Header Include

ការបកប្រែជាភាសាស្វាហុីលី - មជ្ឈមណ្ឌលបកប្រែរ៉ូវ៉ាដ

បកប្រែដោយក្រុមមជ្ឈមណ្ឌលរ៉ូវ៉ាតនៃការបកប្រែ ដោយសហការជាមួយសមាគមអំពាវនាវនៅរ៉ាប់វ៉ា និងសមាគមបម្រើមាតិកាអ៊ីស្លាមជាភាសាផ្សេងៗ។

QR Code https://quran.islamcontent.com/km/swahili_rwwad

عَمَّ يَتَسَآءَلُونَ

Wanaulizana kuhusu nini?

Wanaulizana kuhusu nini?

عَنِ ٱلنَّبَإِ ٱلۡعَظِيمِ

Kuhusu Ile habari kuu.

Kuhusu Ile habari kuu.

ٱلَّذِي هُمۡ فِيهِ مُخۡتَلِفُونَ

Ambayo kwayo wanahitalifiana.

Ambayo kwayo wanahitalifiana.

كَلَّا سَيَعۡلَمُونَ

La! Karibu watakuja jua.

La! Karibu watakuja jua.

ثُمَّ كَلَّا سَيَعۡلَمُونَ

Tena la! Karibu watakuja jua.

Tena la! Karibu watakuja jua.

أَلَمۡ نَجۡعَلِ ٱلۡأَرۡضَ مِهَٰدٗا

Kwani hatukuifanya ardhi kama tandiko?

Kwani hatukuifanya ardhi kama tandiko?

وَٱلۡجِبَالَ أَوۡتَادٗا

Na milima kama vigingi?

Na milima kama vigingi?

وَخَلَقۡنَٰكُمۡ أَزۡوَٰجٗا

Na tukakuumbeni kwa jozi?

Na tukakuumbeni kwa jozi?

وَجَعَلۡنَا نَوۡمَكُمۡ سُبَاتٗا

Na tukakufanya kulala kwenu ni mapumziko?

Na tukakufanya kulala kwenu ni mapumziko?

وَجَعَلۡنَا ٱلَّيۡلَ لِبَاسٗا

Na tukaufanya usiku ni nguo?

Na tukaufanya usiku ni nguo?

وَجَعَلۡنَا ٱلنَّهَارَ مَعَاشٗا

Na tukaufanya mchana ni wa kuchumia maisha?

Na tukaufanya mchana ni wa kuchumia maisha?

وَبَنَيۡنَا فَوۡقَكُمۡ سَبۡعٗا شِدَادٗا

Na tukajenga juu yenu saba zenye nguvu?

Na tukajenga juu yenu saba zenye nguvu?

وَجَعَلۡنَا سِرَاجٗا وَهَّاجٗا

Na tukaifanya taa yenye mwanga na joto.

Na tukaifanya taa yenye mwanga na joto.

وَأَنزَلۡنَا مِنَ ٱلۡمُعۡصِرَٰتِ مَآءٗ ثَجَّاجٗا

Na tukateremsha maji yanayoanguka kwa kasi kutoka mawinguni.

Na tukateremsha maji yanayoanguka kwa kasi kutoka mawinguni.

لِّنُخۡرِجَ بِهِۦ حَبّٗا وَنَبَاتٗا

Ili tutoe kwayo nafaka na mimea.

Ili tutoe kwayo nafaka na mimea.

وَجَنَّٰتٍ أَلۡفَافًا

Na mabustani yenye miti iliyokamatana.

Na mabustani yenye miti iliyokamatana.

إِنَّ يَوۡمَ ٱلۡفَصۡلِ كَانَ مِيقَٰتٗا

Hakika Siku ya uamuzi imewekewa wakati wake.

Hakika Siku ya uamuzi imewekewa wakati wake.

يَوۡمَ يُنفَخُ فِي ٱلصُّورِ فَتَأۡتُونَ أَفۡوَاجٗا

Siku litakapopulizwa baragumu, nanyi mtakuja kwa makundi.

Siku litakapopulizwa baragumu, nanyi mtakuja kwa makundi.

وَفُتِحَتِ ٱلسَّمَآءُ فَكَانَتۡ أَبۡوَٰبٗا

Na mbingu zitafunguliwa, ziwe milango.

Na mbingu zitafunguliwa, ziwe milango.

وَسُيِّرَتِ ٱلۡجِبَالُ فَكَانَتۡ سَرَابًا

Na milima itaondolewa na itakuwa kama sarabi.

Na milima itaondolewa na itakuwa kama sarabi.

إِنَّ جَهَنَّمَ كَانَتۡ مِرۡصَادٗا

Hakika Jahannamu inangojea!

Hakika Jahannamu inangojea!

لِّلطَّٰغِينَ مَـَٔابٗا

Kwa walioasi ndio makazi yao.

Kwa walioasi ndio makazi yao.

لَّٰبِثِينَ فِيهَآ أَحۡقَابٗا

Wakae humo karne baada ya karne.

