Header Include

Swahili translation - Rowad Translation Center

translated by Rowwad Translation Center, in cooperation with the Islamic Propagation Office in Rabwah and the Association for Serving Islamic Content in Languages.

QR Code https://quran.islamcontent.com/ceb/swahili_rwwad

وَٱلصَّٰٓفَّٰتِ صَفّٗا

Ninaapa kwa wanaojipanga kwa safu.

Ninaapa kwa wanaojipanga kwa safu.

فَٱلزَّٰجِرَٰتِ زَجۡرٗا

Na kwa wenye kukataza mabaya.

Na kwa wenye kukataza mabaya.

فَٱلتَّٰلِيَٰتِ ذِكۡرًا

Na kwa wenye kusoma Ukumbusho.

Na kwa wenye kusoma Ukumbusho.

إِنَّ إِلَٰهَكُمۡ لَوَٰحِدٞ

Hakika Mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja.

Hakika Mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja.

رَّبُّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَا وَرَبُّ ٱلۡمَشَٰرِقِ

Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na yaliyomo kati yake, na ni Mola Mlezi wa mashariki zote.

Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na yaliyomo kati yake, na ni Mola Mlezi wa mashariki zote.

إِنَّا زَيَّنَّا ٱلسَّمَآءَ ٱلدُّنۡيَا بِزِينَةٍ ٱلۡكَوَاكِبِ

Hakika Sisi tumeipamba mbingu ya karibu kwa pambo la nyota.

Hakika Sisi tumeipamba mbingu ya karibu kwa pambo la nyota.

وَحِفۡظٗا مِّن كُلِّ شَيۡطَٰنٖ مَّارِدٖ

Na kulinda na kila shetani muasi.

Na kulinda na kila shetani muasi.

لَّا يَسَّمَّعُونَ إِلَى ٱلۡمَلَإِ ٱلۡأَعۡلَىٰ وَيُقۡذَفُونَ مِن كُلِّ جَانِبٖ

Wasiweze kuwasikiliza viumbe watukufu. Na wanafukuzwa huko kila upande.

Wasiweze kuwasikiliza viumbe watukufu. Na wanafukuzwa huko kila upande.

دُحُورٗاۖ وَلَهُمۡ عَذَابٞ وَاصِبٌ

Wakifurushwa. Na wanayo adhabu ya kudumu.

Wakifurushwa. Na wanayo adhabu ya kudumu.

إِلَّا مَنۡ خَطِفَ ٱلۡخَطۡفَةَ فَأَتۡبَعَهُۥ شِهَابٞ ثَاقِبٞ

Isipokuwa anayenyakua kitu kidogo, na mara humfwatia kimondo kinachong'ara.

Isipokuwa anayenyakua kitu kidogo, na mara humfwatia kimondo kinachong'ara.

فَٱسۡتَفۡتِهِمۡ أَهُمۡ أَشَدُّ خَلۡقًا أَم مَّنۡ خَلَقۡنَآۚ إِنَّا خَلَقۡنَٰهُم مِّن طِينٖ لَّازِبِۭ

Hebu waulize: Je! Wao ni wenye umbo gumu zaidi au hao wengine tuliowaumba. Hakika Sisi tuliwaumba wao kwa udongo unaonata.

Hebu waulize: Je! Wao ni wenye umbo gumu zaidi au hao wengine tuliowaumba. Hakika Sisi tuliwaumba wao kwa udongo unaonata.

بَلۡ عَجِبۡتَ وَيَسۡخَرُونَ

Bali unastaajabu, na wao wanafanya masihara.

Bali unastaajabu, na wao wanafanya masihara.

وَإِذَا ذُكِّرُواْ لَا يَذۡكُرُونَ

Na wanapokumbushwa, hawakumbuki.

Na wanapokumbushwa, hawakumbuki.

وَإِذَا رَأَوۡاْ ءَايَةٗ يَسۡتَسۡخِرُونَ

Na wanapoona Ishara, wanafanya masihara.

Na wanapoona Ishara, wanafanya masihara.

وَقَالُوٓاْ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا سِحۡرٞ مُّبِينٌ

Na husema: Haya si chochote isipokuwa ni uchawi tu ulio dhahiri.

Na husema: Haya si chochote isipokuwa ni uchawi tu ulio dhahiri.

أَءِذَا مِتۡنَا وَكُنَّا تُرَابٗا وَعِظَٰمًا أَءِنَّا لَمَبۡعُوثُونَ

Ati tukishakufa na tukawa udongo na mifupa ndio kweli tutafufuliwa?

Ati tukishakufa na tukawa udongo na mifupa ndio kweli tutafufuliwa?

أَوَءَابَآؤُنَا ٱلۡأَوَّلُونَ

Hata baba zetu wa zamani?

Hata baba zetu wa zamani?

قُلۡ نَعَمۡ وَأَنتُمۡ دَٰخِرُونَ

Sema: Naam! Hali nanyi ni madhalili.

Sema: Naam! Hali nanyi ni madhalili.

فَإِنَّمَا هِيَ زَجۡرَةٞ وَٰحِدَةٞ فَإِذَا هُمۡ يَنظُرُونَ

Huko utapigwa ukelele mmoja tu! Na hapo ndipo wataona!

Huko utapigwa ukelele mmoja tu! Na hapo ndipo wataona!

وَقَالُواْ يَٰوَيۡلَنَا هَٰذَا يَوۡمُ ٱلدِّينِ

Watasema: Ole wetu! Hii ndiyo Siku ya Malipo.

Watasema: Ole wetu! Hii ndiyo Siku ya Malipo.

هَٰذَا يَوۡمُ ٱلۡفَصۡلِ ٱلَّذِي كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ

Hii ndiyo Siku ya Hukumu mliyokuwa mkiikadhibisha.

Hii ndiyo Siku ya Hukumu mliyokuwa mkiikadhibisha.

