Header Include

Terjemahan Berbahasa Sawahili - Ali Muhsin Al-Barwani

Terjemahan Makna Al-Qur`ān Al-Karīm ke Bahasa Sawahili oleh Ali Muhsin Al-Barwani

QR Code https://quran.islamcontent.com/id/swahili_barawani

وَٱلضُّحَىٰ

Naapa kwa mchana!

Naapa kwa wakati wa kupanda juu jua, na ni wakati wa uchangamfu na kazi!
Naapa kwa mchana!

وَٱلَّيۡلِ إِذَا سَجَىٰ

Na kwa usiku unapo tanda!

Na naapa kwa usiku unapo tulia na ukatanda kote kiza chake!
Na kwa usiku unapo tanda!

مَا وَدَّعَكَ رَبُّكَ وَمَا قَلَىٰ

Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe.

Ewe Muhammad! Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukuchukia.
Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe.

وَلَلۡأٓخِرَةُ خَيۡرٞ لَّكَ مِنَ ٱلۡأُولَىٰ

Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko ulio tangulia.

Na matokeo ya mambo yako, mwisho wake, yatakuwa bora kuliko mwanzo wake.
Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko ulio tangulia.

وَلَسَوۡفَ يُعۡطِيكَ رَبُّكَ فَتَرۡضَىٰٓ

Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike.

Na ninaapa kuwa bila ya shaka hapo Mola wako Mlezi atakupa kheri za duniani na Akhera hata utaridhia.
Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike.

أَلَمۡ يَجِدۡكَ يَتِيمٗا فَـَٔاوَىٰ

Kwani hakukukuta yatima akakupa makaazi?

Kwani hakukukuta wewe yatima unahitaji wa kukutunza naye akakupa makaazi ya kukuhifadhi kwa mwenye kukuangalia vyema kwa mambo yako?
Kwani hakukukuta yatima akakupa makaazi?

وَوَجَدَكَ ضَآلّٗا فَهَدَىٰ

Na akakukuta umepotea akakuongoa?

Na akakuona umebabaika hukukinaika na itikadi zilizo kuzunguka, naye akakuongoa kwenye Njia ya Haki?
Na akakukuta umepotea akakuongoa?

وَوَجَدَكَ عَآئِلٗا فَأَغۡنَىٰ

Akakukuta mhitaji akakutosheleza?

Akakukuta fakiri wa mali naye akakutajirisha kwa kukupa riziki?
Akakukuta mhitaji akakutosheleza?

فَأَمَّا ٱلۡيَتِيمَ فَلَا تَقۡهَرۡ

Basi yatima usimwonee!

Ikiwa hii ndiyo hali yetu nawe, basi yatima usimdhili,
Basi yatima usimwonee!

وَأَمَّا ٱلسَّآئِلَ فَلَا تَنۡهَرۡ

Na anaye omba au kuuliza usimkaripie!

Na mwenye kuomba au kuuliza usimjibu kwa ukavu,
Na anaye omba au kuuliza usimkaripie!

وَأَمَّا بِنِعۡمَةِ رَبِّكَ فَحَدِّثۡ

Na neema za Mola wako Mlezi zisimlie.

Na ama neema za Mola wako Mlezi zitangaze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kuwa ndio kudhihirisha neema.
Na neema za Mola wako Mlezi zisimlie.
Footer Include