Header Include

ترجمهٔ سواحلی ـ علی محسن البروانی

ترجمهٔ معانی قرآن کریم به زبان سواحلی ـ ترجمهٔ علی محسن البروانی.

QR Code https://quran.islamcontent.com/fa/swahili_barawani

ٱلۡحَآقَّةُ

Tukio la haki.

Kiyama ni Tukio litakalo tukia kwa haki, yaani kwa kweli.
Tukio la haki.

مَا ٱلۡحَآقَّةُ

Nini hilo Tukio la haki?

Nini hicho Kiyama kitacho tokea kweli?
Nini hilo Tukio la haki?

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡحَآقَّةُ

Na nini kitakujuulisha nini hilo Tukio la haki?

Na kitu gani kitacho kujuvya ukweli wake, na kitacho kupa sura ya kitisho chake na shida zake?
Na nini kitakujuulisha nini hilo Tukio la haki?

كَذَّبَتۡ ثَمُودُ وَعَادُۢ بِٱلۡقَارِعَةِ

Thamudi na A'di waliukadhibisha Msiba unao situsha.

Kina Thamudi na kina A'di walikanusha Kiyama kinacho wagutua walimwengu wote kwa kitisho chake na shida zake.
Thamudi na A'di waliukadhibisha Msiba unao situsha.

فَأَمَّا ثَمُودُ فَأُهۡلِكُواْ بِٱلطَّاغِيَةِ

Basi Thamudi waliangamizwa kwa balaa kubwa mno.

Ama Thamudi basi walihilikiwa kwa tukio lilio pindukia mipaka yote kwa ukali wake.
Basi Thamudi waliangamizwa kwa balaa kubwa mno.

وَأَمَّا عَادٞ فَأُهۡلِكُواْ بِرِيحٖ صَرۡصَرٍ عَاتِيَةٖ

Na ama A'di waliangamizwa kwa upepo mkali usio zuilika.

Na ama A'di waliangamizwa kwa upepo ubaridi na mkali,
Na ama A'di waliangamizwa kwa upepo mkali usio zuilika.

سَخَّرَهَا عَلَيۡهِمۡ سَبۡعَ لَيَالٖ وَثَمَٰنِيَةَ أَيَّامٍ حُسُومٗاۖ فَتَرَى ٱلۡقَوۡمَ فِيهَا صَرۡعَىٰ كَأَنَّهُمۡ أَعۡجَازُ نَخۡلٍ خَاوِيَةٖ

Alio wapelekea masiku saba, na siku nane, mfululizo bila ya kusita. Utaona watu wamepinduka kama kwamba ni magongo ya mitende yalio wazi ndani.

Mwenyezi Mungu aliwasalitisha nao muda wa masiku saba, na siku nane zilizo fuatana mfululizo, utaona walio patikana na upepo huo wamekuwa maiti kama magogo ya mitende yaliyo kuwa matupu ndani yake. ("Masiku" ni wingi wa "Usiku"; "Siku" wingi wake ni "Siku" vile vile.)
Alio wapelekea masiku saba, na siku nane, mfululizo bila ya kusita. Utaona watu wamepinduka kama kwamba ni magongo ya mitende yalio wazi ndani.

فَهَلۡ تَرَىٰ لَهُم مِّنۢ بَاقِيَةٖ

Basi je! Unamwona mmoja wao aliye baki?

Je! Unamwona yeyote aliye bakia katika hao?
Basi je! Unamwona mmoja wao aliye baki?

وَجَآءَ فِرۡعَوۡنُ وَمَن قَبۡلَهُۥ وَٱلۡمُؤۡتَفِكَٰتُ بِٱلۡخَاطِئَةِ

Na Firauni na walio mtangulia, na miji iliyo pinduliwa chini juu, walileta khatia.

Akaja Firauni, na mataifa mengine yaliyo kufuru kabla yake, na wale jamaa walio acha mwendo wa haki na vitendo vya maumbile wakafanya vitendo vichafu kabisa hata miji yao ikapinduliwa juu chini.
Na Firauni na walio mtangulia, na miji iliyo pinduliwa chini juu, walileta khatia.

فَعَصَوۡاْ رَسُولَ رَبِّهِمۡ فَأَخَذَهُمۡ أَخۡذَةٗ رَّابِيَةً

Wakamuasi Mtume wa Mola wao Mlezi, ndipo Yeye Mola akawakamata kwa mkamato ulio zidi nguvu.

