Header Include

الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني

ترجمها علي محسن البرواني.

QR Code https://quran.islamcontent.com/74/swahili_barawani

وَٱلۡفَجۡرِ

Naapa kwa alfajiri! [1]

[1] Naapa kwa mwangaza wa asubuhi unapo ufukuza usiku.
Naapa kwa alfajiri! [1]

وَلَيَالٍ عَشۡرٖ

Na kwa masiku kumi! [2]

[2] Na kwa masiku kumi yaliyo tukuzwa na Mwenyezi Mungu. (Na hayo ni masiku kumi ya mwanzo wa Mwezi wa Alhaj, Mfungo Tatu).
Na kwa masiku kumi! [2]

وَٱلشَّفۡعِ وَٱلۡوَتۡرِ

Na kwa viwili viwili na kimoja kimoja! [3]

[3] Na shafi' yaani hisabu inayo gawika kwa mbili, kama 4, 6, 8 n.k. na witri, yaani isiyo gawika kwa mbili, kama 1, 3, 5 n.k. katika kila kitu.
Na kwa viwili viwili na kimoja kimoja! [3]

وَٱلَّيۡلِ إِذَا يَسۡرِ

Na kwa usiku unapo pita! [4]

[4] Na kwa usiku unapo pita kwa kwenda ulimwengu kwa namna ya ajabu.
Na kwa usiku unapo pita! [4]

هَلۡ فِي ذَٰلِكَ قَسَمٞ لِّذِي حِجۡرٍ

Je! Hapana katika haya kiapo kwa mwenye akili? [5]

[5] Je! Katika vitu vilivyo tajwa vinavyo onekana kwa akili hapana kiapo cha kukinaisha?
Je! Hapana katika haya kiapo kwa mwenye akili? [5]

أَلَمۡ تَرَ كَيۡفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِعَادٍ

Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo wafanya kina A'di? [6]

[6] Kwani hujui jinsi Mola wako Mlezi alivyo wateremshia adhabu yake kaumu ya Hud, ?
Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo wafanya kina A'di? [6]

إِرَمَ ذَاتِ ٱلۡعِمَادِ

Wa Iram, wenye majumba marefu? [7]

[7] Watu wa Iram wenye majengo marefu?
Wa Iram, wenye majumba marefu? [7]

ٱلَّتِي لَمۡ يُخۡلَقۡ مِثۡلُهَا فِي ٱلۡبِلَٰدِ

Ambao haukuumbwa mfano wake katika nchi? [8]

[8] Ambayo haikupata kujengwa mfano wake kwa umadhubuti na ujenzi katika nchi.
Ambao haukuumbwa mfano wake katika nchi? [8]

وَثَمُودَ ٱلَّذِينَ جَابُواْ ٱلصَّخۡرَ بِٱلۡوَادِ

Na Thamudi walio chonga majabali huko bondeni? [9]

[9] Kwani hukujua jinsi Mola wako Mlezi alivyo teremsha adhabu yake kwa Thamudi, kaumu ya Saleh, walio chonga majabali kujengea nyumba zao huko bondeni?
Na Thamudi walio chonga majabali huko bondeni? [9]

وَفِرۡعَوۡنَ ذِي ٱلۡأَوۡتَادِ

Na Firauni mwenye vigingi? [10]

[10] Au kwani hukujua vipi Mola wako Mlezi alivyo wateremshia adhabu yake Firauni mwenye majeshi yaliyo upa nguvu ufalme wake kama vigingi vinavyo simamisha makhema?
Na Firauni mwenye vigingi? [10]

ٱلَّذِينَ طَغَوۡاْ فِي ٱلۡبِلَٰدِ

Ambao walifanya jeuri katika nchi? [11]

[11] Ambao walipita mipaka katika nchi?
Ambao walifanya jeuri katika nchi? [11]

فَأَكۡثَرُواْ فِيهَا ٱلۡفَسَادَ

Wakakithirisha humo ufisadi? [12]

