Header Include

የስዋሂሊ ትርጉም - ሩዋድ የትርጉም ማዕከል

ሩዋድ የትርጉም ማዕከል ከ ረብዋ የዳዕዋ ማህበር እና ከ የእስልምና ይዘት በተለያዩ ቋንቋዎች አገልግሎት ማህበር ጋር በመተባበር የተተረጎመ

QR Code https://quran.islamcontent.com/am/swahili_rwwad

وَٱلنَّجۡمِ إِذَا هَوَىٰ

Ninaapa kwa nyota inapotua.

Ninaapa kwa nyota inapotua.

مَا ضَلَّ صَاحِبُكُمۡ وَمَا غَوَىٰ

Mwenzenu huyu hakupotea, wala hakukosea.

Mwenzenu huyu hakupotea, wala hakukosea.

وَمَا يَنطِقُ عَنِ ٱلۡهَوَىٰٓ

Wala hatamki kwa matamanio.

Wala hatamki kwa matamanio.

إِنۡ هُوَ إِلَّا وَحۡيٞ يُوحَىٰ

Hayakuwa haya ila ni ufunuo uliofunuliwa.

Hayakuwa haya ila ni ufunuo uliofunuliwa.

عَلَّمَهُۥ شَدِيدُ ٱلۡقُوَىٰ

Amemfundisha aliye Mwingi wa nguvu.

Amemfundisha aliye Mwingi wa nguvu.

ذُو مِرَّةٖ فَٱسۡتَوَىٰ

Mwenye kutua, akatulia.

Mwenye kutua, akatulia.

وَهُوَ بِٱلۡأُفُقِ ٱلۡأَعۡلَىٰ

Naye yuko juu kabisa upeo wa macho.

Naye yuko juu kabisa upeo wa macho.

ثُمَّ دَنَا فَتَدَلَّىٰ

Kisha akakaribia na akateremka.

Kisha akakaribia na akateremka.

فَكَانَ قَابَ قَوۡسَيۡنِ أَوۡ أَدۡنَىٰ

Akawa ni kama baina ya mipinde miwili, au karibu zaidi.

Akawa ni kama baina ya mipinde miwili, au karibu zaidi.

فَأَوۡحَىٰٓ إِلَىٰ عَبۡدِهِۦ مَآ أَوۡحَىٰ

Akamfunulia mja wake (Mwenyezi Mungu) alichomfunulia.

Akamfunulia mja wake (Mwenyezi Mungu) alichomfunulia.

مَا كَذَبَ ٱلۡفُؤَادُ مَا رَأَىٰٓ

Ufahamu wa moyo wake haukukanusha uliyoyaona.

Ufahamu wa moyo wake haukukanusha uliyoyaona.

أَفَتُمَٰرُونَهُۥ عَلَىٰ مَا يَرَىٰ

Je, mnabishana naye kwa aliyoyaona?

Je, mnabishana naye kwa aliyoyaona?

وَلَقَدۡ رَءَاهُ نَزۡلَةً أُخۡرَىٰ

Na akamwona mara nyingine.

Na akamwona mara nyingine.

عِندَ سِدۡرَةِ ٱلۡمُنتَهَىٰ

Penye Mkunazi wa mwisho.

Penye Mkunazi wa mwisho.

عِندَهَا جَنَّةُ ٱلۡمَأۡوَىٰٓ

Karibu yake ndiyo ipo Bustani ya mbinguni inayokaliwa.

Karibu yake ndiyo ipo Bustani ya mbinguni inayokaliwa.

إِذۡ يَغۡشَى ٱلسِّدۡرَةَ مَا يَغۡشَىٰ

Kilipoufunika huo Mkunazi hicho kilichoufunika.

Kilipoufunika huo Mkunazi hicho kilichoufunika.

مَا زَاغَ ٱلۡبَصَرُ وَمَا طَغَىٰ

Jicho halikuhangaika wala halikuruka mpaka.

