Header Include

Swahili translation - Rowad Translation Center

translated by Rowwad Translation Center, in cooperation with the Islamic Propagation Office in Rabwah and the Association for Serving Islamic Content in Languages.

QR Code https://quran.islamcontent.com/tg/swahili_rwwad

وَٱلۡمُرۡسَلَٰتِ عُرۡفٗا

Ninaapa kwa zinazotumwa kwa upole!

Ninaapa kwa zinazotumwa kwa upole!

فَٱلۡعَٰصِفَٰتِ عَصۡفٗا

Na zinazovuma kwa kasi!

Na zinazovuma kwa kasi!

وَٱلنَّٰشِرَٰتِ نَشۡرٗا

Na zikaeneza maeneo yote!

Na zikaeneza maeneo yote!

فَٱلۡفَٰرِقَٰتِ فَرۡقٗا

Na zinazofarikisha zikatawanya!

Na zinazofarikisha zikatawanya!

فَٱلۡمُلۡقِيَٰتِ ذِكۡرًا

Na zinazopeleka mawaidha!

Na zinazopeleka mawaidha!

عُذۡرًا أَوۡ نُذۡرًا

Kuwa udhuru au kuonya.

Kuwa udhuru au kuonya.

إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَوَٰقِعٞ

Hakika mnayoahidiwa bila ya shaka yatakuwa!

Hakika mnayoahidiwa bila ya shaka yatakuwa!

فَإِذَا ٱلنُّجُومُ طُمِسَتۡ

Wakati nyota zitakapofutwa.

Wakati nyota zitakapofutwa.

وَإِذَا ٱلسَّمَآءُ فُرِجَتۡ

Na mbingu zitakapopasuliwa.

Na mbingu zitakapopasuliwa.

وَإِذَا ٱلۡجِبَالُ نُسِفَتۡ

Na milima itakapopeperushwa.

Na milima itakapopeperushwa.

وَإِذَا ٱلرُّسُلُ أُقِّتَتۡ

Na Mitume watakapowekewa wakati wao.

Na Mitume watakapowekewa wakati wao.

لِأَيِّ يَوۡمٍ أُجِّلَتۡ

Kwa siku gani hiyo wamewekewa muda huo?

Kwa siku gani hiyo wamewekewa muda huo?

لِيَوۡمِ ٱلۡفَصۡلِ

Kwa Siku ya kupambanua!

Kwa Siku ya kupambanua!

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلۡفَصۡلِ

Na nini kitakachokujuulisha siku ya kupambanua ni nini?

Na nini kitakachokujuulisha siku ya kupambanua ni nini?

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao, siku hiyo hao wanaokanusha!

Ole wao, siku hiyo hao wanaokanusha!

أَلَمۡ نُهۡلِكِ ٱلۡأَوَّلِينَ

Kwani hatukuwaangamiza waliotangulia?

Kwani hatukuwaangamiza waliotangulia?

ثُمَّ نُتۡبِعُهُمُ ٱلۡأٓخِرِينَ

Kisha tukawafuatilizia waliofuatia?

Kisha tukawafuatilizia waliofuatia?

كَذَٰلِكَ نَفۡعَلُ بِٱلۡمُجۡرِمِينَ

Ndio kama hivi tuwatendavyo wakosefu!

Ndio kama hivi tuwatendavyo wakosefu!

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao wanaokanusha!

Ole wao siku hiyo hao wanaokanusha!

أَلَمۡ نَخۡلُقكُّم مِّن مَّآءٖ مَّهِينٖ

Kwani hatukukuumbeni kwa maji ya kudharauliwa?

Kwani hatukukuumbeni kwa maji ya kudharauliwa?

فَجَعَلۡنَٰهُ فِي قَرَارٖ مَّكِينٍ

Kisha tukayaweka mahali pa utulivu madhubuti?

Kisha tukayaweka mahali pa utulivu madhubuti?

إِلَىٰ قَدَرٖ مَّعۡلُومٖ

Mpaka muda maalumu?

Mpaka muda maalumu?

فَقَدَرۡنَا فَنِعۡمَ ٱلۡقَٰدِرُونَ

Tukakadiria na Sisi ni wabora wa kukadiria.

Tukakadiria na Sisi ni wabora wa kukadiria.

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao wanaokanusha!

Ole wao siku hiyo hao wanaokanusha!

أَلَمۡ نَجۡعَلِ ٱلۡأَرۡضَ كِفَاتًا

Kwani hatukuifanya ardhi yenye kukusanya.

Kwani hatukuifanya ardhi yenye kukusanya.

أَحۡيَآءٗ وَأَمۡوَٰتٗا

Walio hai na maiti?

Walio hai na maiti?