Kila umma katika hawa walimuasi Mtume wa Mola wao Mlezi. Naye Mwenyezi Mungu akawashika kwa kuwaadhibu kwa mshiko ulio zidi ukali.
Wakamuasi Mtume wa Mola wao Mlezi, ndipo Yeye Mola akawakamata kwa mkamato ulio zidi nguvu.

إِنَّا لَمَّا طَغَا ٱلۡمَآءُ حَمَلۡنَٰكُمۡ فِي ٱلۡجَارِيَةِ

Maji yalipo furika Sisi tulikupandisheni katika safina,

Maji yalipo zidi ukomo wake, na yakapanda juu ya milima katika tukio la tofani ya Nuhu, Sisi tulikupandisheni, yaani kwa kuwapandisha wazee wenu wa asli, katika safina inayo kwenda baharini.
Maji yalipo furika Sisi tulikupandisheni katika safina,

لِنَجۡعَلَهَا لَكُمۡ تَذۡكِرَةٗ وَتَعِيَهَآ أُذُنٞ وَٰعِيَةٞ

Ili tuyafanye hayo kuwa ni waadhi kwenu na kila sikio linalo sikia liyahifadhi.

Ili kulifanya tukio hilo la kuwaokoa Waumini na kuwazamisha makafiri liwe zingatio na mawaidha kwenu, na lihifadhiwe na kila sikio lenye kuhifadhi linalo sikia.
Ili tuyafanye hayo kuwa ni waadhi kwenu na kila sikio linalo sikia liyahifadhi.

فَإِذَا نُفِخَ فِي ٱلصُّورِ نَفۡخَةٞ وَٰحِدَةٞ

. Na litapo pulizwa barugumu mpulizo mmoja tu,

Litakapo pulizwa barugumu kwa mpulizo mmoja,
. Na litapo pulizwa barugumu mpulizo mmoja tu,

وَحُمِلَتِ ٱلۡأَرۡضُ وَٱلۡجِبَالُ فَدُكَّتَا دَكَّةٗ وَٰحِدَةٗ

Na ardhi na milima ikaondolewa, na ikavunjwa kwa mvunjo mmoja,

Na ardhi na milima ikaondolewa pahala ilipo, na ikavunjwa mara moja,
Na ardhi na milima ikaondolewa, na ikavunjwa kwa mvunjo mmoja,

فَيَوۡمَئِذٖ وَقَعَتِ ٱلۡوَاقِعَةُ

Siku hiyo ndio Tukio litatukia.

Siku hiyo ndiyo kitashuka cha kushuka,
Siku hiyo ndio Tukio litatukia.

وَٱنشَقَّتِ ٱلسَّمَآءُ فَهِيَ يَوۡمَئِذٖ وَاهِيَةٞ

Na mbingu zitapasuka, kwani siku hiyo zitakuwa dhaifu kabisa.

Na mbingu zitapasuka kwa kuondoka hukumu zake na sharia zake, kwani siku hiyo zitakuwa dhaifu baada ya kuwa madhubuti zenye nguvu.
Na mbingu zitapasuka, kwani siku hiyo zitakuwa dhaifu kabisa.

وَٱلۡمَلَكُ عَلَىٰٓ أَرۡجَآئِهَاۚ وَيَحۡمِلُ عَرۡشَ رَبِّكَ فَوۡقَهُمۡ يَوۡمَئِذٖ ثَمَٰنِيَةٞ

Na Malaika watakuwa pembezoni mwa mbingu; na wanane juu ya hawa watakuwa wamebeba Kiti cha Enzi cha Mola wako Mlezi.

Na Malaika pembezoni mwake, na wapo Malaika wanane siku hiyo watakao beba Kiti cha Enzi cha Mola wako Mlezi, juu ya Malaika hawa wengine.
Na Malaika watakuwa pembezoni mwa mbingu; na wanane juu ya hawa watakuwa wamebeba Kiti cha Enzi cha Mola wako Mlezi.

يَوۡمَئِذٖ تُعۡرَضُونَ لَا تَخۡفَىٰ مِنكُمۡ خَافِيَةٞ

Siku hiyo mtahudhurishwa - haitafichika siri yoyote yenu.

