Header Include

Swahili translation - Rowad Translation Center

translated by Rowwad Translation Center, in cooperation with the Islamic Propagation Office in Rabwah and the Association for Serving Islamic Content in Languages.

QR Code https://quran.islamcontent.com/mk/swahili_rwwad

إِذَا ٱلشَّمۡسُ كُوِّرَتۡ

Jua litakapokunjwa,

Jua litakapokunjwa,

وَإِذَا ٱلنُّجُومُ ٱنكَدَرَتۡ

Na nyota zikazimwa,

Na nyota zikazimwa,

وَإِذَا ٱلۡجِبَالُ سُيِّرَتۡ

Na milima ikaondolewa,

Na milima ikaondolewa,

وَإِذَا ٱلۡعِشَارُ عُطِّلَتۡ

Na ngamia wenye mimba pevu watakapoachwa wasishughulikiwe,

Na ngamia wenye mimba pevu watakapoachwa wasishughulikiwe,

وَإِذَا ٱلۡوُحُوشُ حُشِرَتۡ

Na wanyama wa mwituni wakakusanywa,

Na wanyama wa mwituni wakakusanywa,

وَإِذَا ٱلۡبِحَارُ سُجِّرَتۡ

Na bahari zikawaka moto,

Na bahari zikawaka moto,

وَإِذَا ٱلنُّفُوسُ زُوِّجَتۡ

Na nafsi zikaunganishwa,

Na nafsi zikaunganishwa,

وَإِذَا ٱلۡمَوۡءُۥدَةُ سُئِلَتۡ

Na msichana aliyezikwa hai atakapoulizwa,

Na msichana aliyezikwa hai atakapoulizwa,

بِأَيِّ ذَنۢبٖ قُتِلَتۡ

Kwa kosa gani aliuliwa?

Kwa kosa gani aliuliwa?

وَإِذَا ٱلصُّحُفُ نُشِرَتۡ

Na madaftari yatakapoenezwa,

Na madaftari yatakapoenezwa,

وَإِذَا ٱلسَّمَآءُ كُشِطَتۡ

Na mbingu itakapotanduliwa,

Na mbingu itakapotanduliwa,

وَإِذَا ٱلۡجَحِيمُ سُعِّرَتۡ

Na Jahannamu itakapochochewa,

Na Jahannamu itakapochochewa,

وَإِذَا ٱلۡجَنَّةُ أُزۡلِفَتۡ

Na Bustani ya mbinguni ikasongezwa karibu,

Na Bustani ya mbinguni ikasongezwa karibu,

عَلِمَتۡ نَفۡسٞ مَّآ أَحۡضَرَتۡ

Kila nafsi itajua ilichokihudhurisha.

Kila nafsi itajua ilichokihudhurisha.

فَلَآ أُقۡسِمُ بِٱلۡخُنَّسِ

Ninaapa kwa nyota zinaporejea nyuma.

Ninaapa kwa nyota zinaporejea nyuma.

ٱلۡجَوَارِ ٱلۡكُنَّسِ

Zinazokwenda, kisha zikajificha.

Zinazokwenda, kisha zikajificha.

وَٱلَّيۡلِ إِذَا عَسۡعَسَ

Na kwa usiku unapopungua.

Na kwa usiku unapopungua.

وَٱلصُّبۡحِ إِذَا تَنَفَّسَ

Na kwa asubuhi inapopambazuka.

Na kwa asubuhi inapopambazuka.

إِنَّهُۥ لَقَوۡلُ رَسُولٖ كَرِيمٖ

Kwamba hakika bila ya shaka hii ni kauli ya Mjumbe mtukufu.

Kwamba hakika bila ya shaka hii ni kauli ya Mjumbe mtukufu.

ذِي قُوَّةٍ عِندَ ذِي ٱلۡعَرۡشِ مَكِينٖ

Mwenye nguvu na mwenye cheo kwa huyo Mwenye Kiti cha Enzi.

Mwenye nguvu na mwenye cheo kwa huyo Mwenye Kiti cha Enzi.

مُّطَاعٖ ثَمَّ أَمِينٖ

Anayetiiwa, tena muaminifu.

Anayetiiwa, tena muaminifu.

وَمَا صَاحِبُكُم بِمَجۡنُونٖ

Na wala huyu mwenzenu hana wazimu.

Na wala huyu mwenzenu hana wazimu.

وَلَقَدۡ رَءَاهُ بِٱلۡأُفُقِ ٱلۡمُبِينِ

Na hakika yeye alimwona kwenye upeo wa macho ulio safi.

Na hakika yeye alimwona kwenye upeo wa macho ulio safi.

وَمَا هُوَ عَلَى ٱلۡغَيۡبِ بِضَنِينٖ

Wala yeye si bahili kwa mambo ya ghaibu.

Wala yeye si bahili kwa mambo ya ghaibu.

وَمَا هُوَ بِقَوۡلِ شَيۡطَٰنٖ رَّجِيمٖ

Wala hii si kauli ya Shetani aliyelaaniwa.

Wala hii si kauli ya Shetani aliyelaaniwa.

فَأَيۡنَ تَذۡهَبُونَ

Basi mnakwenda wapi?

Basi mnakwenda wapi?

إِنۡ هُوَ إِلَّا ذِكۡرٞ لِّلۡعَٰلَمِينَ

Haikuwa hii ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.

Haikuwa hii ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.

لِمَن شَآءَ مِنكُمۡ أَن يَسۡتَقِيمَ

Kwa yule miongoni mwenu anayetaka kwenda sawa.

Kwa yule miongoni mwenu anayetaka kwenda sawa.

وَمَا تَشَآءُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُ رَبُّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Wala nyinyi hamtataka isipokuwa atake Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Wala nyinyi hamtataka isipokuwa atake Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Footer Include