۞ ٱحۡشُرُواْ ٱلَّذِينَ ظَلَمُواْ وَأَزۡوَٰجَهُمۡ وَمَا كَانُواْ يَعۡبُدُونَ

Wakusanyeni wale waliodhulumu, na wote walio mfano wao, na hao ambao wao walikuwa wakiwaabudu.

Wakusanyeni wale waliodhulumu, na wote walio mfano wao, na hao ambao wao walikuwa wakiwaabudu.

مِن دُونِ ٱللَّهِ فَٱهۡدُوهُمۡ إِلَىٰ صِرَٰطِ ٱلۡجَحِيمِ

Badala ya Mwenyezi Mungu. Waongozeni njia ya Jahannamu!

Badala ya Mwenyezi Mungu. Waongozeni njia ya Jahannamu!

وَقِفُوهُمۡۖ إِنَّهُم مَّسۡـُٔولُونَ

Na wasimamisheni. Hakika hao wataulizwa:

Na wasimamisheni. Hakika hao wataulizwa:

مَا لَكُمۡ لَا تَنَاصَرُونَ

Mna nini? Mbona hamsaidiani?

Mna nini? Mbona hamsaidiani?

بَلۡ هُمُ ٱلۡيَوۡمَ مُسۡتَسۡلِمُونَ

Bali hii leo, watasalimu amri.

Bali hii leo, watasalimu amri.

وَأَقۡبَلَ بَعۡضُهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖ يَتَسَآءَلُونَ

Wataelekeana wao kwa wao kuulizana.

Wataelekeana wao kwa wao kuulizana.

قَالُوٓاْ إِنَّكُمۡ كُنتُمۡ تَأۡتُونَنَا عَنِ ٱلۡيَمِينِ

Watasema: Kwa hakika nyinyi mlikuwa mkitujia upande wa kulia.

Watasema: Kwa hakika nyinyi mlikuwa mkitujia upande wa kulia.

قَالُواْ بَل لَّمۡ تَكُونُواْ مُؤۡمِنِينَ

Watasema (wakubwa): Bali nyinyi wenyewe hamkuwa Waumini.

Watasema (wakubwa): Bali nyinyi wenyewe hamkuwa Waumini.

وَمَا كَانَ لَنَا عَلَيۡكُم مِّن سُلۡطَٰنِۭۖ بَلۡ كُنتُمۡ قَوۡمٗا طَٰغِينَ

Sisi hatukuwa na mamlaka juu yenu, bali nyinyi wenyewe mlikuwa wapotovu.

Sisi hatukuwa na mamlaka juu yenu, bali nyinyi wenyewe mlikuwa wapotovu.

فَحَقَّ عَلَيۡنَا قَوۡلُ رَبِّنَآۖ إِنَّا لَذَآئِقُونَ

Basi hukumu ya Mola wetu Mlezi imekwisha tuthibitikia. Hakika bila ya shaka tutaonja tu adhabu.

Basi hukumu ya Mola wetu Mlezi imekwisha tuthibitikia. Hakika bila ya shaka tutaonja tu adhabu.

فَأَغۡوَيۡنَٰكُمۡ إِنَّا كُنَّا غَٰوِينَ

Tulikupotezeni kwa sababu sisi wenyewe tulikuwa wapotovu.

Tulikupotezeni kwa sababu sisi wenyewe tulikuwa wapotovu.

فَإِنَّهُمۡ يَوۡمَئِذٖ فِي ٱلۡعَذَابِ مُشۡتَرِكُونَ

Basi wao kwa hakika siku hiyo watashirikiana katika adhabu pamoja.

Basi wao kwa hakika siku hiyo watashirikiana katika adhabu pamoja.

إِنَّا كَذَٰلِكَ نَفۡعَلُ بِٱلۡمُجۡرِمِينَ

Hivyo ndivyo tutakavyowafanyia wahalifu.

Hivyo ndivyo tutakavyowafanyia wahalifu.

إِنَّهُمۡ كَانُوٓاْ إِذَا قِيلَ لَهُمۡ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا ٱللَّهُ يَسۡتَكۡبِرُونَ

Wao walipokuwa wakiambiwa, "La ilaha illallaahu (Hapana mungu ila Mwenyezi Mungu tu)", wanajivuna.

Wao walipokuwa wakiambiwa, "La ilaha illallaahu (Hapana mungu ila Mwenyezi Mungu tu)", wanajivuna.

وَيَقُولُونَ أَئِنَّا لَتَارِكُوٓاْ ءَالِهَتِنَا لِشَاعِرٖ مَّجۡنُونِۭ

Na wakisema: Hivyo sisi tuiache miungu yetu kwa ajili ya huyu mtunga mashairi mwendawazimu?

Na wakisema: Hivyo sisi tuiache miungu yetu kwa ajili ya huyu mtunga mashairi mwendawazimu?

بَلۡ جَآءَ بِٱلۡحَقِّ وَصَدَّقَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Bali huyu amekuja kwa haki, na amewasadikisha Mitume.

Bali huyu amekuja kwa haki, na amewasadikisha Mitume.

إِنَّكُمۡ لَذَآئِقُواْ ٱلۡعَذَابِ ٱلۡأَلِيمِ

Hakika nyinyi bila ya shaka mtaionja adhabu chungu.

Hakika nyinyi bila ya shaka mtaionja adhabu chungu.

وَمَا تُجۡزَوۡنَ إِلَّا مَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ

Wala hamlipwi isipokuwa hayo mliyokuwa mkiyafanya.

Wala hamlipwi isipokuwa hayo mliyokuwa mkiyafanya.

إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلۡمُخۡلَصِينَ

Isipokuwa waja wa Mwenyezi Mungu walioteuliwa.

Isipokuwa waja wa Mwenyezi Mungu walioteuliwa.

أُوْلَٰٓئِكَ لَهُمۡ رِزۡقٞ مَّعۡلُومٞ

Hao ndio watakaopata riziki maalumu.

Hao ndio watakaopata riziki maalumu.

