Header Include

Swahili translation - Rowad Translation Center

translated by Rowwad Translation Center, in cooperation with the Islamic Propagation Office in Rabwah and the Association for Serving Islamic Content in Languages.

QR Code https://quran.islamcontent.com/om/swahili_rwwad

ٱلۡحَآقَّةُ

Tukio la haki.

Tukio la haki.

مَا ٱلۡحَآقَّةُ

Nini hilo Tukio la haki?

Nini hilo Tukio la haki?

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡحَآقَّةُ

Na nini kitakachokujulisha nini hilo Tukio la haki?

Na nini kitakachokujulisha nini hilo Tukio la haki?

كَذَّبَتۡ ثَمُودُ وَعَادُۢ بِٱلۡقَارِعَةِ

Thamudi na A'di waliukadhibisha Msiba unaoshtusha.

Thamudi na A'di waliukadhibisha Msiba unaoshtusha.

فَأَمَّا ثَمُودُ فَأُهۡلِكُواْ بِٱلطَّاغِيَةِ

Basi Thamudi waliangamizwa kwa balaa kubwa mno.

Basi Thamudi waliangamizwa kwa balaa kubwa mno.

وَأَمَّا عَادٞ فَأُهۡلِكُواْ بِرِيحٖ صَرۡصَرٍ عَاتِيَةٖ

Na ama A'di waliangamizwa kwa upepo mkali usiozuilika.

Na ama A'di waliangamizwa kwa upepo mkali usiozuilika.

سَخَّرَهَا عَلَيۡهِمۡ سَبۡعَ لَيَالٖ وَثَمَٰنِيَةَ أَيَّامٍ حُسُومٗاۖ فَتَرَى ٱلۡقَوۡمَ فِيهَا صَرۡعَىٰ كَأَنَّهُمۡ أَعۡجَازُ نَخۡلٍ خَاوِيَةٖ

Aliowapelekea usiku saba, na michana minane, mfululizo bila ya kusita. Utaona watu wamepinduka kama kwamba ni magongo ya mitende yaliyo wazi ndani.

Aliowapelekea usiku saba, na michana minane, mfululizo bila ya kusita. Utaona watu wamepinduka kama kwamba ni magongo ya mitende yaliyo wazi ndani.

فَهَلۡ تَرَىٰ لَهُم مِّنۢ بَاقِيَةٖ

Basi je! Unamwona mmoja wao aliyebaki?

Basi je! Unamwona mmoja wao aliyebaki?

وَجَآءَ فِرۡعَوۡنُ وَمَن قَبۡلَهُۥ وَٱلۡمُؤۡتَفِكَٰتُ بِٱلۡخَاطِئَةِ

Na Firauni na waliomtangulia, na miji iliyopinduliwa chini juu, walileta dhambi kubwa.

Na Firauni na waliomtangulia, na miji iliyopinduliwa chini juu, walileta dhambi kubwa.

فَعَصَوۡاْ رَسُولَ رَبِّهِمۡ فَأَخَذَهُمۡ أَخۡذَةٗ رَّابِيَةً

Akamuasi Mtume wa Mola wao Mlezi, ndipo Yeye Mola akawakamata kwa mkamato uliozidi nguvu.

Akamuasi Mtume wa Mola wao Mlezi, ndipo Yeye Mola akawakamata kwa mkamato uliozidi nguvu.

إِنَّا لَمَّا طَغَا ٱلۡمَآءُ حَمَلۡنَٰكُمۡ فِي ٱلۡجَارِيَةِ

Maji yalipofurika Sisi tulikupandisheni katika safina.

Maji yalipofurika Sisi tulikupandisheni katika safina.

لِنَجۡعَلَهَا لَكُمۡ تَذۡكِرَةٗ وَتَعِيَهَآ أُذُنٞ وَٰعِيَةٞ

Ili tuyafanye hayo kuwa ni waadhi kwenu na kila sikio linalosikia liyahifadhi.

Ili tuyafanye hayo kuwa ni waadhi kwenu na kila sikio linalosikia liyahifadhi.

فَإِذَا نُفِخَ فِي ٱلصُّورِ نَفۡخَةٞ وَٰحِدَةٞ

Na litapopulizwa baragumu mpulizo mmoja tu.

Na litapopulizwa baragumu mpulizo mmoja tu.

وَحُمِلَتِ ٱلۡأَرۡضُ وَٱلۡجِبَالُ فَدُكَّتَا دَكَّةٗ وَٰحِدَةٗ

Na ardhi na milima ikaondolewa, na ikavunjwa kwa mvunjo mmoja.

Na ardhi na milima ikaondolewa, na ikavunjwa kwa mvunjo mmoja.

فَيَوۡمَئِذٖ وَقَعَتِ ٱلۡوَاقِعَةُ

Siku hiyo ndio Tukio litatokea.

