Header Include

Swahili translation - Rowad Translation Center

translated by Rowwad Translation Center, in cooperation with the Islamic Propagation Office in Rabwah and the Association for Serving Islamic Content in Languages.

QR Code https://quran.islamcontent.com/so/swahili_rwwad

طسٓمٓ

Tw'a Siin Miim.[1]

[1] Herufi hizi "Tw'aa, Sin, Miim" na herufi nyinginezo za mkato zilizo mwanzoni mwa sura mbalimbali zinaonyesha hali ya ushindi wa Qur-ani. Kwani, washirikina walipewa changamoto kwayo, lakini wakashindwa na hawakuweza kuipinga, ilhali inajumuisha herufi hizi zinazounda lugha ya Kiarabu. Kwa hivyo, kutoweza kwa Waarabu kuleta kitu kama hicho - ingawa walikuwa ndio watu wenye ufasaha zaidi - kunaonyesha kwamba Qur-ani ni ufunuo (wahyi) kutoka kwa Mwenyezi Mungu.
Tw'a Siin Miim.[1]

تِلۡكَ ءَايَٰتُ ٱلۡكِتَٰبِ ٱلۡمُبِينِ

Hizi ni Aya za Kitabu kinachobainisha.

Hizi ni Aya za Kitabu kinachobainisha.

لَعَلَّكَ بَٰخِعٞ نَّفۡسَكَ أَلَّا يَكُونُواْ مُؤۡمِنِينَ

Huenda ukaihiliki nafsi yako kwa kuwa hawawi Waumini.

Huenda ukaihiliki nafsi yako kwa kuwa hawawi Waumini.

إِن نَّشَأۡ نُنَزِّلۡ عَلَيۡهِم مِّنَ ٱلسَّمَآءِ ءَايَةٗ فَظَلَّتۡ أَعۡنَٰقُهُمۡ لَهَا خَٰضِعِينَ

Tungependa, tungeliwateremshia kutoka mbinguni Ishara zikashinda zimezinyenyekea shingo zao.

Tungependa, tungeliwateremshia kutoka mbinguni Ishara zikashinda zimezinyenyekea shingo zao.

وَمَا يَأۡتِيهِم مِّن ذِكۡرٖ مِّنَ ٱلرَّحۡمَٰنِ مُحۡدَثٍ إِلَّا كَانُواْ عَنۡهُ مُعۡرِضِينَ

Wala hauwafikii ukumbusho mpya kutoka kwa Arrahman (Mwingi wa rehema), isipokuwa wao huupa mgongo.

Wala hauwafikii ukumbusho mpya kutoka kwa Arrahman (Mwingi wa rehema), isipokuwa wao huupa mgongo.

فَقَدۡ كَذَّبُواْ فَسَيَأۡتِيهِمۡ أَنۢبَٰٓؤُاْ مَا كَانُواْ بِهِۦ يَسۡتَهۡزِءُونَ

Kwa yakini wamekwishakanusha; kwa hivyo zitakuja wafikia habari za yale waliyokuwa wakiyafanyia stihizai.

Kwa yakini wamekwishakanusha; kwa hivyo zitakuja wafikia habari za yale waliyokuwa wakiyafanyia stihizai.

أَوَلَمۡ يَرَوۡاْ إِلَى ٱلۡأَرۡضِ كَمۡ أَنۢبَتۡنَا فِيهَا مِن كُلِّ زَوۡجٖ كَرِيمٍ

Je, hawakuiona ardhi, ni mimea mingapi tumeiotesha humo, ya kila namna nzuri?

Je, hawakuiona ardhi, ni mimea mingapi tumeiotesha humo, ya kila namna nzuri?

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ

Hakika katika haya zipo Ishara. Lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.

Hakika katika haya zipo Ishara. Lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.

Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.

وَإِذۡ نَادَىٰ رَبُّكَ مُوسَىٰٓ أَنِ ٱئۡتِ ٱلۡقَوۡمَ ٱلظَّٰلِمِينَ

Na Mola wako Mlezi, alipomwita Musa, akamwambia: Nenda kwa kaumu madhalimu.

Na Mola wako Mlezi, alipomwita Musa, akamwambia: Nenda kwa kaumu madhalimu.

قَوۡمَ فِرۡعَوۡنَۚ أَلَا يَتَّقُونَ

Kaumu wa Firauni. Kwani hawamchi Mwenyezi Mungu?

Kaumu wa Firauni. Kwani hawamchi Mwenyezi Mungu?

قَالَ رَبِّ إِنِّيٓ أَخَافُ أَن يُكَذِّبُونِ

Akasema: Mola wangu Mlezi, hakika mimi ninachelea kwamba watanikadhibisha.

Akasema: Mola wangu Mlezi, hakika mimi ninachelea kwamba watanikadhibisha.

وَيَضِيقُ صَدۡرِي وَلَا يَنطَلِقُ لِسَانِي فَأَرۡسِلۡ إِلَىٰ هَٰرُونَ

Na kifua changu kina dhiki, na ulimi wangu haukunjuki vyema. Basi mtumie ujumbe Harun.

Na kifua changu kina dhiki, na ulimi wangu haukunjuki vyema. Basi mtumie ujumbe Harun.

وَلَهُمۡ عَلَيَّ ذَنۢبٞ فَأَخَافُ أَن يَقۡتُلُونِ

Na wao wana dhambi niliyowafanyia, kwa hivyo ninahofu wanaweza kuniua.

Na wao wana dhambi niliyowafanyia, kwa hivyo ninahofu wanaweza kuniua.

قَالَ كَلَّاۖ فَٱذۡهَبَا بِـَٔايَٰتِنَآۖ إِنَّا مَعَكُم مُّسۡتَمِعُونَ

Akasema: Sivyo hivyo kabisa! Nendeni na miujiza yetu. Hakika Sisi tu pamoja nanyi, tunasikiliza.

Akasema: Sivyo hivyo kabisa! Nendeni na miujiza yetu. Hakika Sisi tu pamoja nanyi, tunasikiliza.

فَأۡتِيَا فِرۡعَوۡنَ فَقُولَآ إِنَّا رَسُولُ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Basi nendeni kwa Firauni na mwambieni: Hakika sisi ni Mitume wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Basi nendeni kwa Firauni na mwambieni: Hakika sisi ni Mitume wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

أَنۡ أَرۡسِلۡ مَعَنَا بَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ

Kwamba: Waachilie Wana wa Israili waende pamoja nasi.

Kwamba: Waachilie Wana wa Israili waende pamoja nasi.

قَالَ أَلَمۡ نُرَبِّكَ فِينَا وَلِيدٗا وَلَبِثۡتَ فِينَا مِنۡ عُمُرِكَ سِنِينَ

(Firauni) akasema: Je, sisi hatukukulea wewe utotoni, na ukakaa miongoni mwetu katika umri wako miaka mingi?

(Firauni) akasema: Je, sisi hatukukulea wewe utotoni, na ukakaa miongoni mwetu katika umri wako miaka mingi?

وَفَعَلۡتَ فَعۡلَتَكَ ٱلَّتِي فَعَلۡتَ وَأَنتَ مِنَ ٱلۡكَٰفِرِينَ

Na ukatenda kitendo chako ulichotenda, nawe ukawa miongoni mwa wenye kukufuru?

Na ukatenda kitendo chako ulichotenda, nawe ukawa miongoni mwa wenye kukufuru?

قَالَ فَعَلۡتُهَآ إِذٗا وَأَنَا۠ مِنَ ٱلضَّآلِّينَ

(Musa) akasema: Nilitenda hayo hapo nilipokuwa miongoni mwa wale waliopotea.

(Musa) akasema: Nilitenda hayo hapo nilipokuwa miongoni mwa wale waliopotea.

