Header Include

Swahili translation - Rowad Translation Center

translated by Rowwad Translation Center, in cooperation with the Islamic Propagation Office in Rabwah and the Association for Serving Islamic Content in Languages.

QR Code https://quran.islamcontent.com/om/swahili_rwwad

وَٱلذَّٰرِيَٰتِ ذَرۡوٗا

Ninaapa kwa pepo zinazotawanya.

Ninaapa kwa pepo zinazotawanya.

فَٱلۡحَٰمِلَٰتِ وِقۡرٗا

Na zinazobeba mizigo.

Na zinazobeba mizigo.

فَٱلۡجَٰرِيَٰتِ يُسۡرٗا

Na zinazokwenda kwa wepesi.

Na zinazokwenda kwa wepesi.

فَٱلۡمُقَسِّمَٰتِ أَمۡرًا

Na zinazogawanya kwa amri.

Na zinazogawanya kwa amri.

إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَصَادِقٞ

Hakika mnayoahidiwa bila ya shaka ni ya ukweli.

Hakika mnayoahidiwa bila ya shaka ni ya ukweli.

وَإِنَّ ٱلدِّينَ لَوَٰقِعٞ

Na kwa hakika malipo bila ya shaka yatatokea.

Na kwa hakika malipo bila ya shaka yatatokea.

وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلۡحُبُكِ

Ninaapa kwa mbingu zenye njia.

Ninaapa kwa mbingu zenye njia.

إِنَّكُمۡ لَفِي قَوۡلٖ مُّخۡتَلِفٖ

Hakika nyinyi bila ya shaka mmo katika kauli inayohitalifiana.

Hakika nyinyi bila ya shaka mmo katika kauli inayohitalifiana.

يُؤۡفَكُ عَنۡهُ مَنۡ أُفِكَ

Anageuzwa kutokana na haki mwenye kugeuzwa.

Anageuzwa kutokana na haki mwenye kugeuzwa.

قُتِلَ ٱلۡخَرَّٰصُونَ

Wazushi wameangamizwa.

Wazushi wameangamizwa.

ٱلَّذِينَ هُمۡ فِي غَمۡرَةٖ سَاهُونَ

Ambao wameghafilika katika ujinga.

Ambao wameghafilika katika ujinga.

يَسۡـَٔلُونَ أَيَّانَ يَوۡمُ ٱلدِّينِ

Wanauliza: 'Ni lini hiyo siku ya malipo?'

Wanauliza: 'Ni lini hiyo siku ya malipo?'

يَوۡمَ هُمۡ عَلَى ٱلنَّارِ يُفۡتَنُونَ

Hiyo ni siku watakayoadhibiwa Motoni.

Hiyo ni siku watakayoadhibiwa Motoni.

ذُوقُواْ فِتۡنَتَكُمۡ هَٰذَا ٱلَّذِي كُنتُم بِهِۦ تَسۡتَعۡجِلُونَ

Onjeni adhabu yenu! Haya ndiyo mliyokuwa mkiyafanyia haraka.

Onjeni adhabu yenu! Haya ndiyo mliyokuwa mkiyafanyia haraka.

إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي جَنَّٰتٖ وَعُيُونٍ

Hakika wacha Mungu watakuwa katika Mabustani ya mbinguni na chemchemi.

Hakika wacha Mungu watakuwa katika Mabustani ya mbinguni na chemchemi.

ءَاخِذِينَ مَآ ءَاتَىٰهُمۡ رَبُّهُمۡۚ إِنَّهُمۡ كَانُواْ قَبۡلَ ذَٰلِكَ مُحۡسِنِينَ

Wanapokea yale aliyowapa Mola wao Mlezi. Kwa hakika hao walikuwa kabla ya haya wakifanya mema.

Wanapokea yale aliyowapa Mola wao Mlezi. Kwa hakika hao walikuwa kabla ya haya wakifanya mema.

كَانُواْ قَلِيلٗا مِّنَ ٱلَّيۡلِ مَا يَهۡجَعُونَ

Walikuwa wakilala kidogo tu usiku.

Walikuwa wakilala kidogo tu usiku.

وَبِٱلۡأَسۡحَارِ هُمۡ يَسۡتَغۡفِرُونَ

Na kabla ya alfajiri wakiomba maghfira.

Na kabla ya alfajiri wakiomba maghfira.

وَفِيٓ أَمۡوَٰلِهِمۡ حَقّٞ لِّلسَّآئِلِ وَٱلۡمَحۡرُومِ

Na katika mali yao ipo haki ya mwenye kuomba na asiyeomba.

Na katika mali yao ipo haki ya mwenye kuomba na asiyeomba.

وَفِي ٱلۡأَرۡضِ ءَايَٰتٞ لِّلۡمُوقِنِينَ

Na katika ardhi zipo Ishara kwa wenye yakini.