Siku hiyo ndio Tukio litatokea.

وَٱنشَقَّتِ ٱلسَّمَآءُ فَهِيَ يَوۡمَئِذٖ وَاهِيَةٞ

Na mbingu zitapasuka, kwani siku hiyo zitakuwa dhaifu kabisa.

Na mbingu zitapasuka, kwani siku hiyo zitakuwa dhaifu kabisa.

وَٱلۡمَلَكُ عَلَىٰٓ أَرۡجَآئِهَاۚ وَيَحۡمِلُ عَرۡشَ رَبِّكَ فَوۡقَهُمۡ يَوۡمَئِذٖ ثَمَٰنِيَةٞ

Na Malaika watakuwa pembezoni mwa mbingu; na wanane juu ya hawa watakuwa wamebeba Kiti cha Enzi cha Mola wako Mlezi.

Na Malaika watakuwa pembezoni mwa mbingu; na wanane juu ya hawa watakuwa wamebeba Kiti cha Enzi cha Mola wako Mlezi.

يَوۡمَئِذٖ تُعۡرَضُونَ لَا تَخۡفَىٰ مِنكُمۡ خَافِيَةٞ

Siku hiyo mtahudhurishwa - haitafichika siri yoyote yenu.

Siku hiyo mtahudhurishwa - haitafichika siri yoyote yenu.

فَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ بِيَمِينِهِۦ فَيَقُولُ هَآؤُمُ ٱقۡرَءُواْ كِتَٰبِيَهۡ

Basi ama atakayepewa kitabu chake kwa mkono wake wa kulia, atasema: Haya someni kitabu changu!

Basi ama atakayepewa kitabu chake kwa mkono wake wa kulia, atasema: Haya someni kitabu changu!

إِنِّي ظَنَنتُ أَنِّي مُلَٰقٍ حِسَابِيَهۡ

Hakika nilijua ya kuwa nitapokea hisabu yangu.

Hakika nilijua ya kuwa nitapokea hisabu yangu.

فَهُوَ فِي عِيشَةٖ رَّاضِيَةٖ

Basi yeye atakuwa katika maisha ya kupendeza.

Basi yeye atakuwa katika maisha ya kupendeza.

فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٖ

Katika Bustani ya juu.

Katika Bustani ya juu.

قُطُوفُهَا دَانِيَةٞ

Matunda yake ya karibu.

Matunda yake ya karibu.

كُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ هَنِيٓـَٔۢا بِمَآ أَسۡلَفۡتُمۡ فِي ٱلۡأَيَّامِ ٱلۡخَالِيَةِ

Waambiwe: Kuleni na mnywe kwa furaha kwa sababu ya mlivyotanguliza katika siku zilizopita.

Waambiwe: Kuleni na mnywe kwa furaha kwa sababu ya mlivyotanguliza katika siku zilizopita.

وَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ بِشِمَالِهِۦ فَيَقُولُ يَٰلَيۡتَنِي لَمۡ أُوتَ كِتَٰبِيَهۡ

Na ama atakayepewa kitabu chake katika mkono wake wa kushoto, basi yeye atasema: "Laiti nisingelipewa kitabu changu!

Na ama atakayepewa kitabu chake katika mkono wake wa kushoto, basi yeye atasema: "Laiti nisingelipewa kitabu changu!

وَلَمۡ أَدۡرِ مَا حِسَابِيَهۡ

Wala nisingelijua nini hisabu yangu.

Wala nisingelijua nini hisabu yangu.

يَٰلَيۡتَهَا كَانَتِ ٱلۡقَاضِيَةَ

Laiti mauti ndiyo yangelikuwa ya kunimaliza kabisa.

Laiti mauti ndiyo yangelikuwa ya kunimaliza kabisa.

مَآ أَغۡنَىٰ عَنِّي مَالِيَهۡۜ

Mali yangu hayakunifaa kitu.

Mali yangu hayakunifaa kitu.

هَلَكَ عَنِّي سُلۡطَٰنِيَهۡ

Madaraka yangu yamenipotea."

Madaraka yangu yamenipotea."

خُذُوهُ فَغُلُّوهُ

(Pasemwe): Mshikeni! Mtieni pingu!

(Pasemwe): Mshikeni! Mtieni pingu!

ثُمَّ ٱلۡجَحِيمَ صَلُّوهُ

Kisha mtupeni Motoni!

Kisha mtupeni Motoni!

ثُمَّ فِي سِلۡسِلَةٖ ذَرۡعُهَا سَبۡعُونَ ذِرَاعٗا فَٱسۡلُكُوهُ

Tena mtatizeni katika mnyororo wenye urefu wa dhiraa sabini!

Tena mtatizeni katika mnyororo wenye urefu wa dhiraa sabini!