Siku hiyo ndio mtaletwa kwa ajili ya kuhisabiwa. Wala haifichikani siri yenu yoyote mliyo kuwa mkiificha.
Siku hiyo mtahudhurishwa - haitafichika siri yoyote yenu.

فَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ بِيَمِينِهِۦ فَيَقُولُ هَآؤُمُ ٱقۡرَءُواْ كِتَٰبِيَهۡ

Basi ama atakaye pewa kitabu chake kwa mkono wake wa kulia, atasema: Haya someni kitabu changu!

Ama mwenye kupewa kitabu chake kwa mkono wake wa kulia, atasema akiwatangazia furaha yake walio karibu naye: Chukueni msome kitabu changu!
Basi ama atakaye pewa kitabu chake kwa mkono wake wa kulia, atasema: Haya someni kitabu changu!

إِنِّي ظَنَنتُ أَنِّي مُلَٰقٍ حِسَابِيَهۡ

Hakika nalijua ya kuwa nitapokea hisabu yangu.

Mimi nilikuwa na yakini tangu duniani kuwa nitapata hisabu yangu, basi nikajitayarisha nafsi yangu kwa mkutano huu.
Hakika nalijua ya kuwa nitapokea hisabu yangu.

فَهُوَ فِي عِيشَةٖ رَّاضِيَةٖ

Basi yeye atakuwa katika maisha ya kupendeza,

Basi huyo atakuwa katika maisha yaliyo enea kupendeza.
Basi yeye atakuwa katika maisha ya kupendeza,

فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٖ

Katika Bustani ya juu,

Katika Bustani ya pahali na daraja ya juu.
Katika Bustani ya juu,

قُطُوفُهَا دَانِيَةٞ

Matunda yake yakaribu.

Matunda yake yakaribu kwa kuyachuma. (kuyatunda).
Matunda yake yakaribu.

كُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ هَنِيٓـَٔۢا بِمَآ أَسۡلَفۡتُمۡ فِي ٱلۡأَيَّامِ ٱلۡخَالِيَةِ

Waambiwe: Kuleni na mnywe kwa furaha kwa sababu ya mlivyo tanguliza katika siku zilizo pita.

Kuleni na mnywe kwa kula na kunywa kusio na karaha, wala maudhi, kwa sababu ya vitendo vyema mlivyo kwisha vitanguliza katika siku za duniani zilizo pita.
Waambiwe: Kuleni na mnywe kwa furaha kwa sababu ya mlivyo tanguliza katika siku zilizo pita.

وَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ بِشِمَالِهِۦ فَيَقُولُ يَٰلَيۡتَنِي لَمۡ أُوتَ كِتَٰبِيَهۡ

Na ama atakaye pewa kitabu chake katika mkono wake wa kushoto, basi yeye atasema: Laiti nisingeli pewa kitabu changu!

Ama mwenye kupewa kitabu chake kwa mkono wake wa kushoto atasema kwa majuto na huzuni: Laiti kuwa sikupewa kitabu changu,
Na ama atakaye pewa kitabu chake katika mkono wake wa kushoto, basi yeye atasema: Laiti nisingeli pewa kitabu changu!

وَلَمۡ أَدۡرِ مَا حِسَابِيَهۡ

Wala nisingeli jua nini hisabu yangu.

Wala sikuijua hisabu yangu!
Wala nisingeli jua nini hisabu yangu.

يَٰلَيۡتَهَا كَانَتِ ٱلۡقَاضِيَةَ

Laiti mauti ndiyo yangeli kuwa ya kunimaliza kabisa.

Laiti kuwa kule kufa niliko kwisha kufa kungeli kuwa ndio kumalizika kwangu kwa mwisho, wala nisingeli fufuliwa tena!
Laiti mauti ndiyo yangeli kuwa ya kunimaliza kabisa.

مَآ أَغۡنَىٰ عَنِّي مَالِيَهۡۜ

Mali yangu hayakunifaa kitu.

Hapana chochote nilicho kimiliki duniani kilicho nifaa.
Mali yangu hayakunifaa kitu.

هَلَكَ عَنِّي سُلۡطَٰنِيَهۡ

Madaraka yangu yamenipotea.

Uzima wangu umenipotea, na nguvu zangu zimenitoka.
Madaraka yangu yamenipotea.

