Header Include

Swahili translation - Rowad Translation Center

translated by Rowwad Translation Center, in cooperation with the Islamic Propagation Office in Rabwah and the Association for Serving Islamic Content in Languages.

QR Code https://quran.islamcontent.com/rn/swahili_rwwad

وَٱلطُّورِ

Ninaapa kwa mlima wa T'ur.

Ninaapa kwa mlima wa T'ur.

وَكِتَٰبٖ مَّسۡطُورٖ

Na Kitabu kilichoandikwa.

Na Kitabu kilichoandikwa.

فِي رَقّٖ مَّنشُورٖ

Katika ngozi iliyokunjuliwa.

Katika ngozi iliyokunjuliwa.

وَٱلۡبَيۡتِ ٱلۡمَعۡمُورِ

Na kwa Nyumba iliyojengwa.

Na kwa Nyumba iliyojengwa.

وَٱلسَّقۡفِ ٱلۡمَرۡفُوعِ

Na kwa dari iliyonyanyuliwa.

Na kwa dari iliyonyanyuliwa.

وَٱلۡبَحۡرِ ٱلۡمَسۡجُورِ

Na kwa bahari iliyojazwa.

Na kwa bahari iliyojazwa.

إِنَّ عَذَابَ رَبِّكَ لَوَٰقِعٞ

Hakika adhabu ya Mola wako Mlezi hapana shaka itatokea.

Hakika adhabu ya Mola wako Mlezi hapana shaka itatokea.

مَّا لَهُۥ مِن دَافِعٖ

Hapana wa kuizuia.

Hapana wa kuizuia.

يَوۡمَ تَمُورُ ٱلسَّمَآءُ مَوۡرٗا

Siku zitakapotikisika mbingu kwa mtikiso.

Siku zitakapotikisika mbingu kwa mtikiso.

وَتَسِيرُ ٱلۡجِبَالُ سَيۡرٗا

Na milima iwe inakwenda kwa mwendo mkubwa.

Na milima iwe inakwenda kwa mwendo mkubwa.

فَوَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Basi ole wao siku hiyo hao wanaokadhibisha.

Basi ole wao siku hiyo hao wanaokadhibisha.

ٱلَّذِينَ هُمۡ فِي خَوۡضٖ يَلۡعَبُونَ

Ambao wanacheza katika mambo ya upuuzi.

Ambao wanacheza katika mambo ya upuuzi.

يَوۡمَ يُدَعُّونَ إِلَىٰ نَارِ جَهَنَّمَ دَعًّا

Siku watakaposukumwa kwenye Moto kwa msukumo wa nguvu.

Siku watakaposukumwa kwenye Moto kwa msukumo wa nguvu.

هَٰذِهِ ٱلنَّارُ ٱلَّتِي كُنتُم بِهَا تُكَذِّبُونَ

(Waambiwe): Huu ndio ule Moto mliokuwa mkiukadhibisha!

(Waambiwe): Huu ndio ule Moto mliokuwa mkiukadhibisha!

أَفَسِحۡرٌ هَٰذَآ أَمۡ أَنتُمۡ لَا تُبۡصِرُونَ

Je, huu ni uchawi, au hamwoni tu?

Je, huu ni uchawi, au hamwoni tu?

ٱصۡلَوۡهَا فَٱصۡبِرُوٓاْ أَوۡ لَا تَصۡبِرُواْ سَوَآءٌ عَلَيۡكُمۡۖ إِنَّمَا تُجۡزَوۡنَ مَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ

Uingieni, mkistahamili au msistahamili - ni mamoja kwenu. Hakika mnalipwa kwa mliyokuwa mkiyatenda.

Uingieni, mkistahamili au msistahamili - ni mamoja kwenu. Hakika mnalipwa kwa mliyokuwa mkiyatenda.

إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي جَنَّٰتٖ وَنَعِيمٖ

Hakika wacha Mungu watakuwa katika Mabustani na neema.

Hakika wacha Mungu watakuwa katika Mabustani na neema.

