hawiya! [9]

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا هِيَهۡ

Na nini kitacho kujuilisha nini hiyo? [10]

[10] Na nini cha kukujuulisha ni nini Hawiya?
Na nini kitacho kujuilisha nini hiyo? [10]

نَارٌ حَامِيَةُۢ

Ni Moto mkali! [11]

[11] Moto ulio mkali, hapana moto unao fikilia ukali wake, hata ukichochewa vipi na kutiwa kuni gani!
Ni Moto mkali! [11]
Footer Include