فَفَرَرۡتُ مِنكُمۡ لَمَّا خِفۡتُكُمۡ فَوَهَبَ لِي رَبِّي حُكۡمٗا وَجَعَلَنِي مِنَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Basi nikawakimbia nilipowahofu, tena Mola wangu Mlezi akanitunukia hukumu, na akanijaalia niwe miongoni mwa Mitume.

Basi nikawakimbia nilipowahofu, tena Mola wangu Mlezi akanitunukia hukumu, na akanijaalia niwe miongoni mwa Mitume.

وَتِلۡكَ نِعۡمَةٞ تَمُنُّهَا عَلَيَّ أَنۡ عَبَّدتَّ بَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ

Na hiyo ndiyo neema ya kunisimbulia, na wewe umewatia utumwani Wana wa Israili?

Na hiyo ndiyo neema ya kunisimbulia, na wewe umewatia utumwani Wana wa Israili?

قَالَ فِرۡعَوۡنُ وَمَا رَبُّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Firauni akasema: Na ni nani huyo Mola Mlezi wa walimwengu wote?

Firauni akasema: Na ni nani huyo Mola Mlezi wa walimwengu wote?

قَالَ رَبُّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَآۖ إِن كُنتُم مُّوقِنِينَ

Akasema: Ndiye Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na vilivyo baina yake, ikiwa nyinyi ni wenye yakini.

Akasema: Ndiye Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na vilivyo baina yake, ikiwa nyinyi ni wenye yakini.

قَالَ لِمَنۡ حَوۡلَهُۥٓ أَلَا تَسۡتَمِعُونَ

(Firauni) akawaambia waliomzunguka: Kwani hamsikilizi?

(Firauni) akawaambia waliomzunguka: Kwani hamsikilizi?

قَالَ رَبُّكُمۡ وَرَبُّ ءَابَآئِكُمُ ٱلۡأَوَّلِينَ

(Musa) akasema: Ndiye Mola wenu Mlezi, na Mola Mlezi wa baba zenu wa kwanza.

(Musa) akasema: Ndiye Mola wenu Mlezi, na Mola Mlezi wa baba zenu wa kwanza.

قَالَ إِنَّ رَسُولَكُمُ ٱلَّذِيٓ أُرۡسِلَ إِلَيۡكُمۡ لَمَجۡنُونٞ

(Firauni) akasema: Hakika huyu Mtume wenu aliyetumwa kwenu ni mwendawazimu.

(Firauni) akasema: Hakika huyu Mtume wenu aliyetumwa kwenu ni mwendawazimu.

قَالَ رَبُّ ٱلۡمَشۡرِقِ وَٱلۡمَغۡرِبِ وَمَا بَيۡنَهُمَآۖ إِن كُنتُمۡ تَعۡقِلُونَ

(Musa) akasema: Ndiye Mola Mlezi wa Mashariki na Magharibi na vilivyo baina yake, ikiwa nyinyi mnatia akilini.

(Musa) akasema: Ndiye Mola Mlezi wa Mashariki na Magharibi na vilivyo baina yake, ikiwa nyinyi mnatia akilini.

قَالَ لَئِنِ ٱتَّخَذۡتَ إِلَٰهًا غَيۡرِي لَأَجۡعَلَنَّكَ مِنَ ٱلۡمَسۡجُونِينَ

(Firauni) akasema: Ukijifanyia mungu mwingine asiyekuwa mimi, basi bila ya shaka nitakufunga gerezani.

(Firauni) akasema: Ukijifanyia mungu mwingine asiyekuwa mimi, basi bila ya shaka nitakufunga gerezani.

قَالَ أَوَلَوۡ جِئۡتُكَ بِشَيۡءٖ مُّبِينٖ

Akasema: Je, hata kama nitakuletea kitu cha kubainisha wazi?

Akasema: Je, hata kama nitakuletea kitu cha kubainisha wazi?

قَالَ فَأۡتِ بِهِۦٓ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّٰدِقِينَ

Akasema: Kilete basi, kama wewe ni katika wakweli.

Akasema: Kilete basi, kama wewe ni katika wakweli.

فَأَلۡقَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِيَ ثُعۡبَانٞ مُّبِينٞ

Basi akaitupa fimbo yake, mara ikawa nyoka wa kuonekana dhahiri.

Basi akaitupa fimbo yake, mara ikawa nyoka wa kuonekana dhahiri.

وَنَزَعَ يَدَهُۥ فَإِذَا هِيَ بَيۡضَآءُ لِلنَّٰظِرِينَ

Na akautoa nje mkono wake, mara ukawa mweupe kwa watazamao.

Na akautoa nje mkono wake, mara ukawa mweupe kwa watazamao.

قَالَ لِلۡمَلَإِ حَوۡلَهُۥٓ إِنَّ هَٰذَا لَسَٰحِرٌ عَلِيمٞ

(Firauni) akawaambia waheshimiwa waliomzunguka: Hakika huyu ni mchawi mtaalamu.

(Firauni) akawaambia waheshimiwa waliomzunguka: Hakika huyu ni mchawi mtaalamu.

يُرِيدُ أَن يُخۡرِجَكُم مِّنۡ أَرۡضِكُم بِسِحۡرِهِۦ فَمَاذَا تَأۡمُرُونَ

Anataka kuwatoa katika nchi yenu kwa uchawi wake. Basi mna shauri gani?

Anataka kuwatoa katika nchi yenu kwa uchawi wake. Basi mna shauri gani?

قَالُوٓاْ أَرۡجِهۡ وَأَخَاهُ وَٱبۡعَثۡ فِي ٱلۡمَدَآئِنِ حَٰشِرِينَ

Wakasema: Mpe muda yeye na kakaye na uwatume mijini wakusanyao watu.

Wakasema: Mpe muda yeye na kakaye na uwatume mijini wakusanyao watu.

يَأۡتُوكَ بِكُلِّ سَحَّارٍ عَلِيمٖ

Wakuletee kila mchawi bingwa mtaalamu.

Wakuletee kila mchawi bingwa mtaalamu.

فَجُمِعَ ٱلسَّحَرَةُ لِمِيقَٰتِ يَوۡمٖ مَّعۡلُومٖ

Basi wakakusanywa wachawi kwa ajili ya miadi ya siku maalumu.

Basi wakakusanywa wachawi kwa ajili ya miadi ya siku maalumu.

وَقِيلَ لِلنَّاسِ هَلۡ أَنتُم مُّجۡتَمِعُونَ

Na watu wakaambiwa: Je, mtakusanyika?

Na watu wakaambiwa: Je, mtakusanyika?

لَعَلَّنَا نَتَّبِعُ ٱلسَّحَرَةَ إِن كَانُواْ هُمُ ٱلۡغَٰلِبِينَ

Huenda tutawafuata wachawi ikiwa wao ndio watakaoshinda.

Huenda tutawafuata wachawi ikiwa wao ndio watakaoshinda.

فَلَمَّا جَآءَ ٱلسَّحَرَةُ قَالُواْ لِفِرۡعَوۡنَ أَئِنَّ لَنَا لَأَجۡرًا إِن كُنَّا نَحۡنُ ٱلۡغَٰلِبِينَ

Basi walipokuja wachawi, wakamwambia Firauni: Je, tutapata ujira ikiwa sisi ndio tutakaoshinda?

Basi walipokuja wachawi, wakamwambia Firauni: Je, tutapata ujira ikiwa sisi ndio tutakaoshinda?

قَالَ نَعَمۡ وَإِنَّكُمۡ إِذٗا لَّمِنَ ٱلۡمُقَرَّبِينَ

Akasema: Ndiyo! Na hakika mtakuwa katika watu wa mbele.

