Header Include

الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

QR Code https://quran.islamcontent.com/ar/swahili_barawani

وَٱلشَّمۡسِ وَضُحَىٰهَا

Naapa kwa jua na mwangaza wake!

Naapa kwa jua na mwangaza wake na kuchomoza kwake na kwa joto lake!
Naapa kwa jua na mwangaza wake!

وَٱلۡقَمَرِ إِذَا تَلَىٰهَا

Na kwa mwezi unapo lifuatia!

Na kwa mwezi unapo lifuata na likawa nyuma yake kwa kutoa mwangaza baada ya kuchwa jua,
Na kwa mwezi unapo lifuatia!

وَٱلنَّهَارِ إِذَا جَلَّىٰهَا

Na kwa mchana unapo lidhihirisha!

Na kwa mchana unapo lidhihirisha jua, likaonekana wazi halikufichikana.
Na kwa mchana unapo lidhihirisha!

وَٱلَّيۡلِ إِذَا يَغۡشَىٰهَا

Na kwa usiku unapo lifunika!

Na kwa usiku unapo lifunika jua, ukawa mwangaza wake hauonekani.
Na kwa usiku unapo lifunika!

وَٱلسَّمَآءِ وَمَا بَنَىٰهَا

Na kwa mbingu na kwa aliye ijenga!

Na kwa mbingu na kwa Mweza Mtukufu aliye inyanyua na akaijenga kwa hikima yake.
Na kwa mbingu na kwa aliye ijenga!

وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا طَحَىٰهَا

Na kwa ardhi na kwa aliye itandaza!

Na kwa ardhi na kwa Mweza Mtukufu aliye ikunjua kwa kila upande, na akaitengeneza kwa ajili ya utulivu, na akaifanya kama tandiko.
Na kwa ardhi na kwa aliye itandaza!

وَنَفۡسٖ وَمَا سَوَّىٰهَا

Na kwa nafsi na kwa aliye itengeneza!

Na kwa nafsi, na aliye iumba na akaiweka sawa, kwa kuipa nguvu,
Na kwa nafsi na kwa aliye itengeneza!

فَأَلۡهَمَهَا فُجُورَهَا وَتَقۡوَىٰهَا

Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake!

Akaifunza jema na baya, na akaipa uweza wa kutenda itakayo katika hayo,
Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake!

قَدۡ أَفۡلَحَ مَن زَكَّىٰهَا

Hakika amefanikiwa aliye itakasa!

Hakika amefuzu mwenye kuisafisha nafsi yake kwa ut'iifu na vitendo vya kheri.
Hakika amefanikiwa aliye itakasa!

وَقَدۡ خَابَ مَن دَسَّىٰهَا

Na hakika amekhasiri aliye iviza.

Na hakika amekhasiri mwenye kuzificha fadhila zake, na akayaua matayarisho aliyo umbwa nayo ya kutenda kheri.
Na hakika amekhasiri aliye iviza.

كَذَّبَتۡ ثَمُودُ بِطَغۡوَىٰهَآ

Kina Thamudi walikadhibisha kwa sababu ya upotofu wao,

Kina Thamudi walimkanusha Nabii wao kwa upotovu wao na jeuri zao,
Kina Thamudi walikadhibisha kwa sababu ya upotofu wao,

إِذِ ٱنۢبَعَثَ أَشۡقَىٰهَا

Alipo simama mwovu wao mkubwa,

Alipo gutuka mwovu wao mkubwa kabisa kutaka kumchinja ngamia.
Alipo simama mwovu wao mkubwa,

فَقَالَ لَهُمۡ رَسُولُ ٱللَّهِ نَاقَةَ ٱللَّهِ وَسُقۡيَٰهَا

Hapo Mtume wa Mwenyezi Mungu alipo waambia: Huyu ni ngamia wa Mwenyezi Mungu, mwacheni anywe maji fungu lake.

Saleh, Mtume wa Mwenyezi Mungu, akawaambia: Mwachilieni huyu ngamia wa Mwenyezi Mungu ale maridhawa katika ardhi ya Mwenyezi Mungu, na tahadharini msimzuie maji katika siku yake aliyo wekewa.
Hapo Mtume wa Mwenyezi Mungu alipo waambia: Huyu ni ngamia wa Mwenyezi Mungu, mwacheni anywe maji fungu lake.

فَكَذَّبُوهُ فَعَقَرُوهَا فَدَمۡدَمَ عَلَيۡهِمۡ رَبُّهُم بِذَنۢبِهِمۡ فَسَوَّىٰهَا

Lakini walimkadhibisha na wakamchinja ngamia, kwa hivyo Mola wao Mlezi aliwaangamiza kwa sababu ya dhambi zao na akawafuta kabisa.

Wakamkadhibisha Mtume wao katika hilo onyo lake, wakamchinja. Mola wao Mlezi akazibomoa nyumba zao kwa sababu ya dhambi zao; akazisawazisha na ardhi!
Lakini walimkadhibisha na wakamchinja ngamia, kwa hivyo Mola wao Mlezi aliwaangamiza kwa sababu ya dhambi zao na akawafuta kabisa.

وَلَا يَخَافُ عُقۡبَٰهَا

Wala Yeye haogopi matokeo yake.

Wala Yeye Mwenyezi Mungu hakhofu matokeo ya adhabu hiyo, kwani hiyo ni malipo ya haki kwa yale waliyo yatenda.
Wala Yeye haogopi matokeo yake.
Footer Include