Jicho halikuhangaika wala halikuruka mpaka.

لَقَدۡ رَأَىٰ مِنۡ ءَايَٰتِ رَبِّهِ ٱلۡكُبۡرَىٰٓ

Kwa yakini aliona katika Ishara kubwa kabisa za Mola wake Mlezi.

Kwa yakini aliona katika Ishara kubwa kabisa za Mola wake Mlezi.

أَفَرَءَيۡتُمُ ٱللَّٰتَ وَٱلۡعُزَّىٰ

Je, mmemuona Lata na Uzza?

Je, mmemuona Lata na Uzza?

وَمَنَوٰةَ ٱلثَّالِثَةَ ٱلۡأُخۡرَىٰٓ

Na Manaat, mwingine wa tatu?

Na Manaat, mwingine wa tatu?

أَلَكُمُ ٱلذَّكَرُ وَلَهُ ٱلۡأُنثَىٰ

Je, nyinyi mnao wana wanaume na Yeye ndio awe na wanawake?

Je, nyinyi mnao wana wanaume na Yeye ndio awe na wanawake?

تِلۡكَ إِذٗا قِسۡمَةٞ ضِيزَىٰٓ

Huo ni mgawanyo wa dhuluma!

Huo ni mgawanyo wa dhuluma!

إِنۡ هِيَ إِلَّآ أَسۡمَآءٞ سَمَّيۡتُمُوهَآ أَنتُمۡ وَءَابَآؤُكُم مَّآ أَنزَلَ ٱللَّهُ بِهَا مِن سُلۡطَٰنٍۚ إِن يَتَّبِعُونَ إِلَّا ٱلظَّنَّ وَمَا تَهۡوَى ٱلۡأَنفُسُۖ وَلَقَدۡ جَآءَهُم مِّن رَّبِّهِمُ ٱلۡهُدَىٰٓ

Hayo hayakuwa ila ni majina mliyowapa nyinyi na baba zenu. Mwenyezi Mungu hakuleta uthibitisho wowote juu ya hayo. Hawafuati ila dhana tu na kipendacho nafsi. Na kwa yakini uongofu ulikwisha wafikia kutoka kwa Mola wao Mlezi.

Hayo hayakuwa ila ni majina mliyowapa nyinyi na baba zenu. Mwenyezi Mungu hakuleta uthibitisho wowote juu ya hayo. Hawafuati ila dhana tu na kipendacho nafsi. Na kwa yakini uongofu ulikwisha wafikia kutoka kwa Mola wao Mlezi.

أَمۡ لِلۡإِنسَٰنِ مَا تَمَنَّىٰ

Ati mtu anakipata kila anachokitamani?

Ati mtu anakipata kila anachokitamani?

فَلِلَّهِ ٱلۡأٓخِرَةُ وَٱلۡأُولَىٰ

Mwenyezi Mungu tu ndiye Mwenye Akhera na dunia.

Mwenyezi Mungu tu ndiye Mwenye Akhera na dunia.

۞ وَكَم مِّن مَّلَكٖ فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ لَا تُغۡنِي شَفَٰعَتُهُمۡ شَيۡـًٔا إِلَّا مِنۢ بَعۡدِ أَن يَأۡذَنَ ٱللَّهُ لِمَن يَشَآءُ وَيَرۡضَىٰٓ

Na wako Malaika wangapi mbinguni, ambao uombezi wao hautafaa chochote isipokuwa baada ya Mwenyezi Mungu kutoa idhini kwa amtakaye na kumridhia.

Na wako Malaika wangapi mbinguni, ambao uombezi wao hautafaa chochote isipokuwa baada ya Mwenyezi Mungu kutoa idhini kwa amtakaye na kumridhia.

