Header Include

Swahili translation - Ali Muhsen Al-Berwani

Translated by Ali Muhsen Al-Berwani

QR Code https://quran.islamcontent.com/kk/swahili_barawani

إِذَا زُلۡزِلَتِ ٱلۡأَرۡضُ زِلۡزَالَهَا

Itakapo tetemeshwa ardhi kwa mtetemeko wake! [1]

[1] Ikitisika ardhi kwa mtikiso mkubwa, na ikasukika kwa ukomo wa kutisika na kusukika kunako mkinika na ikaweza kuchukua!
Itakapo tetemeshwa ardhi kwa mtetemeko wake! [1]

وَأَخۡرَجَتِ ٱلۡأَرۡضُ أَثۡقَالَهَا

Na itakapo toa ardhi mizigo yake! [2]

[2] Na ardhi ikatoa yote yaliomo katika ndani ya tumbo lake, ikiwa khazina au maiti walio kwisha zikwa!
Na itakapo toa ardhi mizigo yake! [2]

وَقَالَ ٱلۡإِنسَٰنُ مَا لَهَا

Na mtu akasema: Ina nini? [3]

[3] Na binaadamu akasema kwa kushtuka na khofu: Ardhi hii ina nini hata inatikisika hivi, na inatoa vilivyomo tumboni mwake, ndio Saa imefika?
Na mtu akasema: Ina nini? [3]

يَوۡمَئِذٖ تُحَدِّثُ أَخۡبَارَهَا

Siku hiyo itahadithia khabari zake. [4]

[4] Siku hiyo ardhi itamsimulia mtu khabari zake zilio mshitua,
Siku hiyo itahadithia khabari zake. [4]

بِأَنَّ رَبَّكَ أَوۡحَىٰ لَهَا

Kwa sababu Mola wake Mlezi ameifunulia! [5]

[5] Kwani Mlezi wake na Muumba wake atakuwa kaifunulia, kaipa Wahyi, na kaiamuru itetemeke na ijisuke suke, ndio ikafanya upesi kutekeleza amri.
Kwa sababu Mola wake Mlezi ameifunulia! [5]

يَوۡمَئِذٖ يَصۡدُرُ ٱلنَّاسُ أَشۡتَاتٗا لِّيُرَوۡاْ أَعۡمَٰلَهُمۡ

Siku hiyo watu watatoka kwa mfarakano wakaonyweshwe vitendo vyao! [6]

[6] Siku hiyo watu watatoka makaburini mbio, nao wamo katika mtafaruku, wapate kuziona hisabu zao na malipo yao aliyo waahidi Mwenyezi Mungu.
Siku hiyo watu watatoka kwa mfarakano wakaonyweshwe vitendo vyao! [6]

فَمَن يَعۡمَلۡ مِثۡقَالَ ذَرَّةٍ خَيۡرٗا يَرَهُۥ

Basi anaye tenda chembe ya wema, atauona! [7]

[7] Basi mwenye kufanya hata kitu chenye uzito wa punje ya mchanga cha kheri ataiona katika daftari lake, na atapata malipo yake.
Basi anaye tenda chembe ya wema, atauona! [7]

وَمَن يَعۡمَلۡ مِثۡقَالَ ذَرَّةٖ شَرّٗا يَرَهُۥ

Na anaye tenda chembe ya uovu atauona! [8]

[8] Na mwenye kufanya shari ya uzito wa chembe ya mchanga ataiona kadhaalika, na atapata malipo yake. Wala Mola wako Mlezi hatamdhulumu yeyote.
Na anaye tenda chembe ya uovu atauona! [8]
Footer Include