وَجَعَلۡنَا فِيهَا رَوَٰسِيَ شَٰمِخَٰتٖ وَأَسۡقَيۡنَٰكُم مَّآءٗ فُرَاتٗا

Na ndani yake tukaweka milima mirefu yenye kuthibiti, na tunakunywesheni maji matamu?

Na ndani yake tukaweka milima mirefu yenye kuthibiti, na tunakunywesheni maji matamu?

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao wanaokanusha!

Ole wao siku hiyo hao wanaokanusha!

ٱنطَلِقُوٓاْ إِلَىٰ مَا كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ

Nendeni kwenye adhabu mliyokuwa mkiikanusha!

Nendeni kwenye adhabu mliyokuwa mkiikanusha!

ٱنطَلِقُوٓاْ إِلَىٰ ظِلّٖ ذِي ثَلَٰثِ شُعَبٖ

Nendeni kwenye kivuli chenye mapande matatu!

Nendeni kwenye kivuli chenye mapande matatu!

لَّا ظَلِيلٖ وَلَا يُغۡنِي مِنَ ٱللَّهَبِ

Hakikingi moto, wala hakiwaepushi na mwako.

Hakikingi moto, wala hakiwaepushi na mwako.

إِنَّهَا تَرۡمِي بِشَرَرٖ كَٱلۡقَصۡرِ

Hakika Moto huo unatoa macheche kama majumba!

Hakika Moto huo unatoa macheche kama majumba!

كَأَنَّهُۥ جِمَٰلَتٞ صُفۡرٞ

Kama kwamba ni ngamia wa rangi ya manjano!

Kama kwamba ni ngamia wa rangi ya manjano!

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao wanaokanusha!

Ole wao siku hiyo hao wanaokanusha!

هَٰذَا يَوۡمُ لَا يَنطِقُونَ

Hii ni siku ambayo hawatatamka kitu.

Hii ni siku ambayo hawatatamka kitu.

وَلَا يُؤۡذَنُ لَهُمۡ فَيَعۡتَذِرُونَ

Wala hawataruhusiwa kutoa udhuru.

Wala hawataruhusiwa kutoa udhuru.

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao waliokanusha!

Ole wao siku hiyo hao waliokanusha!

هَٰذَا يَوۡمُ ٱلۡفَصۡلِۖ جَمَعۡنَٰكُمۡ وَٱلۡأَوَّلِينَ

Hii ndiyo siku ya kupambanua. Tumekukusanyeni nyinyi na waliotangulia.

Hii ndiyo siku ya kupambanua. Tumekukusanyeni nyinyi na waliotangulia.

فَإِن كَانَ لَكُمۡ كَيۡدٞ فَكِيدُونِ

Ikiwa mnayo hila, nifanyieni hila Mimi!

Ikiwa mnayo hila, nifanyieni hila Mimi!

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao waliokanusha!

Ole wao siku hiyo hao waliokanusha!

إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي ظِلَٰلٖ وَعُيُونٖ

Hakika wacha Mungu watakuwa katika vivuli na chemchemi.

Hakika wacha Mungu watakuwa katika vivuli na chemchemi.

وَفَوَٰكِهَ مِمَّا يَشۡتَهُونَ

Na matunda wanayoyapenda.

Na matunda wanayoyapenda.

كُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ هَنِيٓـَٔۢا بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ

Kuleni na kunyweni kwa furaha kwa yale mliyokuwa mkiyatenda.

Kuleni na kunyweni kwa furaha kwa yale mliyokuwa mkiyatenda.

إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ

Hakika ndio kama hivyo tunavyowalipa watendao mema.

Hakika ndio kama hivyo tunavyowalipa watendao mema.

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao wanaokanusha!

Ole wao siku hiyo hao wanaokanusha!

كُلُواْ وَتَمَتَّعُواْ قَلِيلًا إِنَّكُم مُّجۡرِمُونَ

Kuleni na mjifurahishe kidogo tu. Hakika nyinyi ni wakosefu!

Kuleni na mjifurahishe kidogo tu. Hakika nyinyi ni wakosefu!

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao wanaokanusha!

Ole wao siku hiyo hao wanaokanusha!

وَإِذَا قِيلَ لَهُمُ ٱرۡكَعُواْ لَا يَرۡكَعُونَ

Na wakiambiwa: "Inameni!" Hawainami.

Na wakiambiwa: "Inameni!" Hawainami.

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao wanaokanusha!

Ole wao siku hiyo hao wanaokanusha!

فَبِأَيِّ حَدِيثِۭ بَعۡدَهُۥ يُؤۡمِنُونَ

Basi maneno gani baada ya haya watayaamini?

Basi maneno gani baada ya haya watayaamini?
Footer Include