Akasema: Ndiyo! Na hakika mtakuwa katika watu wa mbele.

قَالَ لَهُم مُّوسَىٰٓ أَلۡقُواْ مَآ أَنتُم مُّلۡقُونَ

Musa akawaambia: Tupeni mnavyotaka kutupa.

Musa akawaambia: Tupeni mnavyotaka kutupa.

فَأَلۡقَوۡاْ حِبَالَهُمۡ وَعِصِيَّهُمۡ وَقَالُواْ بِعِزَّةِ فِرۡعَوۡنَ إِنَّا لَنَحۡنُ ٱلۡغَٰلِبُونَ

Basi wakatupa kamba zao na fimbo zao, na wakasema: Kwa nguvu za Firauni hakika sisi hapana shaka ni wenye kushinda.

Basi wakatupa kamba zao na fimbo zao, na wakasema: Kwa nguvu za Firauni hakika sisi hapana shaka ni wenye kushinda.

فَأَلۡقَىٰ مُوسَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِيَ تَلۡقَفُ مَا يَأۡفِكُونَ

Basi Musa akatupa fimbo yake, nayo mara ikavimeza vile walivyovizua.

Basi Musa akatupa fimbo yake, nayo mara ikavimeza vile walivyovizua.

فَأُلۡقِيَ ٱلسَّحَرَةُ سَٰجِدِينَ

Hapo wachawi hao walipinduka wakasujudu.

Hapo wachawi hao walipinduka wakasujudu.

قَالُوٓاْ ءَامَنَّا بِرَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Wakasema: Tumemuamini Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Wakasema: Tumemuamini Mola Mlezi wa walimwengu wote.

رَبِّ مُوسَىٰ وَهَٰرُونَ

Mola Mlezi wa Musa na Harun.

Mola Mlezi wa Musa na Harun.

قَالَ ءَامَنتُمۡ لَهُۥ قَبۡلَ أَنۡ ءَاذَنَ لَكُمۡۖ إِنَّهُۥ لَكَبِيرُكُمُ ٱلَّذِي عَلَّمَكُمُ ٱلسِّحۡرَ فَلَسَوۡفَ تَعۡلَمُونَۚ لَأُقَطِّعَنَّ أَيۡدِيَكُمۡ وَأَرۡجُلَكُم مِّنۡ خِلَٰفٖ وَلَأُصَلِّبَنَّكُمۡ أَجۡمَعِينَ

(Firauni) akasema: Je, mmemuamini kabla ya kuwaruhusu? Bila ya shaka yeye basi ndiye mkubwa wenu aliyewafunza uchawi. Basi mtakuja jua! Nitakatakata mikono yenu na miguu yenu kwa kutofautisha. Na nitawasulubisha misalabani nyote.

(Firauni) akasema: Je, mmemuamini kabla ya kuwaruhusu? Bila ya shaka yeye basi ndiye mkubwa wenu aliyewafunza uchawi. Basi mtakuja jua! Nitakatakata mikono yenu na miguu yenu kwa kutofautisha. Na nitawasulubisha misalabani nyote.

قَالُواْ لَا ضَيۡرَۖ إِنَّآ إِلَىٰ رَبِّنَا مُنقَلِبُونَ

Wakasema: Haidhuru, kwani sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.

Wakasema: Haidhuru, kwani sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.

إِنَّا نَطۡمَعُ أَن يَغۡفِرَ لَنَا رَبُّنَا خَطَٰيَٰنَآ أَن كُنَّآ أَوَّلَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Hakika sisi tunatumai kwamba Mola wetu Mlezi atatusamehe makosa yetu, kwa kuwa tumekuwa wa kwanza wa Waumini.

Hakika sisi tunatumai kwamba Mola wetu Mlezi atatusamehe makosa yetu, kwa kuwa tumekuwa wa kwanza wa Waumini.

۞ وَأَوۡحَيۡنَآ إِلَىٰ مُوسَىٰٓ أَنۡ أَسۡرِ بِعِبَادِيٓ إِنَّكُم مُّتَّبَعُونَ

Na tulimuamrisha Musa kwa ufunuo: Nenda na waja wangu wakati wa usiku. Kwa hakika mtafuatwa.

Na tulimuamrisha Musa kwa ufunuo: Nenda na waja wangu wakati wa usiku. Kwa hakika mtafuatwa.

فَأَرۡسَلَ فِرۡعَوۡنُ فِي ٱلۡمَدَآئِنِ حَٰشِرِينَ

Basi Firauni akawatuma mijini wakusanyaji.

Basi Firauni akawatuma mijini wakusanyaji.

إِنَّ هَٰٓؤُلَآءِ لَشِرۡذِمَةٞ قَلِيلُونَ

(Wakieneza): Hakika hawa ni kikundi kidogo.

(Wakieneza): Hakika hawa ni kikundi kidogo.

وَإِنَّهُمۡ لَنَا لَغَآئِظُونَ

Nao kwa hakika wanatuudhi.

Nao kwa hakika wanatuudhi.

وَإِنَّا لَجَمِيعٌ حَٰذِرُونَ

Na sisi ni wengi, wenye kuchukua hadhari.

Na sisi ni wengi, wenye kuchukua hadhari.

فَأَخۡرَجۡنَٰهُم مِّن جَنَّٰتٖ وَعُيُونٖ

Basi tukawatoa katika mabustani na chemchemi.

Basi tukawatoa katika mabustani na chemchemi.

وَكُنُوزٖ وَمَقَامٖ كَرِيمٖ

Na mahazina, na vyeo vya heshima,

Na mahazina, na vyeo vya heshima,

كَذَٰلِكَۖ وَأَوۡرَثۡنَٰهَا بَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ

Vivyo hivyo, na tukawarithisha hayo Wana wa Israili.

Vivyo hivyo, na tukawarithisha hayo Wana wa Israili.

فَأَتۡبَعُوهُم مُّشۡرِقِينَ

Basi wakawafuata lilipochomoza jua.

Basi wakawafuata lilipochomoza jua.

فَلَمَّا تَرَٰٓءَا ٱلۡجَمۡعَانِ قَالَ أَصۡحَٰبُ مُوسَىٰٓ إِنَّا لَمُدۡرَكُونَ

Na yalipoonana majeshi mawili haya, watu wa Musa wakasema: Hakika sisi bila ya shaka tumekutwa!

Na yalipoonana majeshi mawili haya, watu wa Musa wakasema: Hakika sisi bila ya shaka tumekutwa!

قَالَ كَلَّآۖ إِنَّ مَعِيَ رَبِّي سَيَهۡدِينِ

(Musa) akasema: Hasha! Hakika yu pamoja nami Mola wangu Mlezi. Yeye ataniongoa!

(Musa) akasema: Hasha! Hakika yu pamoja nami Mola wangu Mlezi. Yeye ataniongoa!

فَأَوۡحَيۡنَآ إِلَىٰ مُوسَىٰٓ أَنِ ٱضۡرِب بِّعَصَاكَ ٱلۡبَحۡرَۖ فَٱنفَلَقَ فَكَانَ كُلُّ فِرۡقٖ كَٱلطَّوۡدِ ٱلۡعَظِيمِ

Na tulimletea Musa ufunuo tukamwambia: Piga bahari kwa fimbo yako. Basi ikatengana, na kila sehemu ikawa kama mlima mkubwa.

Na tulimletea Musa ufunuo tukamwambia: Piga bahari kwa fimbo yako. Basi ikatengana, na kila sehemu ikawa kama mlima mkubwa.

وَأَزۡلَفۡنَا ثَمَّ ٱلۡأٓخَرِينَ

Na tukawasongesha hapo karibu wale wengine.

Na tukawasongesha hapo karibu wale wengine.