[12] Na wakazidisha kufanya uharibifu kwa ukafiri na udhalimu?
Wakakithirisha humo ufisadi? [12]

فَصَبَّ عَلَيۡهِمۡ رَبُّكَ سَوۡطَ عَذَابٍ

Basi Mola wako Mlezi aliwapiga mjeledi wa adhabu. [13]

[13] Basi Mola wako Mlezi aliwateremshia adhabu kali ya kuwaunguza.
Basi Mola wako Mlezi aliwapiga mjeledi wa adhabu. [13]

إِنَّ رَبَّكَ لَبِٱلۡمِرۡصَادِ

Hakika Mola wako Mlezi yupo kwenye mavizio anawavizia. [14]

[14] Hakika Mola wako Mlezi anaviangalia vitendo vya watu, na anawahisabia, na atakuja kuwalipa kwavyo.
Hakika Mola wako Mlezi yupo kwenye mavizio anawavizia. [14]

فَأَمَّا ٱلۡإِنسَٰنُ إِذَا مَا ٱبۡتَلَىٰهُ رَبُّهُۥ فَأَكۡرَمَهُۥ وَنَعَّمَهُۥ فَيَقُولُ رَبِّيٓ أَكۡرَمَنِ

Ama mtu anapo jaribiwa na Mola wake Mlezi, akamkirimu na akamneemesha, husema: Mola wangu Mlezi amenikirimu! [15]

[15] Ama mtu akijaribiwa na Mola wake Mlezi na akamkirimu, na akamneemesha kwa mali na cheo na nguvu, basi husema kwa kughurika na hayo: Mola wangu Mlezi amenitukuza kwa kuwa ninastahiki haya!
Ama mtu anapo jaribiwa na Mola wake Mlezi, akamkirimu na akamneemesha, husema: Mola wangu Mlezi amenikirimu! [15]

وَأَمَّآ إِذَا مَا ٱبۡتَلَىٰهُ فَقَدَرَ عَلَيۡهِ رِزۡقَهُۥ فَيَقُولُ رَبِّيٓ أَهَٰنَنِ

Na ama anapo mjaribu akampunguzia riziki yake, husema: Mola wangu Mlezi amenitia unyonge! [16]

[16] Na pindi Mola wake Mlezi akimjaribu mtu kwa kumdhikisha riziki, basi hughafilika na hikima ya hayo na husema: Mola wangu Mlezi kanidhalilisha!
Na ama anapo mjaribu akampunguzia riziki yake, husema: Mola wangu Mlezi amenitia unyonge! [16]

كَلَّاۖ بَل لَّا تُكۡرِمُونَ ٱلۡيَتِيمَ

Sivyo hivyo! Bali nyinyi hamuwakirimu mayatima, [17]

[17] Wacheni mtindo huo! Mambo siyo hayo kama msemavyo; bali nyinyi hamumkirimu yatima;
Sivyo hivyo! Bali nyinyi hamuwakirimu mayatima, [17]

وَلَا تَحَٰٓضُّونَ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلۡمِسۡكِينِ

Wala hamhimizani kulisha masikini; [18]

[18] Wala hamhimizani kuwalisha masikini;
Wala hamhimizani kulisha masikini; [18]

وَتَأۡكُلُونَ ٱلتُّرَاثَ أَكۡلٗا لَّمّٗا

Na mnakula urithi kwa ulaji wa pupa, [19]

[19] Na mnakula mali ya urithi kwa pupa, hamchagui linalo faa na lisilo faa.
Na mnakula urithi kwa ulaji wa pupa, [19]

وَتُحِبُّونَ ٱلۡمَالَ حُبّٗا جَمّٗا

Na mnapenda mali pendo la kupita kiasi. [20]

[20] Na mnayapenda mali mno, yanayo kupelekeeni kupapatika katika kuyakusanya na ubakhili wa kuyatumia.
Na mnapenda mali pendo la kupita kiasi. [20]

كَلَّآۖ إِذَا دُكَّتِ ٱلۡأَرۡضُ دَكّٗا دَكّٗا

Sivyo hivyo! Itakapo vunjwa ardhi vipande vipande, [21]

