Salin sa Wikang Swahili ng Sentro ng Rowad sa Pagsasalin

Pagsasalin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an

Isinalin ito ng isang pangkat ng Sentro ng Rowad sa Pagsasalin sa pakikipagtulungan ng Samahan ng Da‘wah sa Rabwah at Samahan ng Paglilingkod sa Nilalamang Islāmiko sa mga Wika.

QR Code https://quran.islamcontent.com/tl/swahili_rwwad

سَبِّحِ ٱسۡمَ رَبِّكَ ٱلۡأَعۡلَى

Litakase jina la Mola wako Mlezi aliye juu kabisa.

Litakase jina la Mola wako Mlezi aliye juu kabisa.

ٱلَّذِي خَلَقَ فَسَوَّىٰ

Aliyeumba, na akaweka sawa.

Aliyeumba, na akaweka sawa.

وَٱلَّذِي قَدَّرَ فَهَدَىٰ

Na ambaye amekadiria na akaongoa.

Na ambaye amekadiria na akaongoa.

وَٱلَّذِيٓ أَخۡرَجَ ٱلۡمَرۡعَىٰ

Na aliyeotesha malisho.

Na aliyeotesha malisho.

فَجَعَلَهُۥ غُثَآءً أَحۡوَىٰ

Kisha akayafanya makavu, meusi.

Kisha akayafanya makavu, meusi.

سَنُقۡرِئُكَ فَلَا تَنسَىٰٓ

Tutakusomesha wala hutasahau.

Tutakusomesha wala hutasahau.

إِلَّا مَا شَآءَ ٱللَّهُۚ إِنَّهُۥ يَعۡلَمُ ٱلۡجَهۡرَ وَمَا يَخۡفَىٰ

Ila akipenda Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye anayajua yaliyo dhahiri na yaliyofichikana.

Ila akipenda Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye anayajua yaliyo dhahiri na yaliyofichikana.

وَنُيَسِّرُكَ لِلۡيُسۡرَىٰ

Na tutakusahilishia yawe mepesi.

Na tutakusahilishia yawe mepesi.

فَذَكِّرۡ إِن نَّفَعَتِ ٱلذِّكۡرَىٰ

Basi kumbusha, kama makumbusho yanafaa.

Basi kumbusha, kama makumbusho yanafaa.

سَيَذَّكَّرُ مَن يَخۡشَىٰ

Atakumbuka mwenye kuogopa.

Atakumbuka mwenye kuogopa.

وَيَتَجَنَّبُهَا ٱلۡأَشۡقَى

Na atajitenga mbali nayo mpotovu.

Na atajitenga mbali nayo mpotovu.

ٱلَّذِي يَصۡلَى ٱلنَّارَ ٱلۡكُبۡرَىٰ

Ambaye atauingia Moto mkubwa.

Ambaye atauingia Moto mkubwa.

ثُمَّ لَا يَمُوتُ فِيهَا وَلَا يَحۡيَىٰ

Tena humo hatakufa wala hawi hai.

Tena humo hatakufa wala hawi hai.

قَدۡ أَفۡلَحَ مَن تَزَكَّىٰ

Hakika amekwisha fanikiwa aliyejitakasa.

Hakika amekwisha fanikiwa aliyejitakasa.

وَذَكَرَ ٱسۡمَ رَبِّهِۦ فَصَلَّىٰ

Na akakumbuka jina la Mola wake Mlezi, na akasali.

Na akakumbuka jina la Mola wake Mlezi, na akasali.

بَلۡ تُؤۡثِرُونَ ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا

Lakini nyinyi mnapendelea maisha ya dunia!

Lakini nyinyi mnapendelea maisha ya dunia!

وَٱلۡأٓخِرَةُ خَيۡرٞ وَأَبۡقَىٰٓ

Na Akhera ni bora na yenye kudumu zaidi.

Na Akhera ni bora na yenye kudumu zaidi.

إِنَّ هَٰذَا لَفِي ٱلصُّحُفِ ٱلۡأُولَىٰ

Hakika haya yamo katika Vitabu vya mwanzo.

Hakika haya yamo katika Vitabu vya mwanzo.

صُحُفِ إِبۡرَٰهِيمَ وَمُوسَىٰ

Vitabu vya Ibrahimu na Musa.

Vitabu vya Ibrahimu na Musa.