Traducción al suajili - El Centro de Rowad Al- Taryamah
Traducción de los significados del Sagrado Corán
Traducida por el equipo del Centro Rowad At-Taryamah en cooperación con la Asociación de Dawah en Rabwa y la Asociación para el Servicio del Contenido Islámico en Idiomas.
هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلۡغَٰشِيَةِ
Je, imekufikia habari ya Msiba wa kufudikiza?
وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٍ خَٰشِعَةٌ
Siku hiyo nyuso zitainama.
عَامِلَةٞ نَّاصِبَةٞ
Zikifanya kazi, nazo taabani.
تَصۡلَىٰ نَارًا حَامِيَةٗ
Ziingie katika Moto unaowaka.
تُسۡقَىٰ مِنۡ عَيۡنٍ ءَانِيَةٖ
Zikinyweshwa kutoka chemchemi inayochemka.
لَّيۡسَ لَهُمۡ طَعَامٌ إِلَّا مِن ضَرِيعٖ
Hawatakuwa na chakula isipokuwa kichungu chenye miba.
لَّا يُسۡمِنُ وَلَا يُغۡنِي مِن جُوعٖ
Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa.
وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ نَّاعِمَةٞ
Siku hiyo nyuso nyengine zitakuwa kunjufu.
لِّسَعۡيِهَا رَاضِيَةٞ
Zitakuwa radhi kwa juhudi yao.
فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٖ
Katika Bustani ya juu.
لَّا تَسۡمَعُ فِيهَا لَٰغِيَةٗ
Hawatasikia humo upuuzi.
فِيهَا عَيۡنٞ جَارِيَةٞ
Humo imo chemchemi inayomiminika.
فِيهَا سُرُرٞ مَّرۡفُوعَةٞ
Humo vimo viti vilivyonyanyuliwa.
وَأَكۡوَابٞ مَّوۡضُوعَةٞ
Na bilauri zilizopangwa.
وَنَمَارِقُ مَصۡفُوفَةٞ
Na matakia safu safu.
وَزَرَابِيُّ مَبۡثُوثَةٌ
Na mazulia yaliyotandikwa.
أَفَلَا يَنظُرُونَ إِلَى ٱلۡإِبِلِ كَيۡفَ خُلِقَتۡ
Je! Hawamtazami ngamia jinsi alivyoumbwa?
وَإِلَى ٱلسَّمَآءِ كَيۡفَ رُفِعَتۡ
Na mbingu jinsi ilivyoinuliwa?
وَإِلَى ٱلۡجِبَالِ كَيۡفَ نُصِبَتۡ
Na milima jinsi ilivyowekwa imara?
وَإِلَى ٱلۡأَرۡضِ كَيۡفَ سُطِحَتۡ
Na ardhi jinsi ilivyotandazwa?
فَذَكِّرۡ إِنَّمَآ أَنتَ مُذَكِّرٞ
Basi kumbusha! Hakika wewe ni Mkumbushaji.
لَّسۡتَ عَلَيۡهِم بِمُصَيۡطِرٍ
Wewe si mwenye kuwatawalia.
إِلَّا مَن تَوَلَّىٰ وَكَفَرَ
Lakini anayerudi nyuma na kukataa.
فَيُعَذِّبُهُ ٱللَّهُ ٱلۡعَذَابَ ٱلۡأَكۡبَرَ
Basi Mwenyezi Mungu atamuadhibu kwa adhabu iliyo kubwa kabisa!
إِنَّ إِلَيۡنَآ إِيَابَهُمۡ
Hakika ni kwetu Sisi ndio marejeo yao.
ثُمَّ إِنَّ عَلَيۡنَا حِسَابَهُم
Kisha hakika ni juu yetu Sisi hisabu yao!
share_via