فَوَٰكِهُ وَهُم مُّكۡرَمُونَ

Matunda, nao wataheshimiwa.

Matunda, nao wataheshimiwa.

فِي جَنَّٰتِ ٱلنَّعِيمِ

Katika Bustani za neema.

Katika Bustani za neema.

عَلَىٰ سُرُرٖ مُّتَقَٰبِلِينَ

Wako juu ya viti mfano wa kitanda wameelekeana.

Wako juu ya viti mfano wa kitanda wameelekeana.

يُطَافُ عَلَيۡهِم بِكَأۡسٖ مِّن مَّعِينِۭ

Wanazungushiwa kikombe chenye kinywaji cha chemchemi.

Wanazungushiwa kikombe chenye kinywaji cha chemchemi.

بَيۡضَآءَ لَذَّةٖ لِّلشَّٰرِبِينَ

Kinywaji cheupe, kitamu kwa wanywao.

Kinywaji cheupe, kitamu kwa wanywao.

لَا فِيهَا غَوۡلٞ وَلَا هُمۡ عَنۡهَا يُنزَفُونَ

Hakina madhara, wala hakiwaleweshi.

Hakina madhara, wala hakiwaleweshi.

وَعِندَهُمۡ قَٰصِرَٰتُ ٱلطَّرۡفِ عِينٞ

Na watakuwa nao wanawake wenye macho ya staha, mazuri.

Na watakuwa nao wanawake wenye macho ya staha, mazuri.

كَأَنَّهُنَّ بَيۡضٞ مَّكۡنُونٞ

Hao wanawake kama mayai yaliyohifadhika.

Hao wanawake kama mayai yaliyohifadhika.

فَأَقۡبَلَ بَعۡضُهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖ يَتَسَآءَلُونَ

Basi wakaelekeana kuulizana wenyewe kwa wenyewe.

Basi wakaelekeana kuulizana wenyewe kwa wenyewe.

قَالَ قَآئِلٞ مِّنۡهُمۡ إِنِّي كَانَ لِي قَرِينٞ

Aseme msemaji mmoja miongoni mwao: Hakika mimi nilikuwa na rafiki.

Aseme msemaji mmoja miongoni mwao: Hakika mimi nilikuwa na rafiki.

يَقُولُ أَءِنَّكَ لَمِنَ ٱلۡمُصَدِّقِينَ

Aliyekuwa akiniambia: Hivyo wewe ni katika wanaosadiki.

Aliyekuwa akiniambia: Hivyo wewe ni katika wanaosadiki.

أَءِذَا مِتۡنَا وَكُنَّا تُرَابٗا وَعِظَٰمًا أَءِنَّا لَمَدِينُونَ

Ati tukishakufa tukawa udongo na mafupa, ndiyo tutalipwa na kufanyiwa hesabu?

Ati tukishakufa tukawa udongo na mafupa, ndiyo tutalipwa na kufanyiwa hesabu?

قَالَ هَلۡ أَنتُم مُّطَّلِعُونَ

Atasema: Je, nyie mnawaona?

Atasema: Je, nyie mnawaona?

فَٱطَّلَعَ فَرَءَاهُ فِي سَوَآءِ ٱلۡجَحِيمِ

Basi atachungulia amwone katikati ya Jahannamu.

Basi atachungulia amwone katikati ya Jahannamu.

قَالَ تَٱللَّهِ إِن كِدتَّ لَتُرۡدِينِ

Atasema: Wallahi! (Naapa kwa jina la Mwenyezi Mungu) Ulikaribia sana kunipoteza.

Atasema: Wallahi! (Naapa kwa jina la Mwenyezi Mungu) Ulikaribia sana kunipoteza.

وَلَوۡلَا نِعۡمَةُ رَبِّي لَكُنتُ مِنَ ٱلۡمُحۡضَرِينَ

Na lau kuwa si neema ya Mola wangu Mlezi, bila ya shaka ningelikuwa miongoni mwa waliohudhurishwa.

Na lau kuwa si neema ya Mola wangu Mlezi, bila ya shaka ningelikuwa miongoni mwa waliohudhurishwa.

أَفَمَا نَحۡنُ بِمَيِّتِينَ

Je, sisi hatutakufa?

Je, sisi hatutakufa?

إِلَّا مَوۡتَتَنَا ٱلۡأُولَىٰ وَمَا نَحۡنُ بِمُعَذَّبِينَ

Isipokuwa kifo chetu cha kwanza? Wala sisi hatutaadhibiwa.

Isipokuwa kifo chetu cha kwanza? Wala sisi hatutaadhibiwa.

إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡعَظِيمُ

Hakika huku bila ya shaka ndiko kufuzu kukubwa.

Hakika huku bila ya shaka ndiko kufuzu kukubwa.

لِمِثۡلِ هَٰذَا فَلۡيَعۡمَلِ ٱلۡعَٰمِلُونَ

Kwa mfano wa haya na watende watendao.

Kwa mfano wa haya na watende watendao.

أَذَٰلِكَ خَيۡرٞ نُّزُلًا أَمۡ شَجَرَةُ ٱلزَّقُّومِ

Je, kukaribishwa hivi si ndiyo bora, au mti wa Zaqqum?

Je, kukaribishwa hivi si ndiyo bora, au mti wa Zaqqum?

إِنَّا جَعَلۡنَٰهَا فِتۡنَةٗ لِّلظَّٰلِمِينَ

Hakika Sisi tumeufanya huo kuwa ni mateso kwa waliodhulumu.

Hakika Sisi tumeufanya huo kuwa ni mateso kwa waliodhulumu.

إِنَّهَا شَجَرَةٞ تَخۡرُجُ فِيٓ أَصۡلِ ٱلۡجَحِيمِ

Hakika huo ni mti unaotoka katikati ya Jahannamu.

Hakika huo ni mti unaotoka katikati ya Jahannamu.