وَأَنجَيۡنَا مُوسَىٰ وَمَن مَّعَهُۥٓ أَجۡمَعِينَ

Tukawaokoa Musa na wale waliokuwa pamoja naye wote.

Tukawaokoa Musa na wale waliokuwa pamoja naye wote.

ثُمَّ أَغۡرَقۡنَا ٱلۡأٓخَرِينَ

Kisha tukawazamisha hao wengine.

Kisha tukawazamisha hao wengine.

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ

Hakika bila ya shaka katika hayo ipo Ishara; lakini wengi wao si wenye kuamini.

Hakika bila ya shaka katika hayo ipo Ishara; lakini wengi wao si wenye kuamini.

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

Na kwa hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.

Na kwa hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.

وَٱتۡلُ عَلَيۡهِمۡ نَبَأَ إِبۡرَٰهِيمَ

Na wasomee habari za Ibrahim.

Na wasomee habari za Ibrahim.

إِذۡ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوۡمِهِۦ مَا تَعۡبُدُونَ

Alipomwambia baba yake na kaumu yake: Mnaabudu nini?

Alipomwambia baba yake na kaumu yake: Mnaabudu nini?

قَالُواْ نَعۡبُدُ أَصۡنَامٗا فَنَظَلُّ لَهَا عَٰكِفِينَ

Wakasema: Tunaabudu masanamu, daima tunayanyenyekea.

Wakasema: Tunaabudu masanamu, daima tunayanyenyekea.

قَالَ هَلۡ يَسۡمَعُونَكُمۡ إِذۡ تَدۡعُونَ

Akasema: Je, yanawasikia mnapoyaita?

Akasema: Je, yanawasikia mnapoyaita?

أَوۡ يَنفَعُونَكُمۡ أَوۡ يَضُرُّونَ

Au yanawafaa, au yanawadhuru?

Au yanawafaa, au yanawadhuru?

قَالُواْ بَلۡ وَجَدۡنَآ ءَابَآءَنَا كَذَٰلِكَ يَفۡعَلُونَ

Wakasema: Bali tuliwakuta baba zetu wakifanya hivyo hivyo.

Wakasema: Bali tuliwakuta baba zetu wakifanya hivyo hivyo.

قَالَ أَفَرَءَيۡتُم مَّا كُنتُمۡ تَعۡبُدُونَ

Akasema: "Je, mmewaona hawa mnaowaabudu?

Akasema: "Je, mmewaona hawa mnaowaabudu?

أَنتُمۡ وَءَابَآؤُكُمُ ٱلۡأَقۡدَمُونَ

Nyinyi na baba zenu wa zamani?

Nyinyi na baba zenu wa zamani?

فَإِنَّهُمۡ عَدُوّٞ لِّيٓ إِلَّا رَبَّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Kwani hakika hao ni adui zangu, isipokuwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Kwani hakika hao ni adui zangu, isipokuwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

ٱلَّذِي خَلَقَنِي فَهُوَ يَهۡدِينِ

Ambaye ndiye aliyeniumba, na Yeye ndiye ananiongoa.

Ambaye ndiye aliyeniumba, na Yeye ndiye ananiongoa.

وَٱلَّذِي هُوَ يُطۡعِمُنِي وَيَسۡقِينِ

Na ambaye ndiye ananilisha na kuninywesha.

Na ambaye ndiye ananilisha na kuninywesha.

وَإِذَا مَرِضۡتُ فَهُوَ يَشۡفِينِ

Na ninapougua, ni Yeye ndiye anayeniponesha.

Na ninapougua, ni Yeye ndiye anayeniponesha.

وَٱلَّذِي يُمِيتُنِي ثُمَّ يُحۡيِينِ

Na ambaye atanifisha, na kisha atanihuisha.

Na ambaye atanifisha, na kisha atanihuisha.

وَٱلَّذِيٓ أَطۡمَعُ أَن يَغۡفِرَ لِي خَطِيٓـَٔتِي يَوۡمَ ٱلدِّينِ

Na ambaye ndiye ninayemtumai kunisamehe makosa yangu Siku ya Malipo.

Na ambaye ndiye ninayemtumai kunisamehe makosa yangu Siku ya Malipo.

رَبِّ هَبۡ لِي حُكۡمٗا وَأَلۡحِقۡنِي بِٱلصَّٰلِحِينَ

Mola wangu Mlezi! Nitunukie hukumu na uniunganishe na walio wema.

Mola wangu Mlezi! Nitunukie hukumu na uniunganishe na walio wema.

وَٱجۡعَل لِّي لِسَانَ صِدۡقٖ فِي ٱلۡأٓخِرِينَ

Na unijalie nitajwe kwa wema na watu watakaokuja baadaye.

Na unijalie nitajwe kwa wema na watu watakaokuja baadaye.

وَٱجۡعَلۡنِي مِن وَرَثَةِ جَنَّةِ ٱلنَّعِيمِ

Na unijalie katika warithi wa Bustani za neema.

Na unijalie katika warithi wa Bustani za neema.

وَٱغۡفِرۡ لِأَبِيٓ إِنَّهُۥ كَانَ مِنَ ٱلضَّآلِّينَ

Na umsamehe baba yangu, kwani hakika alikuwa miongoni mwa wapotovu.

Na umsamehe baba yangu, kwani hakika alikuwa miongoni mwa wapotovu.

وَلَا تُخۡزِنِي يَوۡمَ يُبۡعَثُونَ

Wala usinihizi Siku watakapofufuliwa.

Wala usinihizi Siku watakapofufuliwa.

يَوۡمَ لَا يَنفَعُ مَالٞ وَلَا بَنُونَ

Siku ambayo kwamba mali haitafaa kitu wala wana.

Siku ambayo kwamba mali haitafaa kitu wala wana.

إِلَّا مَنۡ أَتَى ٱللَّهَ بِقَلۡبٖ سَلِيمٖ

Isipokuwa mwenye kumjia Mwenyezi Mungu na moyo safi."

Isipokuwa mwenye kumjia Mwenyezi Mungu na moyo safi."

وَأُزۡلِفَتِ ٱلۡجَنَّةُ لِلۡمُتَّقِينَ

Na Bustani ya mbiguni itasogezwa kwa wacha Mungu.

Na Bustani ya mbiguni itasogezwa kwa wacha Mungu.

وَبُرِّزَتِ ٱلۡجَحِيمُ لِلۡغَاوِينَ

Na Jahannamu itadhihirishwa kwa wapotovu.

Na Jahannamu itadhihirishwa kwa wapotovu.

وَقِيلَ لَهُمۡ أَيۡنَ مَا كُنتُمۡ تَعۡبُدُونَ

Na wataambiwa: Wako wapi mliokuwa mkiwaabudu.

Na wataambiwa: Wako wapi mliokuwa mkiwaabudu.

مِن دُونِ ٱللَّهِ هَلۡ يَنصُرُونَكُمۡ أَوۡ يَنتَصِرُونَ

Badala ya Mwenyezi Mungu? Je, wanawasaidia, au wanajisaidia wenyewe?

Badala ya Mwenyezi Mungu? Je, wanawasaidia, au wanajisaidia wenyewe?

فَكُبۡكِبُواْ فِيهَا هُمۡ وَٱلۡغَاوُۥنَ

Basi watavurumizwa humo wao na hao wakosefu.

Basi watavurumizwa humo wao na hao wakosefu.

وَجُنُودُ إِبۡلِيسَ أَجۡمَعُونَ

Na majeshi ya Ibilisi yote.

Na majeshi ya Ibilisi yote.