فَٰكِهِينَ بِمَآ ءَاتَىٰهُمۡ رَبُّهُمۡ وَوَقَىٰهُمۡ رَبُّهُمۡ عَذَابَ ٱلۡجَحِيمِ

Wakifurahi kwa yale aliyowapa Mola wao Mlezi. Na Mola wao Mlezi atawalinda kutokana na adhabu ya Motoni.

Wakifurahi kwa yale aliyowapa Mola wao Mlezi. Na Mola wao Mlezi atawalinda kutokana na adhabu ya Motoni.

كُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ هَنِيٓـَٔۢا بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ

Kuleni na kunyweni kwa raha kabisa kwa sababu ya mliyokuwa mkiyatenda.

Kuleni na kunyweni kwa raha kabisa kwa sababu ya mliyokuwa mkiyatenda.

مُتَّكِـِٔينَ عَلَىٰ سُرُرٖ مَّصۡفُوفَةٖۖ وَزَوَّجۡنَٰهُم بِحُورٍ عِينٖ

Watakuwa wameegemea juu ya viti vya enzi vilivyopangwa kwa safu. Na tutawaoza mahurulaini.

Watakuwa wameegemea juu ya viti vya enzi vilivyopangwa kwa safu. Na tutawaoza mahurulaini.

وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَٱتَّبَعَتۡهُمۡ ذُرِّيَّتُهُم بِإِيمَٰنٍ أَلۡحَقۡنَا بِهِمۡ ذُرِّيَّتَهُمۡ وَمَآ أَلَتۡنَٰهُم مِّنۡ عَمَلِهِم مِّن شَيۡءٖۚ كُلُّ ٱمۡرِيِٕۭ بِمَا كَسَبَ رَهِينٞ

Na wale walioamini na dhuriya zao wakawafuata kwa Imani, tutawakutanisha nao dhuriya zao, na wala hatutawapunja hata kidogo katika vitendo vyao. Kila mtu lazima atapata alichokichuma.

Na wale walioamini na dhuriya zao wakawafuata kwa Imani, tutawakutanisha nao dhuriya zao, na wala hatutawapunja hata kidogo katika vitendo vyao. Kila mtu lazima atapata alichokichuma.

وَأَمۡدَدۡنَٰهُم بِفَٰكِهَةٖ وَلَحۡمٖ مِّمَّا يَشۡتَهُونَ

Na tutawapa matunda, na nyama kama watakavyopenda.

Na tutawapa matunda, na nyama kama watakavyopenda.

يَتَنَٰزَعُونَ فِيهَا كَأۡسٗا لَّا لَغۡوٞ فِيهَا وَلَا تَأۡثِيمٞ

Watapeana humo bilauri zisizo na vinywaji vya kuleta maneno ya upuuzi wala dhambi.

Watapeana humo bilauri zisizo na vinywaji vya kuleta maneno ya upuuzi wala dhambi.

۞ وَيَطُوفُ عَلَيۡهِمۡ غِلۡمَانٞ لَّهُمۡ كَأَنَّهُمۡ لُؤۡلُؤٞ مَّكۡنُونٞ

Iwe wanawapitia watumishi wao kama kwamba ni lulu zilizomo katika chaza.

Iwe wanawapitia watumishi wao kama kwamba ni lulu zilizomo katika chaza.

وَأَقۡبَلَ بَعۡضُهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖ يَتَسَآءَلُونَ

Wataelekeana wakiulizana.

Wataelekeana wakiulizana.

قَالُوٓاْ إِنَّا كُنَّا قَبۡلُ فِيٓ أَهۡلِنَا مُشۡفِقِينَ

Waseme: Hakika tulikuwa zamani pamoja na ahali zetu tukiogopa mno.

Waseme: Hakika tulikuwa zamani pamoja na ahali zetu tukiogopa mno.

فَمَنَّ ٱللَّهُ عَلَيۡنَا وَوَقَىٰنَا عَذَابَ ٱلسَّمُومِ

Basi Mwenyezi Mungu akatufanyia hisani na akatulinda mbali adhabu ya upepo wa Moto.

Basi Mwenyezi Mungu akatufanyia hisani na akatulinda mbali adhabu ya upepo wa Moto.

