La traduction swahilie - Centre de traduction Rawwâd
Traduction des sens du Noble Coran
L'équipe du Centre Rawwâd At-Tarjamah (Les Pionniers de la Traduction) l'a traduite.
وَٱلتِّينِ وَٱلزَّيۡتُونِ
Ninaapa kwa tini na zaituni!
وَطُورِ سِينِينَ
Na kwa Mlima wa Sinai!
وَهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ ٱلۡأَمِينِ
Na kwa Mji huu wenye amani mno!
لَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ فِيٓ أَحۡسَنِ تَقۡوِيمٖ
Bila ya shaka tumemuumba mtu kwa umbo lilio bora kabisa.
ثُمَّ رَدَدۡنَٰهُ أَسۡفَلَ سَٰفِلِينَ
Kisha tukamrudisha kuwa chini kuliko walio chini!
إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ فَلَهُمۡ أَجۡرٌ غَيۡرُ مَمۡنُونٖ
Isipokuwa wale walioamini na wakatenda mema, hao watapata ujira usiokwisha.
فَمَا يُكَذِّبُكَ بَعۡدُ بِٱلدِّينِ
Basi ni kipi baadaye kitakachokukukadhibishia malipo?
أَلَيۡسَ ٱللَّهُ بِأَحۡكَمِ ٱلۡحَٰكِمِينَ
Kwani Mwenyezi Mungu si muadilifu zaidi kuliko wote wanaohukumu?
share_via