Header Include

Swahili translation - Rowad Translation Center

translated by Rowwad Translation Center, in cooperation with the Islamic Propagation Office in Rabwah and the Association for Serving Islamic Content in Languages.

QR Code https://quran.islamcontent.com/sw/swahili_rwwad

إِذَا وَقَعَتِ ٱلۡوَاقِعَةُ

Litakapotokea hilo Tukio.

Litakapotokea hilo Tukio.

لَيۡسَ لِوَقۡعَتِهَا كَاذِبَةٌ

Hapana cha kukanusha kutokea kwake.

Hapana cha kukanusha kutokea kwake.

خَافِضَةٞ رَّافِعَةٌ

Literemshalo linyanyualo.

Literemshalo linyanyualo.

إِذَا رُجَّتِ ٱلۡأَرۡضُ رَجّٗا

Itakapotikiswa ardhi kwa mtikiso.

Itakapotikiswa ardhi kwa mtikiso.

وَبُسَّتِ ٱلۡجِبَالُ بَسّٗا

Na milima itakaposagwasagwa.

Na milima itakaposagwasagwa.

فَكَانَتۡ هَبَآءٗ مُّنۢبَثّٗا

Basi iwe mavumbi yanayopeperushwa.

Basi iwe mavumbi yanayopeperushwa.

وَكُنتُمۡ أَزۡوَٰجٗا ثَلَٰثَةٗ

Na nyinyi mtakuwa namna tatu.

Na nyinyi mtakuwa namna tatu.

فَأَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ

Basi watakuwepo wa kuliani; je, ni wepi wa kuliani?

Basi watakuwepo wa kuliani; je, ni wepi wa kuliani?

وَأَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ

Na wa kushotoni; je, ni wepi wa kushotoni?

Na wa kushotoni; je, ni wepi wa kushotoni?

وَٱلسَّٰبِقُونَ ٱلسَّٰبِقُونَ

Na wa mbele watakuwa mbele.

Na wa mbele watakuwa mbele.

أُوْلَٰٓئِكَ ٱلۡمُقَرَّبُونَ

Hao ndio watakaowekwa karibu (na Mwenyezi Mungu).

Hao ndio watakaowekwa karibu (na Mwenyezi Mungu).

فِي جَنَّٰتِ ٱلنَّعِيمِ

Katika Bustani zenye neema.

Katika Bustani zenye neema.

ثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأَوَّلِينَ

Fungu kubwa katika wa mwanzo.

Fungu kubwa katika wa mwanzo.

وَقَلِيلٞ مِّنَ ٱلۡأٓخِرِينَ

Na wachache katika wa mwisho.

Na wachache katika wa mwisho.

عَلَىٰ سُرُرٖ مَّوۡضُونَةٖ

Watakuwa juu ya viti vya fakhari vilivyotonewa.

Watakuwa juu ya viti vya fakhari vilivyotonewa.

مُّتَّكِـِٔينَ عَلَيۡهَا مُتَقَٰبِلِينَ

Wakiviegemea wakielekeana.

Wakiviegemea wakielekeana.

يَطُوفُ عَلَيۡهِمۡ وِلۡدَٰنٞ مُّخَلَّدُونَ

Wakitumikiwa na wavulana wa ujana wa milele.

Wakitumikiwa na wavulana wa ujana wa milele.

بِأَكۡوَابٖ وَأَبَارِيقَ وَكَأۡسٖ مِّن مَّعِينٖ

Kwa vikombe na mabirika na bilauri za vinywaji kutoka chemchemi safi.

Kwa vikombe na mabirika na bilauri za vinywaji kutoka chemchemi safi.

لَّا يُصَدَّعُونَ عَنۡهَا وَلَا يُنزِفُونَ

Hawataumwa kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawatoleweshwa.

Hawataumwa kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawatoleweshwa.

وَفَٰكِهَةٖ مِّمَّا يَتَخَيَّرُونَ

Na matunda wayapendayo.

Na matunda wayapendayo.

وَلَحۡمِ طَيۡرٖ مِّمَّا يَشۡتَهُونَ

Na nyama za ndege kama wanavyotamani.

Na nyama za ndege kama wanavyotamani.

وَحُورٌ عِينٞ

Na Mahurulaini.