خُذُوهُ فَغُلُّوهُ

(Pasemwe): Mshikeni! Mtieni pingu!

Wataambiwa walinzi wa Jahannamu: Mshikeni, na mfungeni mikono yake kwenye shingo yake.
(Pasemwe): Mshikeni! Mtieni pingu!

ثُمَّ ٱلۡجَحِيمَ صَلُّوهُ

Kisha mtupeni Motoni!

Kisha msimtie popote ila ndani ya Moto wa Jahannamu,
Kisha mtupeni Motoni!

ثُمَّ فِي سِلۡسِلَةٖ ذَرۡعُهَا سَبۡعُونَ ذِرَاعٗا فَٱسۡلُكُوهُ

Tena mtatizeni katika mnyororo wenye urefu wa dhiraa sabiini!

Kisha mfungeni kwenye mnyororo mrefu kabisa.
Tena mtatizeni katika mnyororo wenye urefu wa dhiraa sabiini!

إِنَّهُۥ كَانَ لَا يُؤۡمِنُ بِٱللَّهِ ٱلۡعَظِيمِ

Kwani huyo hakika alikuwa hamuamini Mwenyezi Mungu Mtukufu,

Hakika huyo alikuwa hamsadiki Mwenyezi Mungu Mtukufu,
Kwani huyo hakika alikuwa hamuamini Mwenyezi Mungu Mtukufu,

وَلَا يَحُضُّ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلۡمِسۡكِينِ

Wala hahimizi kulisha masikini.

Wala hamhimizi yoyote kuwalisha masikini.
Wala hahimizi kulisha masikini.

فَلَيۡسَ لَهُ ٱلۡيَوۡمَ هَٰهُنَا حَمِيمٞ

Basi leo hapa hana jamaa wa kumwonea uchungu,

Basi hii leo huyu kafiri hana jamaa wa kumtetea,
Basi leo hapa hana jamaa wa kumwonea uchungu,

وَلَا طَعَامٌ إِلَّا مِنۡ غِسۡلِينٖ

Wala hana chakula ila usaha wa watu wa Motoni.

Wala hana chakula ila usaha wa watu wa Motoni, ambao kwa hakika ni mchanganyiko wa damu na usaha.
Wala hana chakula ila usaha wa watu wa Motoni.

لَّا يَأۡكُلُهُۥٓ إِلَّا ٱلۡخَٰطِـُٔونَ

Chakula hicho hawakili ila wakosefu.

Hawakili chakula hicho ila wakosefu walio kusudia kufanya maasi yao, na wakakamia kuendelea nayo.
Chakula hicho hawakili ila wakosefu.

فَلَآ أُقۡسِمُ بِمَا تُبۡصِرُونَ

Basi naapa kwa mnavyo viona,

Basi naapa kwa mnavyo viona katika vinavyo onekana,
Basi naapa kwa mnavyo viona,

وَمَا لَا تُبۡصِرُونَ

Na msivyo viona,

Basi naapa kwa mnavyo viona katika vinavyo onekana, na msivyo viona katika ulimwengu wa ghaibu,
Na msivyo viona,

إِنَّهُۥ لَقَوۡلُ رَسُولٖ كَرِيمٖ

Kwa hakika hii ni kauli iliyo letwa na Mjumbe mwenye hishima.

Kwamba hakika Qur'ani bila ya shaka inatoka kwa Mwenyezi Mungu kwa ulimi wa Mjumbe mwenye cheo cha juu.
Kwa hakika hii ni kauli iliyo letwa na Mjumbe mwenye hishima.

وَمَا هُوَ بِقَوۡلِ شَاعِرٖۚ قَلِيلٗا مَّا تُؤۡمِنُونَ

Wala si kauli ya mtunga mashairi. Ni machache sana mnayo yaamini.

Wala Qur'ani si maneno ya mtunga mashairi kama mnavyo dai. Ama nyinyi ni chache mno imani yenu ya kuwa Qur'ani inatoka kwa Mwenyezi Mungu.
Wala si kauli ya mtunga mashairi. Ni machache sana mnayo yaamini.

وَلَا بِقَوۡلِ كَاهِنٖۚ قَلِيلٗا مَّا تَذَكَّرُونَ

Wala si kauli ya kuhani. Ni machache mnayo yakumbuka.

