Header Include

Swahili translation - Rowad Translation Center

translated by Rowwad Translation Center, in cooperation with the Islamic Propagation Office in Rabwah and the Association for Serving Islamic Content in Languages.

QR Code https://quran.islamcontent.com/ceb/swahili_rwwad

الٓرۚ تِلۡكَ ءَايَٰتُ ٱلۡكِتَٰبِ وَقُرۡءَانٖ مُّبِينٖ

Alif Lam Ra.[1] Hizi ni Aya za Kitabu na Qur-ani inayobainisha.

[1] Herufi hizi "Alif Laam Raa" na herufi nyinginezo za mkato zilizo mwanzoni mwa sura mbalimbali zinaonyesha hali ya ushindi wa Qur-ani. Kwani, washirikina walipewa changamoto kwayo, lakini wakashindwa na hawakuweza kuipinga, ilhali inajumuisha herufi hizi zinazounda lugha ya Kiarabu. Kwa hivyo, kutoweza kwa Waarabu kuleta kitu kama hicho - ingawa walikuwa ndio watu wenye ufasaha zaidi - kunaonyesha kwamba Qur-ani ni ufunuo (wahyi) kutoka kwa Mwenyezi Mungu.
Alif Lam Ra.[1] Hizi ni Aya za Kitabu na Qur-ani inayobainisha.

رُّبَمَا يَوَدُّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لَوۡ كَانُواْ مُسۡلِمِينَ

Huenda ikawa wale waliokufuru wakatamani kwamba wangekuwa Waislamu.

Huenda ikawa wale waliokufuru wakatamani kwamba wangekuwa Waislamu.

ذَرۡهُمۡ يَأۡكُلُواْ وَيَتَمَتَّعُواْ وَيُلۡهِهِمُ ٱلۡأَمَلُۖ فَسَوۡفَ يَعۡلَمُونَ

Waache wale, na wastarehe, na yawazuge matumaini. Basi watakujajua.

Waache wale, na wastarehe, na yawazuge matumaini. Basi watakujajua.

وَمَآ أَهۡلَكۡنَا مِن قَرۡيَةٍ إِلَّا وَلَهَا كِتَابٞ مَّعۡلُومٞ

Na hatukuuangamiza mji wowote ule isipokuwa ulikuwa na muda wake maalumu ulioandikiwa.

Na hatukuuangamiza mji wowote ule isipokuwa ulikuwa na muda wake maalumu ulioandikiwa.

مَّا تَسۡبِقُ مِنۡ أُمَّةٍ أَجَلَهَا وَمَا يَسۡتَـٔۡخِرُونَ

Hawawezi umma wowote kuutangulia muda wao, wala kuchelewa.

Hawawezi umma wowote kuutangulia muda wao, wala kuchelewa.

وَقَالُواْ يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِي نُزِّلَ عَلَيۡهِ ٱلذِّكۡرُ إِنَّكَ لَمَجۡنُونٞ

Na walisema, "Ewe uliyeteremshiwa Ukumbusho! Hakika wewe ni mwendawazimu.

Na walisema, "Ewe uliyeteremshiwa Ukumbusho! Hakika wewe ni mwendawazimu.

لَّوۡمَا تَأۡتِينَا بِٱلۡمَلَٰٓئِكَةِ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّٰدِقِينَ

Mbona hutuletei Malaika ikiwa wewe ni miongoni mwa wakweli?"

Mbona hutuletei Malaika ikiwa wewe ni miongoni mwa wakweli?"

مَا نُنَزِّلُ ٱلۡمَلَٰٓئِكَةَ إِلَّا بِٱلۡحَقِّ وَمَا كَانُوٓاْ إِذٗا مُّنظَرِينَ

Sisi hatuwateremshi Malaika isipokuwa kwa sababu ya haki, na hapo hawatapewa muhula.

Sisi hatuwateremshi Malaika isipokuwa kwa sababu ya haki, na hapo hawatapewa muhula.

إِنَّا نَحۡنُ نَزَّلۡنَا ٱلذِّكۡرَ وَإِنَّا لَهُۥ لَحَٰفِظُونَ

Hakika Sisi ndio tuliouteremsha Ukumbusho huu, na hakika Sisi ndio tutakaoulinda.

Hakika Sisi ndio tuliouteremsha Ukumbusho huu, na hakika Sisi ndio tutakaoulinda.

وَلَقَدۡ أَرۡسَلۡنَا مِن قَبۡلِكَ فِي شِيَعِ ٱلۡأَوَّلِينَ

Na hakika tulikwishatuma Mitume kabla yako kwa mataifa ya mwanzo.