[21] Wacheni vitendo hivyo! Kwani inakungojeeni siku itapo lazwa ardhi iwe sawa sawa,
Sivyo hivyo! Itakapo vunjwa ardhi vipande vipande, [21]

وَجَآءَ رَبُّكَ وَٱلۡمَلَكُ صَفّٗا صَفّٗا

Na akaja Mola wako Mlezi na Malaika safu safu, [22]

[22] Na aje Mola wako Mlezi kama anavyo stahiki kuja kwake Subhanahu na Malaika waje kwa safu safu;
Na akaja Mola wako Mlezi na Malaika safu safu, [22]

وَجِاْيٓءَ يَوۡمَئِذِۭ بِجَهَنَّمَۚ يَوۡمَئِذٖ يَتَذَكَّرُ ٱلۡإِنسَٰنُ وَأَنَّىٰ لَهُ ٱلذِّكۡرَىٰ

Na ikaletwa Jahannamu siku hiyo, siku hiyo mtu atakumbuka! Lakini kukumbuka huko kutamfaa nini? [23]

[23] Na siku hiyo iletwe Jahannamu, nyumba ya adhabu, siku hiyo yatapo tokea hayo mwanaadamu atakumbuka aliyo yaharibu - lakini wapi! Kukumbuka huko kumfae nini, na wakati umekwisha pita?
Na ikaletwa Jahannamu siku hiyo, siku hiyo mtu atakumbuka! Lakini kukumbuka huko kutamfaa nini? [23]

يَقُولُ يَٰلَيۡتَنِي قَدَّمۡتُ لِحَيَاتِي

Atasema: Laiti ningeli jitangulizia kwa uhai wangu! [24]

[24] Atasema kwa majuto: Laiti ningeli jitangulizia katika dunia vitendo vyema vya kunifaa katika maisha ya Akhera!
Atasema: Laiti ningeli jitangulizia kwa uhai wangu! [24]

فَيَوۡمَئِذٖ لَّا يُعَذِّبُ عَذَابَهُۥٓ أَحَدٞ

Basi siku hiyo hataadhibu yeyote namna ya kuadhibu kwake. [25]

[25] Siku hiyo zitakuwa hali hizi, haadhibu mtu kama adhabu ya Mwenyezi Mungu, wala hafungi mtu kama afungavyo Yeye.
Basi siku hiyo hataadhibu yeyote namna ya kuadhibu kwake. [25]

وَلَا يُوثِقُ وَثَاقَهُۥٓ أَحَدٞ

Wala hatafunga yeyote kama kufunga kwake. [26]

[26] Siku hiyo zitakuwa hali hizi, haadhibu mtu kama adhabu ya Mwenyezi Mungu, wala hafungi mtu kama afungavyo Yeye.
Wala hatafunga yeyote kama kufunga kwake. [26]

يَٰٓأَيَّتُهَا ٱلنَّفۡسُ ٱلۡمُطۡمَئِنَّةُ

Ewe nafsi iliyo tua! [27]

[27] Ewe nafsi uliye tulia juu ya Haki!
Ewe nafsi iliyo tua! [27]

ٱرۡجِعِيٓ إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةٗ مَّرۡضِيَّةٗ

Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha. [28]

[28] Rejea kwenye radhi ya Mola wako Mlezi nawe uradhi kwa neema ulio pewa, nawe umemridhisha kwa a'mali uliyo ikadimisha.
Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha. [28]

فَٱدۡخُلِي فِي عِبَٰدِي

Basi ingia miongoni mwa waja wangu, [29]

[29] Basi ingia katika kundi la waja wangu walio wema!
Basi ingia miongoni mwa waja wangu, [29]

وَٱدۡخُلِي جَنَّتِي

Na ingia katika Pepo yangu. [30]

[30] Na ingia katika Pepo yangu, nyumba ya neema ya milele!
Na ingia katika Pepo yangu. [30]
Footer Include