Header Include

Swahili translation - Rowad Translation Center

translated by Rowwad Translation Center, in cooperation with the Islamic Propagation Office in Rabwah and the Association for Serving Islamic Content in Languages.

QR Code https://quran.islamcontent.com/so/swahili_rwwad

يَٰٓأَيُّهَا ٱلۡمُدَّثِّرُ

Ewe uliyejigubika!

Ewe uliyejigubika!

قُمۡ فَأَنذِرۡ

Simama uonye!

Simama uonye!

وَرَبَّكَ فَكَبِّرۡ

Na Mola wako Mlezi mtukuze!

Na Mola wako Mlezi mtukuze!

وَثِيَابَكَ فَطَهِّرۡ

Na nguo zako, zisafishe.

Na nguo zako, zisafishe.

وَٱلرُّجۡزَ فَٱهۡجُرۡ

Na yaliyo machafu yahame!

Na yaliyo machafu yahame!

وَلَا تَمۡنُن تَسۡتَكۡثِرُ

Wala usitoe kwa kutaraji kuzidishiwa.

Wala usitoe kwa kutaraji kuzidishiwa.

وَلِرَبِّكَ فَٱصۡبِرۡ

Na kwa ajili ya Mola wako Mlezi, subiri!

Na kwa ajili ya Mola wako Mlezi, subiri!

فَإِذَا نُقِرَ فِي ٱلنَّاقُورِ

Basi litakapopulizwa baragumu.

Basi litakapopulizwa baragumu.

فَذَٰلِكَ يَوۡمَئِذٖ يَوۡمٌ عَسِيرٌ

Siku hiyo, basi, itakuwa siku ngumu.

Siku hiyo, basi, itakuwa siku ngumu.

عَلَى ٱلۡكَٰفِرِينَ غَيۡرُ يَسِيرٖ

Kwa makafiri haitakuwa nyepesi.

Kwa makafiri haitakuwa nyepesi.

ذَرۡنِي وَمَنۡ خَلَقۡتُ وَحِيدٗا

Niache peke yangu na niliyemuumba.

Niache peke yangu na niliyemuumba.

وَجَعَلۡتُ لَهُۥ مَالٗا مَّمۡدُودٗا

Na nikamjaalia awe na mali mengi.

Na nikamjaalia awe na mali mengi.

وَبَنِينَ شُهُودٗا

Na wana wanaoonekana.

Na wana wanaoonekana.

وَمَهَّدتُّ لَهُۥ تَمۡهِيدٗا

Na nikamtegenezea mambo vizuri kabisa.

Na nikamtegenezea mambo vizuri kabisa.

ثُمَّ يَطۡمَعُ أَنۡ أَزِيدَ

Kisha anatumai nimzidishie!

Kisha anatumai nimzidishie!

كَلَّآۖ إِنَّهُۥ كَانَ لِأٓيَٰتِنَا عَنِيدٗا

Hasha! Kwani hakika yeye alikuwa akizifanyia ukaidi Aya zetu!

Hasha! Kwani hakika yeye alikuwa akizifanyia ukaidi Aya zetu!

سَأُرۡهِقُهُۥ صَعُودًا

Nitamtesa kwa mateso yasiowezekana.

Nitamtesa kwa mateso yasiowezekana.

إِنَّهُۥ فَكَّرَ وَقَدَّرَ

Kwani hakika yeye alifikiri na akapima.

Kwani hakika yeye alifikiri na akapima.

فَقُتِلَ كَيۡفَ قَدَّرَ

Basi ameangamia! Vipi alivyopima!

Basi ameangamia! Vipi alivyopima!

ثُمَّ قُتِلَ كَيۡفَ قَدَّرَ

Tena ameangamia! Vipi alivyopima!

Tena ameangamia! Vipi alivyopima!

ثُمَّ نَظَرَ

Kisha akatazama.

Kisha akatazama.

ثُمَّ عَبَسَ وَبَسَرَ

Kisha akakunja kipaji, na akanuna.

Kisha akakunja kipaji, na akanuna.

ثُمَّ أَدۡبَرَ وَٱسۡتَكۡبَرَ

Kisha akaipa kisogo haki, na akatakabari.

Kisha akaipa kisogo haki, na akatakabari.

فَقَالَ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا سِحۡرٞ يُؤۡثَرُ

Na akasema: Haya si chochote ila ni uchawi ulionukuliwa.

Na akasema: Haya si chochote ila ni uchawi ulionukuliwa.

إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا قَوۡلُ ٱلۡبَشَرِ

Haya si chochote ila kauli ya binadamu.

Haya si chochote ila kauli ya binadamu.

سَأُصۡلِيهِ سَقَرَ

Nitakuja mtia kwenye Moto wa Saqar.

Nitakuja mtia kwenye Moto wa Saqar.

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا سَقَرُ

Na nini kitakujuulisha ni nini huo Moto wa Saqar?

Na nini kitakujuulisha ni nini huo Moto wa Saqar?

لَا تُبۡقِي وَلَا تَذَرُ

Haubakishi wala hausazi.

Haubakishi wala hausazi.

لَوَّاحَةٞ لِّلۡبَشَرِ

Unababua ngozi iwe nyeusi.

Unababua ngozi iwe nyeusi.

عَلَيۡهَا تِسۡعَةَ عَشَرَ

Juu yake wapo kumi na tisa.

Juu yake wapo kumi na tisa.

وَمَا جَعَلۡنَآ أَصۡحَٰبَ ٱلنَّارِ إِلَّا مَلَٰٓئِكَةٗۖ وَمَا جَعَلۡنَا عِدَّتَهُمۡ إِلَّا فِتۡنَةٗ لِّلَّذِينَ كَفَرُواْ لِيَسۡتَيۡقِنَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ وَيَزۡدَادَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِيمَٰنٗا وَلَا يَرۡتَابَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡمُؤۡمِنُونَ وَلِيَقُولَ ٱلَّذِينَ فِي قُلُوبِهِم مَّرَضٞ وَٱلۡكَٰفِرُونَ مَاذَآ أَرَادَ ٱللَّهُ بِهَٰذَا مَثَلٗاۚ كَذَٰلِكَ يُضِلُّ ٱللَّهُ مَن يَشَآءُ وَيَهۡدِي مَن يَشَآءُۚ وَمَا يَعۡلَمُ جُنُودَ رَبِّكَ إِلَّا هُوَۚ وَمَا هِيَ إِلَّا ذِكۡرَىٰ لِلۡبَشَرِ

Na hatukuwafanya walinzi wa Motoni ila ni Malaika, wala hatukuifanya idadi yao hiyo ila kuwatatanisha waliokufuru, wapate kuwa na yakini waliopewa Kitabu, na wazidi Imani wale walioamini, wala wasiwe na shaka waliopewa Kitabu na Waumini, na wapate kusema wenye maradhi katika nyoyo zao na makafiri: "Mwenyezi Mungu amekusudia nini kwa mfano huu?" Ndiyo kama hivyo Mwenyezi Mungu humwacha apotee amtakaye, na humwongoa amtakaye. Na hapana yeyote anayejua majeshi ya Mola wako Mlezi ila Yeye tu. Na haya si chochote ila ni ukumbusho kwa binadamu.

Na hatukuwafanya walinzi wa Motoni ila ni Malaika, wala hatukuifanya idadi yao hiyo ila kuwatatanisha waliokufuru, wapate kuwa na yakini waliopewa Kitabu, na wazidi Imani wale walioamini, wala wasiwe na shaka waliopewa Kitabu na Waumini, na wapate kusema wenye maradhi katika nyoyo zao na makafiri: "Mwenyezi Mungu amekusudia nini kwa mfano huu?" Ndiyo kama hivyo Mwenyezi Mungu humwacha apotee amtakaye, na humwongoa amtakaye. Na hapana yeyote anayejua majeshi ya Mola wako Mlezi ila Yeye tu. Na haya si chochote ila ni ukumbusho kwa binadamu.

كَلَّا وَٱلۡقَمَرِ

Hasha! Naapa kwa mwezi!

Hasha! Naapa kwa mwezi!

وَٱلَّيۡلِ إِذۡ أَدۡبَرَ

Na kwa usiku unapokucha!

Na kwa usiku unapokucha!

وَٱلصُّبۡحِ إِذَآ أَسۡفَرَ

Na kwa asubuhi inapopambazuka!

Na kwa asubuhi inapopambazuka!

إِنَّهَا لَإِحۡدَى ٱلۡكُبَرِ

Hakika huo Moto ni katika mambo yaliyo makubwa kabisa!

Hakika huo Moto ni katika mambo yaliyo makubwa kabisa!

نَذِيرٗا لِّلۡبَشَرِ

Ni onyo kwa binaadamu.

Ni onyo kwa binaadamu.

لِمَن شَآءَ مِنكُمۡ أَن يَتَقَدَّمَ أَوۡ يَتَأَخَّرَ

Kwa anayetaka miongoni mwenu kutangulia au kuchelewa.