طَلۡعُهَا كَأَنَّهُۥ رُءُوسُ ٱلشَّيَٰطِينِ

Mashada ya matunda yake kama kwamba ni vichwa vya mashetani.

Mashada ya matunda yake kama kwamba ni vichwa vya mashetani.

فَإِنَّهُمۡ لَأٓكِلُونَ مِنۡهَا فَمَالِـُٔونَ مِنۡهَا ٱلۡبُطُونَ

Basi hakika bila ya shaka hao watayala hayo, na wajaze matumbo kwayo.

Basi hakika bila ya shaka hao watayala hayo, na wajaze matumbo kwayo.

ثُمَّ إِنَّ لَهُمۡ عَلَيۡهَا لَشَوۡبٗا مِّنۡ حَمِيمٖ

Kisha juu yake wanyweshwe mchanganyo wa maji ya moto yaliyochemka.

Kisha juu yake wanyweshwe mchanganyo wa maji ya moto yaliyochemka.

ثُمَّ إِنَّ مَرۡجِعَهُمۡ لَإِلَى ٱلۡجَحِيمِ

Kisha hakika marejeo yao bila ya shaka yatakuwa Jahimu.

Kisha hakika marejeo yao bila ya shaka yatakuwa Jahimu.

إِنَّهُمۡ أَلۡفَوۡاْ ءَابَآءَهُمۡ ضَآلِّينَ

Hakika waliwakuta baba zao wamepotea.

Hakika waliwakuta baba zao wamepotea.

فَهُمۡ عَلَىٰٓ ءَاثَٰرِهِمۡ يُهۡرَعُونَ

Na wao wakafanya haraka kufuata nyayo zao.

Na wao wakafanya haraka kufuata nyayo zao.

وَلَقَدۡ ضَلَّ قَبۡلَهُمۡ أَكۡثَرُ ٱلۡأَوَّلِينَ

Na bila ya shaka walikwisha potea kabla yao wengi wa watu wa zamani.

Na bila ya shaka walikwisha potea kabla yao wengi wa watu wa zamani.

وَلَقَدۡ أَرۡسَلۡنَا فِيهِم مُّنذِرِينَ

Na Sisi hakika tuliwapelekea waonyaji.

Na Sisi hakika tuliwapelekea waonyaji.

فَٱنظُرۡ كَيۡفَ كَانَ عَٰقِبَةُ ٱلۡمُنذَرِينَ

Basi hebu angalia ulikuwaje mwisho wa walioonywa.

Basi hebu angalia ulikuwaje mwisho wa walioonywa.

إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلۡمُخۡلَصِينَ

Isipokuwa waja wa Mwenyezi Mungu waliosafishwa.

Isipokuwa waja wa Mwenyezi Mungu waliosafishwa.

وَلَقَدۡ نَادَىٰنَا نُوحٞ فَلَنِعۡمَ ٱلۡمُجِيبُونَ

Na hakika Nuhu alituita, na Sisi ni bora wa waitikiaji.

Na hakika Nuhu alituita, na Sisi ni bora wa waitikiaji.

وَنَجَّيۡنَٰهُ وَأَهۡلَهُۥ مِنَ ٱلۡكَرۡبِ ٱلۡعَظِيمِ

Na tulimwokoa yeye na ahali zake kutokana na msiba mkubwa.

Na tulimwokoa yeye na ahali zake kutokana na msiba mkubwa.

وَجَعَلۡنَا ذُرِّيَّتَهُۥ هُمُ ٱلۡبَاقِينَ

Na tuliwajaalia dhuria zake ndio wenye kubakia.

Na tuliwajaalia dhuria zake ndio wenye kubakia.

وَتَرَكۡنَا عَلَيۡهِ فِي ٱلۡأٓخِرِينَ

Na tukamwachia (sifa njema) kwa waliokuja baadaye.

Na tukamwachia (sifa njema) kwa waliokuja baadaye.

سَلَٰمٌ عَلَىٰ نُوحٖ فِي ٱلۡعَٰلَمِينَ

Iwe salama kwa Nuhu ulimwenguni kote!

Iwe salama kwa Nuhu ulimwenguni kote!

إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ

Kwa hakika hivi ndivyo tunavyowalipa wanaofanya mema.

Kwa hakika hivi ndivyo tunavyowalipa wanaofanya mema.

إِنَّهُۥ مِنۡ عِبَادِنَا ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Hakika yeye ni katika waja wetu walioamini.

Hakika yeye ni katika waja wetu walioamini.

ثُمَّ أَغۡرَقۡنَا ٱلۡأٓخَرِينَ

Kisha tukawazamisha wale wengine.

Kisha tukawazamisha wale wengine.

۞ وَإِنَّ مِن شِيعَتِهِۦ لَإِبۡرَٰهِيمَ

Na hakika Ibrahim alikuwa katika kundi lake.

Na hakika Ibrahim alikuwa katika kundi lake.

إِذۡ جَآءَ رَبَّهُۥ بِقَلۡبٖ سَلِيمٍ

Alipomjia Mola wake Mlezi kwa moyo mzima.

Alipomjia Mola wake Mlezi kwa moyo mzima.

إِذۡ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوۡمِهِۦ مَاذَا تَعۡبُدُونَ

Alimwambia baba yake na watu wake: Mnaabudu nini?

Alimwambia baba yake na watu wake: Mnaabudu nini?

أَئِفۡكًا ءَالِهَةٗ دُونَ ٱللَّهِ تُرِيدُونَ

Kwa kuzua tu mnataka miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu?

Kwa kuzua tu mnataka miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu?

فَمَا ظَنُّكُم بِرَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Mnamdhania nini Mola Mlezi wa walimwengu wote?"

Mnamdhania nini Mola Mlezi wa walimwengu wote?"

فَنَظَرَ نَظۡرَةٗ فِي ٱلنُّجُومِ

Kisha akapiga jicho kutazama nyota.

Kisha akapiga jicho kutazama nyota.

