Header Include

الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

QR Code https://quran.islamcontent.com/ar/swahili_barawani

وَٱلۡمُرۡسَلَٰتِ عُرۡفٗا

Naapa kwa zinazo tumwa kwa upole! 

Naapa kwa Aya zilizo tumwa kwa ulimi wa Jibrili kumpelekea Muhammad kwa upole wa kawaida na kheri,
Naapa kwa zinazo tumwa kwa upole! 

فَٱلۡعَٰصِفَٰتِ عَصۡفٗا

Na zinazo vuma kwa kasi!

Na kwa Aya zenye kuzitwaa kwa nguvu dini nyengine zote za uwongo zikizipeperushia mbali,
Na zinazo vuma kwa kasi!

وَٱلنَّٰشِرَٰتِ نَشۡرٗا

Na zikaeneza maeneo yote!

Na kwa Aya zenye kueneza hikima na uwongofu katika nyoyo za walimwengu kwa uenezi mkubwa mno,
Na zikaeneza maeneo yote!

فَٱلۡفَٰرِقَٰتِ فَرۡقٗا

Na zinazo farikisha zikatawanya!

Na zenye kufarikisha baina ya kweli na uwongo kwa mfarakano ulio wazi kabisa,
Na zinazo farikisha zikatawanya!

فَٱلۡمُلۡقِيَٰتِ ذِكۡرًا

Na zinazo peleka mawaidha!

Na zenye kuwapa watu mawaidha ya kuwanufaisha,
Na zinazo peleka mawaidha!

عُذۡرًا أَوۡ نُذۡرًا

Kwa kuudhuru au kuonya,

Ili iwe ni udhuru kwao na onyo wasiwe na hoja,
Kwa kuudhuru au kuonya,

إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَوَٰقِعٞ

Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka yatakuwa!

Hakika haya mliyo ahidiwa ya kuja Kiyama kwa yakini yatatimia tu bila ya shaka yoyote.
Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka yatakuwa!

فَإِذَا ٱلنُّجُومُ طُمِسَتۡ

Wakati nyota zitakapo futwa,

Basi nyota zitapo ondolewa kabisa,
Wakati nyota zitakapo futwa,

وَإِذَا ٱلسَّمَآءُ فُرِجَتۡ

Na mbingu zitakapo pasuliwa,

Na mbingu zitapo pasuka,
Na mbingu zitakapo pasuliwa,

وَإِذَا ٱلۡجِبَالُ نُسِفَتۡ

Na milima itakapo peperushwa,

Na milima ikavurugwa na ikapeperushiwa mbali na upepo,
Na milima itakapo peperushwa,

وَإِذَا ٱلرُّسُلُ أُقِّتَتۡ

Na Mitume watakapo wekewa wakati wao,

Na Mitume wakawekewa wakati maalumu wahudhurie kwa ajili ya kuwatolea ushahidi kaumu zao.
Na Mitume watakapo wekewa wakati wao,

لِأَيِّ يَوۡمٍ أُجِّلَتۡ

Kwa siku gani hiyo wamewekewa muda huo?

Kwa ajili ya siku gani yametayarishwa mambo haya makubwa makubwa?
Kwa siku gani hiyo wamewekewa muda huo?

لِيَوۡمِ ٱلۡفَصۡلِ

Kwa siku ya kupambanua!

Kwa ajili ya siku watakapo pambanuliwa baina ya viumbe.
Kwa siku ya kupambanua!

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلۡفَصۡلِ

Na nini kitakacho kujuulisha siku ya kupambanua ni nini?

Na nini cha kukujuvya ina nini hiyo siku ya kupambanua?
Na nini kitakacho kujuulisha siku ya kupambanua ni nini?

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao, siku hiyo hao wanao kanusha!

Ni maangamio ya milele siku hiyo kwa hao wanao kadhibisha walio waahidi Mitume!
Ole wao, siku hiyo hao wanao kanusha!

أَلَمۡ نُهۡلِكِ ٱلۡأَوَّلِينَ

Kwani hatukuwaangamiza walio tangulia?

Kwani hatukuwaangamiza mataifa ya zamani yaliyo kadhibisha,
Kwani hatukuwaangamiza walio tangulia?

ثُمَّ نُتۡبِعُهُمُ ٱلۡأٓخِرِينَ

Kisha tukawafuatilizia walio fuatia?

Na kisha tukawafuatilizia hao wenginewe tukawateketeza hali kadhaalika,
Kisha tukawafuatilizia walio fuatia?

كَذَٰلِكَ نَفۡعَلُ بِٱلۡمُجۡرِمِينَ

Ndio kama hivi tuwatendavyo wakosefu!