إِنَّا كُنَّا مِن قَبۡلُ نَدۡعُوهُۖ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلۡبَرُّ ٱلرَّحِيمُ

Hakika sisi zamani tulikuwa tukimwomba Yeye tu. Hakika Yeye ndiye Mwema Mwingi wa kurehemu.

Hakika sisi zamani tulikuwa tukimwomba Yeye tu. Hakika Yeye ndiye Mwema Mwingi wa kurehemu.

فَذَكِّرۡ فَمَآ أَنتَ بِنِعۡمَتِ رَبِّكَ بِكَاهِنٖ وَلَا مَجۡنُونٍ

Basi kumbusha! Kwani wewe, kwa neema ya Mola wako Mlezi, si kuhani wala mwendawazimu.

Basi kumbusha! Kwani wewe, kwa neema ya Mola wako Mlezi, si kuhani wala mwendawazimu.

أَمۡ يَقُولُونَ شَاعِرٞ نَّتَرَبَّصُ بِهِۦ رَيۡبَ ٱلۡمَنُونِ

Au wanasema: Huyu ni mtunga mashairi, tunamtarajia kupatilizwa na dahari.

Au wanasema: Huyu ni mtunga mashairi, tunamtarajia kupatilizwa na dahari.

قُلۡ تَرَبَّصُواْ فَإِنِّي مَعَكُم مِّنَ ٱلۡمُتَرَبِّصِينَ

Sema: Tarajieni, na mimi pia ni pamoja nanyi katika kutarajia.

Sema: Tarajieni, na mimi pia ni pamoja nanyi katika kutarajia.

أَمۡ تَأۡمُرُهُمۡ أَحۡلَٰمُهُم بِهَٰذَآۚ أَمۡ هُمۡ قَوۡمٞ طَاغُونَ

Au hizo akili zao ndio zinawaamrisha haya, au wao basi ni watu majeuri tu?

Au hizo akili zao ndio zinawaamrisha haya, au wao basi ni watu majeuri tu?

أَمۡ يَقُولُونَ تَقَوَّلَهُۥۚ بَل لَّا يُؤۡمِنُونَ

Au ndiyo wanasema: 'Ameitunga hii!' Bali basi tu hawaamini!

Au ndiyo wanasema: 'Ameitunga hii!' Bali basi tu hawaamini!

فَلۡيَأۡتُواْ بِحَدِيثٖ مِّثۡلِهِۦٓ إِن كَانُواْ صَٰدِقِينَ

Basi nawalete masimulizi kama haya ikiwa wao wanasema kweli.

Basi nawalete masimulizi kama haya ikiwa wao wanasema kweli.

أَمۡ خُلِقُواْ مِنۡ غَيۡرِ شَيۡءٍ أَمۡ هُمُ ٱلۡخَٰلِقُونَ

Au wao wameumbwa pasipo kutokana na kitu chochote, au ni wao ndio waumbaji?

Au wao wameumbwa pasipo kutokana na kitu chochote, au ni wao ndio waumbaji?

أَمۡ خَلَقُواْ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَۚ بَل لَّا يُوقِنُونَ

Au wao wameziumba mbingu na ardhi? Bali hawana yakini.

Au wao wameziumba mbingu na ardhi? Bali hawana yakini.

أَمۡ عِندَهُمۡ خَزَآئِنُ رَبِّكَ أَمۡ هُمُ ٱلۡمُصَۜيۡطِرُونَ

Au wanazo hazina za Mola wako Mlezi au wao ndio wenye madaraka?

Au wanazo hazina za Mola wako Mlezi au wao ndio wenye madaraka?

أَمۡ لَهُمۡ سُلَّمٞ يَسۡتَمِعُونَ فِيهِۖ فَلۡيَأۡتِ مُسۡتَمِعُهُم بِسُلۡطَٰنٖ مُّبِينٍ

Au wanazo ngazi za kusikilizia? Basi huyo msikilizaji wao na alete hoja iliyo wazi!

Au wanazo ngazi za kusikilizia? Basi huyo msikilizaji wao na alete hoja iliyo wazi!