Na hakika tulikwishatuma Mitume kabla yako kwa mataifa ya mwanzo.

وَمَا يَأۡتِيهِم مِّن رَّسُولٍ إِلَّا كَانُواْ بِهِۦ يَسۡتَهۡزِءُونَ

Na hakuwajia Mtume yeyote isipokuwa walikuwa wakimfanyia stihizai.

Na hakuwajia Mtume yeyote isipokuwa walikuwa wakimfanyia stihizai.

كَذَٰلِكَ نَسۡلُكُهُۥ فِي قُلُوبِ ٱلۡمُجۡرِمِينَ

Na kama hivi ndivyo tunavyoyaingiza katika nyoyo za wahalifu.

Na kama hivi ndivyo tunavyoyaingiza katika nyoyo za wahalifu.

لَا يُؤۡمِنُونَ بِهِۦ وَقَدۡ خَلَتۡ سُنَّةُ ٱلۡأَوَّلِينَ

Hawayaamini haya, na ilhali imekwishawapitia desturi ya wa mwanzo.

Hawayaamini haya, na ilhali imekwishawapitia desturi ya wa mwanzo.

وَلَوۡ فَتَحۡنَا عَلَيۡهِم بَابٗا مِّنَ ٱلسَّمَآءِ فَظَلُّواْ فِيهِ يَعۡرُجُونَ

Na lau tungeliwafungulia mlango huko mbinguni, wakawa wanapanda kupitia humo,

Na lau tungeliwafungulia mlango huko mbinguni, wakawa wanapanda kupitia humo,

لَقَالُوٓاْ إِنَّمَا سُكِّرَتۡ أَبۡصَٰرُنَا بَلۡ نَحۡنُ قَوۡمٞ مَّسۡحُورُونَ

Basi wangelisema: Hakika macho yetu yameleweshwa tu. Bali sisi wenyewe ni kaumu tuliofanyiwa uchawi.

Basi wangelisema: Hakika macho yetu yameleweshwa tu. Bali sisi wenyewe ni kaumu tuliofanyiwa uchawi.

وَلَقَدۡ جَعَلۡنَا فِي ٱلسَّمَآءِ بُرُوجٗا وَزَيَّنَّٰهَا لِلنَّٰظِرِينَ

Na hakika tumeweka katika mbingu vituo vya sayari, na tumezipamba kwa wenye kuangalia.

Na hakika tumeweka katika mbingu vituo vya sayari, na tumezipamba kwa wenye kuangalia.

وَحَفِظۡنَٰهَا مِن كُلِّ شَيۡطَٰنٖ رَّجِيمٍ

Na tumezilinda kutokana na kila shetani aliyelaaniwa.

Na tumezilinda kutokana na kila shetani aliyelaaniwa.

إِلَّا مَنِ ٱسۡتَرَقَ ٱلسَّمۡعَ فَأَتۡبَعَهُۥ شِهَابٞ مُّبِينٞ

Isipokuwa mwenye kusikiliza kwa kuibia, naye hufuatwa na kijinga cha moto kilicho dhahiri.

Isipokuwa mwenye kusikiliza kwa kuibia, naye hufuatwa na kijinga cha moto kilicho dhahiri.

وَٱلۡأَرۡضَ مَدَدۡنَٰهَا وَأَلۡقَيۡنَا فِيهَا رَوَٰسِيَ وَأَنۢبَتۡنَا فِيهَا مِن كُلِّ شَيۡءٖ مَّوۡزُونٖ

Na ardhi tumeitandaza, na humo tumeweka milima madhubuti, na tumeotesha ndani yake katika kila kitu kwa kiasi chake.

Na ardhi tumeitandaza, na humo tumeweka milima madhubuti, na tumeotesha ndani yake katika kila kitu kwa kiasi chake.

وَجَعَلۡنَا لَكُمۡ فِيهَا مَعَٰيِشَ وَمَن لَّسۡتُمۡ لَهُۥ بِرَٰزِقِينَ

Na tumewafanyia humo vitu vya maisha yenu, na ya hao ambao nyinyi sio wenye kuwaruzuku.

Na tumewafanyia humo vitu vya maisha yenu, na ya hao ambao nyinyi sio wenye kuwaruzuku.

وَإِن مِّن شَيۡءٍ إِلَّا عِندَنَا خَزَآئِنُهُۥ وَمَا نُنَزِّلُهُۥٓ إِلَّا بِقَدَرٖ مَّعۡلُومٖ

Na hakuna chochote ila asili yake inatokana na Sisi; wala hatukiteremshi isipokuwa kwa kipimo maalumu.