فَقَالَ إِنِّي سَقِيمٞ

Akasema: Hakika mimi ni mgonjwa!

Akasema: Hakika mimi ni mgonjwa!

فَتَوَلَّوۡاْ عَنۡهُ مُدۡبِرِينَ

Nao wakamwacha, wakampa kisogo.

Nao wakamwacha, wakampa kisogo.

فَرَاغَ إِلَىٰٓ ءَالِهَتِهِمۡ فَقَالَ أَلَا تَأۡكُلُونَ

Basi akaiendea miungu yao kwa siri, akaiambia: Mbona hamli?

Basi akaiendea miungu yao kwa siri, akaiambia: Mbona hamli?

مَا لَكُمۡ لَا تَنطِقُونَ

Mna nini hata hamsemi?

Mna nini hata hamsemi?

فَرَاغَ عَلَيۡهِمۡ ضَرۡبَۢا بِٱلۡيَمِينِ

Kisha akaigeukia kuipiga kwa mkono wa kulia.

Kisha akaigeukia kuipiga kwa mkono wa kulia.

فَأَقۡبَلُوٓاْ إِلَيۡهِ يَزِفُّونَ

Basi wakamjia upesi upesi.

Basi wakamjia upesi upesi.

قَالَ أَتَعۡبُدُونَ مَا تَنۡحِتُونَ

Akasema: Hivyo mnaviabudu vitu mnavyovichonga wenyewe?

Akasema: Hivyo mnaviabudu vitu mnavyovichonga wenyewe?

وَٱللَّهُ خَلَقَكُمۡ وَمَا تَعۡمَلُونَ

Na hali Mwenyezi Mungu ndiye aliyekuumbeni nyinyi na hivyo mnavyovifanya!

Na hali Mwenyezi Mungu ndiye aliyekuumbeni nyinyi na hivyo mnavyovifanya!

قَالُواْ ٱبۡنُواْ لَهُۥ بُنۡيَٰنٗا فَأَلۡقُوهُ فِي ٱلۡجَحِيمِ

Wakasema: Mjengeeni jengo, na kisha mtupeni motoni humo!

Wakasema: Mjengeeni jengo, na kisha mtupeni motoni humo!

فَأَرَادُواْ بِهِۦ كَيۡدٗا فَجَعَلۡنَٰهُمُ ٱلۡأَسۡفَلِينَ

Basi walitaka kumfanyia vitimbi, lakini tukawafanya wao ndio wa chini zaidi.

Basi walitaka kumfanyia vitimbi, lakini tukawafanya wao ndio wa chini zaidi.

وَقَالَ إِنِّي ذَاهِبٌ إِلَىٰ رَبِّي سَيَهۡدِينِ

Na akasema: Hakika mimi nahama, nakwenda kwa Mola wangu Mlezi; Yeye ataniongoa.

Na akasema: Hakika mimi nahama, nakwenda kwa Mola wangu Mlezi; Yeye ataniongoa.

رَبِّ هَبۡ لِي مِنَ ٱلصَّٰلِحِينَ

Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni mwa watenda mema.

Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni mwa watenda mema.

فَبَشَّرۡنَٰهُ بِغُلَٰمٍ حَلِيمٖ

Basi tukambashiria mwana aliye mpole.

Basi tukambashiria mwana aliye mpole.

فَلَمَّا بَلَغَ مَعَهُ ٱلسَّعۡيَ قَالَ يَٰبُنَيَّ إِنِّيٓ أَرَىٰ فِي ٱلۡمَنَامِ أَنِّيٓ أَذۡبَحُكَ فَٱنظُرۡ مَاذَا تَرَىٰۚ قَالَ يَٰٓأَبَتِ ٱفۡعَلۡ مَا تُؤۡمَرُۖ سَتَجِدُنِيٓ إِن شَآءَ ٱللَّهُ مِنَ ٱلصَّٰبِرِينَ

Basi alipofika makamo ya kwenda na kurudi pamoja naye, alimwambia: Ewe mwanangu! Hakika mimi nimeona usingizini kuwa ninakuchinja. Basi angalia wewe, waonaje? Akasema: Ewe baba yangu! Tenda unavyoamrishwa, utanikuta mimi, Insha Allah (Mwenyezi Mungu akipenda), katika wanaosubiri.

Basi alipofika makamo ya kwenda na kurudi pamoja naye, alimwambia: Ewe mwanangu! Hakika mimi nimeona usingizini kuwa ninakuchinja. Basi angalia wewe, waonaje? Akasema: Ewe baba yangu! Tenda unavyoamrishwa, utanikuta mimi, Insha Allah (Mwenyezi Mungu akipenda), katika wanaosubiri.

فَلَمَّآ أَسۡلَمَا وَتَلَّهُۥ لِلۡجَبِينِ

Basi wote wawili walipojisalimisha, na akamlaza juu ya kipaji.

Basi wote wawili walipojisalimisha, na akamlaza juu ya kipaji.

وَنَٰدَيۡنَٰهُ أَن يَٰٓإِبۡرَٰهِيمُ

Tulimwita: Ewe Ibrahim!

Tulimwita: Ewe Ibrahim!

قَدۡ صَدَّقۡتَ ٱلرُّءۡيَآۚ إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ

Umekwisha itimiliza ndoto. Hakika hivi ndivyo tunavyowalipa wanaotenda mema.

Umekwisha itimiliza ndoto. Hakika hivi ndivyo tunavyowalipa wanaotenda mema.

إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ ٱلۡبَلَٰٓؤُاْ ٱلۡمُبِينُ

Hakika haya ni majaribio yaliyo dhahiri.

Hakika haya ni majaribio yaliyo dhahiri.

وَفَدَيۡنَٰهُ بِذِبۡحٍ عَظِيمٖ

Basi tukamtolea fidia kwa dhabihu mtukufu.

Basi tukamtolea fidia kwa dhabihu mtukufu.

