Header Include

Swahili translation - Rowad Translation Center

translated by Rowwad Translation Center, in cooperation with the Islamic Propagation Office in Rabwah and the Association for Serving Islamic Content in Languages.

QR Code https://quran.islamcontent.com/rn/swahili_rwwad

نٓۚ وَٱلۡقَلَمِ وَمَا يَسۡطُرُونَ

Nuun. Ninaapa kwa kalamu na yale wayaandikayo.[1]

[1] Herufi hii "Nuun" na herufi nyinginezo za mkato zilizo mwanzoni mwa sura mbalimbali zinaonyesha hali ya ushindi wa Qur-ani. Kwani, washirikina walipewa changamoto kwayo, lakini wakashindwa na hawakuweza kuipinga, ilhali inajumuisha herufi hizi zinazounda lugha ya Kiarabu. Kwa hivyo, kutoweza kwa Waarabu kuleta kitu kama hicho - ingawa walikuwa ndio watu wenye ufasaha zaidi - kunaonyesha kwamba Qur-ani ni ufunuo (wahyi) kutoka kwa Mwenyezi Mungu.
Nuun. Ninaapa kwa kalamu na yale wayaandikayo.[1]

مَآ أَنتَ بِنِعۡمَةِ رَبِّكَ بِمَجۡنُونٖ

Kwa neema ya Mola wako Mlezi wewe si mwendawazimu.

Kwa neema ya Mola wako Mlezi wewe si mwendawazimu.

وَإِنَّ لَكَ لَأَجۡرًا غَيۡرَ مَمۡنُونٖ

Na kwa hakika wewe una malipo yasiyokatika.

Na kwa hakika wewe una malipo yasiyokatika.

وَإِنَّكَ لَعَلَىٰ خُلُقٍ عَظِيمٖ

Na hakika wewe una tabia tukufu.

Na hakika wewe una tabia tukufu.

فَسَتُبۡصِرُ وَيُبۡصِرُونَ

Karibu utaona, na wao wataona.

Karibu utaona, na wao wataona.

بِأَييِّكُمُ ٱلۡمَفۡتُونُ

Ni nani kati yenu aliyepandwa na wazimu.

Ni nani kati yenu aliyepandwa na wazimu.

إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعۡلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِۦ وَهُوَ أَعۡلَمُ بِٱلۡمُهۡتَدِينَ

Hakika Mola wako Mlezi ndiye ajuaye zaidi ni nani aliyeipotea njia yake, na Yeye ndiye anayewajua zaidi walioongoka.

Hakika Mola wako Mlezi ndiye ajuaye zaidi ni nani aliyeipotea njia yake, na Yeye ndiye anayewajua zaidi walioongoka.

فَلَا تُطِعِ ٱلۡمُكَذِّبِينَ

Basi usiwatii wanaokadhibisha.

Basi usiwatii wanaokadhibisha.

وَدُّواْ لَوۡ تُدۡهِنُ فَيُدۡهِنُونَ

Walitamani lau ungelainisha ili nao wakulainishie.

Walitamani lau ungelainisha ili nao wakulainishie.

وَلَا تُطِعۡ كُلَّ حَلَّافٖ مَّهِينٍ

Wala usimtii kila mwingi wa kuapa, anayedharauliwa.

Wala usimtii kila mwingi wa kuapa, anayedharauliwa.

هَمَّازٖ مَّشَّآءِۭ بِنَمِيمٖ

Mwenye kukejeli mno, anayetangatanga akieneza maneno ya kufitini.

Mwenye kukejeli mno, anayetangatanga akieneza maneno ya kufitini.

مَّنَّاعٖ لِّلۡخَيۡرِ مُعۡتَدٍ أَثِيمٍ

Mwenye kuzuia mno heri, dhalimu, mwingi wa madhambi.

Mwenye kuzuia mno heri, dhalimu, mwingi wa madhambi.

عُتُلِّۭ بَعۡدَ ذَٰلِكَ زَنِيمٍ

Mkatili, na juu ya hayo, ni mshari aliyejipachika tu.

Mkatili, na juu ya hayo, ni mshari aliyejipachika tu.

