斯瓦希里语翻译 - 拉瓦德翻译中心。
《古兰经》含义翻译
由拉瓦德翻译中心团队与拉布瓦 الدعوة协会和伊斯兰内容服务协会合作翻译。
وَٱلۡعَٰدِيَٰتِ ضَبۡحٗا
Ninaapa kwa farasi waendao mbio wakipumua.
فَٱلۡمُورِيَٰتِ قَدۡحٗا
Na wakitoa moto kwa kupiga kwato zao chini.
فَٱلۡمُغِيرَٰتِ صُبۡحٗا
Wakishambulia wakati wa asubuhi.
فَأَثَرۡنَ بِهِۦ نَقۡعٗا
Huku wakitimua vumbi.
فَوَسَطۡنَ بِهِۦ جَمۡعًا
Na wakijitoma kati ya kundi.
إِنَّ ٱلۡإِنسَٰنَ لِرَبِّهِۦ لَكَنُودٞ
Hakika mwanadamu ni mtovu wa fadhila kwa Mola wake Mlezi!
وَإِنَّهُۥ عَلَىٰ ذَٰلِكَ لَشَهِيدٞ
Na hakika yeye mwenyewe bila ya shaka ni shahidi wa hayo!
وَإِنَّهُۥ لِحُبِّ ٱلۡخَيۡرِ لَشَدِيدٌ
Naye hakika bila ya shaka ana nguvu za kupenda mali!
۞ أَفَلَا يَعۡلَمُ إِذَا بُعۡثِرَ مَا فِي ٱلۡقُبُورِ
Kwani hajui watakapofufuliwa waliomo makaburini?
وَحُصِّلَ مَا فِي ٱلصُّدُورِ
Na yakakusanywa yaliyomo vifuani?
إِنَّ رَبَّهُم بِهِمۡ يَوۡمَئِذٖ لَّخَبِيرُۢ
Hakika Mola wao Mlezi siku hiyo bila ya shaka atakuwa na habari zao wote!
share_via