قَالُواْ وَهُمۡ فِيهَا يَخۡتَصِمُونَ

Watasema, na hali ya kuwa wanazozana humo:

Watasema, na hali ya kuwa wanazozana humo:

تَٱللَّهِ إِن كُنَّا لَفِي ضَلَٰلٖ مُّبِينٍ

"Tallahi! Kwa yakini tulikuwa katika upotovu ulio dhahiri.

"Tallahi! Kwa yakini tulikuwa katika upotovu ulio dhahiri.

إِذۡ نُسَوِّيكُم بِرَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Tulipowafanya nyinyi ni sawa na Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Tulipowafanya nyinyi ni sawa na Mola Mlezi wa walimwengu wote.

وَمَآ أَضَلَّنَآ إِلَّا ٱلۡمُجۡرِمُونَ

Na hawakutupoteza isipokuwa wale wakosefu.

Na hawakutupoteza isipokuwa wale wakosefu.

فَمَا لَنَا مِن شَٰفِعِينَ

Basi hatuna waombezi wowote.

Basi hatuna waombezi wowote.

وَلَا صَدِيقٍ حَمِيمٖ

Wala rafiki wa dhati.

Wala rafiki wa dhati.

فَلَوۡ أَنَّ لَنَا كَرَّةٗ فَنَكُونَ مِنَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Laiti tungelipata kurejea tena, tungelikuwa katika Waumini."

Laiti tungelipata kurejea tena, tungelikuwa katika Waumini."

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ

Hakika katika haya ipo Ishara, lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.

Hakika katika haya ipo Ishara, lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwingi wa kurehemu.

Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwingi wa kurehemu.

كَذَّبَتۡ قَوۡمُ نُوحٍ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Kaumu ya Nuhu waliwakadhibisha Mitume.

Kaumu ya Nuhu waliwakadhibisha Mitume.

إِذۡ قَالَ لَهُمۡ أَخُوهُمۡ نُوحٌ أَلَا تَتَّقُونَ

Alipowaambia ndugu yao, Nuhu: Je, hamumchi Mwenyezi Mungu?

Alipowaambia ndugu yao, Nuhu: Je, hamumchi Mwenyezi Mungu?

إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٞ

Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.

Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.

فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini mimi.

Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini mimi.

وَمَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ مِنۡ أَجۡرٍۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Na siwaulizi juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko isipokuwa kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Na siwaulizi juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko isipokuwa kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini mimi.

Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini mimi.

۞ قَالُوٓاْ أَنُؤۡمِنُ لَكَ وَٱتَّبَعَكَ ٱلۡأَرۡذَلُونَ

Wakasema: Je, tukuamini wewe, ilhali wanaokufuata ni watu duni?

Wakasema: Je, tukuamini wewe, ilhali wanaokufuata ni watu duni?

قَالَ وَمَا عِلۡمِي بِمَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ

Akasema: Ninayajuaje waliyokuwa wakiyafanya?

Akasema: Ninayajuaje waliyokuwa wakiyafanya?

إِنۡ حِسَابُهُمۡ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّيۖ لَوۡ تَشۡعُرُونَ

Hesabu yao haiko isipokuwa kwa Mola wao Mlezi, laiti mngelitambua!

Hesabu yao haiko isipokuwa kwa Mola wao Mlezi, laiti mngelitambua!

وَمَآ أَنَا۠ بِطَارِدِ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Wala mimi si wa kuwafukuza Waumini.

Wala mimi si wa kuwafukuza Waumini.

إِنۡ أَنَا۠ إِلَّا نَذِيرٞ مُّبِينٞ

Mimi si chochote isipokuwa ni Mwonyaji wa dhahiri shahiri.

Mimi si chochote isipokuwa ni Mwonyaji wa dhahiri shahiri.

قَالُواْ لَئِن لَّمۡ تَنتَهِ يَٰنُوحُ لَتَكُونَنَّ مِنَ ٱلۡمَرۡجُومِينَ

Wakasema: Ikiwa huachi, ewe Nuhu, bila ya shaka utapigwa mawe.

Wakasema: Ikiwa huachi, ewe Nuhu, bila ya shaka utapigwa mawe.

قَالَ رَبِّ إِنَّ قَوۡمِي كَذَّبُونِ

Akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika watu wangu wamenikadhibisha.

Akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika watu wangu wamenikadhibisha.

فَٱفۡتَحۡ بَيۡنِي وَبَيۡنَهُمۡ فَتۡحٗا وَنَجِّنِي وَمَن مَّعِيَ مِنَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Basi hukumu baina yangu na wao kwa hukumu yako, na uniokoe mimi na walio pamoja nami miongoni mwa Waumini.

Basi hukumu baina yangu na wao kwa hukumu yako, na uniokoe mimi na walio pamoja nami miongoni mwa Waumini.

فَأَنجَيۡنَٰهُ وَمَن مَّعَهُۥ فِي ٱلۡفُلۡكِ ٱلۡمَشۡحُونِ

Kwa hivyo tukamwokoa yeye na waliokuwa pamoja naye katika marikebu iliyosheheni.

Kwa hivyo tukamwokoa yeye na waliokuwa pamoja naye katika marikebu iliyosheheni.

ثُمَّ أَغۡرَقۡنَا بَعۡدُ ٱلۡبَاقِينَ

Kisha tukawazamisha baadaye waliobakia.

Kisha tukawazamisha baadaye waliobakia.

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ

Hakika katika haya ipo Ishara, lakini si wengi wao waliokuwa Waumini.

Hakika katika haya ipo Ishara, lakini si wengi wao waliokuwa Waumini.

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.

Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.

كَذَّبَتۡ عَادٌ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Kina 'Aad waliwakanusha Mitume.

Kina 'Aad waliwakanusha Mitume.

إِذۡ قَالَ لَهُمۡ أَخُوهُمۡ هُودٌ أَلَا تَتَّقُونَ

Alipowaambia ndugu yao, Hud: Je, hamumchi Mungu?

Alipowaambia ndugu yao, Hud: Je, hamumchi Mungu?

إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٞ

Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.

Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.

فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini mimi.

Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini mimi.

وَمَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ مِنۡ أَجۡرٍۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Wala siwaulizi juu yake ujira wowote, kwani ujira wangu hauko isipokuwa kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Wala siwaulizi juu yake ujira wowote, kwani ujira wangu hauko isipokuwa kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

أَتَبۡنُونَ بِكُلِّ رِيعٍ ءَايَةٗ تَعۡبَثُونَ

Je, mnajenga juu ya kila mnyanyuko kumbusho la kufanyia upuuzi?

Je, mnajenga juu ya kila mnyanyuko kumbusho la kufanyia upuuzi?

وَتَتَّخِذُونَ مَصَانِعَ لَعَلَّكُمۡ تَخۡلُدُونَ

Na mnajenga majengo ya kifahari kama kwamba mtaishi milele!

Na mnajenga majengo ya kifahari kama kwamba mtaishi milele!

وَإِذَا بَطَشۡتُم بَطَشۡتُمۡ جَبَّارِينَ

Na mnapotumia nguvu, mnatumia nguvu kwa ujabari.

Na mnapotumia nguvu, mnatumia nguvu kwa ujabari.

فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini.

Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini.

وَٱتَّقُواْ ٱلَّذِيٓ أَمَدَّكُم بِمَا تَعۡلَمُونَ

Na mcheni aliyewapa haya mnayoyajua.

Na mcheni aliyewapa haya mnayoyajua.

أَمَدَّكُم بِأَنۡعَٰمٖ وَبَنِينَ

Aliwapa wanyama wa kufuga na wana.

Aliwapa wanyama wa kufuga na wana.

وَجَنَّٰتٖ وَعُيُونٍ

Na mabustani na chemchemi.

Na mabustani na chemchemi.