Na Mahurulaini.

كَأَمۡثَٰلِ ٱللُّؤۡلُوِٕ ٱلۡمَكۡنُونِ

Walio kama mfano wa lulu zilizohifadhiwa.

Walio kama mfano wa lulu zilizohifadhiwa.

جَزَآءَۢ بِمَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ

Ni malipo kwa waliyokuwa wakiyatenda.

Ni malipo kwa waliyokuwa wakiyatenda.

لَا يَسۡمَعُونَ فِيهَا لَغۡوٗا وَلَا تَأۡثِيمًا

Humo hawatasikia porojo wala maneno ya dhambi.

Humo hawatasikia porojo wala maneno ya dhambi.

إِلَّا قِيلٗا سَلَٰمٗا سَلَٰمٗا

Isipokuwa maneno ya Salama, Salama.

Isipokuwa maneno ya Salama, Salama.

وَأَصۡحَٰبُ ٱلۡيَمِينِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡيَمِينِ

Na wale wa mkono wa kulia, ni yepi yatakuwa ya wa kuliani?

Na wale wa mkono wa kulia, ni yepi yatakuwa ya wa kuliani?

فِي سِدۡرٖ مَّخۡضُودٖ

Katika mikunazi isiyo na miba.

Katika mikunazi isiyo na miba.

وَطَلۡحٖ مَّنضُودٖ

Na migomba iliyopangiliwa.

Na migomba iliyopangiliwa.

وَظِلّٖ مَّمۡدُودٖ

Na kivuli kilichotanda.

Na kivuli kilichotanda.

وَمَآءٖ مَّسۡكُوبٖ

Na maji yanayomiminika.

Na maji yanayomiminika.

وَفَٰكِهَةٖ كَثِيرَةٖ

Na matunda mengi.

Na matunda mengi.

لَّا مَقۡطُوعَةٖ وَلَا مَمۡنُوعَةٖ

Hayatindikii wala hayakatazwi.

Hayatindikii wala hayakatazwi.

وَفُرُشٖ مَّرۡفُوعَةٍ

Na matandiko yaliyonyanyuliwa.

Na matandiko yaliyonyanyuliwa.

إِنَّآ أَنشَأۡنَٰهُنَّ إِنشَآءٗ

Hakika Sisi tutawaumba (Mahurulaini) upya.

Hakika Sisi tutawaumba (Mahurulaini) upya.

فَجَعَلۡنَٰهُنَّ أَبۡكَارًا

Na tutawafanya vijana.

Na tutawafanya vijana.

عُرُبًا أَتۡرَابٗا

Wanapendana na waume zao, hirimu moja.

Wanapendana na waume zao, hirimu moja.

لِّأَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ

Kwa ajili ya watu wa kuliani.

Kwa ajili ya watu wa kuliani.

ثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأَوَّلِينَ

Fungu kubwa katika wa mwanzo.

Fungu kubwa katika wa mwanzo.

وَثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأٓخِرِينَ

Na fungu kubwa katika wa mwisho.

Na fungu kubwa katika wa mwisho.

وَأَصۡحَٰبُ ٱلشِّمَالِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلشِّمَالِ

Na watu wa kushotoni; je ni yepi ya wa kushotoni?

Na watu wa kushotoni; je ni yepi ya wa kushotoni?

فِي سَمُومٖ وَحَمِيمٖ

Katika upepo wa moto, na maji yanayochemka.

Katika upepo wa moto, na maji yanayochemka.

وَظِلّٖ مِّن يَحۡمُومٖ

Na kivuli cha moshi mweusi.

Na kivuli cha moshi mweusi.

لَّا بَارِدٖ وَلَا كَرِيمٍ

Si baridi wala cha kustarehesha.

Si baridi wala cha kustarehesha.

إِنَّهُمۡ كَانُواْ قَبۡلَ ذَٰلِكَ مُتۡرَفِينَ

Hakika hao walikuwa kabla ya haya wakiishi maisha ya anasa.

Hakika hao walikuwa kabla ya haya wakiishi maisha ya anasa.

وَكَانُواْ يُصِرُّونَ عَلَى ٱلۡحِنثِ ٱلۡعَظِيمِ

Na walikuwa wakiendelea tu kufanya madhambi makubwa.

