Header Include

Swahili translation - Rowad Translation Center

translated by Rowwad Translation Center, in cooperation with the Islamic Propagation Office in Rabwah and the Association for Serving Islamic Content in Languages.

QR Code https://quran.islamcontent.com/ceb/swahili_rwwad

لَآ أُقۡسِمُ بِهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ

Ninaapa kwa Mji huu!

Ninaapa kwa Mji huu!

وَأَنتَ حِلُّۢ بِهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ

Nawe unaukaa Mji huu.

Nawe unaukaa Mji huu.

وَوَالِدٖ وَمَا وَلَدَ

Na ninaapa kwa mzazi na alichokizaa.

Na ninaapa kwa mzazi na alichokizaa.

لَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ فِي كَبَدٍ

Hakika tumemuumba mtu katika taabu.

Hakika tumemuumba mtu katika taabu.

أَيَحۡسَبُ أَن لَّن يَقۡدِرَ عَلَيۡهِ أَحَدٞ

Ati anadhani hapana yeyote atakayemuweza?

Ati anadhani hapana yeyote atakayemuweza?

يَقُولُ أَهۡلَكۡتُ مَالٗا لُّبَدًا

Anasema: Nimeteketeza chungu ya mali.

Anasema: Nimeteketeza chungu ya mali.

أَيَحۡسَبُ أَن لَّمۡ يَرَهُۥٓ أَحَدٌ

Ati anadhani ya kuwa hapana yeyote anayemwona?

Ati anadhani ya kuwa hapana yeyote anayemwona?

أَلَمۡ نَجۡعَل لَّهُۥ عَيۡنَيۡنِ

Kwani hatukumpa macho mawili?

Kwani hatukumpa macho mawili?

وَلِسَانٗا وَشَفَتَيۡنِ

Na ulimi, na midomo miwili?

Na ulimi, na midomo miwili?

وَهَدَيۡنَٰهُ ٱلنَّجۡدَيۡنِ

Na tukambainishia zote njia mbili?

Na tukambainishia zote njia mbili?

فَلَا ٱقۡتَحَمَ ٱلۡعَقَبَةَ

Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani.

Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani.

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡعَقَبَةُ

Na nini kitakachokujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani?

Na nini kitakachokujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani?

فَكُّ رَقَبَةٍ

Kumkomboa mtumwa.

Kumkomboa mtumwa.

أَوۡ إِطۡعَٰمٞ فِي يَوۡمٖ ذِي مَسۡغَبَةٖ

Au kumlisha siku ya njaa,

Au kumlisha siku ya njaa,

يَتِيمٗا ذَا مَقۡرَبَةٍ

Yatima aliye jamaa.

Yatima aliye jamaa.

أَوۡ مِسۡكِينٗا ذَا مَتۡرَبَةٖ

Au masikini aliye vumbini.

Au masikini aliye vumbini.

ثُمَّ كَانَ مِنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَتَوَاصَوۡاْ بِٱلصَّبۡرِ وَتَوَاصَوۡاْ بِٱلۡمَرۡحَمَةِ

Tena awe miongoni mwa walioamini na wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumiana.

Tena awe miongoni mwa walioamini na wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumiana.

أُوْلَٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ

Hao ndio watu wa kheri wa kuliani.

Hao ndio watu wa kheri wa kuliani.

وَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ بِـَٔايَٰتِنَا هُمۡ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ

Lakini waliozikataa Ishara zetu, hao ndio watu wa shari wa kushotoni.

Lakini waliozikataa Ishara zetu, hao ndio watu wa shari wa kushotoni.

عَلَيۡهِمۡ نَارٞ مُّؤۡصَدَةُۢ

Juu yao utakuwa Moto uliofungiwa kila upande.

Juu yao utakuwa Moto uliofungiwa kila upande.
Footer Include