إِنَّ ٱلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ بِٱلۡأٓخِرَةِ لَيُسَمُّونَ ٱلۡمَلَٰٓئِكَةَ تَسۡمِيَةَ ٱلۡأُنثَىٰ

Hakika wale wasioamini Akhera bila ya shaka wao ndio wanawaita Malaika kwa majina ya kike.

Hakika wale wasioamini Akhera bila ya shaka wao ndio wanawaita Malaika kwa majina ya kike.

وَمَا لَهُم بِهِۦ مِنۡ عِلۡمٍۖ إِن يَتَّبِعُونَ إِلَّا ٱلظَّنَّۖ وَإِنَّ ٱلظَّنَّ لَا يُغۡنِي مِنَ ٱلۡحَقِّ شَيۡـٔٗا

Nao hawana elimu yoyote kwa hayo isipokuwa wanafuata dhana tu. Na dhana haisaidii chochote mbele ya haki.

Nao hawana elimu yoyote kwa hayo isipokuwa wanafuata dhana tu. Na dhana haisaidii chochote mbele ya haki.

فَأَعۡرِضۡ عَن مَّن تَوَلَّىٰ عَن ذِكۡرِنَا وَلَمۡ يُرِدۡ إِلَّا ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا

Basi mwachilie mbali anayeupa kisogo ukumbusho wetu, na wala hataki ila maisha ya dunia.

Basi mwachilie mbali anayeupa kisogo ukumbusho wetu, na wala hataki ila maisha ya dunia.

ذَٰلِكَ مَبۡلَغُهُم مِّنَ ٱلۡعِلۡمِۚ إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعۡلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِۦ وَهُوَ أَعۡلَمُ بِمَنِ ٱهۡتَدَىٰ

Huo ndio mwisho wao wa elimu. Hakika Mola wako Mlezi ndiye anayemjua zaidi mwenye kuipotea njia yake, na Yeye ndiye anayemjua zaidi mwenye kuongoka.

Huo ndio mwisho wao wa elimu. Hakika Mola wako Mlezi ndiye anayemjua zaidi mwenye kuipotea njia yake, na Yeye ndiye anayemjua zaidi mwenye kuongoka.

وَلِلَّهِ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِ لِيَجۡزِيَ ٱلَّذِينَ أَسَٰٓـُٔواْ بِمَا عَمِلُواْ وَيَجۡزِيَ ٱلَّذِينَ أَحۡسَنُواْ بِٱلۡحُسۡنَى

Ni vya Mwenyezi Mungu vyote vilivyo mbinguni na vilivyo katika ardhi, ili awalipe wale waliotenda ubaya kwa waliyoyatenda, na wale waliotenda mema awalipe mema.

Ni vya Mwenyezi Mungu vyote vilivyo mbinguni na vilivyo katika ardhi, ili awalipe wale waliotenda ubaya kwa waliyoyatenda, na wale waliotenda mema awalipe mema.

ٱلَّذِينَ يَجۡتَنِبُونَ كَبَٰٓئِرَ ٱلۡإِثۡمِ وَٱلۡفَوَٰحِشَ إِلَّا ٱللَّمَمَۚ إِنَّ رَبَّكَ وَٰسِعُ ٱلۡمَغۡفِرَةِۚ هُوَ أَعۡلَمُ بِكُمۡ إِذۡ أَنشَأَكُم مِّنَ ٱلۡأَرۡضِ وَإِذۡ أَنتُمۡ أَجِنَّةٞ فِي بُطُونِ أُمَّهَٰتِكُمۡۖ فَلَا تُزَكُّوٓاْ أَنفُسَكُمۡۖ هُوَ أَعۡلَمُ بِمَنِ ٱتَّقَىٰٓ

Ambao wanajiweka mbali na madhambi makuu na vitendo vichafu, isipokuwa makosa hafifu. Hakika Mola wako Mlezi ni Mkunjufu wa maghfira, naye anakujueni sana tangu alipokuumbeni kutoka kwenye ardhi, na mlipokuwa mimba matumboni mwa mama zenu. Basi msijione watakatifu. Yeye anamjua sana mwenye kujikinga akawa mbali na maovu.

