Swahili translation - Ali Muhsen Al-Berwani
Translated by Ali Muhsen Al-Berwani
إِذَا ٱلشَّمۡسُ كُوِّرَتۡ
Jua litakapo kunjwa! [1]
وَإِذَا ٱلنُّجُومُ ٱنكَدَرَتۡ
Na nyota zikazimwa! [2]
وَإِذَا ٱلۡجِبَالُ سُيِّرَتۡ
Na milima ikaondolewa! [3]
وَإِذَا ٱلۡعِشَارُ عُطِّلَتۡ
Na ngamia wenye mimba pevu watakapo achwa wasishughulikiwe, [4]
وَإِذَا ٱلۡوُحُوشُ حُشِرَتۡ
Na wanyama wa mwituni wakakusanywa! [5]
وَإِذَا ٱلۡبِحَارُ سُجِّرَتۡ
Na bahari zikawaka moto! [6]
وَإِذَا ٱلنُّفُوسُ زُوِّجَتۡ
Na nafsi zikaunganishwa! [7]
وَإِذَا ٱلۡمَوۡءُۥدَةُ سُئِلَتۡ
Na msichana aliye zikwa hai atapo ulizwa! [8]
بِأَيِّ ذَنۢبٖ قُتِلَتۡ
Kwa kosa gani aliuliwa? [9]
وَإِذَا ٱلصُّحُفُ نُشِرَتۡ
Na madaftari yatakapo enezwa, [10]
وَإِذَا ٱلسَّمَآءُ كُشِطَتۡ
Na mbingu itapo tanduliwa, [11]
وَإِذَا ٱلۡجَحِيمُ سُعِّرَتۡ
Na Jahannamu itapo chochewa, [12]
وَإِذَا ٱلۡجَنَّةُ أُزۡلِفَتۡ
Na Pepo ikasogezwa, [13]
عَلِمَتۡ نَفۡسٞ مَّآ أَحۡضَرَتۡ
Kila nafsi itajua ilicho kihudhurisha. [14]
فَلَآ أُقۡسِمُ بِٱلۡخُنَّسِ
Naapa kwa nyota zinapo rejea nyuma, [15]
ٱلۡجَوَارِ ٱلۡكُنَّسِ
Zinazo kwenda, kisha zikajificha, [16]
وَٱلَّيۡلِ إِذَا عَسۡعَسَ
Na kwa usiku unapo pungua, [17]
وَٱلصُّبۡحِ إِذَا تَنَفَّسَ
Na kwa asubuhi inapo pambazuka, [18]
إِنَّهُۥ لَقَوۡلُ رَسُولٖ كَرِيمٖ
Kwamba hakika bila ya shaka hii ni kauli ya Mjumbe mtukufu, [19]
ذِي قُوَّةٍ عِندَ ذِي ٱلۡعَرۡشِ مَكِينٖ
Mwenye nguvu na mwenye cheo kwa huyo Mwenye Kiti cha Enzi, [20]
مُّطَاعٖ ثَمَّ أَمِينٖ
Anaye t'iiwa, tena muaminifu. [21]
وَمَا صَاحِبُكُم بِمَجۡنُونٖ
Na wala huyu mwenzenu hana wazimu. [22]
وَلَقَدۡ رَءَاهُ بِٱلۡأُفُقِ ٱلۡمُبِينِ
Na hakika yeye alimwona kwenye upeo wa macho ulio safi. [23]
وَمَا هُوَ عَلَى ٱلۡغَيۡبِ بِضَنِينٖ
Wala yeye si bakhili kwa mambo ya ghaibu. [24]
وَمَا هُوَ بِقَوۡلِ شَيۡطَٰنٖ رَّجِيمٖ
Wala hii si kauli ya Shetani maluuni. [25]
فَأَيۡنَ تَذۡهَبُونَ
Basi mnakwenda wapi? [26]
إِنۡ هُوَ إِلَّا ذِكۡرٞ لِّلۡعَٰلَمِينَ
Haikuwa hii ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote. [27]
لِمَن شَآءَ مِنكُمۡ أَن يَسۡتَقِيمَ
Kwa yule miongoni mwenu anaye taka kwenda sawa. [28]
وَمَا تَشَآءُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُ رَبُّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Wala nyinyi hamtataka isipo kuwa atake Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote. [29]
مشاركة عبر