ترجمهٔ سواحلی ـ علی محسن البروانی
ترجمهٔ معانی قرآن کریم به زبان سواحلی ـ ترجمهٔ علی محسن البروانی.
إِذَا زُلۡزِلَتِ ٱلۡأَرۡضُ زِلۡزَالَهَا
Itakapo tetemeshwa ardhi kwa mtetemeko wake!
Ikitisika ardhi kwa mtikiso mkubwa, na ikasukika kwa ukomo wa kutisika na kusukika kunako mkinika na ikaweza kuchukua!
Itakapo tetemeshwa ardhi kwa mtetemeko wake!
وَأَخۡرَجَتِ ٱلۡأَرۡضُ أَثۡقَالَهَا
Na itakapo toa ardhi mizigo yake!
Na ardhi ikatoa yote yaliomo katika ndani ya tumbo lake, ikiwa khazina au maiti walio kwisha zikwa!
Na itakapo toa ardhi mizigo yake!
وَقَالَ ٱلۡإِنسَٰنُ مَا لَهَا
Na mtu akasema: Ina nini?
Na binaadamu akasema kwa kushtuka na khofu: Ardhi hii ina nini hata inatikisika hivi, na inatoa vilivyomo tumboni mwake, ndio Saa imefika?
Na mtu akasema: Ina nini?
يَوۡمَئِذٖ تُحَدِّثُ أَخۡبَارَهَا
Siku hiyo itahadithia khabari zake.
Siku hiyo ardhi itamsimulia mtu khabari zake zilio mshitua,
Siku hiyo itahadithia khabari zake.
بِأَنَّ رَبَّكَ أَوۡحَىٰ لَهَا
Kwa sababu Mola wake Mlezi ameifunulia!
Kwani Mlezi wake na Muumba wake atakuwa kaifunulia, kaipa Wahyi, na kaiamuru itetemeke na ijisuke suke, ndio ikafanya upesi kutekeleza amri.
Kwa sababu Mola wake Mlezi ameifunulia!
يَوۡمَئِذٖ يَصۡدُرُ ٱلنَّاسُ أَشۡتَاتٗا لِّيُرَوۡاْ أَعۡمَٰلَهُمۡ
Siku hiyo watu watatoka kwa mfarakano wakaonyweshwe vitendo vyao!
Siku hiyo watu watatoka makaburini mbio, nao wamo katika mtafaruku, wapate kuziona hisabu zao na malipo yao aliyo waahidi Mwenyezi Mungu.
Siku hiyo watu watatoka kwa mfarakano wakaonyweshwe vitendo vyao!
فَمَن يَعۡمَلۡ مِثۡقَالَ ذَرَّةٍ خَيۡرٗا يَرَهُۥ
Basi anaye tenda chembe ya wema, atauona!
Basi mwenye kufanya hata kitu chenye uzito wa punje ya mchanga cha kheri ataiona katika daftari lake, na atapata malipo yake.
Basi anaye tenda chembe ya wema, atauona!
وَمَن يَعۡمَلۡ مِثۡقَالَ ذَرَّةٖ شَرّٗا يَرَهُۥ
Na anaye tenda chembe ya uovu atauona!
Na mwenye kufanya shari ya uzito wa chembe ya mchanga ataiona kadhaalika, na atapata malipo yake. Wala Mola wako Mlezi hatamdhulumu yeyote.
Na anaye tenda chembe ya uovu atauona!
مشاركة عبر