Na hakuna chochote ila asili yake inatokana na Sisi; wala hatukiteremshi isipokuwa kwa kipimo maalumu.

وَأَرۡسَلۡنَا ٱلرِّيَٰحَ لَوَٰقِحَ فَأَنزَلۡنَا مِنَ ٱلسَّمَآءِ مَآءٗ فَأَسۡقَيۡنَٰكُمُوهُ وَمَآ أَنتُمۡ لَهُۥ بِخَٰزِنِينَ

Na tunazipeleka pepo za kupandishia, na tunateremsha kutoka mbinguni maji, kisha tukakunywesheni maji hayo. Wala si nyinyi mnayoyaweka.

Na tunazipeleka pepo za kupandishia, na tunateremsha kutoka mbinguni maji, kisha tukakunywesheni maji hayo. Wala si nyinyi mnayoyaweka.

وَإِنَّا لَنَحۡنُ نُحۡيِۦ وَنُمِيتُ وَنَحۡنُ ٱلۡوَٰرِثُونَ

Na hakika Sisi ndio tunaohuisha na tunaofisha. Na Sisi ndio Warithi.

Na hakika Sisi ndio tunaohuisha na tunaofisha. Na Sisi ndio Warithi.

وَلَقَدۡ عَلِمۡنَا ٱلۡمُسۡتَقۡدِمِينَ مِنكُمۡ وَلَقَدۡ عَلِمۡنَا ٱلۡمُسۡتَـٔۡخِرِينَ

Na hakika tunawajua waliotangulia katika nyinyi, na tunawajua waliobaki nyuma.

Na hakika tunawajua waliotangulia katika nyinyi, na tunawajua waliobaki nyuma.

وَإِنَّ رَبَّكَ هُوَ يَحۡشُرُهُمۡۚ إِنَّهُۥ حَكِيمٌ عَلِيمٞ

Na hakika Mola wako Mlezi ndiye atakayewakusanya. Hakika Yeye ni Mwenye hekima, Mwenye kujua mno.

Na hakika Mola wako Mlezi ndiye atakayewakusanya. Hakika Yeye ni Mwenye hekima, Mwenye kujua mno.

وَلَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ مِن صَلۡصَٰلٖ مِّنۡ حَمَإٖ مَّسۡنُونٖ

Na hakika tulimuumba Mtu kwa udongo unaotoa sauti, unaotokana na matope yaliyotiwa sura.

Na hakika tulimuumba Mtu kwa udongo unaotoa sauti, unaotokana na matope yaliyotiwa sura.

وَٱلۡجَآنَّ خَلَقۡنَٰهُ مِن قَبۡلُ مِن نَّارِ ٱلسَّمُومِ

Naye Jini tulimuumba hapo kabla kutokana na moto wa upepo umoto.

Naye Jini tulimuumba hapo kabla kutokana na moto wa upepo umoto.

وَإِذۡ قَالَ رَبُّكَ لِلۡمَلَٰٓئِكَةِ إِنِّي خَٰلِقُۢ بَشَرٗا مِّن صَلۡصَٰلٖ مِّنۡ حَمَإٖ مَّسۡنُونٖ

Na Mola wako Mlezi alipowaambia Malaika: Hakika Mimi nitamuumba mtu kwa udongo unaotoa sauti, unaotokana na matope yaliyotiwa sura.

Na Mola wako Mlezi alipowaambia Malaika: Hakika Mimi nitamuumba mtu kwa udongo unaotoa sauti, unaotokana na matope yaliyotiwa sura.

فَإِذَا سَوَّيۡتُهُۥ وَنَفَخۡتُ فِيهِ مِن رُّوحِي فَقَعُواْ لَهُۥ سَٰجِدِينَ

Basi nitakapomtengeneza sawasawa, na nikampulizia katika roho yangu, basi angukeni kumsujudia.

Basi nitakapomtengeneza sawasawa, na nikampulizia katika roho yangu, basi angukeni kumsujudia.

فَسَجَدَ ٱلۡمَلَٰٓئِكَةُ كُلُّهُمۡ أَجۡمَعُونَ

Basi Malaika wote pamoja walimsujudia.

Basi Malaika wote pamoja walimsujudia.

إِلَّآ إِبۡلِيسَ أَبَىٰٓ أَن يَكُونَ مَعَ ٱلسَّٰجِدِينَ

Isipokuwa Iblisi. Yeye alikataa kuwa pamoja na waliosujudu.

Isipokuwa Iblisi. Yeye alikataa kuwa pamoja na waliosujudu.

قَالَ يَٰٓإِبۡلِيسُ مَا لَكَ أَلَّا تَكُونَ مَعَ ٱلسَّٰجِدِينَ

(Mwenyezi Mungu) akasema: Ewe Iblisi! Una nini hata hukuwa pamoja na waliosujudu?