Na walikuwa wakiendelea tu kufanya madhambi makubwa.

وَكَانُواْ يَقُولُونَ أَئِذَا مِتۡنَا وَكُنَّا تُرَابٗا وَعِظَٰمًا أَءِنَّا لَمَبۡعُوثُونَ

Na walikuwa wakisema: 'Tutakapokufa na tukawa udongo na mafupa, ati ndiyo tutafufuliwa?

Na walikuwa wakisema: 'Tutakapokufa na tukawa udongo na mafupa, ati ndiyo tutafufuliwa?

أَوَءَابَآؤُنَا ٱلۡأَوَّلُونَ

Au baba zetu wa zamani?'

Au baba zetu wa zamani?'

قُلۡ إِنَّ ٱلۡأَوَّلِينَ وَٱلۡأٓخِرِينَ

Sema: 'Hakika wa zamani na wa mwisho.'

Sema: 'Hakika wa zamani na wa mwisho.'

لَمَجۡمُوعُونَ إِلَىٰ مِيقَٰتِ يَوۡمٖ مَّعۡلُومٖ

Bila ya shaka watakusanywa kwa wakati wa siku maalumu.

Bila ya shaka watakusanywa kwa wakati wa siku maalumu.

ثُمَّ إِنَّكُمۡ أَيُّهَا ٱلضَّآلُّونَ ٱلۡمُكَذِّبُونَ

Kisha nyinyi, mliopotea, mnaokanusha.

Kisha nyinyi, mliopotea, mnaokanusha.

لَأٓكِلُونَ مِن شَجَرٖ مِّن زَقُّومٖ

Kwa yakini mtakula mti wa Zaqqumu.

Kwa yakini mtakula mti wa Zaqqumu.

فَمَالِـُٔونَ مِنۡهَا ٱلۡبُطُونَ

Na kwa mti huo mtajaza matumbo.

Na kwa mti huo mtajaza matumbo.

فَشَٰرِبُونَ عَلَيۡهِ مِنَ ٱلۡحَمِيمِ

Na juu yake mtakunywa maji yanayochemka.

Na juu yake mtakunywa maji yanayochemka.

فَشَٰرِبُونَ شُرۡبَ ٱلۡهِيمِ

Tena mtakunywa kama wanavyokunywa ngamia wenye kiu.

Tena mtakunywa kama wanavyokunywa ngamia wenye kiu.

هَٰذَا نُزُلُهُمۡ يَوۡمَ ٱلدِّينِ

Hiyo ndiyo karamu yao ya kuwakaribisha Siku ya Malipo.

Hiyo ndiyo karamu yao ya kuwakaribisha Siku ya Malipo.

نَحۡنُ خَلَقۡنَٰكُمۡ فَلَوۡلَا تُصَدِّقُونَ

Sisi tumekuumbeni; basi hamsadiki?

Sisi tumekuumbeni; basi hamsadiki?

أَفَرَءَيۡتُم مَّا تُمۡنُونَ

Je, mnaiona mbegu ya uzazi mnayoidondokesha?

Je, mnaiona mbegu ya uzazi mnayoidondokesha?

ءَأَنتُمۡ تَخۡلُقُونَهُۥٓ أَمۡ نَحۡنُ ٱلۡخَٰلِقُونَ

Je, mnaiumba nyinyi, au ni Sisi ndio Waumbaji?

Je, mnaiumba nyinyi, au ni Sisi ndio Waumbaji?

نَحۡنُ قَدَّرۡنَا بَيۡنَكُمُ ٱلۡمَوۡتَ وَمَا نَحۡنُ بِمَسۡبُوقِينَ

Sisi tumekuwekeeni mauti; na wala Sisi hatushindwi.

Sisi tumekuwekeeni mauti; na wala Sisi hatushindwi.

عَلَىٰٓ أَن نُّبَدِّلَ أَمۡثَٰلَكُمۡ وَنُنشِئَكُمۡ فِي مَا لَا تَعۡلَمُونَ

Kuwaleta wengine badala yenu na kukuumbeni nyinyi kwa umbo msilolijua.

Kuwaleta wengine badala yenu na kukuumbeni nyinyi kwa umbo msilolijua.