أَن كَانَ ذَا مَالٖ وَبَنِينَ

Ati kwa kuwa ana mali na watoto!

Ati kwa kuwa ana mali na watoto!

إِذَا تُتۡلَىٰ عَلَيۡهِ ءَايَٰتُنَا قَالَ أَسَٰطِيرُ ٱلۡأَوَّلِينَ

Anaposomewa Aya zetu, husema: "(Hizi ni) simulizi za uongo za watu wa zamani!"

Anaposomewa Aya zetu, husema: "(Hizi ni) simulizi za uongo za watu wa zamani!"

سَنَسِمُهُۥ عَلَى ٱلۡخُرۡطُومِ

Tutamtia alama kwenye pua yake.

Tutamtia alama kwenye pua yake.

إِنَّا بَلَوۡنَٰهُمۡ كَمَا بَلَوۡنَآ أَصۡحَٰبَ ٱلۡجَنَّةِ إِذۡ أَقۡسَمُواْ لَيَصۡرِمُنَّهَا مُصۡبِحِينَ

Hakika tuliwajaribu hawa kama tulivyowajaribu wale wenye shamba, walipoapa kwamba lazima watayavuna mazao yake itakapokuwa asubuhi.

Hakika tuliwajaribu hawa kama tulivyowajaribu wale wenye shamba, walipoapa kwamba lazima watayavuna mazao yake itakapokuwa asubuhi.

وَلَا يَسۡتَثۡنُونَ

Wala hawakusema: "Mwenyezi Mungu akipenda!"

Wala hawakusema: "Mwenyezi Mungu akipenda!"

فَطَافَ عَلَيۡهَا طَآئِفٞ مِّن رَّبِّكَ وَهُمۡ نَآئِمُونَ

Basi lilitokea tukio juu yake kutoka kwa Mola wako Mlezi, nao wamelala!

Basi lilitokea tukio juu yake kutoka kwa Mola wako Mlezi, nao wamelala!

فَأَصۡبَحَتۡ كَٱلصَّرِيمِ

Likawa kama usiku wa giza.

Likawa kama usiku wa giza.

فَتَنَادَوۡاْ مُصۡبِحِينَ

Kisha asubuhi wakaitana.

Kisha asubuhi wakaitana.

أَنِ ٱغۡدُواْ عَلَىٰ حَرۡثِكُمۡ إِن كُنتُمۡ صَٰرِمِينَ

Ya kwamba: "Nendeni mapema kondeni mwenu ikiwa mnataka kuvuna."

Ya kwamba: "Nendeni mapema kondeni mwenu ikiwa mnataka kuvuna."

فَٱنطَلَقُواْ وَهُمۡ يَتَخَٰفَتُونَ

Basi walikwenda huku wananong'onezana.

Basi walikwenda huku wananong'onezana.

أَن لَّا يَدۡخُلَنَّهَا ٱلۡيَوۡمَ عَلَيۡكُم مِّسۡكِينٞ

Ya kuwa: "Leo kamwe masikini mmoja asikuingilieni."

Ya kuwa: "Leo kamwe masikini mmoja asikuingilieni."

وَغَدَوۡاْ عَلَىٰ حَرۡدٖ قَٰدِرِينَ

Na walikwenda asubuhi, nao wameshikilia azimio hilo.

Na walikwenda asubuhi, nao wameshikilia azimio hilo.

فَلَمَّا رَأَوۡهَا قَالُوٓاْ إِنَّا لَضَآلُّونَ

Basi walipoliona, wakasema: Hakika tumepotea!

Basi walipoliona, wakasema: Hakika tumepotea!

بَلۡ نَحۡنُ مَحۡرُومُونَ

Bali tumenyimwa!

Bali tumenyimwa!

قَالَ أَوۡسَطُهُمۡ أَلَمۡ أَقُل لَّكُمۡ لَوۡلَا تُسَبِّحُونَ

Mbora wao akasema: Sikukwambieni, kwa nini hamumtakasi Mwenyezi Mungu?

Mbora wao akasema: Sikukwambieni, kwa nini hamumtakasi Mwenyezi Mungu?

قَالُواْ سُبۡحَٰنَ رَبِّنَآ إِنَّا كُنَّا ظَٰلِمِينَ

Wakasema: Ametakasika Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tulikuwa wenye kudhulumu.