وَتَرَكۡنَا عَلَيۡهِ فِي ٱلۡأٓخِرِينَ

Na tukamwachia (sifa njema) kwa watu waliokuja baadaye.

Na tukamwachia (sifa njema) kwa watu waliokuja baadaye.

سَلَٰمٌ عَلَىٰٓ إِبۡرَٰهِيمَ

Iwe salama kwa Ibrahim!

Iwe salama kwa Ibrahim!

كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ

Hivi ndivyo tunavyowalipa wanaofanya mema.

Hivi ndivyo tunavyowalipa wanaofanya mema.

إِنَّهُۥ مِنۡ عِبَادِنَا ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Hakika yeye ni katika waja wetu walioamini.

Hakika yeye ni katika waja wetu walioamini.

وَبَشَّرۡنَٰهُ بِإِسۡحَٰقَ نَبِيّٗا مِّنَ ٱلصَّٰلِحِينَ

Na tukambashiria kuzaliwa Is-haqa, naye ni Nabii miongoni mwa watu wema.

Na tukambashiria kuzaliwa Is-haqa, naye ni Nabii miongoni mwa watu wema.

وَبَٰرَكۡنَا عَلَيۡهِ وَعَلَىٰٓ إِسۡحَٰقَۚ وَمِن ذُرِّيَّتِهِمَا مُحۡسِنٞ وَظَالِمٞ لِّنَفۡسِهِۦ مُبِينٞ

Na tukambarikia yeye na Is-haqa. Na miongoni mwa dhuria zao walitokea wema na wenye kudhulumu nafsi zao waziwazi.

Na tukambarikia yeye na Is-haqa. Na miongoni mwa dhuria zao walitokea wema na wenye kudhulumu nafsi zao waziwazi.

وَلَقَدۡ مَنَنَّا عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَٰرُونَ

Na kwa hakika tuliwafanyia hisani Musa na Haruni.

Na kwa hakika tuliwafanyia hisani Musa na Haruni.

وَنَجَّيۡنَٰهُمَا وَقَوۡمَهُمَا مِنَ ٱلۡكَرۡبِ ٱلۡعَظِيمِ

Na tukawaokoa wao na watu wao kutokana na dhiki kubwa.

Na tukawaokoa wao na watu wao kutokana na dhiki kubwa.

وَنَصَرۡنَٰهُمۡ فَكَانُواْ هُمُ ٱلۡغَٰلِبِينَ

Na tukawanusuru; na wakawa wao ndio wenye kushinda.

Na tukawanusuru; na wakawa wao ndio wenye kushinda.

وَءَاتَيۡنَٰهُمَا ٱلۡكِتَٰبَ ٱلۡمُسۡتَبِينَ

Na tukawapa wawili hao Kitabu kinachobainisha.

Na tukawapa wawili hao Kitabu kinachobainisha.

وَهَدَيۡنَٰهُمَا ٱلصِّرَٰطَ ٱلۡمُسۡتَقِيمَ

Na tukawaongoa kwenye njia iliyonyooka.

Na tukawaongoa kwenye njia iliyonyooka.

وَتَرَكۡنَا عَلَيۡهِمَا فِي ٱلۡأٓخِرِينَ

Na tukawaachia (sifa njema) katika watu waliokuja baadaye.

Na tukawaachia (sifa njema) katika watu waliokuja baadaye.

سَلَٰمٌ عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَٰرُونَ

Iwe salama kwa Musa na Haruni!

Iwe salama kwa Musa na Haruni!

إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ

Hakika hivyo ndivyo tunavyowalipa walio wema.

Hakika hivyo ndivyo tunavyowalipa walio wema.

إِنَّهُمَا مِنۡ عِبَادِنَا ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Hakika wawili hao ni katika waja wetu walioamini.

Hakika wawili hao ni katika waja wetu walioamini.

وَإِنَّ إِلۡيَاسَ لَمِنَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Na hakika Ilyas bila ya shaka alikuwa miongoni mwa Mitume.

Na hakika Ilyas bila ya shaka alikuwa miongoni mwa Mitume.

إِذۡ قَالَ لِقَوۡمِهِۦٓ أَلَا تَتَّقُونَ

Alipowaambia watu wake: Hamumchi Mungu?

Alipowaambia watu wake: Hamumchi Mungu?

أَتَدۡعُونَ بَعۡلٗا وَتَذَرُونَ أَحۡسَنَ ٱلۡخَٰلِقِينَ

Mnamwomba Baa'li na mnamwacha Mbora wa waumbaji.

Mnamwomba Baa'li na mnamwacha Mbora wa waumbaji.

ٱللَّهَ رَبَّكُمۡ وَرَبَّ ءَابَآئِكُمُ ٱلۡأَوَّلِينَ

Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa zamani?

Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa zamani?

فَكَذَّبُوهُ فَإِنَّهُمۡ لَمُحۡضَرُونَ

Wakamkadhibisha. Basi kwa hakika watahudhurishwa.

Wakamkadhibisha. Basi kwa hakika watahudhurishwa.

إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلۡمُخۡلَصِينَ

Isipokuwa waja wa Mwenyezi Mungu waliosafishwa.

Isipokuwa waja wa Mwenyezi Mungu waliosafishwa.

وَتَرَكۡنَا عَلَيۡهِ فِي ٱلۡأٓخِرِينَ

Na tumemwachia (sifa nzuri) kwa waliokuja baadaye.

Na tumemwachia (sifa nzuri) kwa waliokuja baadaye.

سَلَٰمٌ عَلَىٰٓ إِلۡ يَاسِينَ

Iwe salama kwa Ilyas.

Iwe salama kwa Ilyas.

إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ

Hakika hivyo ndivyo tunavyowalipa walio wema.

Hakika hivyo ndivyo tunavyowalipa walio wema.

إِنَّهُۥ مِنۡ عِبَادِنَا ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Hakika yeye ni katika waja wetu walioamini.

Hakika yeye ni katika waja wetu walioamini.