إِنِّيٓ أَخَافُ عَلَيۡكُمۡ عَذَابَ يَوۡمٍ عَظِيمٖ

Hakika mimi ninawahofia adhabu ya Siku Kubwa.

Hakika mimi ninawahofia adhabu ya Siku Kubwa.

قَالُواْ سَوَآءٌ عَلَيۡنَآ أَوَعَظۡتَ أَمۡ لَمۡ تَكُن مِّنَ ٱلۡوَٰعِظِينَ

Wakasema: Ni mamoja kwetu, ukitupa mawaidha au hukuwa miongoni mwa watoao mawaidha.

Wakasema: Ni mamoja kwetu, ukitupa mawaidha au hukuwa miongoni mwa watoao mawaidha.

إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا خُلُقُ ٱلۡأَوَّلِينَ

Haya si chochote isipokuwa ni mtindo wa watu wa tokea zamani.

Haya si chochote isipokuwa ni mtindo wa watu wa tokea zamani.

وَمَا نَحۡنُ بِمُعَذَّبِينَ

Wala sisi hatutaadhibiwa.

Wala sisi hatutaadhibiwa.

فَكَذَّبُوهُ فَأَهۡلَكۡنَٰهُمۡۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ

Wakamkadhibisha; nasi tukawaangamiza. Hakika bila ya shaka katika haya ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.

Wakamkadhibisha; nasi tukawaangamiza. Hakika bila ya shaka katika haya ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.

Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.

كَذَّبَتۡ ثَمُودُ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Kina Thamud waliwakadhibisha Mitume.

Kina Thamud waliwakadhibisha Mitume.

إِذۡ قَالَ لَهُمۡ أَخُوهُمۡ صَٰلِحٌ أَلَا تَتَّقُونَ

Alipowaambia ndugu yao Saleh: Je, hamumchi Mungu?

Alipowaambia ndugu yao Saleh: Je, hamumchi Mungu?

إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٞ

Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.

Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.

فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini.

Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini.

وَمَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ مِنۡ أَجۡرٍۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Wala siwaulizi ujira wowote juu yake. Ujira wangu hauko isipokuwa kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Wala siwaulizi ujira wowote juu yake. Ujira wangu hauko isipokuwa kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

أَتُتۡرَكُونَ فِي مَا هَٰهُنَآ ءَامِنِينَ

Je, mtaachwa salama salimini katika haya yaliyopo hapa?

Je, mtaachwa salama salimini katika haya yaliyopo hapa?

فِي جَنَّٰتٖ وَعُيُونٖ

Katika mabustani, na chemchemi?

Katika mabustani, na chemchemi?

وَزُرُوعٖ وَنَخۡلٖ طَلۡعُهَا هَضِيمٞ

Na konde na mitende yenye makole yaliyowiva.

Na konde na mitende yenye makole yaliyowiva.

وَتَنۡحِتُونَ مِنَ ٱلۡجِبَالِ بُيُوتٗا فَٰرِهِينَ

Na mnachonga milimani majumba kwa ustadi.

Na mnachonga milimani majumba kwa ustadi.

فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini mimi.

Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini mimi.

وَلَا تُطِيعُوٓاْ أَمۡرَ ٱلۡمُسۡرِفِينَ

Wala msitii amri za waliopitiliza mipaka.

Wala msitii amri za waliopitiliza mipaka.

ٱلَّذِينَ يُفۡسِدُونَ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَلَا يُصۡلِحُونَ

Ambao wanafanya uharibifu katika nchi, wala hawatengenezi.

Ambao wanafanya uharibifu katika nchi, wala hawatengenezi.

قَالُوٓاْ إِنَّمَآ أَنتَ مِنَ ٱلۡمُسَحَّرِينَ

Wakasema: Hakika wewe ni miongoni mwa waliorogwa.

Wakasema: Hakika wewe ni miongoni mwa waliorogwa.

مَآ أَنتَ إِلَّا بَشَرٞ مِّثۡلُنَا فَأۡتِ بِـَٔايَةٍ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّٰدِقِينَ

Wewe si chochote isipokuwa ni mtu kama sisi. Basi leta Ishara ikiwa wewe ni miongoni mwa wakweli.

Wewe si chochote isipokuwa ni mtu kama sisi. Basi leta Ishara ikiwa wewe ni miongoni mwa wakweli.

قَالَ هَٰذِهِۦ نَاقَةٞ لَّهَا شِرۡبٞ وَلَكُمۡ شِرۡبُ يَوۡمٖ مَّعۡلُومٖ

Akasema: Huyu ngamia jike; awe na zamu yake ya kunywa, na nyinyi muwe na zamu yenu ya kunywa katika siku maalumu.

Akasema: Huyu ngamia jike; awe na zamu yake ya kunywa, na nyinyi muwe na zamu yenu ya kunywa katika siku maalumu.

وَلَا تَمَسُّوهَا بِسُوٓءٖ فَيَأۡخُذَكُمۡ عَذَابُ يَوۡمٍ عَظِيمٖ

Wala msimguse kwa wovu, ikawashika adhabu ya Siku Kubwa.

Wala msimguse kwa wovu, ikawashika adhabu ya Siku Kubwa.

فَعَقَرُوهَا فَأَصۡبَحُواْ نَٰدِمِينَ

Lakini wakamuua, na wakawa wenye kujuta.

Lakini wakamuua, na wakawa wenye kujuta.

فَأَخَذَهُمُ ٱلۡعَذَابُۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ

Basi ikawapata adhabu. Hakika katika hayo ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.

Basi ikawapata adhabu. Hakika katika hayo ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.

Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.

كَذَّبَتۡ قَوۡمُ لُوطٍ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Watu wa Luti waliwakadhibisha Mitume.

Watu wa Luti waliwakadhibisha Mitume.

إِذۡ قَالَ لَهُمۡ أَخُوهُمۡ لُوطٌ أَلَا تَتَّقُونَ

Alipowaambia ndugu yao, Luti: Je, hamumchi Mungu?

Alipowaambia ndugu yao, Luti: Je, hamumchi Mungu?

إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٞ

Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.

Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.

فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

Basi mcheni Mwenyezi Mungu na nitiini mimi.

Basi mcheni Mwenyezi Mungu na nitiini mimi.

وَمَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ مِنۡ أَجۡرٍۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Wala mimi sikuwauliza ujira wowote juu yake; ujira wangu hauko isipokuwa kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Wala mimi sikuwauliza ujira wowote juu yake; ujira wangu hauko isipokuwa kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

أَتَأۡتُونَ ٱلذُّكۡرَانَ مِنَ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Je, katika viumbe vyote mnawaingilia wanaume?

Je, katika viumbe vyote mnawaingilia wanaume?

وَتَذَرُونَ مَا خَلَقَ لَكُمۡ رَبُّكُم مِّنۡ أَزۡوَٰجِكُمۚ بَلۡ أَنتُمۡ قَوۡمٌ عَادُونَ

Na mnaacha alichowaumbia Mola wenu Mlezi katika wake zenu? Ama kweli nyinyi ni watu mnaoruka mipaka!

Na mnaacha alichowaumbia Mola wenu Mlezi katika wake zenu? Ama kweli nyinyi ni watu mnaoruka mipaka!

قَالُواْ لَئِن لَّمۡ تَنتَهِ يَٰلُوطُ لَتَكُونَنَّ مِنَ ٱلۡمُخۡرَجِينَ

Wakasema: Ewe Luti! Usipoacha, hapana shaka utakuwa miongoni mwa wanaotolewa mji!

Wakasema: Ewe Luti! Usipoacha, hapana shaka utakuwa miongoni mwa wanaotolewa mji!

قَالَ إِنِّي لِعَمَلِكُم مِّنَ ٱلۡقَالِينَ

Akasema: Hakika mimi ni katika wanaokichukia hiki kitendo chenu.