Wakae humo karne baada ya karne.

لَّا يَذُوقُونَ فِيهَا بَرۡدٗا وَلَا شَرَابًا

Hawataonja humo chochote kibaridi wala kinywaji.

Hawataonja humo chochote kibaridi wala kinywaji.

إِلَّا حَمِيمٗا وَغَسَّاقٗا

Ila maji ya moto sana na usaha.

Ila maji ya moto sana na usaha.

جَزَآءٗ وِفَاقًا

Ndio malipo mwafaka.

Ndio malipo mwafaka.

إِنَّهُمۡ كَانُواْ لَا يَرۡجُونَ حِسَابٗا

Hakika hao hawakuwa wakitaraji kuwa kuna hesabu (juu ya matendo yao).

Hakika hao hawakuwa wakitaraji kuwa kuna hesabu (juu ya matendo yao).

وَكَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَا كِذَّابٗا

Na wakakanusha Aya zetu kwa nguvu.

Na wakakanusha Aya zetu kwa nguvu.

وَكُلَّ شَيۡءٍ أَحۡصَيۡنَٰهُ كِتَٰبٗا

Na kila kitu Sisi tumekidhibiti kwa kukiandika.

Na kila kitu Sisi tumekidhibiti kwa kukiandika.

فَذُوقُواْ فَلَن نَّزِيدَكُمۡ إِلَّا عَذَابًا

Basi onjeni! Nasi hatutakuzidishieni ila adhabu!

Basi onjeni! Nasi hatutakuzidishieni ila adhabu!

إِنَّ لِلۡمُتَّقِينَ مَفَازًا

Hakika wacha Mungu wanastahiki kufuzu.

Hakika wacha Mungu wanastahiki kufuzu.

حَدَآئِقَ وَأَعۡنَٰبٗا

Mabustani na mizabibu.

Mabustani na mizabibu.

وَكَوَاعِبَ أَتۡرَابٗا

Na wake wazuri waliolingana nao.

Na wake wazuri waliolingana nao.

وَكَأۡسٗا دِهَاقٗا

Na bilauri zilizojaa.

Na bilauri zilizojaa.

لَّا يَسۡمَعُونَ فِيهَا لَغۡوٗا وَلَا كِذَّٰبٗا

Hawatasikia humo upuuzi wala uongo.

Hawatasikia humo upuuzi wala uongo.

جَزَآءٗ مِّن رَّبِّكَ عَطَآءً حِسَابٗا

Malipo kutoka kwa Mola wako Mlezi, kipawa cha kutosha.

Malipo kutoka kwa Mola wako Mlezi, kipawa cha kutosha.

رَّبِّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَا ٱلرَّحۡمَٰنِۖ لَا يَمۡلِكُونَ مِنۡهُ خِطَابٗا

Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilivyo baina yake, Arrahman (Mwingi wa rehema); hawamiliki usemi mbele yake!

Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilivyo baina yake, Arrahman (Mwingi wa rehema); hawamiliki usemi mbele yake!

يَوۡمَ يَقُومُ ٱلرُّوحُ وَٱلۡمَلَٰٓئِكَةُ صَفّٗاۖ لَّا يَتَكَلَّمُونَ إِلَّا مَنۡ أَذِنَ لَهُ ٱلرَّحۡمَٰنُ وَقَالَ صَوَابٗا

Siku atakaposimama Roho na Malaika kwa safu. Hawatasema ila yule ambaye Mwingi wa rehema atamruhusu, na atasema yaliyo sawa tu.

Siku atakaposimama Roho na Malaika kwa safu. Hawatasema ila yule ambaye Mwingi wa rehema atamruhusu, na atasema yaliyo sawa tu.

ذَٰلِكَ ٱلۡيَوۡمُ ٱلۡحَقُّۖ فَمَن شَآءَ ٱتَّخَذَ إِلَىٰ رَبِّهِۦ مَـَٔابًا

Hiyo ndiyo Siku ya haki. Basi anayetaka, na ashike njia arejee kwa Mola wake Mlezi.

Hiyo ndiyo Siku ya haki. Basi anayetaka, na ashike njia arejee kwa Mola wake Mlezi.

إِنَّآ أَنذَرۡنَٰكُمۡ عَذَابٗا قَرِيبٗا يَوۡمَ يَنظُرُ ٱلۡمَرۡءُ مَا قَدَّمَتۡ يَدَاهُ وَيَقُولُ ٱلۡكَافِرُ يَٰلَيۡتَنِي كُنتُ تُرَٰبَۢا

Hakika tumekuhadharisheni adhabu iliyo karibu kufika; Siku ambayo mtu ataona yale yaliyotangulizwa na mikono yake; na kafiri atasema: Laiti ningelikuwa udongo!

Hakika tumekuhadharisheni adhabu iliyo karibu kufika; Siku ambayo mtu ataona yale yaliyotangulizwa na mikono yake; na kafiri atasema: Laiti ningelikuwa udongo!
Footer Include