وَإِنَّ لُوطٗا لَّمِنَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Na hakika Lut'i bila ya shaka ni miongoni mwa Mitume.

Na hakika Lut'i bila ya shaka ni miongoni mwa Mitume.

إِذۡ نَجَّيۡنَٰهُ وَأَهۡلَهُۥٓ أَجۡمَعِينَ

Tulipomwokoa yeye na ahali zake wote.

Tulipomwokoa yeye na ahali zake wote.

إِلَّا عَجُوزٗا فِي ٱلۡغَٰبِرِينَ

Isipokuwa mwanamke mkongwe katika wale waliobakia nyuma.

Isipokuwa mwanamke mkongwe katika wale waliobakia nyuma.

ثُمَّ دَمَّرۡنَا ٱلۡأٓخَرِينَ

Kisha tukawaangamiza wale wengineo.

Kisha tukawaangamiza wale wengineo.

وَإِنَّكُمۡ لَتَمُرُّونَ عَلَيۡهِم مُّصۡبِحِينَ

Na hakika nyinyi mnawapitia wakati wa asubuhi.

Na hakika nyinyi mnawapitia wakati wa asubuhi.

وَبِٱلَّيۡلِۚ أَفَلَا تَعۡقِلُونَ

Na usiku. Basi je, hamyatii akilini?

Na usiku. Basi je, hamyatii akilini?

وَإِنَّ يُونُسَ لَمِنَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Na hakika Yunus alikuwa miongoni mwa Mitume.

Na hakika Yunus alikuwa miongoni mwa Mitume.

إِذۡ أَبَقَ إِلَى ٱلۡفُلۡكِ ٱلۡمَشۡحُونِ

Alipokimbia akenda katika jahazi lililosheheni.

Alipokimbia akenda katika jahazi lililosheheni.

فَسَاهَمَ فَكَانَ مِنَ ٱلۡمُدۡحَضِينَ

Akaingia katika kupigiwa kura, na akawa katika walioshindwa.

Akaingia katika kupigiwa kura, na akawa katika walioshindwa.

فَٱلۡتَقَمَهُ ٱلۡحُوتُ وَهُوَ مُلِيمٞ

Samaki akammeza hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa.

Samaki akammeza hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa.

فَلَوۡلَآ أَنَّهُۥ كَانَ مِنَ ٱلۡمُسَبِّحِينَ

Na ingelikuwa hakuwa katika wanaomtakasa Mwenyezi Mungu.

Na ingelikuwa hakuwa katika wanaomtakasa Mwenyezi Mungu.

لَلَبِثَ فِي بَطۡنِهِۦٓ إِلَىٰ يَوۡمِ يُبۡعَثُونَ

Bila ya shaka angelikaa ndani yake mpaka siku ya kufufuliwa.

Bila ya shaka angelikaa ndani yake mpaka siku ya kufufuliwa.

۞ فَنَبَذۡنَٰهُ بِٱلۡعَرَآءِ وَهُوَ سَقِيمٞ

Lakini tulimtupa ufukweni patupu, hali yu mgonjwa.

Lakini tulimtupa ufukweni patupu, hali yu mgonjwa.

وَأَنۢبَتۡنَا عَلَيۡهِ شَجَرَةٗ مِّن يَقۡطِينٖ

Na tukauotesha juu yake mmea wa aina ya mung'unye.

Na tukauotesha juu yake mmea wa aina ya mung'unye.

وَأَرۡسَلۡنَٰهُ إِلَىٰ مِاْئَةِ أَلۡفٍ أَوۡ يَزِيدُونَ

Na tulimtuma kwa watu laki moja au zaidi.

Na tulimtuma kwa watu laki moja au zaidi.

فَـَٔامَنُواْ فَمَتَّعۡنَٰهُمۡ إِلَىٰ حِينٖ

Basi wakaamini, na tukawastarehesha kwa muda.

Basi wakaamini, na tukawastarehesha kwa muda.

فَٱسۡتَفۡتِهِمۡ أَلِرَبِّكَ ٱلۡبَنَاتُ وَلَهُمُ ٱلۡبَنُونَ

Basi waulize: Ati Mola wako Mlezi ndiye mwenye watoto wa kike, na wao wanao watoto wa kiume?

Basi waulize: Ati Mola wako Mlezi ndiye mwenye watoto wa kike, na wao wanao watoto wa kiume?

أَمۡ خَلَقۡنَا ٱلۡمَلَٰٓئِكَةَ إِنَٰثٗا وَهُمۡ شَٰهِدُونَ

Au tumewaumba Malaika kuwa ni wanawake, na wao wakashuhudia?

Au tumewaumba Malaika kuwa ni wanawake, na wao wakashuhudia?

أَلَآ إِنَّهُم مِّنۡ إِفۡكِهِمۡ لَيَقُولُونَ

Tazama, hakika ni kwa uzushi wao ndio wanasema.

Tazama, hakika ni kwa uzushi wao ndio wanasema.

وَلَدَ ٱللَّهُ وَإِنَّهُمۡ لَكَٰذِبُونَ

Mwenyezi Mungu amezaa! Ama hakika bila ya shaka hao ni waongo!

Mwenyezi Mungu amezaa! Ama hakika bila ya shaka hao ni waongo!

أَصۡطَفَى ٱلۡبَنَاتِ عَلَى ٱلۡبَنِينَ

Ati amehiari watoto wa kike kuliko wanaume?

Ati amehiari watoto wa kike kuliko wanaume?

مَا لَكُمۡ كَيۡفَ تَحۡكُمُونَ

Mna nini? Mnahukumu vipi nyinyi?

Mna nini? Mnahukumu vipi nyinyi?

أَفَلَا تَذَكَّرُونَ

Hamkumbuki?

Hamkumbuki?

أَمۡ لَكُمۡ سُلۡطَٰنٞ مُّبِينٞ

Au mnayo hoja iliyo wazi?

Au mnayo hoja iliyo wazi?