Wakasema: Ametakasika Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tulikuwa wenye kudhulumu.

فَأَقۡبَلَ بَعۡضُهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖ يَتَلَٰوَمُونَ

Basi wakaelekeana kulaumiana wao kwa wao.

Basi wakaelekeana kulaumiana wao kwa wao.

قَالُواْ يَٰوَيۡلَنَآ إِنَّا كُنَّا طَٰغِينَ

Wakasema: Ole wetu! Hakika sisi tulikuwa tumeikiuka mipaka!

Wakasema: Ole wetu! Hakika sisi tulikuwa tumeikiuka mipaka!

عَسَىٰ رَبُّنَآ أَن يُبۡدِلَنَا خَيۡرٗا مِّنۡهَآ إِنَّآ إِلَىٰ رَبِّنَا رَٰغِبُونَ

Asaa Mola wetu Mlezi akatubadilishia lililo bora kuliko hili. Hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.

Asaa Mola wetu Mlezi akatubadilishia lililo bora kuliko hili. Hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.

كَذَٰلِكَ ٱلۡعَذَابُۖ وَلَعَذَابُ ٱلۡأٓخِرَةِ أَكۡبَرُۚ لَوۡ كَانُواْ يَعۡلَمُونَ

Namna hivi yanakuwa mateso, na bila ya shaka mateso ya Akhera ni makubwa zaidi, laiti wangelijua!

Namna hivi yanakuwa mateso, na bila ya shaka mateso ya Akhera ni makubwa zaidi, laiti wangelijua!

إِنَّ لِلۡمُتَّقِينَ عِندَ رَبِّهِمۡ جَنَّٰتِ ٱلنَّعِيمِ

Hakika wacha Mungu watakuwa na Bustani za neema kwa Mola wao Mlezi.

Hakika wacha Mungu watakuwa na Bustani za neema kwa Mola wao Mlezi.

أَفَنَجۡعَلُ ٱلۡمُسۡلِمِينَ كَٱلۡمُجۡرِمِينَ

Kwani tutawafanya Waislamu kama wahalifu?

Kwani tutawafanya Waislamu kama wahalifu?

مَا لَكُمۡ كَيۡفَ تَحۡكُمُونَ

Mna nini? Mnahukumu vipi?

Mna nini? Mnahukumu vipi?

أَمۡ لَكُمۡ كِتَٰبٞ فِيهِ تَدۡرُسُونَ

Au mnacho kitabu ambacho ndani yake mnasoma?

Au mnacho kitabu ambacho ndani yake mnasoma?

إِنَّ لَكُمۡ فِيهِ لَمَا تَخَيَّرُونَ

Kuwa mtapata humo mnayoyapenda?

Kuwa mtapata humo mnayoyapenda?

أَمۡ لَكُمۡ أَيۡمَٰنٌ عَلَيۡنَا بَٰلِغَةٌ إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِ إِنَّ لَكُمۡ لَمَا تَحۡكُمُونَ

Au mnazo ahadi za viapo juu yetu za kufika Siku ya Kiyama ya kuwa hakika mtapata kila mnayojihukumia?

Au mnazo ahadi za viapo juu yetu za kufika Siku ya Kiyama ya kuwa hakika mtapata kila mnayojihukumia?

سَلۡهُمۡ أَيُّهُم بِذَٰلِكَ زَعِيمٌ

Waulize: Ni nani miongoni mwao mdhamini wa haya?

Waulize: Ni nani miongoni mwao mdhamini wa haya?

أَمۡ لَهُمۡ شُرَكَآءُ فَلۡيَأۡتُواْ بِشُرَكَآئِهِمۡ إِن كَانُواْ صَٰدِقِينَ

Au wanao washirika? Basi wawalete washirika wao wakiwa wanasema kweli.

Au wanao washirika? Basi wawalete washirika wao wakiwa wanasema kweli.