Ambao wanajiweka mbali na madhambi makuu na vitendo vichafu, isipokuwa makosa hafifu. Hakika Mola wako Mlezi ni Mkunjufu wa maghfira, naye anakujueni sana tangu alipokuumbeni kutoka kwenye ardhi, na mlipokuwa mimba matumboni mwa mama zenu. Basi msijione watakatifu. Yeye anamjua sana mwenye kujikinga akawa mbali na maovu.

أَفَرَءَيۡتَ ٱلَّذِي تَوَلَّىٰ

Je, umemwona yule aliyegeuka akaenda zake?

Je, umemwona yule aliyegeuka akaenda zake?

وَأَعۡطَىٰ قَلِيلٗا وَأَكۡدَىٰٓ

Na akapeana kidogo, kisha akajizuia?

Na akapeana kidogo, kisha akajizuia?

أَعِندَهُۥ عِلۡمُ ٱلۡغَيۡبِ فَهُوَ يَرَىٰٓ

Je, anayo huyo elimu ya ghaibu, basi ndiyo anaona?

Je, anayo huyo elimu ya ghaibu, basi ndiyo anaona?

أَمۡ لَمۡ يُنَبَّأۡ بِمَا فِي صُحُفِ مُوسَىٰ

Au hakuambiwa yaliyomo katika Vitabu vya Musa?

Au hakuambiwa yaliyomo katika Vitabu vya Musa?

وَإِبۡرَٰهِيمَ ٱلَّذِي وَفَّىٰٓ

Na vya Ibrahimu aliyetimiza ahadi?

Na vya Ibrahimu aliyetimiza ahadi?

أَلَّا تَزِرُ وَازِرَةٞ وِزۡرَ أُخۡرَىٰ

Ya kwamba hakika nafsi iliyobeba madhambi haibebi madhambi ya mwengine?

Ya kwamba hakika nafsi iliyobeba madhambi haibebi madhambi ya mwengine?

وَأَن لَّيۡسَ لِلۡإِنسَٰنِ إِلَّا مَا سَعَىٰ

Na ya kwamba hatapata mtu ila aliyoyafanya mwenyewe?

Na ya kwamba hatapata mtu ila aliyoyafanya mwenyewe?

وَأَنَّ سَعۡيَهُۥ سَوۡفَ يُرَىٰ

Na kwamba vitendo vyake vitaonekana?

Na kwamba vitendo vyake vitaonekana?

ثُمَّ يُجۡزَىٰهُ ٱلۡجَزَآءَ ٱلۡأَوۡفَىٰ

Kisha ndio atalipwa malipo yake kwa hayo kwa ukamilifu.

Kisha ndio atalipwa malipo yake kwa hayo kwa ukamilifu.

وَأَنَّ إِلَىٰ رَبِّكَ ٱلۡمُنتَهَىٰ

Na kwamba kwa Mola wako Mlezi ndiyo mwisho.

Na kwamba kwa Mola wako Mlezi ndiyo mwisho.

وَأَنَّهُۥ هُوَ أَضۡحَكَ وَأَبۡكَىٰ

Na kwamba Yeye ndiye anayeleta kicheko na kilio.

Na kwamba Yeye ndiye anayeleta kicheko na kilio.

وَأَنَّهُۥ هُوَ أَمَاتَ وَأَحۡيَا

Na kwamba Yeye ndiye anayefisha na kuhuisha.

Na kwamba Yeye ndiye anayefisha na kuhuisha.

وَأَنَّهُۥ خَلَقَ ٱلزَّوۡجَيۡنِ ٱلذَّكَرَ وَٱلۡأُنثَىٰ

Na kwamba Yeye ndiye aliyeumba jozi, dume na jike.

Na kwamba Yeye ndiye aliyeumba jozi, dume na jike.

