Header Include

Swahili translation - Rowad Translation Center

translated by Rowwad Translation Center, in cooperation with the Islamic Propagation Office in Rabwah and the Association for Serving Islamic Content in Languages.

QR Code https://quran.islamcontent.com/sr/swahili_rwwad

هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلۡغَٰشِيَةِ

Je, imekufikia habari ya Msiba wa kufudikiza?

Je, imekufikia habari ya Msiba wa kufudikiza?

وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٍ خَٰشِعَةٌ

Siku hiyo nyuso zitainama.

Siku hiyo nyuso zitainama.

عَامِلَةٞ نَّاصِبَةٞ

Zikifanya kazi, nazo taabani.

Zikifanya kazi, nazo taabani.

تَصۡلَىٰ نَارًا حَامِيَةٗ

Ziingie katika Moto unaowaka.

Ziingie katika Moto unaowaka.

تُسۡقَىٰ مِنۡ عَيۡنٍ ءَانِيَةٖ

Zikinyweshwa kutoka chemchemi inayochemka.

Zikinyweshwa kutoka chemchemi inayochemka.

لَّيۡسَ لَهُمۡ طَعَامٌ إِلَّا مِن ضَرِيعٖ

Hawatakuwa na chakula isipokuwa kichungu chenye miba.

Hawatakuwa na chakula isipokuwa kichungu chenye miba.

لَّا يُسۡمِنُ وَلَا يُغۡنِي مِن جُوعٖ

Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa.

Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa.

وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ نَّاعِمَةٞ

Siku hiyo nyuso nyengine zitakuwa kunjufu.

Siku hiyo nyuso nyengine zitakuwa kunjufu.

لِّسَعۡيِهَا رَاضِيَةٞ

Zitakuwa radhi kwa juhudi yao.

Zitakuwa radhi kwa juhudi yao.

فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٖ

Katika Bustani ya juu.

Katika Bustani ya juu.

لَّا تَسۡمَعُ فِيهَا لَٰغِيَةٗ

Hawatasikia humo upuuzi.

Hawatasikia humo upuuzi.

فِيهَا عَيۡنٞ جَارِيَةٞ

Humo imo chemchemi inayomiminika.

Humo imo chemchemi inayomiminika.

فِيهَا سُرُرٞ مَّرۡفُوعَةٞ

Humo vimo viti vilivyonyanyuliwa.

Humo vimo viti vilivyonyanyuliwa.

وَأَكۡوَابٞ مَّوۡضُوعَةٞ

Na bilauri zilizopangwa.

Na bilauri zilizopangwa.

وَنَمَارِقُ مَصۡفُوفَةٞ

Na matakia safu safu.

Na matakia safu safu.

وَزَرَابِيُّ مَبۡثُوثَةٌ

Na mazulia yaliyotandikwa.

Na mazulia yaliyotandikwa.

أَفَلَا يَنظُرُونَ إِلَى ٱلۡإِبِلِ كَيۡفَ خُلِقَتۡ

Je! Hawamtazami ngamia jinsi alivyoumbwa?

Je! Hawamtazami ngamia jinsi alivyoumbwa?

وَإِلَى ٱلسَّمَآءِ كَيۡفَ رُفِعَتۡ

Na mbingu jinsi ilivyoinuliwa?

Na mbingu jinsi ilivyoinuliwa?

وَإِلَى ٱلۡجِبَالِ كَيۡفَ نُصِبَتۡ

Na milima jinsi ilivyowekwa imara?

Na milima jinsi ilivyowekwa imara?

وَإِلَى ٱلۡأَرۡضِ كَيۡفَ سُطِحَتۡ

Na ardhi jinsi ilivyotandazwa?

Na ardhi jinsi ilivyotandazwa?

فَذَكِّرۡ إِنَّمَآ أَنتَ مُذَكِّرٞ

Basi kumbusha! Hakika wewe ni Mkumbushaji.

Basi kumbusha! Hakika wewe ni Mkumbushaji.

لَّسۡتَ عَلَيۡهِم بِمُصَيۡطِرٍ

Wewe si mwenye kuwatawalia.

Wewe si mwenye kuwatawalia.

إِلَّا مَن تَوَلَّىٰ وَكَفَرَ

Lakini anayerudi nyuma na kukataa.

Lakini anayerudi nyuma na kukataa.

فَيُعَذِّبُهُ ٱللَّهُ ٱلۡعَذَابَ ٱلۡأَكۡبَرَ

Basi Mwenyezi Mungu atamuadhibu kwa adhabu iliyo kubwa kabisa!

Basi Mwenyezi Mungu atamuadhibu kwa adhabu iliyo kubwa kabisa!

إِنَّ إِلَيۡنَآ إِيَابَهُمۡ

Hakika ni kwetu Sisi ndio marejeo yao.

Hakika ni kwetu Sisi ndio marejeo yao.

ثُمَّ إِنَّ عَلَيۡنَا حِسَابَهُم

Kisha hakika ni juu yetu Sisi hisabu yao!

Kisha hakika ni juu yetu Sisi hisabu yao!
Footer Include