فَأۡتُواْ بِكِتَٰبِكُمۡ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ

Basi leteni Kitabu chenu kama nyinyi ni wakweli.

Basi leteni Kitabu chenu kama nyinyi ni wakweli.

وَجَعَلُواْ بَيۡنَهُۥ وَبَيۡنَ ٱلۡجِنَّةِ نَسَبٗاۚ وَلَقَدۡ عَلِمَتِ ٱلۡجِنَّةُ إِنَّهُمۡ لَمُحۡضَرُونَ

Na wameweka mahusiano ya nasaba baina yake na majini; na majini wamekwishajua bila ya shaka kuwa wao watahudhurishwa.

Na wameweka mahusiano ya nasaba baina yake na majini; na majini wamekwishajua bila ya shaka kuwa wao watahudhurishwa.

سُبۡحَٰنَ ٱللَّهِ عَمَّا يَصِفُونَ

Ametakasika Mwenyezi Mungu mbali na hayo wanayomsingizia.

Ametakasika Mwenyezi Mungu mbali na hayo wanayomsingizia.

إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلۡمُخۡلَصِينَ

Isipokuwa waja wa Mwenyezi Mungu waliosafishwa.

Isipokuwa waja wa Mwenyezi Mungu waliosafishwa.

فَإِنَّكُمۡ وَمَا تَعۡبُدُونَ

Basi hakika nyinyi na mnaowaabudu.

Basi hakika nyinyi na mnaowaabudu.

مَآ أَنتُمۡ عَلَيۡهِ بِفَٰتِنِينَ

Hamwezi kuwapoteza.

Hamwezi kuwapoteza.

إِلَّا مَنۡ هُوَ صَالِ ٱلۡجَحِيمِ

Isipokuwa yule atakayeingia Motoni.

Isipokuwa yule atakayeingia Motoni.

وَمَا مِنَّآ إِلَّا لَهُۥ مَقَامٞ مَّعۡلُومٞ

Na hapana katika sisi ila anapo mahali pake maalumu.

Na hapana katika sisi ila anapo mahali pake maalumu.

وَإِنَّا لَنَحۡنُ ٱلصَّآفُّونَ

Na hakika bila ya shaka sisi ndio wajipangao safu.

Na hakika bila ya shaka sisi ndio wajipangao safu.

وَإِنَّا لَنَحۡنُ ٱلۡمُسَبِّحُونَ

Na hakika sisi ndio wenye kutakasa.

Na hakika sisi ndio wenye kutakasa.

وَإِن كَانُواْ لَيَقُولُونَ

Na walikuwapo waliokuwa wakisema.

Na walikuwapo waliokuwa wakisema.

لَوۡ أَنَّ عِندَنَا ذِكۡرٗا مِّنَ ٱلۡأَوَّلِينَ

Tungelikuwa na Ukumbusho kama wa watu wa zamani.

Tungelikuwa na Ukumbusho kama wa watu wa zamani.

لَكُنَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلۡمُخۡلَصِينَ

Bila ya shaka tungelikuwa ni waja wa Mwenyezi Mungu wenye kumkusudia Yeye tu.

Bila ya shaka tungelikuwa ni waja wa Mwenyezi Mungu wenye kumkusudia Yeye tu.

فَكَفَرُواْ بِهِۦۖ فَسَوۡفَ يَعۡلَمُونَ

Lakini waliukufuru. Basi watakuja jua.

Lakini waliukufuru. Basi watakuja jua.

وَلَقَدۡ سَبَقَتۡ كَلِمَتُنَا لِعِبَادِنَا ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Na bila ya shaka neno letu lilikwisha tangulia kwa waja wetu waliotumwa.

Na bila ya shaka neno letu lilikwisha tangulia kwa waja wetu waliotumwa.

إِنَّهُمۡ لَهُمُ ٱلۡمَنصُورُونَ

Ya kuwa wao bila ya shaka ndio watakaonusuriwa.

Ya kuwa wao bila ya shaka ndio watakaonusuriwa.

وَإِنَّ جُندَنَا لَهُمُ ٱلۡغَٰلِبُونَ

Na kwamba jeshi letu ndilo litakaloshinda.

Na kwamba jeshi letu ndilo litakaloshinda.

فَتَوَلَّ عَنۡهُمۡ حَتَّىٰ حِينٖ

Basi waachilie mbali kwa muda.

Basi waachilie mbali kwa muda.

وَأَبۡصِرۡهُمۡ فَسَوۡفَ يُبۡصِرُونَ

Na watazame, nao wataona.

Na watazame, nao wataona.

أَفَبِعَذَابِنَا يَسۡتَعۡجِلُونَ

Je, wanaiharakishia adhabu yetu?

Je, wanaiharakishia adhabu yetu?

فَإِذَا نَزَلَ بِسَاحَتِهِمۡ فَسَآءَ صَبَاحُ ٱلۡمُنذَرِينَ

Basi itakaposhuka uwanjani kwao, itakuwa asubuhi mbaya kwa walioonywa.

Basi itakaposhuka uwanjani kwao, itakuwa asubuhi mbaya kwa walioonywa.

وَتَوَلَّ عَنۡهُمۡ حَتَّىٰ حِينٖ

Na waache kwa muda.

Na waache kwa muda.

وَأَبۡصِرۡ فَسَوۡفَ يُبۡصِرُونَ

Na tazama, na wao wataona.

Na tazama, na wao wataona.

سُبۡحَٰنَ رَبِّكَ رَبِّ ٱلۡعِزَّةِ عَمَّا يَصِفُونَ

Ametakasika Mola wako Mlezi Mwenye utukufu mbali na yale wanayomzulia.

Ametakasika Mola wako Mlezi Mwenye utukufu mbali na yale wanayomzulia.

وَسَلَٰمٌ عَلَى ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Na Salamu juu ya Mitume.

Na Salamu juu ya Mitume.

وَٱلۡحَمۡدُ لِلَّهِ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Footer Include