Akasema: Hakika mimi ni katika wanaokichukia hiki kitendo chenu.

رَبِّ نَجِّنِي وَأَهۡلِي مِمَّا يَعۡمَلُونَ

Mola wangu Mlezi! Niokoe mimi na ahali zangu na haya wayatendayo.

Mola wangu Mlezi! Niokoe mimi na ahali zangu na haya wayatendayo.

فَنَجَّيۡنَٰهُ وَأَهۡلَهُۥٓ أَجۡمَعِينَ

Basi tukamwokoa yeye na ahali zake wote.

Basi tukamwokoa yeye na ahali zake wote.

إِلَّا عَجُوزٗا فِي ٱلۡغَٰبِرِينَ

Isipokuwa kikongwe katika waliokaa nyuma.

Isipokuwa kikongwe katika waliokaa nyuma.

ثُمَّ دَمَّرۡنَا ٱلۡأٓخَرِينَ

Kisha tukawaangamiza wale wengine.

Kisha tukawaangamiza wale wengine.

وَأَمۡطَرۡنَا عَلَيۡهِم مَّطَرٗاۖ فَسَآءَ مَطَرُ ٱلۡمُنذَرِينَ

Na tukawanyeshea mvua, basi ni ovu mno mvua ya waliyoonywa.

Na tukawanyeshea mvua, basi ni ovu mno mvua ya waliyoonywa.

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ

Hakika katika hayo ipo Ishara. Na hawakuwa wengi wao wenye kuamini.

Hakika katika hayo ipo Ishara. Na hawakuwa wengi wao wenye kuamini.

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.

Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.

كَذَّبَ أَصۡحَٰبُ لۡـَٔيۡكَةِ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Watu wa Machakani waliwakanusha Mitume.

Watu wa Machakani waliwakanusha Mitume.

إِذۡ قَالَ لَهُمۡ شُعَيۡبٌ أَلَا تَتَّقُونَ

Shuaibu alipowaambia: Je, hamumchi Mungu?

Shuaibu alipowaambia: Je, hamumchi Mungu?

إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٞ

Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.

Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.

فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini mimi.

Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini mimi.

وَمَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ مِنۡ أَجۡرٍۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Wala siwaulizi ujira wowote juu yake. Ujira wangu hauko isipokuwa kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Wala siwaulizi ujira wowote juu yake. Ujira wangu hauko isipokuwa kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

۞ أَوۡفُواْ ٱلۡكَيۡلَ وَلَا تَكُونُواْ مِنَ ٱلۡمُخۡسِرِينَ

Timizeni kipimo sawasawa, wala msiwe katika wanaopunja.

Timizeni kipimo sawasawa, wala msiwe katika wanaopunja.

وَزِنُواْ بِٱلۡقِسۡطَاسِ ٱلۡمُسۡتَقِيمِ

Na pimeni kwa haki iliyonyooka.

Na pimeni kwa haki iliyonyooka.

وَلَا تَبۡخَسُواْ ٱلنَّاسَ أَشۡيَآءَهُمۡ وَلَا تَعۡثَوۡاْ فِي ٱلۡأَرۡضِ مُفۡسِدِينَ

Wala msiwapunje watu vitu vyao, wala msifanye jeuri katika ardhi kwa kufanya uharibifu.

Wala msiwapunje watu vitu vyao, wala msifanye jeuri katika ardhi kwa kufanya uharibifu.

وَٱتَّقُواْ ٱلَّذِي خَلَقَكُمۡ وَٱلۡجِبِلَّةَ ٱلۡأَوَّلِينَ

Na mcheni aliyewaumba nyinyi na vizazi vilivyotangulia.

Na mcheni aliyewaumba nyinyi na vizazi vilivyotangulia.

قَالُوٓاْ إِنَّمَآ أَنتَ مِنَ ٱلۡمُسَحَّرِينَ

Wakasema: Hakika wewe ni katika waliorogwa.

Wakasema: Hakika wewe ni katika waliorogwa.

وَمَآ أَنتَ إِلَّا بَشَرٞ مِّثۡلُنَا وَإِن نَّظُنُّكَ لَمِنَ ٱلۡكَٰذِبِينَ

Na wewe si chochote isipokuwa ni mtu tu kama sisi, na kwa yakini tunakuona wewe ni katika waongo.

Na wewe si chochote isipokuwa ni mtu tu kama sisi, na kwa yakini tunakuona wewe ni katika waongo.

فَأَسۡقِطۡ عَلَيۡنَا كِسَفٗا مِّنَ ٱلسَّمَآءِ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّٰدِقِينَ

Hebu tuangushie vipande kutoka mbinguni ikiwa wewe ni miongoni mwa wakweli.

Hebu tuangushie vipande kutoka mbinguni ikiwa wewe ni miongoni mwa wakweli.

قَالَ رَبِّيٓ أَعۡلَمُ بِمَا تَعۡمَلُونَ

Akasema: Mola wangu Mlezi anajua zaidi mnayoyatenda.

Akasema: Mola wangu Mlezi anajua zaidi mnayoyatenda.

فَكَذَّبُوهُ فَأَخَذَهُمۡ عَذَابُ يَوۡمِ ٱلظُّلَّةِۚ إِنَّهُۥ كَانَ عَذَابَ يَوۡمٍ عَظِيمٍ

Basi walimkanusha, na ikawashika adhabu ya Siku ya kivuli. Hakika hiyo ilikuwa adhabu ya Siku kubwa.

Basi walimkanusha, na ikawashika adhabu ya Siku ya kivuli. Hakika hiyo ilikuwa adhabu ya Siku kubwa.

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ

Hakika katika hayo ipo Ishara, lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.

Hakika katika hayo ipo Ishara, lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Yeye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.

Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Yeye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.

وَإِنَّهُۥ لَتَنزِيلُ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Na bila ya shaka hii ni Uteremsho wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Na bila ya shaka hii ni Uteremsho wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

نَزَلَ بِهِ ٱلرُّوحُ ٱلۡأَمِينُ

Ameuteremsha Roho muaminifu.

Ameuteremsha Roho muaminifu.

عَلَىٰ قَلۡبِكَ لِتَكُونَ مِنَ ٱلۡمُنذِرِينَ

Juu ya moyo wako, ili uwe katika Waonyaji.

Juu ya moyo wako, ili uwe katika Waonyaji.

بِلِسَانٍ عَرَبِيّٖ مُّبِينٖ

Kwa ulimi wa Kiarabu ulio wazi.

Kwa ulimi wa Kiarabu ulio wazi.

وَإِنَّهُۥ لَفِي زُبُرِ ٱلۡأَوَّلِينَ

Na hakika bila ya shaka haya yamo katika Vitabu vya kale.

Na hakika bila ya shaka haya yamo katika Vitabu vya kale.

أَوَلَمۡ يَكُن لَّهُمۡ ءَايَةً أَن يَعۡلَمَهُۥ عُلَمَٰٓؤُاْ بَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ

Je, haikuwa kwao ni Ishara kwamba wanayajua haya wanachuoni wa Wana wa Israili?

Je, haikuwa kwao ni Ishara kwamba wanayajua haya wanachuoni wa Wana wa Israili?

وَلَوۡ نَزَّلۡنَٰهُ عَلَىٰ بَعۡضِ ٱلۡأَعۡجَمِينَ

Na lau kuwa tungeliiteremsha juu ya mmoja wa wasiokuwa Waarabu.

Na lau kuwa tungeliiteremsha juu ya mmoja wa wasiokuwa Waarabu.

فَقَرَأَهُۥ عَلَيۡهِم مَّا كَانُواْ بِهِۦ مُؤۡمِنِينَ

Na akawasomea, wasingelikuwa wenye kuamini.

