Header Include

Swahili translation - Rowad Translation Center

translated by Rowwad Translation Center, in cooperation with the Islamic Propagation Office in Rabwah and the Association for Serving Islamic Content in Languages.

QR Code https://quran.islamcontent.com/rn/swahili_rwwad

وَٱلسَّمَآءِ وَٱلطَّارِقِ

Ninaapa kwa mbingu na kinachokuja usiku!

Ninaapa kwa mbingu na kinachokuja usiku!

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلطَّارِقُ

Na nini kitakachokujulisha ni nini hicho kinachokuja usiku?

Na nini kitakachokujulisha ni nini hicho kinachokuja usiku?

ٱلنَّجۡمُ ٱلثَّاقِبُ

Ni Nyota yenye mwanga mkali.

Ni Nyota yenye mwanga mkali.

إِن كُلُّ نَفۡسٖ لَّمَّا عَلَيۡهَا حَافِظٞ

Hapana nafsi ila inaye mwangalizi.

Hapana nafsi ila inaye mwangalizi.

فَلۡيَنظُرِ ٱلۡإِنسَٰنُ مِمَّ خُلِقَ

Hebu na ajitazame mwanadamu ameumbwa kwa kitu gani?

Hebu na ajitazame mwanadamu ameumbwa kwa kitu gani?

خُلِقَ مِن مَّآءٖ دَافِقٖ

Ameumbwa kwa maji yatokayo kwa kuchupa.

Ameumbwa kwa maji yatokayo kwa kuchupa.

يَخۡرُجُ مِنۢ بَيۡنِ ٱلصُّلۡبِ وَٱلتَّرَآئِبِ

Yatokayo baina ya mifupa ya mgongo na mbavu.

Yatokayo baina ya mifupa ya mgongo na mbavu.

إِنَّهُۥ عَلَىٰ رَجۡعِهِۦ لَقَادِرٞ

Hakika Yeye ana uweza wa kumrudisha.

Hakika Yeye ana uweza wa kumrudisha.

يَوۡمَ تُبۡلَى ٱلسَّرَآئِرُ

Siku zitakapodhihirishwa siri.

Siku zitakapodhihirishwa siri.

فَمَا لَهُۥ مِن قُوَّةٖ وَلَا نَاصِرٖ

Basi hatakuwa na nguvu wala msaidizi.

Basi hatakuwa na nguvu wala msaidizi.

وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلرَّجۡعِ

Ninaapa kwa mbingu yenye marejeo!

Ninaapa kwa mbingu yenye marejeo!

وَٱلۡأَرۡضِ ذَاتِ ٱلصَّدۡعِ

Na kwa ardhi inayopasuka!

Na kwa ardhi inayopasuka!

إِنَّهُۥ لَقَوۡلٞ فَصۡلٞ

Hakika hii ni kauli ya kupambanua.

Hakika hii ni kauli ya kupambanua.

وَمَا هُوَ بِٱلۡهَزۡلِ

Wala si mzaha.

Wala si mzaha.

إِنَّهُمۡ يَكِيدُونَ كَيۡدٗا

Hakika wao wanapanga mpango.

Hakika wao wanapanga mpango.

وَأَكِيدُ كَيۡدٗا

Na Mimi napanga mpango.

Na Mimi napanga mpango.

فَمَهِّلِ ٱلۡكَٰفِرِينَ أَمۡهِلۡهُمۡ رُوَيۡدَۢا

Basi wape muhula makafiri - wape muhula pole pole.

Basi wape muhula makafiri - wape muhula pole pole.
Footer Include