أَمۡ لَهُ ٱلۡبَنَٰتُ وَلَكُمُ ٱلۡبَنُونَ

Au Yeye Mwenyezi Mungu ana wasichana, na nyinyi ndio mna wavulana?

Au Yeye Mwenyezi Mungu ana wasichana, na nyinyi ndio mna wavulana?

أَمۡ تَسۡـَٔلُهُمۡ أَجۡرٗا فَهُم مِّن مَّغۡرَمٖ مُّثۡقَلُونَ

Au wewe unawaomba ujira, na kwa hivyo ndio wanaelemewa na uzito wa gharama?

Au wewe unawaomba ujira, na kwa hivyo ndio wanaelemewa na uzito wa gharama?

أَمۡ عِندَهُمُ ٱلۡغَيۡبُ فَهُمۡ يَكۡتُبُونَ

Au wanayo elimu ya ghaibu, nao wameandika?

Au wanayo elimu ya ghaibu, nao wameandika?

أَمۡ يُرِيدُونَ كَيۡدٗاۖ فَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ هُمُ ٱلۡمَكِيدُونَ

Au wanataka kufanya vitimbi tu? Lakini hao waliokufuru ndio watakaotegeka.

Au wanataka kufanya vitimbi tu? Lakini hao waliokufuru ndio watakaotegeka.

أَمۡ لَهُمۡ إِلَٰهٌ غَيۡرُ ٱللَّهِۚ سُبۡحَٰنَ ٱللَّهِ عَمَّا يُشۡرِكُونَ

Au wanaye mungu asiyekuwa Mwenyezi Mungu? Ametakasika Mwenyezi Mungu mbali na hao wanaowashirikisha naye.

Au wanaye mungu asiyekuwa Mwenyezi Mungu? Ametakasika Mwenyezi Mungu mbali na hao wanaowashirikisha naye.

وَإِن يَرَوۡاْ كِسۡفٗا مِّنَ ٱلسَّمَآءِ سَاقِطٗا يَقُولُواْ سَحَابٞ مَّرۡكُومٞ

Na hata wangeona pande linatoka mbinguni linaanguka wangesema: Ni mawingu yaliyobebana.

Na hata wangeona pande linatoka mbinguni linaanguka wangesema: Ni mawingu yaliyobebana.

فَذَرۡهُمۡ حَتَّىٰ يُلَٰقُواْ يَوۡمَهُمُ ٱلَّذِي فِيهِ يُصۡعَقُونَ

Basi waache mpaka wakutane na siku yao watakapohilikishwa.

Basi waache mpaka wakutane na siku yao watakapohilikishwa.

يَوۡمَ لَا يُغۡنِي عَنۡهُمۡ كَيۡدُهُمۡ شَيۡـٔٗا وَلَا هُمۡ يُنصَرُونَ

Siku ambayo hila zao hazitawafaa hata kidogo, wala wao hawatanusuriwa.

Siku ambayo hila zao hazitawafaa hata kidogo, wala wao hawatanusuriwa.

وَإِنَّ لِلَّذِينَ ظَلَمُواْ عَذَابٗا دُونَ ذَٰلِكَ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَهُمۡ لَا يَعۡلَمُونَ

Na hakika wale waliodhulumu watapata adhabu nyingine isiyokuwa hii, lakini wengi wao hawajui.

Na hakika wale waliodhulumu watapata adhabu nyingine isiyokuwa hii, lakini wengi wao hawajui.

وَٱصۡبِرۡ لِحُكۡمِ رَبِّكَ فَإِنَّكَ بِأَعۡيُنِنَاۖ وَسَبِّحۡ بِحَمۡدِ رَبِّكَ حِينَ تَقُومُ

Na ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi. Kwani wewe hakika uko mbele ya macho yetu.

Na ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi. Kwani wewe hakika uko mbele ya macho yetu.

وَمِنَ ٱلَّيۡلِ فَسَبِّحۡهُ وَإِدۡبَٰرَ ٱلنُّجُومِ

Na usiku pia mtakase, na zinapokuchwa nyota.

Na usiku pia mtakase, na zinapokuchwa nyota.
Footer Include