وَلَقَدۡ عَلِمۡتُمُ ٱلنَّشۡأَةَ ٱلۡأُولَىٰ فَلَوۡلَا تَذَكَّرُونَ

Na bila ya shaka mlikwisha jua umbo la kwanza, basi kwa nini hamkumbuki?

Na bila ya shaka mlikwisha jua umbo la kwanza, basi kwa nini hamkumbuki?

أَفَرَءَيۡتُم مَّا تَحۡرُثُونَ

Je, mnaona hivyo mnavyovipanda?

Je, mnaona hivyo mnavyovipanda?

ءَأَنتُمۡ تَزۡرَعُونَهُۥٓ أَمۡ نَحۡنُ ٱلزَّٰرِعُونَ

Je, ni nyinyi mnayoyaotesha au ni Sisi ndio wenye kuotesha?

Je, ni nyinyi mnayoyaotesha au ni Sisi ndio wenye kuotesha?

لَوۡ نَشَآءُ لَجَعَلۡنَٰهُ حُطَٰمٗا فَظَلۡتُمۡ تَفَكَّهُونَ

Tungelitaka, tungeliyafanya yakawa mapepe, mkabaki mnastaajabu.

Tungelitaka, tungeliyafanya yakawa mapepe, mkabaki mnastaajabu.

إِنَّا لَمُغۡرَمُونَ

Mkisema: 'Hakika sisi tumegharimika.'

Mkisema: 'Hakika sisi tumegharimika.'

بَلۡ نَحۡنُ مَحۡرُومُونَ

Bali sisi tumenyimwa.

Bali sisi tumenyimwa.

أَفَرَءَيۡتُمُ ٱلۡمَآءَ ٱلَّذِي تَشۡرَبُونَ

Je, mnayaona maji mnayoyanywa?

Je, mnayaona maji mnayoyanywa?

ءَأَنتُمۡ أَنزَلۡتُمُوهُ مِنَ ٱلۡمُزۡنِ أَمۡ نَحۡنُ ٱلۡمُنزِلُونَ

Je, ni nyinyi mnaoyateremsha kutoka mawinguni au ni Sisi ndio wenye kuyateremsha?

Je, ni nyinyi mnaoyateremsha kutoka mawinguni au ni Sisi ndio wenye kuyateremsha?

لَوۡ نَشَآءُ جَعَلۡنَٰهُ أُجَاجٗا فَلَوۡلَا تَشۡكُرُونَ

Tungelipenda, tungeliyafanya ya chumvi. Basi mbona hamshukuru?

Tungelipenda, tungeliyafanya ya chumvi. Basi mbona hamshukuru?

أَفَرَءَيۡتُمُ ٱلنَّارَ ٱلَّتِي تُورُونَ

Je, mnauona moto mnaouwasha?

Je, mnauona moto mnaouwasha?

ءَأَنتُمۡ أَنشَأۡتُمۡ شَجَرَتَهَآ أَمۡ نَحۡنُ ٱلۡمُنشِـُٔونَ

Ni nyinyi mliouumba mti wake au Sisi ndio Waumbaji?

Ni nyinyi mliouumba mti wake au Sisi ndio Waumbaji?

نَحۡنُ جَعَلۡنَٰهَا تَذۡكِرَةٗ وَمَتَٰعٗا لِّلۡمُقۡوِينَ

Sisi tumeufanya uwe ni ukumbusho na manufaa kwa walioko nyikani.

Sisi tumeufanya uwe ni ukumbusho na manufaa kwa walioko nyikani.

فَسَبِّحۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلۡعَظِيمِ

Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkuu.

Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkuu.

۞ فَلَآ أُقۡسِمُ بِمَوَٰقِعِ ٱلنُّجُومِ

Basi ninaapa kwa maanguko ya nyota.

Basi ninaapa kwa maanguko ya nyota.

وَإِنَّهُۥ لَقَسَمٞ لَّوۡ تَعۡلَمُونَ عَظِيمٌ

Na hakika bila ya shaka hiki ni kiapo kikubwa, laiti mngelijua!

Na hakika bila ya shaka hiki ni kiapo kikubwa, laiti mngelijua!

إِنَّهُۥ لَقُرۡءَانٞ كَرِيمٞ

Hakika hii bila ya shaka ni Qur-ani Tukufu.

