Traducción al suajili - El Centro de Rowad Al- Taryamah

Traducción de los significados del Sagrado Corán

Traducida por el equipo del Centro Rowad At-Taryamah en cooperación con la Asociación de Dawah en Rabwa y la Asociación para el Servicio del Contenido Islámico en Idiomas.

QR Code https://quran.islamcontent.com/es/swahili_rwwad

وَٱلضُّحَىٰ

Ninaapa kwa wakati wa kabla ya adhuhuri!

Ninaapa kwa wakati wa kabla ya adhuhuri!

وَٱلَّيۡلِ إِذَا سَجَىٰ

Na kwa usiku unapotanda!

Na kwa usiku unapotanda!

مَا وَدَّعَكَ رَبُّكَ وَمَا قَلَىٰ

Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe.

Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe.

وَلَلۡأٓخِرَةُ خَيۡرٞ لَّكَ مِنَ ٱلۡأُولَىٰ

Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko uliotangulia.

Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko uliotangulia.

وَلَسَوۡفَ يُعۡطِيكَ رَبُّكَ فَتَرۡضَىٰٓ

Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike.

Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike.

أَلَمۡ يَجِدۡكَ يَتِيمٗا فَـَٔاوَىٰ

Kwani hakukukuta yatima, akakupa makazi?

Kwani hakukukuta yatima, akakupa makazi?

وَوَجَدَكَ ضَآلّٗا فَهَدَىٰ

Na akakukuta umepotea, akakuongoa?

Na akakukuta umepotea, akakuongoa?

وَوَجَدَكَ عَآئِلٗا فَأَغۡنَىٰ

Akakukuta mhitaji akakutosheleza?

Akakukuta mhitaji akakutosheleza?

فَأَمَّا ٱلۡيَتِيمَ فَلَا تَقۡهَرۡ

Basi yatima usimwonee!

Basi yatima usimwonee!

وَأَمَّا ٱلسَّآئِلَ فَلَا تَنۡهَرۡ

Na anayeomba au kuuliza usimkaripie!

Na anayeomba au kuuliza usimkaripie!

وَأَمَّا بِنِعۡمَةِ رَبِّكَ فَحَدِّثۡ

Na neema za Mola wako Mlezi zisimulie.

Na neema za Mola wako Mlezi zisimulie.