Kwa madhambi waliyo yafanya na walivyo mkataa Mwenyezi Mungu?
Ndio kama hivi tuwatendavyo wakosefu!

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

Siku hiyo ni siku ya kuteketezwa walio kadhibisha, kama tulivyo waahidi.
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

أَلَمۡ نَخۡلُقكُّم مِّن مَّآءٖ مَّهِينٖ

Kwani hatukukuumbeni kwa maji ya kudharauliwa?

Kwani hatukukuumbeni kutokana na maji yaliyo dhalili, nayo ni manii,
Kwani hatukukuumbeni kwa maji ya kudharauliwa?

فَجَعَلۡنَٰهُ فِي قَرَارٖ مَّكِينٍ

Kisha tukayaweka mahali pa utulivu madhubuti?

Na tukayaweka maji haya katika pahala patulivu,
Kisha tukayaweka mahali pa utulivu madhubuti?

إِلَىٰ قَدَرٖ مَّعۡلُومٖ

Mpaka muda maalumu?

Mpaka kutimilia kuumbwa kwake na kutengenezwa kwake kwa muda anao ujua Mwenyezi Mungu.
Mpaka muda maalumu?

فَقَدَرۡنَا فَنِعۡمَ ٱلۡقَٰدِرُونَ

Tukakadiria na Sisi ni wabora wa kukadiria.

Nasi tukaweka vipimo katika kuumbwa kwake, na kutengenezwa kwake, na kutoka kwake. Basi wabora wa kupima na kukadiria ni Sisi.
Tukakadiria na Sisi ni wabora wa kukadiria.

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

Ole wao hao wanao kadhibisha neema za kuumba na kukadiria.
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

أَلَمۡ نَجۡعَلِ ٱلۡأَرۡضَ كِفَاتًا

Kwani hatukuifanya ardhi yenye kukusanya

Kwani hatukuifanya ardhi kuwa imekusanya juu ya mgongo wake
Kwani hatukuifanya ardhi yenye kukusanya

أَحۡيَآءٗ وَأَمۡوَٰتٗا

Walio hai na maiti?

Viumbe vilivyo hai visio hisabika, na vilio kufa visio kadirika,
Walio hai na maiti?

وَجَعَلۡنَا فِيهَا رَوَٰسِيَ شَٰمِخَٰتٖ وَأَسۡقَيۡنَٰكُم مَّآءٗ فُرَاتٗا

Na ndani yake tukaweka milima mirefu yenye kuthibiti, na tunakunywesheni maji matamu?

Na tukaweka milima iliyo thibiti imara mirefu, na tukakunywesheni maji matamu?
Na ndani yake tukaweka milima mirefu yenye kuthibiti, na tunakunywesheni maji matamu?

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

Wataangamia siku hiyo hao wanao kadhibisha neema hizi!
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

ٱنطَلِقُوٓاْ إِلَىٰ مَا كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ

Nendeni kwenye adhabu mliyo kuwa mkiikanusha!

Siku ya kupambanua wataambiwa makafiri: Nendeni huko Motoni mliko kuwa mkikukanusha.
Nendeni kwenye adhabu mliyo kuwa mkiikanusha!

ٱنطَلِقُوٓاْ إِلَىٰ ظِلّٖ ذِي ثَلَٰثِ شُعَبٖ

Nendeni kwenye kivuli chenye mapande matatu!

Nendeni kwenye joto la moshi wa Jahannamu ulio gawika kwa ukubwa wake mapande matatu.
Nendeni kwenye kivuli chenye mapande matatu!

لَّا ظَلِيلٖ وَلَا يُغۡنِي مِنَ ٱللَّهَبِ

Hakikingi moto, wala hakiwaepushi na mwako.

Hapana cha kujikinga na joto la siku hiyo, wala kivuli hicho hakipunguzi joto la mwako hata kidogo.
Hakikingi moto, wala hakiwaepushi na mwako.

إِنَّهَا تَرۡمِي بِشَرَرٖ كَٱلۡقَصۡرِ

Hakika Moto huo unatoa macheche kama majumba!

Moto huo hutupa macheche yenye ukubwa kama majumba,
Hakika Moto huo unatoa macheche kama majumba!

كَأَنَّهُۥ جِمَٰلَتٞ صُفۡرٞ

Kama kwamba ni ngamia wa rangi ya manjano!

Au utaona hayo macheche kama ngamia weusi wenye kuingia rangi ya manjano.
Kama kwamba ni ngamia wa rangi ya manjano!

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

Wataangamia siku hiyo wanao kanusha kwamba hizi ndizo sifa za Moto.
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

هَٰذَا يَوۡمُ لَا يَنطِقُونَ

Hii ni siku ambayo hawatatamka kitu,

Haya uliyo simuliwa yatatokea katika siku ambayo hawatatamka kitu cha kuwanufaisha,
Hii ni siku ambayo hawatatamka kitu,

وَلَا يُؤۡذَنُ لَهُمۡ فَيَعۡتَذِرُونَ

Wala hawataruhusiwa kutoa udhuru.