يَوۡمَ يُكۡشَفُ عَن سَاقٖ وَيُدۡعَوۡنَ إِلَى ٱلسُّجُودِ فَلَا يَسۡتَطِيعُونَ

Siku utakapowekwa wazi muundi, na wataitwa kusujudu, lakini hawataweza

Siku utakapowekwa wazi muundi, na wataitwa kusujudu, lakini hawataweza

خَٰشِعَةً أَبۡصَٰرُهُمۡ تَرۡهَقُهُمۡ ذِلَّةٞۖ وَقَدۡ كَانُواْ يُدۡعَوۡنَ إِلَى ٱلسُّجُودِ وَهُمۡ سَٰلِمُونَ

Macho yao yatainama chini, fedheha itawafunika. Na hakika walikuwa wakiitwa wasujudu walipokuwa wazima.

Macho yao yatainama chini, fedheha itawafunika. Na hakika walikuwa wakiitwa wasujudu walipokuwa wazima.

فَذَرۡنِي وَمَن يُكَذِّبُ بِهَٰذَا ٱلۡحَدِيثِۖ سَنَسۡتَدۡرِجُهُم مِّنۡ حَيۡثُ لَا يَعۡلَمُونَ

Basi niache na wanaokadhibisha maneno haya! Tutawavutia kidogo kidogo kutokea mahali wasipopajua.

Basi niache na wanaokadhibisha maneno haya! Tutawavutia kidogo kidogo kutokea mahali wasipopajua.

وَأُمۡلِي لَهُمۡۚ إِنَّ كَيۡدِي مَتِينٌ

Na ninawapururia muhula; hakika hila zangu ni imara.

Na ninawapururia muhula; hakika hila zangu ni imara.

أَمۡ تَسۡـَٔلُهُمۡ أَجۡرٗا فَهُم مِّن مَّغۡرَمٖ مُّثۡقَلُونَ

Au unawaomba ujira, na wao wanaemewa na gharama hiyo?

Au unawaomba ujira, na wao wanaemewa na gharama hiyo?

أَمۡ عِندَهُمُ ٱلۡغَيۡبُ فَهُمۡ يَكۡتُبُونَ

Au iko kwao siri, basi wao wanaiandika?

Au iko kwao siri, basi wao wanaiandika?

فَٱصۡبِرۡ لِحُكۡمِ رَبِّكَ وَلَا تَكُن كَصَاحِبِ ٱلۡحُوتِ إِذۡ نَادَىٰ وَهُوَ مَكۡظُومٞ

Basi ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi, wala usiwe kama mmezwa na samaki, aliponadi naye kazongwa.

Basi ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi, wala usiwe kama mmezwa na samaki, aliponadi naye kazongwa.

لَّوۡلَآ أَن تَدَٰرَكَهُۥ نِعۡمَةٞ مِّن رَّبِّهِۦ لَنُبِذَ بِٱلۡعَرَآءِ وَهُوَ مَذۡمُومٞ

Kama isingelimfikia neema kutoka kwa Mola wake Mlezi, bila ya shaka angelitupwa ufukweni naye ni mwenye kulaumiwa.

Kama isingelimfikia neema kutoka kwa Mola wake Mlezi, bila ya shaka angelitupwa ufukweni naye ni mwenye kulaumiwa.

فَٱجۡتَبَٰهُ رَبُّهُۥ فَجَعَلَهُۥ مِنَ ٱلصَّٰلِحِينَ

Lakini Mola wake Mlezi alimteua na akamfanya miongoni mwa watu wema.

Lakini Mola wake Mlezi alimteua na akamfanya miongoni mwa watu wema.

وَإِن يَكَادُ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لَيُزۡلِقُونَكَ بِأَبۡصَٰرِهِمۡ لَمَّا سَمِعُواْ ٱلذِّكۡرَ وَيَقُولُونَ إِنَّهُۥ لَمَجۡنُونٞ

Na waliokufuru hukaribia kukutelezesha kwa macho yao, wanaposikia mawaidha, na wanasema: Hakika yeye ni mwendawazimu.

Na waliokufuru hukaribia kukutelezesha kwa macho yao, wanaposikia mawaidha, na wanasema: Hakika yeye ni mwendawazimu.

وَمَا هُوَ إِلَّا ذِكۡرٞ لِّلۡعَٰلَمِينَ

Na hayakuwa haya, ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.

Na hayakuwa haya, ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.
Footer Include