إِنَّهُۥ كَانَ لَا يُؤۡمِنُ بِٱللَّهِ ٱلۡعَظِيمِ

Kwani huyo hakika alikuwa hamuamini Mwenyezi Mungu Mtukufu.

Kwani huyo hakika alikuwa hamuamini Mwenyezi Mungu Mtukufu.

وَلَا يَحُضُّ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلۡمِسۡكِينِ

Wala hahimizi kulisha masikini.

Wala hahimizi kulisha masikini.

فَلَيۡسَ لَهُ ٱلۡيَوۡمَ هَٰهُنَا حَمِيمٞ

Basi leo hapa hana jamaa wa kumwonea uchungu.

Basi leo hapa hana jamaa wa kumwonea uchungu.

وَلَا طَعَامٌ إِلَّا مِنۡ غِسۡلِينٖ

Wala hana chakula ila usaha wa watu wa Motoni.

Wala hana chakula ila usaha wa watu wa Motoni.

لَّا يَأۡكُلُهُۥٓ إِلَّا ٱلۡخَٰطِـُٔونَ

Chakula hicho hawakili ila wakosefu.

Chakula hicho hawakili ila wakosefu.

فَلَآ أُقۡسِمُ بِمَا تُبۡصِرُونَ

Basi ninaapa kwa mnavyoviona.

Basi ninaapa kwa mnavyoviona.

وَمَا لَا تُبۡصِرُونَ

Na msivyoviona.

Na msivyoviona.

إِنَّهُۥ لَقَوۡلُ رَسُولٖ كَرِيمٖ

Kwa hakika hii ni kauli iliyoletwa na Mjumbe mwenye heshima.

Kwa hakika hii ni kauli iliyoletwa na Mjumbe mwenye heshima.

وَمَا هُوَ بِقَوۡلِ شَاعِرٖۚ قَلِيلٗا مَّا تُؤۡمِنُونَ

Wala si kauli ya mtunga mashairi. Ni machache sana mnayoyaamini.

Wala si kauli ya mtunga mashairi. Ni machache sana mnayoyaamini.

وَلَا بِقَوۡلِ كَاهِنٖۚ قَلِيلٗا مَّا تَذَكَّرُونَ

Wala si kauli ya kuhani. Ni machache mnayoyakumbuka.

Wala si kauli ya kuhani. Ni machache mnayoyakumbuka.

تَنزِيلٞ مِّن رَّبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Ni uteremsho utokao kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Ni uteremsho utokao kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

وَلَوۡ تَقَوَّلَ عَلَيۡنَا بَعۡضَ ٱلۡأَقَاوِيلِ

Na lau kama angelituzulia baadhi ya maneno tu.

Na lau kama angelituzulia baadhi ya maneno tu.

لَأَخَذۡنَا مِنۡهُ بِٱلۡيَمِينِ

Bila ya shaka tungelimshika kwa mkono wa kulia.

Bila ya shaka tungelimshika kwa mkono wa kulia.

ثُمَّ لَقَطَعۡنَا مِنۡهُ ٱلۡوَتِينَ

Kisha kwa hakika tungelimkata mshipa mkubwa wa moyo!

Kisha kwa hakika tungelimkata mshipa mkubwa wa moyo!

فَمَا مِنكُم مِّنۡ أَحَدٍ عَنۡهُ حَٰجِزِينَ

Na hapana yeyote katika nyinyi ambaye angeliweza kutuzuia kumfikia.

Na hapana yeyote katika nyinyi ambaye angeliweza kutuzuia kumfikia.

وَإِنَّهُۥ لَتَذۡكِرَةٞ لِّلۡمُتَّقِينَ

Kwa hakika hii ni mawaidha kwa wacha Mungu.

Kwa hakika hii ni mawaidha kwa wacha Mungu.

وَإِنَّا لَنَعۡلَمُ أَنَّ مِنكُم مُّكَذِّبِينَ

Na hakika Sisi bila ya shaka tunajua kwamba miongoni mwenu wapo wanaokadhibisha.

Na hakika Sisi bila ya shaka tunajua kwamba miongoni mwenu wapo wanaokadhibisha.

وَإِنَّهُۥ لَحَسۡرَةٌ عَلَى ٱلۡكَٰفِرِينَ

Na hakika bila ya shaka itakuwa ni majuto kwa wanaokataa.

Na hakika bila ya shaka itakuwa ni majuto kwa wanaokataa.

وَإِنَّهُۥ لَحَقُّ ٱلۡيَقِينِ

Na hakika hii bila ya shaka ni haki ya yakini.

Na hakika hii bila ya shaka ni haki ya yakini.

فَسَبِّحۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلۡعَظِيمِ

Basi litakase jina la Mola wako Mlezi Mtukufu.

Basi litakase jina la Mola wako Mlezi Mtukufu.
Footer Include