مِن نُّطۡفَةٍ إِذَا تُمۡنَىٰ

Kutokana na mbegu ya uzazi inapomiminwa.

Kutokana na mbegu ya uzazi inapomiminwa.

وَأَنَّ عَلَيۡهِ ٱلنَّشۡأَةَ ٱلۡأُخۡرَىٰ

Na kwamba ni juu yake ufufuo mwengine.

Na kwamba ni juu yake ufufuo mwengine.

وَأَنَّهُۥ هُوَ أَغۡنَىٰ وَأَقۡنَىٰ

Na kwamba ni Yeye ndiye anayetosheleza na kukinaisha.

Na kwamba ni Yeye ndiye anayetosheleza na kukinaisha.

وَأَنَّهُۥ هُوَ رَبُّ ٱلشِّعۡرَىٰ

Na kwamba hakika Yeye ndiye Mola Mlezi wa nyota ya Shii'ra.

Na kwamba hakika Yeye ndiye Mola Mlezi wa nyota ya Shii'ra.

وَأَنَّهُۥٓ أَهۡلَكَ عَادًا ٱلۡأُولَىٰ

Na kwamba Yeye ndiye aliyewaangamiza 'Adi wa kwanza.

Na kwamba Yeye ndiye aliyewaangamiza 'Adi wa kwanza.

وَثَمُودَاْ فَمَآ أَبۡقَىٰ

Na Thamudi hakuwabakisha.

Na Thamudi hakuwabakisha.

وَقَوۡمَ نُوحٖ مِّن قَبۡلُۖ إِنَّهُمۡ كَانُواْ هُمۡ أَظۡلَمَ وَأَطۡغَىٰ

Na kabla yao kaumu ya Nuhu. Na hao hakika walikuwa ni madhalimu zaidi, na waovu zaidi.

Na kabla yao kaumu ya Nuhu. Na hao hakika walikuwa ni madhalimu zaidi, na waovu zaidi.

وَٱلۡمُؤۡتَفِكَةَ أَهۡوَىٰ

Na miji iliyopinduliwa, ni Yeye aliyeipindua.

Na miji iliyopinduliwa, ni Yeye aliyeipindua.

فَغَشَّىٰهَا مَا غَشَّىٰ

Vikaifunika vilivyofunika.

Vikaifunika vilivyofunika.

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكَ تَتَمَارَىٰ

Basi neema gani ya Mola wako Mlezi unayoifanyia shaka?

Basi neema gani ya Mola wako Mlezi unayoifanyia shaka?

هَٰذَا نَذِيرٞ مِّنَ ٱلنُّذُرِ ٱلۡأُولَىٰٓ

Hili ni onyo katika maonyo yale yale ya zamani.

Hili ni onyo katika maonyo yale yale ya zamani.

أَزِفَتِ ٱلۡأٓزِفَةُ

Kiyama kimekaribia!

Kiyama kimekaribia!

لَيۡسَ لَهَا مِن دُونِ ٱللَّهِ كَاشِفَةٌ

Hapana wa kukifichua isipokuwa Mwenyezi Mungu.

Hapana wa kukifichua isipokuwa Mwenyezi Mungu.

أَفَمِنۡ هَٰذَا ٱلۡحَدِيثِ تَعۡجَبُونَ

Je, mnayastaajabia maneno haya?

Je, mnayastaajabia maneno haya?

وَتَضۡحَكُونَ وَلَا تَبۡكُونَ

Na mnacheka, wala hamlii?

Na mnacheka, wala hamlii?

وَأَنتُمۡ سَٰمِدُونَ

Nanyi mmeghafilika?

Nanyi mmeghafilika?

فَٱسۡجُدُواْۤ لِلَّهِۤ وَٱعۡبُدُواْ۩

Basi msujudieni Mwenyezi Mungu, na mumuabudu.

Basi msujudieni Mwenyezi Mungu, na mumuabudu.
Footer Include