Na akawasomea, wasingelikuwa wenye kuamini.

كَذَٰلِكَ سَلَكۡنَٰهُ فِي قُلُوبِ ٱلۡمُجۡرِمِينَ

Namna hivi tunaingiza katika nyoyo za wahalifu.

Namna hivi tunaingiza katika nyoyo za wahalifu.

لَا يُؤۡمِنُونَ بِهِۦ حَتَّىٰ يَرَوُاْ ٱلۡعَذَابَ ٱلۡأَلِيمَ

Hawataiamini mpaka waione adhabu chungu.

Hawataiamini mpaka waione adhabu chungu.

فَيَأۡتِيَهُم بَغۡتَةٗ وَهُمۡ لَا يَشۡعُرُونَ

Basi itawafikia kwa ghafla, na hali hawana habari.

Basi itawafikia kwa ghafla, na hali hawana habari.

فَيَقُولُواْ هَلۡ نَحۡنُ مُنظَرُونَ

Na watasema: "Je, tutapewa muhula?"

Na watasema: "Je, tutapewa muhula?"

أَفَبِعَذَابِنَا يَسۡتَعۡجِلُونَ

Basi je, wanaihimiza adhabu yetu?

Basi je, wanaihimiza adhabu yetu?

أَفَرَءَيۡتَ إِن مَّتَّعۡنَٰهُمۡ سِنِينَ

Waonaje kama tukiwastarehesha kwa miaka.

Waonaje kama tukiwastarehesha kwa miaka.

ثُمَّ جَآءَهُم مَّا كَانُواْ يُوعَدُونَ

Kisha yakawafikia waliyokuwa wakiahidiwa.

Kisha yakawafikia waliyokuwa wakiahidiwa.

مَآ أَغۡنَىٰ عَنۡهُم مَّا كَانُواْ يُمَتَّعُونَ

Yatawafaa nini yale waliyostareheshewa?

Yatawafaa nini yale waliyostareheshewa?

وَمَآ أَهۡلَكۡنَا مِن قَرۡيَةٍ إِلَّا لَهَا مُنذِرُونَ

Wala hatukuangamiza mji wowote isipokuwa ulikuwa na waonyaji.

Wala hatukuangamiza mji wowote isipokuwa ulikuwa na waonyaji.

ذِكۡرَىٰ وَمَا كُنَّا ظَٰلِمِينَ

Kuwa ni ukumbusho. Wala Sisi hatukuwa wenye kudhulumu.

Kuwa ni ukumbusho. Wala Sisi hatukuwa wenye kudhulumu.

وَمَا تَنَزَّلَتۡ بِهِ ٱلشَّيَٰطِينُ

Wala Mashetani hawakuteremka nayo.

Wala Mashetani hawakuteremka nayo.

وَمَا يَنۢبَغِي لَهُمۡ وَمَا يَسۡتَطِيعُونَ

Wala haitakiwi kwao, na wala hawawezi.

Wala haitakiwi kwao, na wala hawawezi.

إِنَّهُمۡ عَنِ ٱلسَّمۡعِ لَمَعۡزُولُونَ

Hakika hao wametengwa na kusikia.

Hakika hao wametengwa na kusikia.

فَلَا تَدۡعُ مَعَ ٱللَّهِ إِلَٰهًا ءَاخَرَ فَتَكُونَ مِنَ ٱلۡمُعَذَّبِينَ

Basi usimwombe mungu mwingine pamoja na Mwenyezi Mungu ukawa miongoni mwa watakaoadhibiwa.

Basi usimwombe mungu mwingine pamoja na Mwenyezi Mungu ukawa miongoni mwa watakaoadhibiwa.

وَأَنذِرۡ عَشِيرَتَكَ ٱلۡأَقۡرَبِينَ

Na uwaonye jamaa zako walio karibu nawe.

Na uwaonye jamaa zako walio karibu nawe.

وَٱخۡفِضۡ جَنَاحَكَ لِمَنِ ٱتَّبَعَكَ مِنَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Na watwae kwa upole wanaokufuata miongoni mwa Waumini.

Na watwae kwa upole wanaokufuata miongoni mwa Waumini.

فَإِنۡ عَصَوۡكَ فَقُلۡ إِنِّي بَرِيٓءٞ مِّمَّا تَعۡمَلُونَ

Na ikiwa watakuasi, basi sema: Mimi ninajitenga mbali na hayo mnayoyatenda.

Na ikiwa watakuasi, basi sema: Mimi ninajitenga mbali na hayo mnayoyatenda.

وَتَوَكَّلۡ عَلَى ٱلۡعَزِيزِ ٱلرَّحِيمِ

Na umtegemee Mtukufu Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.

Na umtegemee Mtukufu Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.

ٱلَّذِي يَرَىٰكَ حِينَ تَقُومُ

Ambaye anakuona unaposimama.

Ambaye anakuona unaposimama.

وَتَقَلُّبَكَ فِي ٱلسَّٰجِدِينَ

Na mageuko yako katika wanaosujudu.

Na mageuko yako katika wanaosujudu.

إِنَّهُۥ هُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡعَلِيمُ

Hakika Yeye ndiye Mwenye kusikia, Mwenye kujua zaidi.

Hakika Yeye ndiye Mwenye kusikia, Mwenye kujua zaidi.

هَلۡ أُنَبِّئُكُمۡ عَلَىٰ مَن تَنَزَّلُ ٱلشَّيَٰطِينُ

Je, niwaambieni nani wanawashukia Mashetani?

Je, niwaambieni nani wanawashukia Mashetani?

تَنَزَّلُ عَلَىٰ كُلِّ أَفَّاكٍ أَثِيمٖ

Wanamshukia kila mzushi mkubwa mwingi wa dhambi.

Wanamshukia kila mzushi mkubwa mwingi wa dhambi.

يُلۡقُونَ ٱلسَّمۡعَ وَأَكۡثَرُهُمۡ كَٰذِبُونَ

Wanawapelekea yale wanayoyasikia; na wengi wao ni waongo.

Wanawapelekea yale wanayoyasikia; na wengi wao ni waongo.

وَٱلشُّعَرَآءُ يَتَّبِعُهُمُ ٱلۡغَاوُۥنَ

Na watungaji mashairi ni wapotovu ndio wanawafuata.

Na watungaji mashairi ni wapotovu ndio wanawafuata.

أَلَمۡ تَرَ أَنَّهُمۡ فِي كُلِّ وَادٖ يَهِيمُونَ

Je, huwaoni kwamba wao wanatangatanga katika kila bonde?

Je, huwaoni kwamba wao wanatangatanga katika kila bonde?

وَأَنَّهُمۡ يَقُولُونَ مَا لَا يَفۡعَلُونَ

Na kwamba wao husema wasiyoyatenda?

Na kwamba wao husema wasiyoyatenda?

إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ وَذَكَرُواْ ٱللَّهَ كَثِيرٗا وَٱنتَصَرُواْ مِنۢ بَعۡدِ مَا ظُلِمُواْۗ وَسَيَعۡلَمُ ٱلَّذِينَ ظَلَمُوٓاْ أَيَّ مُنقَلَبٖ يَنقَلِبُونَ

Isipokuwa wale walioamini, na wakatenda mema, na wakamkumbuka Mwenyezi Mungu kwa wingi, na wakajitetea wanapodhulumiwa. Na wanaodhulumu watakuja jua mgeuko gani watakaogeuka.

Isipokuwa wale walioamini, na wakatenda mema, na wakamkumbuka Mwenyezi Mungu kwa wingi, na wakajitetea wanapodhulumiwa. Na wanaodhulumu watakuja jua mgeuko gani watakaogeuka.
Footer Include