Header Include

الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

QR Code https://quran.islamcontent.com/ar/swahili_barawani

أَلَمۡ تَرَ كَيۡفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِأَصۡحَٰبِ ٱلۡفِيلِ

Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo watenda wale wenye tembo?

Hakika, ewe Muhammad, unajua kwa ujuzi usio ingiliwa na shaka yoyote, alivyo fanya Mola wako Mlezi kuwafanyia wale watu wenye tembo (ndovu), wakataka kuishambulia Nyumba takatifu ya Al-Kaaba.
Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo watenda wale wenye tembo?

أَلَمۡ يَجۡعَلۡ كَيۡدَهُمۡ فِي تَضۡلِيلٖ

Kwani hakujaalia vitimbi vyao kuharibika?

Unajua ya kwamba hakika Mwenyezi Mungu amejaalia juhudi yao kutaka kuibomoa Al-Kaaba ivize na ipotelee mbali. Juhudi yao ikapeperuka, na wao wasipate makusudio yao.
Kwani hakujaalia vitimbi vyao kuharibika?

وَأَرۡسَلَ عَلَيۡهِمۡ طَيۡرًا أَبَابِيلَ

Na akawapelekea ndege makundi kwa makundi,

Na Mwenyezi Mungu aliwasalitisha na majeshi ya ndege yaliyo watokea makundi kwa makundi yakifuatana, na yakawazunguka kila upande.
Na akawapelekea ndege makundi kwa makundi,

تَرۡمِيهِم بِحِجَارَةٖ مِّن سِجِّيلٖ

Wakiwatupia mawe ya udongo wa Motoni,

Wakiwatupia mawe kutoka Jahannamu.
Wakiwatupia mawe ya udongo wa Motoni,

فَجَعَلَهُمۡ كَعَصۡفٖ مَّأۡكُولِۭ

Akawafanya kama majani yaliyo liwa!

Akawafanya kama majani ya mimea yaliyo sibiwa yakatilifu.
Akawafanya kama majani yaliyo liwa!
Footer Include