Na katika ardhi zipo Ishara kwa wenye yakini.

وَفِيٓ أَنفُسِكُمۡۚ أَفَلَا تُبۡصِرُونَ

Na pia katika nafsi zenu - Je, hamwoni?

Na pia katika nafsi zenu - Je, hamwoni?

وَفِي ٱلسَّمَآءِ رِزۡقُكُمۡ وَمَا تُوعَدُونَ

Na katika mbingu ziko riziki zenu na yale mnayoahidiwa.

Na katika mbingu ziko riziki zenu na yale mnayoahidiwa.

فَوَرَبِّ ٱلسَّمَآءِ وَٱلۡأَرۡضِ إِنَّهُۥ لَحَقّٞ مِّثۡلَ مَآ أَنَّكُمۡ تَنطِقُونَ

Basi ninaapa kwa Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, hakika haya ni kweli kama ilivyo kweli kuwa nyinyi mnasema.

Basi ninaapa kwa Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, hakika haya ni kweli kama ilivyo kweli kuwa nyinyi mnasema.

هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ضَيۡفِ إِبۡرَٰهِيمَ ٱلۡمُكۡرَمِينَ

Je, imekufikia hadithi ya wageni wa Ibrahim wanaoheshimiwa?

Je, imekufikia hadithi ya wageni wa Ibrahim wanaoheshimiwa?

إِذۡ دَخَلُواْ عَلَيۡهِ فَقَالُواْ سَلَٰمٗاۖ قَالَ سَلَٰمٞ قَوۡمٞ مُّنكَرُونَ

Walipoingia kwake na wakasema: 'Salama!' Na yeye akasema: 'Salama! Nyinyi ni watu nisiowajua.'

Walipoingia kwake na wakasema: 'Salama!' Na yeye akasema: 'Salama! Nyinyi ni watu nisiowajua.'

فَرَاغَ إِلَىٰٓ أَهۡلِهِۦ فَجَآءَ بِعِجۡلٖ سَمِينٖ

Basi akaenda kwa ahali yake na akaja na ndama aliyenona.

Basi akaenda kwa ahali yake na akaja na ndama aliyenona.

فَقَرَّبَهُۥٓ إِلَيۡهِمۡ قَالَ أَلَا تَأۡكُلُونَ

Akawakaribishia, akasema: 'Mbona hamli?'

Akawakaribishia, akasema: 'Mbona hamli?'

فَأَوۡجَسَ مِنۡهُمۡ خِيفَةٗۖ قَالُواْ لَا تَخَفۡۖ وَبَشَّرُوهُ بِغُلَٰمٍ عَلِيمٖ

Kwa hivyo, akahisi kuwaogopa katika nafsi yake. Wakasema: 'Usiwe na hofu.' Basi wakambashiria kupata kijana mwenye elimu.

Kwa hivyo, akahisi kuwaogopa katika nafsi yake. Wakasema: 'Usiwe na hofu.' Basi wakambashiria kupata kijana mwenye elimu.

فَأَقۡبَلَتِ ٱمۡرَأَتُهُۥ فِي صَرَّةٖ فَصَكَّتۡ وَجۡهَهَا وَقَالَتۡ عَجُوزٌ عَقِيمٞ

Ndipo mkewe akawaelekea kwa sauti ya kelele huku anajipiga usoni kwa mastaajabu, akasema: "Mimi ni kikongwe na tasa!"

Ndipo mkewe akawaelekea kwa sauti ya kelele huku anajipiga usoni kwa mastaajabu, akasema: "Mimi ni kikongwe na tasa!"

قَالُواْ كَذَٰلِكِ قَالَ رَبُّكِۖ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلۡحَكِيمُ ٱلۡعَلِيمُ

Wakasema: Ndivyo vivyo hivyo alivyosema Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye hekima, Mwenye kujua.

Wakasema: Ndivyo vivyo hivyo alivyosema Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye hekima, Mwenye kujua.

۞ قَالَ فَمَا خَطۡبُكُمۡ أَيُّهَا ٱلۡمُرۡسَلُونَ

Akasema: 'Basi ujumbe wenu ni nini, enyi mliotumwa?'

Akasema: 'Basi ujumbe wenu ni nini, enyi mliotumwa?'

قَالُوٓاْ إِنَّآ أُرۡسِلۡنَآ إِلَىٰ قَوۡمٖ مُّجۡرِمِينَ

Wakasema: 'Hakika sisi tumetumwa kwa watu wakosefu.

Wakasema: 'Hakika sisi tumetumwa kwa watu wakosefu.

لِنُرۡسِلَ عَلَيۡهِمۡ حِجَارَةٗ مِّن طِينٖ

Tuwatupie mawe ya udongo.