Wala hawatakuwa na idhini ya kutamka, wala hawatatoa udhuru, kwani hawana udhuru.
Wala hawataruhusiwa kutoa udhuru.

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao walio kanusha!

Wataangamia siku hiyo wanayo ikadhibisha siku hii.
Ole wao siku hiyo hao walio kanusha!

هَٰذَا يَوۡمُ ٱلۡفَصۡلِۖ جَمَعۡنَٰكُمۡ وَٱلۡأَوَّلِينَ

Hii ndiyo siku ya kupambanua. Tumekukusanyeni nyinyi na walio tangulia.

Hii ndiyo siku ya kufafanua baina ya mwenye ukweli, na mwenye uwongo, kwa kuwa kila mmoja atalipwa kwa mujibu wa anavyo stahiki. Enyi mnao mkadhibisha Muhammad! Tumekujaalieni nyinyi na walio kutangulieni walio kadhibisha mfano wenu,
Hii ndiyo siku ya kupambanua. Tumekukusanyeni nyinyi na walio tangulia.

فَإِن كَانَ لَكُمۡ كَيۡدٞ فَكِيدُونِ

kiwa mnayo hila, nifanyieni hila Mimi!

Kama mnayo hila ya kujikinga na adhabu basi fanyeni hila hiyo. Basi njooni muepukane na adhabu yangu.
kiwa mnayo hila, nifanyieni hila Mimi!

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao walio kanusha!

Wataangamia siku hiyo wanayo ikadhibisha ahadi ya Mwenyezi Mungu.
Ole wao siku hiyo hao walio kanusha!

إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي ظِلَٰلٖ وَعُيُونٖ

Hakika wachamngu watakuwa katika vivuli na chemchem,

Hakika wachamngu wenye kujikinga na adhabu ya Mwenyezi Mungu watakuwa katika kivuli kikubwa, na chemchem zinazo miminika,
Hakika wachamngu watakuwa katika vivuli na chemchem,

وَفَوَٰكِهَ مِمَّا يَشۡتَهُونَ

Na matunda wanayo yapenda,

Na matunda wanayo yaonea ladha, na wanayo yapenda,
Na matunda wanayo yapenda,

كُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ هَنِيٓـَٔۢا بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ

Kuleni na kunyweni kwa furaha kwa yale mliyo kuwa mkiyatenda.

Wataambiwa kwa kuamkiwa na kukirimiwa: Kuleni na mnywe chakula na vinywaji kwa starehe kwa sababu ya vitendo vyema mlivyo kuwa mkivitenda duniani.
Kuleni na kunyweni kwa furaha kwa yale mliyo kuwa mkiyatenda.

إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ

Hakika ndio kama hivyo tunavyo walipa watendao mema.

Hakika Sisi huwalipa mfano wa malipo hayo matukufu watu wema.
Hakika ndio kama hivyo tunavyo walipa watendao mema.

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

Wataangamia siku hiyo wanayo ikadhibisha Pepo.
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

كُلُواْ وَتَمَتَّعُواْ قَلِيلًا إِنَّكُم مُّجۡرِمُونَ

Kuleni na mjifurahishe kidogo tu. Hakika nyinyi ni wakosefu!

Na makafiri wataambiwa: Kuleni na mjistareheshe kwa starehe isiyo baki muda mrefu, kwani hakika nyinyi ni wakosefu kwa kumshirikisha kwenu Mwenyezi Mungu.
Kuleni na mjifurahishe kidogo tu. Hakika nyinyi ni wakosefu!

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

Wataangamia siku hiyo wanao ikadhibisha neema.
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

وَإِذَا قِيلَ لَهُمُ ٱرۡكَعُواْ لَا يَرۡكَعُونَ

Na wakiambiwa: Inameni! Hawainami.

Na wakiambiwa: Swalini kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, na mnyenyekeeni Yeye, hawanyenyekei wala hawaswali; bali hushikilia kiburi chao!
Na wakiambiwa: Inameni! Hawainami.

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

Wataangamia siku wanao kadhibisha amri za Mwenyezi Mungu na makatazo yake.
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

فَبِأَيِّ حَدِيثِۭ بَعۡدَهُۥ يُؤۡمِنُونَ

Basi maneno gani baada ya haya watayaamini?

Basi maneno gani hawa watayaamini ikiwa hawaiamini Qur'ani, na hali hii ni muujiza ulio toka mbinguni?
Basi maneno gani baada ya haya watayaamini?
Footer Include