Wala Qur'ani haisemi kwa maneno ya kumunyia munyia kama wanenavyo makuhani mlio wazoea. Ni uchache mno kukumbuka kwenu na kuzingatia khitilafu zilioko baina ya Qur'ani na maneno ya makuhani.
Wala si kauli ya kuhani. Ni machache mnayo yakumbuka.

تَنزِيلٞ مِّن رَّبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Ni uteremsho utokao kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Hii ni uteremsho unao toka kwa Mwenye kuwaangalia walimwengu wote kwa kuwaumba na kuwalea.
Ni uteremsho utokao kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

وَلَوۡ تَقَوَّلَ عَلَيۡنَا بَعۡضَ ٱلۡأَقَاوِيلِ

Na lau kama angeli tuzulia baadhi ya maneno tu,

Na lau kuwa angeli dai kitu chochote ambacho tusicho kisema
Na lau kama angeli tuzulia baadhi ya maneno tu,

لَأَخَذۡنَا مِنۡهُ بِٱلۡيَمِينِ

Bila ya shaka tungeli mshika kwa mkono wa kulia,

Basi bila ya shaka tungeli mshika akitoe kama mtu anavyo mkamata mtu kwa mkono wa kulia akammaliza hapo hapo.
Bila ya shaka tungeli mshika kwa mkono wa kulia,

ثُمَّ لَقَطَعۡنَا مِنۡهُ ٱلۡوَتِينَ

Kisha kwa hakika tungeli mkata mshipa mkubwa wa moyo!

Kisha bila ya shaka tungeli mkata mshipa wake wa moyo, afe saa ile ile. (Biblia inasema katika Kumbukumbu la Torati 18.20 "Lakini nabii atakayenena neno kwa kujikinai kwa jina langu, ambalo sikumwagiza kulinena, au atakayenena katika jina la miungu mingine, nabii yule atakufa.")
Kisha kwa hakika tungeli mkata mshipa mkubwa wa moyo!

فَمَا مِنكُم مِّنۡ أَحَدٍ عَنۡهُ حَٰجِزِينَ

Na hapana yeyote katika nyinyi ambaye angeli weza kutuzuia.

Na hapana yeyote katika nyinyi, hata ange kuwa na nguvu namna gani, angeli weza kuzuia adhabu yetu isimfikilie.
Na hapana yeyote katika nyinyi ambaye angeli weza kutuzuia.

وَإِنَّهُۥ لَتَذۡكِرَةٞ لِّلۡمُتَّقِينَ

Kwa hakika hii ni mawaidha kwa wachamngu.

Na hakika Qur'ani ni mawaidha kwa wanao fuata amri za Mwenyezi Mungu, na wanaepuka makatazo yake.
Kwa hakika hii ni mawaidha kwa wachamngu.

وَإِنَّا لَنَعۡلَمُ أَنَّ مِنكُم مُّكَذِّبِينَ

Na hakika Sisi bila ya shaka tunajua kwamba miongoni mwenu wapo wanao kadhibisha.

Na hakika Sisi bila ya shaka tunajua kwamba kati yenu wapo wanao ikanusha Qur'ani.
Na hakika Sisi bila ya shaka tunajua kwamba miongoni mwenu wapo wanao kadhibisha.

وَإِنَّهُۥ لَحَسۡرَةٌ عَلَى ٱلۡكَٰفِرِينَ

Na hakika bila ya shaka itakuwa ni majuto kwa wanao kataa.

Na kwamba hakika hiyo bila ya shaka ni sababu ya majuto ya wanao ikataa, wakati watapo iona adhabu yao, na neema za wenye kusadiki.
Na hakika bila ya shaka itakuwa ni majuto kwa wanao kataa.

وَإِنَّهُۥ لَحَقُّ ٱلۡيَقِينِ

Na hakika hii bila ya shaka ni haki ya yakini.

Na hakika Qur'ani bila ya shaka ni Haki iliyo thibiti, isiyo na shaka yoyote.
Na hakika hii bila ya shaka ni haki ya yakini.

فَسَبِّحۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلۡعَظِيمِ

Basi litakase jina la Mola wako Mlezi Mtukufu.

Basi mtakase Mola wako Mlezi, na dumisha kudhukuru jina lake.
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi Mtukufu.
Footer Include