Hakika hii bila ya shaka ni Qur-ani Tukufu.

فِي كِتَٰبٖ مَّكۡنُونٖ

Katika Kitabu kilichohifadhiwa.

Katika Kitabu kilichohifadhiwa.

لَّا يَمَسُّهُۥٓ إِلَّا ٱلۡمُطَهَّرُونَ

Hapana akigusaye ila waliotakaswa.

Hapana akigusaye ila waliotakaswa.

تَنزِيلٞ مِّن رَّبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Ni uteremsho unaotoka kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Ni uteremsho unaotoka kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

أَفَبِهَٰذَا ٱلۡحَدِيثِ أَنتُم مُّدۡهِنُونَ

Ni maneno haya ndiyo nyinyi mnayapuuza?

Ni maneno haya ndiyo nyinyi mnayapuuza?

وَتَجۡعَلُونَ رِزۡقَكُمۡ أَنَّكُمۡ تُكَذِّبُونَ

Na badala ya kushukuru kwa riziki yenu mnafanya kuwa mnakadhibisha?

Na badala ya kushukuru kwa riziki yenu mnafanya kuwa mnakadhibisha?

فَلَوۡلَآ إِذَا بَلَغَتِ ٱلۡحُلۡقُومَ

Yawaje basi itakapofika roho kwenye koo.

Yawaje basi itakapofika roho kwenye koo.

وَأَنتُمۡ حِينَئِذٖ تَنظُرُونَ

Na nyinyi wakati huo mnatazama!

Na nyinyi wakati huo mnatazama!

وَنَحۡنُ أَقۡرَبُ إِلَيۡهِ مِنكُمۡ وَلَٰكِن لَّا تُبۡصِرُونَ

Na Sisi tuko karibu zaidi naye kuliko nyinyi, lakini hamuoni.

Na Sisi tuko karibu zaidi naye kuliko nyinyi, lakini hamuoni.

فَلَوۡلَآ إِن كُنتُمۡ غَيۡرَ مَدِينِينَ

Na lau kuwa nyinyi hamtalipwa.

Na lau kuwa nyinyi hamtalipwa.

تَرۡجِعُونَهَآ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ

Kwa nini hamuirudishi hiyo roho, ikiwa nyinyi mnasema kweli?

Kwa nini hamuirudishi hiyo roho, ikiwa nyinyi mnasema kweli?

فَأَمَّآ إِن كَانَ مِنَ ٱلۡمُقَرَّبِينَ

Kwa hivyo, akiwa miongoni mwa wale walio karibu na Mwenyezi Mungu.

Kwa hivyo, akiwa miongoni mwa wale walio karibu na Mwenyezi Mungu.

فَرَوۡحٞ وَرَيۡحَانٞ وَجَنَّتُ نَعِيمٖ

Basi ni raha, na manukato, na Bustani zenye neema.

Basi ni raha, na manukato, na Bustani zenye neema.

وَأَمَّآ إِن كَانَ مِنۡ أَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ

Na akiwa katika wale wa upande wa kulia.

Na akiwa katika wale wa upande wa kulia.

فَسَلَٰمٞ لَّكَ مِنۡ أَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ

Basi ni Salamu kwako uliye miongoni mwa wale wa upande wa kulia.

Basi ni Salamu kwako uliye miongoni mwa wale wa upande wa kulia.

وَأَمَّآ إِن كَانَ مِنَ ٱلۡمُكَذِّبِينَ ٱلضَّآلِّينَ

Na ama akiwa katika wale waliokadhibisha, wapotovu.

Na ama akiwa katika wale waliokadhibisha, wapotovu.

فَنُزُلٞ مِّنۡ حَمِيمٖ

Basi karamu ya makaribisho yake ni maji yanayochemka.

Basi karamu ya makaribisho yake ni maji yanayochemka.

وَتَصۡلِيَةُ جَحِيمٍ

Na kutiwa Motoni.

Na kutiwa Motoni.

إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ حَقُّ ٱلۡيَقِينِ

Hakika hii ndiyo haki yenye yakini.

Hakika hii ndiyo haki yenye yakini.

فَسَبِّحۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلۡعَظِيمِ

Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkuu.

Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkuu.
Footer Include