(Mwenyezi Mungu) akasema: Ewe Iblisi! Una nini hata hukuwa pamoja na waliosujudu?

قَالَ لَمۡ أَكُن لِّأَسۡجُدَ لِبَشَرٍ خَلَقۡتَهُۥ مِن صَلۡصَٰلٖ مِّنۡ حَمَإٖ مَّسۡنُونٖ

Akasema: Haiwi mimi nimsujudie mtu uliyemuumba kutokana na udongo unaotoa sauti, unaotokana na matope yaliyotiwa sura.

Akasema: Haiwi mimi nimsujudie mtu uliyemuumba kutokana na udongo unaotoa sauti, unaotokana na matope yaliyotiwa sura.

قَالَ فَٱخۡرُجۡ مِنۡهَا فَإِنَّكَ رَجِيمٞ

(Mwenyezi Mungu) akasema: Basi toka humo, kwani hakika wewe umefukuziliwa mbali!

(Mwenyezi Mungu) akasema: Basi toka humo, kwani hakika wewe umefukuziliwa mbali!

وَإِنَّ عَلَيۡكَ ٱللَّعۡنَةَ إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلدِّينِ

Na hakika juu yako ipo laana mpaka Siku ya Malipo.

Na hakika juu yako ipo laana mpaka Siku ya Malipo.

قَالَ رَبِّ فَأَنظِرۡنِيٓ إِلَىٰ يَوۡمِ يُبۡعَثُونَ

Akasema (Iblisi): Mola wangu Mlezi! Nipe muhula mpaka siku watakapofufuliwa.

Akasema (Iblisi): Mola wangu Mlezi! Nipe muhula mpaka siku watakapofufuliwa.

قَالَ فَإِنَّكَ مِنَ ٱلۡمُنظَرِينَ

(Mwenyezi Mungu) akasema: Hakika wewe ni katika waliopewa muhula.

(Mwenyezi Mungu) akasema: Hakika wewe ni katika waliopewa muhula.

إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلۡوَقۡتِ ٱلۡمَعۡلُومِ

Mpaka siku ya wakati maalumu.

Mpaka siku ya wakati maalumu.

قَالَ رَبِّ بِمَآ أَغۡوَيۡتَنِي لَأُزَيِّنَنَّ لَهُمۡ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَلَأُغۡوِيَنَّهُمۡ أَجۡمَعِينَ

Akasema: Mola wangu Mlezi! Ilivyokuwa umenipoteza, basi hakika nitawapambia katika dunia na hakika nitawapoteza wote.

Akasema: Mola wangu Mlezi! Ilivyokuwa umenipoteza, basi hakika nitawapambia katika dunia na hakika nitawapoteza wote.

إِلَّا عِبَادَكَ مِنۡهُمُ ٱلۡمُخۡلَصِينَ

Isipokuwa waja wako walioteuliwa miongoni mwao.

Isipokuwa waja wako walioteuliwa miongoni mwao.

قَالَ هَٰذَا صِرَٰطٌ عَلَيَّ مُسۡتَقِيمٌ

Akasema: Hii ni njia ya kujia kwangu iliyonyooka.

Akasema: Hii ni njia ya kujia kwangu iliyonyooka.

إِنَّ عِبَادِي لَيۡسَ لَكَ عَلَيۡهِمۡ سُلۡطَٰنٌ إِلَّا مَنِ ٱتَّبَعَكَ مِنَ ٱلۡغَاوِينَ

Hakika waja wangu, wewe hutakuwa na mamlaka juu yao, isipokuwa wale watakaokufuata miongoni mwa wapotovu.

Hakika waja wangu, wewe hutakuwa na mamlaka juu yao, isipokuwa wale watakaokufuata miongoni mwa wapotovu.

وَإِنَّ جَهَنَّمَ لَمَوۡعِدُهُمۡ أَجۡمَعِينَ

Na hakika Jahannamu ndipo mahali pao walipoahidiwa wote.

Na hakika Jahannamu ndipo mahali pao walipoahidiwa wote.

لَهَا سَبۡعَةُ أَبۡوَٰبٖ لِّكُلِّ بَابٖ مِّنۡهُمۡ جُزۡءٞ مَّقۡسُومٌ

Ina milango saba; kila mlango ulitengewa sehemu miongoni mwao.

Ina milango saba; kila mlango ulitengewa sehemu miongoni mwao.

إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي جَنَّٰتٖ وَعُيُونٍ

Hakika wacha Mungu watakuwa katika Mabustani na chemchemi.

