الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني
ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.
قُلۡ أَعُوذُ بِرَبِّ ٱلۡفَلَقِ
Sema: Najikinga kwa Mola Mlezi wa mapambazuko,
Sema najikinga na Mola Mlezi wa asubuhi inapo pambazuka kutokana na usiku.
Sema: Najikinga kwa Mola Mlezi wa mapambazuko,
مِن شَرِّ مَا خَلَقَ
Na shari ya alivyo viumba,
Na shari ya kila chenye shari katika viumbe, ambavyo hapana wa kuzuia shari yao ila Mwenye kumiliki amri yao.
Na shari ya alivyo viumba,
وَمِن شَرِّ غَاسِقٍ إِذَا وَقَبَ
Na shari ya giza la usiku liingiapo,
Na shari ya usiku unapo kuwa totoro.
Na shari ya giza la usiku liingiapo,
وَمِن شَرِّ ٱلنَّفَّٰثَٰتِ فِي ٱلۡعُقَدِ
Na shari ya wanao pulizia mafundoni,
Na shari ya anaye pita baina ya watu kwa sababu ya kuwafisidi.
Na shari ya wanao pulizia mafundoni,
وَمِن شَرِّ حَاسِدٍ إِذَا حَسَدَ
Na shari ya hasidi anapo husudu.
Na shari ya hasidi anaye tamani iondoke neema kwa wengine.
Na shari ya hasidi anapo husudu.
مشاركة عبر