Kwa anayetaka miongoni mwenu kutangulia au kuchelewa.

كُلُّ نَفۡسِۭ بِمَا كَسَبَتۡ رَهِينَةٌ

Kila nafsi imo rahanini kwa mabaya iliyoyachuma.

Kila nafsi imo rahanini kwa mabaya iliyoyachuma.

إِلَّآ أَصۡحَٰبَ ٱلۡيَمِينِ

Isipokuwa watu wa kuliani.

Isipokuwa watu wa kuliani.

فِي جَنَّٰتٖ يَتَسَآءَلُونَ

Hao watakuwa katika Mabustani, wawe wanaulizana

Hao watakuwa katika Mabustani, wawe wanaulizana

عَنِ ٱلۡمُجۡرِمِينَ

Habari za wakosefu:

Habari za wakosefu:

مَا سَلَكَكُمۡ فِي سَقَرَ

Ni nini kilichokupelekeni Motoni?

Ni nini kilichokupelekeni Motoni?

قَالُواْ لَمۡ نَكُ مِنَ ٱلۡمُصَلِّينَ

Waseme: Hatukuwa miongoni mwa waliokuwa wakisali.

Waseme: Hatukuwa miongoni mwa waliokuwa wakisali.

وَلَمۡ نَكُ نُطۡعِمُ ٱلۡمِسۡكِينَ

Wala hatukuwa tukiwalisha masikini.

Wala hatukuwa tukiwalisha masikini.

وَكُنَّا نَخُوضُ مَعَ ٱلۡخَآئِضِينَ

Na tulikuwa tukizama pamoja na waliozama katika maovu.

Na tulikuwa tukizama pamoja na waliozama katika maovu.

وَكُنَّا نُكَذِّبُ بِيَوۡمِ ٱلدِّينِ

Na tulikuwa tukiikanusha Siku ya Malipo.

Na tulikuwa tukiikanusha Siku ya Malipo.

حَتَّىٰٓ أَتَىٰنَا ٱلۡيَقِينُ

Mpaka yakini (yaani mauti) ilipotufikia.

Mpaka yakini (yaani mauti) ilipotufikia.

فَمَا تَنفَعُهُمۡ شَفَٰعَةُ ٱلشَّٰفِعِينَ

Basi hautawafaa kitu uombezi wa waombezi.

Basi hautawafaa kitu uombezi wa waombezi.

فَمَا لَهُمۡ عَنِ ٱلتَّذۡكِرَةِ مُعۡرِضِينَ

Basi wana nini hata wanapuuza onyo hili?

Basi wana nini hata wanapuuza onyo hili?

كَأَنَّهُمۡ حُمُرٞ مُّسۡتَنفِرَةٞ

Kana kwamba wao ni mapunda waliotimuliwa.

Kana kwamba wao ni mapunda waliotimuliwa.

فَرَّتۡ مِن قَسۡوَرَةِۭ

Wanaomkimbia simba!

Wanaomkimbia simba!

بَلۡ يُرِيدُ كُلُّ ٱمۡرِيٕٖ مِّنۡهُمۡ أَن يُؤۡتَىٰ صُحُفٗا مُّنَشَّرَةٗ

Ati kila mmoja katika wao anataka apewe nyaraka zilizofunuliwa.

Ati kila mmoja katika wao anataka apewe nyaraka zilizofunuliwa.

كَلَّاۖ بَل لَّا يَخَافُونَ ٱلۡأٓخِرَةَ

Hasha! Kwani wao hawaiogopi Akhera?

Hasha! Kwani wao hawaiogopi Akhera?

كَلَّآ إِنَّهُۥ تَذۡكِرَةٞ

Hasha! Kwa hakika huu ni ukumbusho!

Hasha! Kwa hakika huu ni ukumbusho!

فَمَن شَآءَ ذَكَرَهُۥ

Basi anayetaka atakumbuka.

Basi anayetaka atakumbuka.

وَمَا يَذۡكُرُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُۚ هُوَ أَهۡلُ ٱلتَّقۡوَىٰ وَأَهۡلُ ٱلۡمَغۡفِرَةِ

Na hawatakumbuka isipokuwa Mwenyezi Mungu atake. Ucha Mungu ni kwake Yeye, na msamaha ni wake Yeye.

Na hawatakumbuka isipokuwa Mwenyezi Mungu atake. Ucha Mungu ni kwake Yeye, na msamaha ni wake Yeye.
Footer Include