Hakika wacha Mungu watakuwa katika Mabustani na chemchemi.

ٱدۡخُلُوهَا بِسَلَٰمٍ ءَامِنِينَ

(Wataambiwa:) Ingieni humo kwa salama na amani.

(Wataambiwa:) Ingieni humo kwa salama na amani.

وَنَزَعۡنَا مَا فِي صُدُورِهِم مِّنۡ غِلٍّ إِخۡوَٰنًا عَلَىٰ سُرُرٖ مُّتَقَٰبِلِينَ

Na tutaondoa chuki iliyokuwa vifuani mwao, wawe ndugu, juu ya viti vya kifahari huku wameelekeana.

Na tutaondoa chuki iliyokuwa vifuani mwao, wawe ndugu, juu ya viti vya kifahari huku wameelekeana.

لَا يَمَسُّهُمۡ فِيهَا نَصَبٞ وَمَا هُم مِّنۡهَا بِمُخۡرَجِينَ

Humo hayatawagusa machovu, wala hawatatolewa humo.

Humo hayatawagusa machovu, wala hawatatolewa humo.

۞ نَبِّئۡ عِبَادِيٓ أَنِّيٓ أَنَا ٱلۡغَفُورُ ٱلرَّحِيمُ

Wape habari waja wangu ya kwamba Mimi ndiye Mwenye kusamehe zaidi, Mwingi wa kurehemu.

Wape habari waja wangu ya kwamba Mimi ndiye Mwenye kusamehe zaidi, Mwingi wa kurehemu.

وَأَنَّ عَذَابِي هُوَ ٱلۡعَذَابُ ٱلۡأَلِيمُ

Na kwamba adhabu yangu ndiyo adhabu iliyo chungu!

Na kwamba adhabu yangu ndiyo adhabu iliyo chungu!

وَنَبِّئۡهُمۡ عَن ضَيۡفِ إِبۡرَٰهِيمَ

Na wape habari za wageni wa Ibrahim.

Na wape habari za wageni wa Ibrahim.

إِذۡ دَخَلُواْ عَلَيۡهِ فَقَالُواْ سَلَٰمٗا قَالَ إِنَّا مِنكُمۡ وَجِلُونَ

Walipoingia kwake na wakasema: Salama! Yeye akasema: Hakika sisi tunawaogopa.

Walipoingia kwake na wakasema: Salama! Yeye akasema: Hakika sisi tunawaogopa.

قَالُواْ لَا تَوۡجَلۡ إِنَّا نُبَشِّرُكَ بِغُلَٰمٍ عَلِيمٖ

Wakasema: Usiogope. Hakika, Sisi tunakubashiria kijana mwenye elimu mno.

Wakasema: Usiogope. Hakika, Sisi tunakubashiria kijana mwenye elimu mno.

قَالَ أَبَشَّرۡتُمُونِي عَلَىٰٓ أَن مَّسَّنِيَ ٱلۡكِبَرُ فَبِمَ تُبَشِّرُونَ

Akasema: Mnanibashiria nami uzee umenishika! Basi ni kwa njia gani mnanibashiria?

Akasema: Mnanibashiria nami uzee umenishika! Basi ni kwa njia gani mnanibashiria?

قَالُواْ بَشَّرۡنَٰكَ بِٱلۡحَقِّ فَلَا تَكُن مِّنَ ٱلۡقَٰنِطِينَ

Wakasema: Tunakubashiria kwa haki, basi usiwe miongoni mwa wanaokata tamaa.

Wakasema: Tunakubashiria kwa haki, basi usiwe miongoni mwa wanaokata tamaa.

قَالَ وَمَن يَقۡنَطُ مِن رَّحۡمَةِ رَبِّهِۦٓ إِلَّا ٱلضَّآلُّونَ

Akasema: Na ni nani anayekata tamaa na rehema ya Mola wake Mlezi isipokuwa wapotovu?

Akasema: Na ni nani anayekata tamaa na rehema ya Mola wake Mlezi isipokuwa wapotovu?

قَالَ فَمَا خَطۡبُكُمۡ أَيُّهَا ٱلۡمُرۡسَلُونَ

Akasema: Hebu mna jambo gani, enyi wajumbe?

Akasema: Hebu mna jambo gani, enyi wajumbe?

قَالُوٓاْ إِنَّآ أُرۡسِلۡنَآ إِلَىٰ قَوۡمٖ مُّجۡرِمِينَ

Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwa kaumu ya wahalifu!

Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwa kaumu ya wahalifu!

إِلَّآ ءَالَ لُوطٍ إِنَّا لَمُنَجُّوهُمۡ أَجۡمَعِينَ

Isipokuwa watu wa familia ya Lut'. Bila ya shaka sisi tutawaokoa hao wote.

