Header Include

الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

QR Code https://quran.islamcontent.com/ar/swahili_barawani

لِإِيلَٰفِ قُرَيۡشٍ

Kwa walivyo zoea Maqureshi,

Hebu staajabuni kwa yanayo walazimu Makureshi! Kuwalazimu safari za musimu wa baridi kwenda Yaman,
Kwa walivyo zoea Maqureshi,

إِۦلَٰفِهِمۡ رِحۡلَةَ ٱلشِّتَآءِ وَٱلصَّيۡفِ

Kuzoea kwao safari za siku za baridi na siku za joto.

Na safari za musimu wa joto kwenda Shamu, kufanya biashara na kutafuta riziki kwa utulivu na amani. (Hizo safari za biashara za Yaman ndizo zilizo waleta Waarabu Afrika Mashariki kwa maelfu ya miaka, na zikauleta Uislamu pande za Afrika kabla ya kuenea Arabuni. Kwani nchi za Afrika Mashariki zilikaliwa na Waarabu kwa maelfu ya miaka. Soma Periplus of the Erythrean Sea, na East Africa and Its Invaders ya Prof. Coupland, na vitabu vya Sir John Gray na Dr. L.W. Hollingsworth.)
Kuzoea kwao safari za siku za baridi na siku za joto.

فَلۡيَعۡبُدُواْ رَبَّ هَٰذَا ٱلۡبَيۡتِ

Basi nawamuabudu Mola Mlezi wa Nyumba hii,

Basi wamtakasie ibada Mola Mlezi wa Nyumba hii aliye wawezesha kuzifanya hizi safari mbili.
Basi nawamuabudu Mola Mlezi wa Nyumba hii,

ٱلَّذِيٓ أَطۡعَمَهُم مِّن جُوعٖ وَءَامَنَهُم مِّنۡ خَوۡفِۭ

Ambaye anawalisha wasipate njaa, na anawalinda na khofu.

Ambaye anawalisha wasione njaa, na hali wao wamo katika bonde lisio na makulima, na akawalinda na khofu na watu wengine pembezoni mwao wananyakuliwa.
Ambaye anawalisha wasipate njaa, na anawalinda na khofu.
Footer Include