La traduction swahilie - Centre de traduction Rawwâd
Traduction des sens du Noble Coran
L'équipe du Centre Rawwâd At-Tarjamah (Les Pionniers de la Traduction) l'a traduite.
وَٱلضُّحَىٰ
Ninaapa kwa wakati wa kabla ya adhuhuri!
وَٱلَّيۡلِ إِذَا سَجَىٰ
Na kwa usiku unapotanda!
مَا وَدَّعَكَ رَبُّكَ وَمَا قَلَىٰ
Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe.
وَلَلۡأٓخِرَةُ خَيۡرٞ لَّكَ مِنَ ٱلۡأُولَىٰ
Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko uliotangulia.
وَلَسَوۡفَ يُعۡطِيكَ رَبُّكَ فَتَرۡضَىٰٓ
Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike.
أَلَمۡ يَجِدۡكَ يَتِيمٗا فَـَٔاوَىٰ
Kwani hakukukuta yatima, akakupa makazi?
وَوَجَدَكَ ضَآلّٗا فَهَدَىٰ
Na akakukuta umepotea, akakuongoa?
وَوَجَدَكَ عَآئِلٗا فَأَغۡنَىٰ
Akakukuta mhitaji akakutosheleza?
فَأَمَّا ٱلۡيَتِيمَ فَلَا تَقۡهَرۡ
Basi yatima usimwonee!
وَأَمَّا ٱلسَّآئِلَ فَلَا تَنۡهَرۡ
Na anayeomba au kuuliza usimkaripie!
وَأَمَّا بِنِعۡمَةِ رَبِّكَ فَحَدِّثۡ
Na neema za Mola wako Mlezi zisimulie.
share_via