Isipokuwa watu wa familia ya Lut'. Bila ya shaka sisi tutawaokoa hao wote.

إِلَّا ٱمۡرَأَتَهُۥ قَدَّرۡنَآ إِنَّهَا لَمِنَ ٱلۡغَٰبِرِينَ

Isipokuwa mkewe. Tumekwishapitisha kwamba huyo hakika atakuwa miongoni mwa watakaosalia nyuma.

Isipokuwa mkewe. Tumekwishapitisha kwamba huyo hakika atakuwa miongoni mwa watakaosalia nyuma.

فَلَمَّا جَآءَ ءَالَ لُوطٍ ٱلۡمُرۡسَلُونَ

Basi wajumbe hao walipowajia watu wa familia ya Lut'.

Basi wajumbe hao walipowajia watu wa familia ya Lut'.

قَالَ إِنَّكُمۡ قَوۡمٞ مُّنكَرُونَ

(Lut') Alisema: Hakika nyinyi ni kaumu msiojulikana.

(Lut') Alisema: Hakika nyinyi ni kaumu msiojulikana.

قَالُواْ بَلۡ جِئۡنَٰكَ بِمَا كَانُواْ فِيهِ يَمۡتَرُونَ

Wakasema: Bali sisi tumekuletea yale waliyokuwa wakiyafanyia shaka.

Wakasema: Bali sisi tumekuletea yale waliyokuwa wakiyafanyia shaka.

وَأَتَيۡنَٰكَ بِٱلۡحَقِّ وَإِنَّا لَصَٰدِقُونَ

Na tumekujia kwa Haki, na hakika sisi ni wakweli.

Na tumekujia kwa Haki, na hakika sisi ni wakweli.

فَأَسۡرِ بِأَهۡلِكَ بِقِطۡعٖ مِّنَ ٱلَّيۡلِ وَٱتَّبِعۡ أَدۡبَٰرَهُمۡ وَلَا يَلۡتَفِتۡ مِنكُمۡ أَحَدٞ وَٱمۡضُواْ حَيۡثُ تُؤۡمَرُونَ

Basi ondoka na ahali zako usiku ungalipo, nawe ufuate nyuma yao, wala yeyote kati yenu asigeuke nyuma. Na mwende huko mnakoamrishwa.

Basi ondoka na ahali zako usiku ungalipo, nawe ufuate nyuma yao, wala yeyote kati yenu asigeuke nyuma. Na mwende huko mnakoamrishwa.

وَقَضَيۡنَآ إِلَيۡهِ ذَٰلِكَ ٱلۡأَمۡرَ أَنَّ دَابِرَ هَٰٓؤُلَآءِ مَقۡطُوعٞ مُّصۡبِحِينَ

Na tukamfunulia hukumu hiyo, ya kwamba hata wa mwisho wao hao ikifika asubuhi atakuwa amekwishakatiliwa mbali.

Na tukamfunulia hukumu hiyo, ya kwamba hata wa mwisho wao hao ikifika asubuhi atakuwa amekwishakatiliwa mbali.

وَجَآءَ أَهۡلُ ٱلۡمَدِينَةِ يَسۡتَبۡشِرُونَ

Na wakaja watu wa mji huo huku wamefurahi mno.

Na wakaja watu wa mji huo huku wamefurahi mno.

قَالَ إِنَّ هَٰٓؤُلَآءِ ضَيۡفِي فَلَا تَفۡضَحُونِ

Akasema: Hakika hawa ni wageni wangu. Basi msinifedheheshe.

Akasema: Hakika hawa ni wageni wangu. Basi msinifedheheshe.

وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَلَا تُخۡزُونِ

Na mcheni Mwenyezi Mungu, wala msinihizi.

Na mcheni Mwenyezi Mungu, wala msinihizi.

قَالُوٓاْ أَوَلَمۡ نَنۡهَكَ عَنِ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Wakasema: Kwani hatukukukataza (kuwakaribisha) walimwengu hawa?

Wakasema: Kwani hatukukukataza (kuwakaribisha) walimwengu hawa?

قَالَ هَٰٓؤُلَآءِ بَنَاتِيٓ إِن كُنتُمۡ فَٰعِلِينَ

Akasema, "Hawa binti zangu (waoeni)[1], ikiwa nyinyi ni watendaji."

[1] Lut'i, amani iwe juu yake, alimaanisha kwamba hawa ni binti zangu miongoni mwa wanawake wenu, basi waoeni hao.
Akasema, "Hawa binti zangu (waoeni)[1], ikiwa nyinyi ni watendaji."