Tuwatupie mawe ya udongo.

مُّسَوَّمَةً عِندَ رَبِّكَ لِلۡمُسۡرِفِينَ

Yaliyotiwa alama kutoka kwa Mola wako Mlezi kwa ajili ya wanaopindukia mipaka.'

Yaliyotiwa alama kutoka kwa Mola wako Mlezi kwa ajili ya wanaopindukia mipaka.'

فَأَخۡرَجۡنَا مَن كَانَ فِيهَا مِنَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Kwa hivyo tukawatoa katika hao wale walioamini.

Kwa hivyo tukawatoa katika hao wale walioamini.

فَمَا وَجَدۡنَا فِيهَا غَيۡرَ بَيۡتٖ مِّنَ ٱلۡمُسۡلِمِينَ

Lakini hatukupata humo ila nyumba moja tu yenye Waislamu!

Lakini hatukupata humo ila nyumba moja tu yenye Waislamu!

وَتَرَكۡنَا فِيهَآ ءَايَةٗ لِّلَّذِينَ يَخَافُونَ ٱلۡعَذَابَ ٱلۡأَلِيمَ

Na tukaacha humo Ishara kwa ajili ya wanaoiogopa adhabu chungu.

Na tukaacha humo Ishara kwa ajili ya wanaoiogopa adhabu chungu.

وَفِي مُوسَىٰٓ إِذۡ أَرۡسَلۡنَٰهُ إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ بِسُلۡطَٰنٖ مُّبِينٖ

Na katika habari za Musa, tulipomtuma kwa Firauni na hoja wazi.

Na katika habari za Musa, tulipomtuma kwa Firauni na hoja wazi.

فَتَوَلَّىٰ بِرُكۡنِهِۦ وَقَالَ سَٰحِرٌ أَوۡ مَجۡنُونٞ

Lakini alipuuza kwa sababu ya nguvu zake na akasema: 'Huyu ni mchawi au mwendawazimu!'

Lakini alipuuza kwa sababu ya nguvu zake na akasema: 'Huyu ni mchawi au mwendawazimu!'

فَأَخَذۡنَٰهُ وَجُنُودَهُۥ فَنَبَذۡنَٰهُمۡ فِي ٱلۡيَمِّ وَهُوَ مُلِيمٞ

Basi tukamkamata yeye na majeshi yake na tukawatupa baharini, huku ni wa kulaumiwa.

Basi tukamkamata yeye na majeshi yake na tukawatupa baharini, huku ni wa kulaumiwa.

وَفِي عَادٍ إِذۡ أَرۡسَلۡنَا عَلَيۡهِمُ ٱلرِّيحَ ٱلۡعَقِيمَ

Na katika habari za 'Adi tulipowatumia upepo wa kukata uzazi.

Na katika habari za 'Adi tulipowatumia upepo wa kukata uzazi.

مَا تَذَرُ مِن شَيۡءٍ أَتَتۡ عَلَيۡهِ إِلَّا جَعَلَتۡهُ كَٱلرَّمِيمِ

Haukuacha chochote ulichokifikia ila ulikifanya kama kilichonyambuka.

Haukuacha chochote ulichokifikia ila ulikifanya kama kilichonyambuka.

وَفِي ثَمُودَ إِذۡ قِيلَ لَهُمۡ تَمَتَّعُواْ حَتَّىٰ حِينٖ

Na katika habari za Thamudi walipoambiwa: 'Jifurahisheni kwa muda mdogo tu.'

Na katika habari za Thamudi walipoambiwa: 'Jifurahisheni kwa muda mdogo tu.'

فَعَتَوۡاْ عَنۡ أَمۡرِ رَبِّهِمۡ فَأَخَذَتۡهُمُ ٱلصَّٰعِقَةُ وَهُمۡ يَنظُرُونَ

Wakaasi amri ya Mola wao Mlezi. Basi ukawanyakua moto wa radi nao wanaona.

Wakaasi amri ya Mola wao Mlezi. Basi ukawanyakua moto wa radi nao wanaona.

فَمَا ٱسۡتَطَٰعُواْ مِن قِيَامٖ وَمَا كَانُواْ مُنتَصِرِينَ

Basi hawakuweza kusimama wala hawakuwa wenye kujitetea.

Basi hawakuweza kusimama wala hawakuwa wenye kujitetea.

وَقَوۡمَ نُوحٖ مِّن قَبۡلُۖ إِنَّهُمۡ كَانُواْ قَوۡمٗا فَٰسِقِينَ

Na kaumu ya Nuhu hapo mbele. Hakika hao walikuwa watu wapotovu.

Na kaumu ya Nuhu hapo mbele. Hakika hao walikuwa watu wapotovu.

