Salin sa Wikang Swahili ng Sentro ng Rowad sa Pagsasalin

Pagsasalin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an

Isinalin ito ng isang pangkat ng Sentro ng Rowad sa Pagsasalin sa pakikipagtulungan ng Samahan ng Da‘wah sa Rabwah at Samahan ng Paglilingkod sa Nilalamang Islāmiko sa mga Wika.

QR Code https://quran.islamcontent.com/tl/swahili_rwwad

وَٱلشَّمۡسِ وَضُحَىٰهَا

Ninaapa kwa jua na mwangaza wake!

Ninaapa kwa jua na mwangaza wake!

وَٱلۡقَمَرِ إِذَا تَلَىٰهَا

Na kwa mwezi unapolifuatia!

Na kwa mwezi unapolifuatia!

وَٱلنَّهَارِ إِذَا جَلَّىٰهَا

Na kwa mchana unapolidhihirisha!

Na kwa mchana unapolidhihirisha!

وَٱلَّيۡلِ إِذَا يَغۡشَىٰهَا

Na kwa usiku unapolifunika!

Na kwa usiku unapolifunika!

وَٱلسَّمَآءِ وَمَا بَنَىٰهَا

Na kwa mbingu na kwa aliyeijenga!

Na kwa mbingu na kwa aliyeijenga!

وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا طَحَىٰهَا

Na kwa ardhi na kwa aliyeitandaza!

Na kwa ardhi na kwa aliyeitandaza!

وَنَفۡسٖ وَمَا سَوَّىٰهَا

Na kwa nafsi na kwa aliyeitengeneza!

Na kwa nafsi na kwa aliyeitengeneza!

فَأَلۡهَمَهَا فُجُورَهَا وَتَقۡوَىٰهَا

Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake.

Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake.

قَدۡ أَفۡلَحَ مَن زَكَّىٰهَا

Hakika amefanikiwa aliyeitakasa.

Hakika amefanikiwa aliyeitakasa.

وَقَدۡ خَابَ مَن دَسَّىٰهَا

Na hakika amehasiri aliyeiviza.

Na hakika amehasiri aliyeiviza.

كَذَّبَتۡ ثَمُودُ بِطَغۡوَىٰهَآ

Kina Thamudi walikadhibisha kwa sababu ya upotovu wao.

Kina Thamudi walikadhibisha kwa sababu ya upotovu wao.

إِذِ ٱنۢبَعَثَ أَشۡقَىٰهَا

Aliposimama mwovu wao mkubwa.

Aliposimama mwovu wao mkubwa.

فَقَالَ لَهُمۡ رَسُولُ ٱللَّهِ نَاقَةَ ٱللَّهِ وَسُقۡيَٰهَا

Hapo Mtume wa Mwenyezi Mungu alipowaambia: Huyu ni ngamia wa Mwenyezi Mungu, mwacheni anywe maji fungu lake.

Hapo Mtume wa Mwenyezi Mungu alipowaambia: Huyu ni ngamia wa Mwenyezi Mungu, mwacheni anywe maji fungu lake.

فَكَذَّبُوهُ فَعَقَرُوهَا فَدَمۡدَمَ عَلَيۡهِمۡ رَبُّهُم بِذَنۢبِهِمۡ فَسَوَّىٰهَا

Lakini walimkadhibisha na wakamchinja ngamia, kwa hivyo Mola wao Mlezi aliwaangamiza kwa sababu ya dhambi zao na akawafuta kabisa.

Lakini walimkadhibisha na wakamchinja ngamia, kwa hivyo Mola wao Mlezi aliwaangamiza kwa sababu ya dhambi zao na akawafuta kabisa.

وَلَا يَخَافُ عُقۡبَٰهَا

Wala Yeye haogopi matokeo yake.

Wala Yeye haogopi matokeo yake.