لَعَمۡرُكَ إِنَّهُمۡ لَفِي سَكۡرَتِهِمۡ يَعۡمَهُونَ

Ninaapa kwa uhai wako! Hakika hao walikuwa katika ulevi wao, wakihangaika ovyo.

Ninaapa kwa uhai wako! Hakika hao walikuwa katika ulevi wao, wakihangaika ovyo.

فَأَخَذَتۡهُمُ ٱلصَّيۡحَةُ مُشۡرِقِينَ

Basi ukelele ukawatwaa wakipambaukiwa.

Basi ukelele ukawatwaa wakipambaukiwa.

فَجَعَلۡنَا عَٰلِيَهَا سَافِلَهَا وَأَمۡطَرۡنَا عَلَيۡهِمۡ حِجَارَةٗ مِّن سِجِّيلٍ

Kwa hivyo, tukaugeuza mji huo juu chini, na tukawanyeshea mvua ya mawe ya udongo wa kutoka Motoni.

Kwa hivyo, tukaugeuza mji huo juu chini, na tukawanyeshea mvua ya mawe ya udongo wa kutoka Motoni.

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَٰتٖ لِّلۡمُتَوَسِّمِينَ

Hakika katika hayo zipo ishara kwa wanaotafakari na kuzingatia.

Hakika katika hayo zipo ishara kwa wanaotafakari na kuzingatia.

وَإِنَّهَا لَبِسَبِيلٖ مُّقِيمٍ

Na hakika miji hii ipo kwenye njia wazi inayopitiwa.

Na hakika miji hii ipo kwenye njia wazi inayopitiwa.

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗ لِّلۡمُؤۡمِنِينَ

Hakika katika hayo ipo ishara kwa Waumini.

Hakika katika hayo ipo ishara kwa Waumini.

وَإِن كَانَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡأَيۡكَةِ لَظَٰلِمِينَ

Na hakika watu wa Kichakani walikuwa madhalimu.

Na hakika watu wa Kichakani walikuwa madhalimu.

فَٱنتَقَمۡنَا مِنۡهُمۡ وَإِنَّهُمَا لَبِإِمَامٖ مُّبِينٖ

Kwa hivyo tukawaadhibu. Na hakika miji miwili hii iko kwenye njia iliyo wazi.

Kwa hivyo tukawaadhibu. Na hakika miji miwili hii iko kwenye njia iliyo wazi.

وَلَقَدۡ كَذَّبَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡحِجۡرِ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Na bila ya shaka wakazi wa Hijr waliwakadhibisha Mitume.

Na bila ya shaka wakazi wa Hijr waliwakadhibisha Mitume.

وَءَاتَيۡنَٰهُمۡ ءَايَٰتِنَا فَكَانُواْ عَنۡهَا مُعۡرِضِينَ

Na tuliwaletea ishara zetu, nao wakawa wanazipa migongo.

Na tuliwaletea ishara zetu, nao wakawa wanazipa migongo.

وَكَانُواْ يَنۡحِتُونَ مِنَ ٱلۡجِبَالِ بُيُوتًا ءَامِنِينَ

Nao walikuwa wakichonga majumba katika milima kwa amani.

Nao walikuwa wakichonga majumba katika milima kwa amani.

فَأَخَذَتۡهُمُ ٱلصَّيۡحَةُ مُصۡبِحِينَ

Basi ukelele ukawatwaa asubuhi.

Basi ukelele ukawatwaa asubuhi.

فَمَآ أَغۡنَىٰ عَنۡهُم مَّا كَانُواْ يَكۡسِبُونَ

Na hayakuwafaa yale waliyokuwa wakiyachuma.

Na hayakuwafaa yale waliyokuwa wakiyachuma.

وَمَا خَلَقۡنَا ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ وَمَا بَيۡنَهُمَآ إِلَّا بِٱلۡحَقِّۗ وَإِنَّ ٱلسَّاعَةَ لَأٓتِيَةٞۖ فَٱصۡفَحِ ٱلصَّفۡحَ ٱلۡجَمِيلَ

Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyo kati yake isipokuwa kwa haki. Na hakika Saa ya Kiyama itafika. Basi samehe msamaha mzuri.

Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyo kati yake isipokuwa kwa haki. Na hakika Saa ya Kiyama itafika. Basi samehe msamaha mzuri.

إِنَّ رَبَّكَ هُوَ ٱلۡخَلَّٰقُ ٱلۡعَلِيمُ

Hakika Mola wako Mlezi ndiye Muumbaji, Mwenye kujua zaidi.

Hakika Mola wako Mlezi ndiye Muumbaji, Mwenye kujua zaidi.