وَٱلسَّمَآءَ بَنَيۡنَٰهَا بِأَيۡيْدٖ وَإِنَّا لَمُوسِعُونَ

Na mbingu tumezifanya kwa nguvu na uwezo na hakika Sisi bila ya shaka ndio wenye uwezo wa kuzitanua.

Na mbingu tumezifanya kwa nguvu na uwezo na hakika Sisi bila ya shaka ndio wenye uwezo wa kuzitanua.

وَٱلۡأَرۡضَ فَرَشۡنَٰهَا فَنِعۡمَ ٱلۡمَٰهِدُونَ

Na ardhi tumeitandaza; basi watandazaji wazuri namna gani Sisi!

Na ardhi tumeitandaza; basi watandazaji wazuri namna gani Sisi!

وَمِن كُلِّ شَيۡءٍ خَلَقۡنَا زَوۡجَيۡنِ لَعَلَّكُمۡ تَذَكَّرُونَ

Na katika kila kitu tumeumba kwa jozi ili mzingatie.

Na katika kila kitu tumeumba kwa jozi ili mzingatie.

فَفِرُّوٓاْ إِلَى ٱللَّهِۖ إِنِّي لَكُم مِّنۡهُ نَذِيرٞ مُّبِينٞ

Basi kimbilieni kwa Mwenyezi Mungu, hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake.

Basi kimbilieni kwa Mwenyezi Mungu, hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake.

وَلَا تَجۡعَلُواْ مَعَ ٱللَّهِ إِلَٰهًا ءَاخَرَۖ إِنِّي لَكُم مِّنۡهُ نَذِيرٞ مُّبِينٞ

Wala msifanye kuwa kuna mungu mwengine pamoja na Mwenyezi Mungu. Hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake.

Wala msifanye kuwa kuna mungu mwengine pamoja na Mwenyezi Mungu. Hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake.

كَذَٰلِكَ مَآ أَتَى ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِم مِّن رَّسُولٍ إِلَّا قَالُواْ سَاحِرٌ أَوۡ مَجۡنُونٌ

Basi ndio hivyo hivyo, hakuwajia kabla yao Mtume ila walisema: 'Huyu ni mchawi au mwendawazimu.'

Basi ndio hivyo hivyo, hakuwajia kabla yao Mtume ila walisema: 'Huyu ni mchawi au mwendawazimu.'

أَتَوَاصَوۡاْ بِهِۦۚ بَلۡ هُمۡ قَوۡمٞ طَاغُونَ

Je, wameambizana kwa haya? Bali hawa ni watu waasi.

Je, wameambizana kwa haya? Bali hawa ni watu waasi.

فَتَوَلَّ عَنۡهُمۡ فَمَآ أَنتَ بِمَلُومٖ

Basi waachilie mbali, nawe hulaumiwi.

Basi waachilie mbali, nawe hulaumiwi.

وَذَكِّرۡ فَإِنَّ ٱلذِّكۡرَىٰ تَنفَعُ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Na kumbusha, kwani ukumbusho huwafaa Waumini.

Na kumbusha, kwani ukumbusho huwafaa Waumini.

وَمَا خَلَقۡتُ ٱلۡجِنَّ وَٱلۡإِنسَ إِلَّا لِيَعۡبُدُونِ

Nami sikuwaumba majini na watu ila waniabudu Mimi.

Nami sikuwaumba majini na watu ila waniabudu Mimi.

مَآ أُرِيدُ مِنۡهُم مِّن رِّزۡقٖ وَمَآ أُرِيدُ أَن يُطۡعِمُونِ

Na sitaki kwao riziki, wala sitaki wanilishe.

Na sitaki kwao riziki, wala sitaki wanilishe.

إِنَّ ٱللَّهَ هُوَ ٱلرَّزَّاقُ ذُو ٱلۡقُوَّةِ ٱلۡمَتِينُ

Hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kuruzuku, Mwenye nguvu, Madhubuti.

Hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kuruzuku, Mwenye nguvu, Madhubuti.

فَإِنَّ لِلَّذِينَ ظَلَمُواْ ذَنُوبٗا مِّثۡلَ ذَنُوبِ أَصۡحَٰبِهِمۡ فَلَا يَسۡتَعۡجِلُونِ

Hakika wale waliodhulumu wana fungu lao la adhabu kama fungu la wenzao. Basi wasiniharakishe.

Hakika wale waliodhulumu wana fungu lao la adhabu kama fungu la wenzao. Basi wasiniharakishe.

فَوَيۡلٞ لِّلَّذِينَ كَفَرُواْ مِن يَوۡمِهِمُ ٱلَّذِي يُوعَدُونَ

Basi ole wao wale walioikanusha siku yao waliyoahidiwa.

Basi ole wao wale walioikanusha siku yao waliyoahidiwa.
Footer Include