وَلَقَدۡ ءَاتَيۡنَٰكَ سَبۡعٗا مِّنَ ٱلۡمَثَانِي وَٱلۡقُرۡءَانَ ٱلۡعَظِيمَ

Na hakika tumekupa (aya) saba zinazosomwa mara kwa mara, na Qur-ani Tukufu.

Na hakika tumekupa (aya) saba zinazosomwa mara kwa mara, na Qur-ani Tukufu.

لَا تَمُدَّنَّ عَيۡنَيۡكَ إِلَىٰ مَا مَتَّعۡنَا بِهِۦٓ أَزۡوَٰجٗا مِّنۡهُمۡ وَلَا تَحۡزَنۡ عَلَيۡهِمۡ وَٱخۡفِضۡ جَنَاحَكَ لِلۡمُؤۡمِنِينَ

Kamwe usivinyoshee macho yako vitu tulivyowastarehesha kwavyo makundi fulani kati yao, wala usiwahuzunikie. Na wainamishie bawa lako (la huruma) Waumini.

Kamwe usivinyoshee macho yako vitu tulivyowastarehesha kwavyo makundi fulani kati yao, wala usiwahuzunikie. Na wainamishie bawa lako (la huruma) Waumini.

وَقُلۡ إِنِّيٓ أَنَا ٱلنَّذِيرُ ٱلۡمُبِينُ

Na sema: Hakika mimi ndiye mwonyaji mwenye kubainisha.

Na sema: Hakika mimi ndiye mwonyaji mwenye kubainisha.

كَمَآ أَنزَلۡنَا عَلَى ٱلۡمُقۡتَسِمِينَ

Kama hivyo tuliwateremshia waliogawa.

Kama hivyo tuliwateremshia waliogawa.

ٱلَّذِينَ جَعَلُواْ ٱلۡقُرۡءَانَ عِضِينَ

Ambao waliifanya Qur-ani vipande vipande.

Ambao waliifanya Qur-ani vipande vipande.

فَوَرَبِّكَ لَنَسۡـَٔلَنَّهُمۡ أَجۡمَعِينَ

Basi ninaapa kwa Mola wako Mlezi! Lazima tutawauliza wote.

Basi ninaapa kwa Mola wako Mlezi! Lazima tutawauliza wote.

عَمَّا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ

Kuhusu yale waliyokuwa wakiyatenda.

Kuhusu yale waliyokuwa wakiyatenda.

فَٱصۡدَعۡ بِمَا تُؤۡمَرُ وَأَعۡرِضۡ عَنِ ٱلۡمُشۡرِكِينَ

Basi wewe yadhihirishe yale uliyoamrishwa, na jitenge mbali na washirikina.

Basi wewe yadhihirishe yale uliyoamrishwa, na jitenge mbali na washirikina.

إِنَّا كَفَيۡنَٰكَ ٱلۡمُسۡتَهۡزِءِينَ

Hakika Sisi tunatosha kukukinga kutokana na wanaofanya stihizai.

Hakika Sisi tunatosha kukukinga kutokana na wanaofanya stihizai.

ٱلَّذِينَ يَجۡعَلُونَ مَعَ ٱللَّهِ إِلَٰهًا ءَاخَرَۚ فَسَوۡفَ يَعۡلَمُونَ

Ambao wanafanya mungu mwingine kuwa pamoja na Mwenyezi Mungu. Basi watakujajua!

Ambao wanafanya mungu mwingine kuwa pamoja na Mwenyezi Mungu. Basi watakujajua!

وَلَقَدۡ نَعۡلَمُ أَنَّكَ يَضِيقُ صَدۡرُكَ بِمَا يَقُولُونَ

Na Sisi tunajua kwa hakika kuwa wewe kifua chako kinaona dhiki kwa hayo wayasemayo.

Na Sisi tunajua kwa hakika kuwa wewe kifua chako kinaona dhiki kwa hayo wayasemayo.

فَسَبِّحۡ بِحَمۡدِ رَبِّكَ وَكُن مِّنَ ٱلسَّٰجِدِينَ

Basi mtakase Mola wako Mlezi kwa kumsifu, na uwe miongoni mwa wanaomsujudia.

Basi mtakase Mola wako Mlezi kwa kumsifu, na uwe miongoni mwa wanaomsujudia.

وَٱعۡبُدۡ رَبَّكَ حَتَّىٰ يَأۡتِيَكَ ٱلۡيَقِينُ

Na muabudu Mola wako Mlezi mpaka ikufikie Yakini.

Na muabudu Mola wako Mlezi mpaka ikufikie Yakini.
Footer Include